CCM pawaka moto Dodoma

Tafadhali kilewo rudi kwenye thread yako ya jana ya 'CCM pawaka moto' kuna deni unadaiwa hujamaliza kule uliwaahidi wana JF badala ya kuanzisha thread nyingine
 


Unashangilia kupona ukimwi
 
Kilewo acha kutuzuga nenda thread yako ya jana na ukiri kuwa wewe ni mwongo
 
Kwa sisi tunaoona mbali ni kwamba CCM haipo bali kuna makundi ambayo yamekuwa yakitumia mwavuli wa chama kujineemesha. Sasa ilipofikia hatua kwamba ufisadi umewaondoa kwenye neema, ndiyo wanapotoa makucha yao hadharani na hivyo kutia saini hukumu ya kifo cha chama (CCM)

CCM ilikufa wakati nyerere alipofariki coz nyerere alikuwa mhimili wa chama.. alikuwa akisema fulani anyang'anywe uanachama inakuwa hivyo. Sasa tatizo hakuna mtu aliyebaki mwenye exclusive power za kumuadabisha mkosaji ndani ya chama kama alivyokuwa nyerere, ndio maana chama kinaelekea kuzikwa muda si mwingi tokea sasa!
 
ngonjera tu hizo...
jf jana kiukweli dodoma kulikuwa hakukaliki, mpaka kikao kinahairishwa hakuna muafaka wowote ule, bali wakaamua kutumia vyombo vya habari kutuliza ghasia kwa wananchi ila mambo si shwari kabisa , wajumbe wamegawnyika makundi matatu
 
jamani ya jana yalikuwa makubwa sana dodoma ccm ndiyo mwisho
 
jamani ya jana yalikuwa makubwa sana dodoma ccm ndiyo mwisho


Kilewo,

Hauleweki, tueleze kinagaubaga yaliyojiri. CCM mwisho kivipi? na Kamati ya Mwinyi ndio hiyo imepewa miezi 2!!!
 
Hii JF ina watu wako kama yule fisi anayesubiri mkono wa binadamu udondoke, mtasubiri maisha. Mkitaka kuiondoa CCM mpaka mupambane nayo na wala sio kutegemea eti watagombana na kisha kutengana.

CCM wanafanya hii circus kwa sababu hakuna upinzani wenye nguvu, siku wakigundua kuna hatari ya kuondolewa, watu kama akina Chenge hawatabaki madarakani.

Upinzani kazi yao kushinda JF badala ya kwenda kwa wananchi vijijini.
 

You are missing the point si wote JF ni wapinzani hata kama wakishinda hapa ni maendeleo ya JF hupendi afterall no one is waiting for CCM to split out it is spliting for itself
 

Kaka mbona ushadanganyika hadi hapo? Mbona amna cha uchaguzi ila ni danganya toto tu, kwani aiwezekani mnajiandikisha watu 100, mnakuja kuambiwa waliopiga ni watu 40 na jamaa wanashinda asilimia 90 ya kura zilizopigwa.

Kwa maanahiyo atahiyo kujiandikisha sio dawa kwani hao waliojiandikisha awaendi kupiga au ata wakipiga unambiwa awajapiga.
 

No wonder wewe ni FIELD MARSHALL
 
Chama Cha Majambazi wajinga sana ati hivi sasa ndio wanampa Mwinyi kutatua matatizo yao. Kwani hawafahamu tangu alifu kwamba Mwinyi hata lile fagio la chuma aliuza kwa mafisadi. Huyu al-maarufu kama mzee wa ruhksa sasa kwa nini RA, EL et al wasiwe ruhksa?
 
jamani ya jana yalikuwa makubwa sana dodoma ccm ndiyo mwisho

Kilewo
Mbona hutupi majibu ya request ya jana, una maana gani , information unazotoa haziungiki bwana??!!
Kilevi/Kilewo vipi?, si uweke mambo wazi
 
Wajumbe wasema Lowassa awajibishwe kwakuwa chama kimechafuka sana na asipo wajibishwa wasilaumiwe kwa yale yatakayo tokea.
Upande wa Lowassa wasema hamna cha kumuwajibisha Lowassa kama ni suala la ufisadi chama kiwajibike na si Lowassa
Kilewo, tupe kulichijiri mpaka mwisho jana kaka!
 
CCM gives Mwinyi team more time

By The guardian reporter

16th February 2010

NEC reviews Isles political developments

JK warns members planning to join CCJ





Former President Ali Hassan Mwinyi



CCM National Executive Committee yesterday extended the mandate of a special committee under former President Ali Hassan Mwinyi for two months to look into the causes of the rift between the government and MPs.
The Mwinyi committee, which presented its report to NEC behind closed doors, was directed by members to return to the drawing board after members were of the view that it did stipulate clearly the source of the friction, The Guardian reliably learnt.
Sources said NEC members questioned the authenticity of the report presented yesterday which was different from the one presented before the Central Committee on Saturday.
Other members of the committee are Pius Msekwa who is also the party Vice-Chairman and Abdulrahman Kinana.
NEC also directed members of the Mwinyi committee to recommend more concrete solutions to end the division, the sources said.
Factions reportedly loyal to former Prime Minister Edward Lowassa and National Assembly Speaker Samuel Sitta have been involved in a bitter war of words for a while now.
The problem is believed to have started after the Parliamentary Select Committee that investigated the Richmond scandal called for the resignation of all top officials, prompting Lowassa's resignation.
Two camps involving CCM MP's have since emerged, one dubbed CCM-Mafisadi, referring to the party figures tarnished by allegations of corruption and the other involving vocal anti-corruption political figures.
But yesterday, under the chairmanship of President Kikwete, NEC was said to have failed to end the rift.
It was reported that the President had asked the Mwinyi committee to work on the report for one more month, but members recommended two months to allow the team to finish its work.
Another item on the agenda that was expected to be discussed yesterday was the state of politics in Zanzibar following the recent reconciliation between Zanzibar President Amani Karume and the Civic United Front (CUF) Secretary General, Seif Shariff Hamad.
However, sources said while the committee recommended that the election should take place, it rejected the idea of forming a coalition and instead recommended the formation of an inclusive government.
Meanwhile, sources said NEC member and former Infrastructure Development minister Andrew Chenge was spared expulsion from the party which had been recommended by some delegates.
The sources added that President Kikwete warned CCM members reported to have been planning to join CCJ (Chama cha Jamii), a party said to be seeking registration.

SOURCE: THE GUARDIAN
 
Kilewo
Mbona hutupi majibu ya request ya jana, una maana gani , information unazotoa haziungiki bwana??!!
Kilevi/Kilewo vipi?, si uweke mambo wazi

Tatito la kilewo anafikiri watu watasahau ajue JF hawasahau kirahisi na hilo doa alilojipaka asifikiri litafutika karibuni tutamkumbusha hata mwaka ujao JF idumu baada ya jana kutoka kwenye kikao cha NEC CCM leo kaibukia kwenye thread ya Ilani za Chadema anasifu Ilani yake siku zinaenda hazigandi kaazi kweli kweli
 
Hawana loloteeeeee wezi watupu woteeeee ni weziiiiii ni nani wa kumuwajibisha nani??? hawana mpango hata kidogo wasani
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…