CCM Shinyanga wammaliza Shibuda

CCM Shinyanga wammaliza Shibuda

WanaCCm wa shinyanga wameshatangaza kuwa Kikwete ndio mgobea pekee wa CCM mkoani humo according to Katibu wa CCM mkoani humo ,Mohamed Mbonde!Tatizo kubwa la shinyanga na mikoa mingi ,watu kama akina Mbonde i guess ni watu wa kuja,hawana passion ya maendeleo ya mkoa.I guess Mh Shibuda he cares about Shinyanga than this unknown Mr Mbonde.


Hayo si Shinyanga tu hiyo ni sera ya CCM. Ni nambari wani. Kama Shibuda hajaweka mbele CCM hawafai huyo, Shikh Yahya alisema atakufa atakaepingana na JK lakini hakufafanuwa kifo cha namna gani/ Pengine alikusudia kifo cha kisiasa ambacho Shibuda anaelekea kwayo.
 
wamwache shibuda agombee na yeye si haki yake jamani.Ila shinyanga jamani unafikiri ukitaka kumtawala mtu si unajifanya tu kama yeye hao waarabu wanaongea kisukuma tu ila hawana mapenzi ya dhati wengi wao wanafiki tu kina salumu mbuzi ndio kwanza sijui kaenda kujenga kiwanda arusha.kina phatom jamani na wengine wengi,ila jamani wabunge nao vibonde tu angallia shy town enzi za mfaume,makune ,derefa na sasa nani sijui shinyanga iko vilevile haiendelei inaendelea kurudi nyuma.
 
Zote hizi ni politics zao na hivyo inatupasa kuwa huru katika maamuzi yao na pia kufanya uchanguzi kuwa huru na haki kwa watu wote
 
Sina lolote na waarabu wa Shy,maana wengi wameassimilate ,na wengi ni sukuma speaking .Ila wengi wameenjoy prosperity generations na generations.angalia vinu vya mafuta,transport etc.also biashara ya diamonds ndio wenyewe tangu miaka na miaka since enzi ya mwadui,hata kabla ya maganzo !

tatizo ni waarabu wa Saudia na brand yao ya islam.



Kumbe si mkabila tu bali pia nimdini. Suwala la dini linakujaje na kimbelembele cha Shibuda. Yeye ametaka kumjaribu Sheikh Yahya sawa wacha tuone naniataibuka mshindi.
 
Mimi nafikiri hapa issue ni Democracy..... Shibuda anatumia haki yake ya kuzaliwa ambayo inalindwa na katiba ya nchi. Sasa whether Mbonde ni mtu kutoka Jupiter au Mars iliyopo Tanzania sio issue, issue ni je ana-mandate ya wana ccm wote wa Shinyanga? hata kama anayo, still Shibuda is right. Kubalini tu kwamba watanzania wameanza kuacha nidhamu ya woga ... that's it.... pinganeni bila kupigana ...ndani ya chama cha siasa ruksaaaa.
 
WanaCCm wa shinyanga wameshatangaza kuwa Kikwete ndio mgobea pekee wa CCM mkoani humo according to Katibu wa CCM mkoani humo ,Mohamed Mbonde!Tatizo kubwa la shinyanga na mikoa mingi ,watu kama akina Mbonde i guess ni watu wa kuja,hawana passion ya maendeleo ya mkoa.I guess Mh Shibuda he cares about Shinyanga than this unknown Mr Mbonde.
Acha kuwapa watu label. kutofautiana isiwe sababu ya kuwaita watu majina mabaya. Hivi huyo shibuja huko kwao amefanya nini??? Au anangojea apate urais ndiyo aendeleze kwao????
 
it seems mfaume,makune na derefa walikuwa sio wanashinyanga.angalia ccm ilivyofanya Bob makani asichaguliwe.wenzet wa bariadi wana msimamo panga pangua
wakina mapesa ,ccm imeshindwa kabisa
 
WAKATI mbunge wa jimbo la Maswa, John Shibuda akisisitiza nia yake ya kugombea urais, CCM mkoani kwake Shinyanga imeamua kumpuuza na kumtangaza Jakaya Kikwete kuwa mgombea pekee wa nafasi hiyo kwa tiketi ya chama hicho tawala.


CCM Shinyanga pia imesema haimtambui mgombea mwingine yeyote wa nafasi hiyo kwa tiketi yake na hata kama atajitokeza haitamuunga mkono.


Katibu wa CCM mkoani Shinyanga, Mohamed Mbonde aliwaambia waandishi wa habari kwenye ukumbi wa chama hicho kuwa chama hakina ugomvi na mtu anayetaka kugombea nafasi ya urais bali azingatie taratibu za chama hicho.


"Sisi wana CCM tumejiwekea utaratibu kwamba kila rais atakayechukuwa madaraka kupitia chama hiki atakaa madarakani kwa muda wa miaka kumi na hata katiba ya chama chetu inasema hivyo na mwanachama kugombea lazima azingatie katiba inasemaje," alisema Mbonde.


Aliongeza kuwa chama hakijapokea taarifa rasmi za kuwepo mmoja wa wabunge anayetaka kugombea nafasi ya urais mbali ya kusikia kwenye vyombo vya habari tu na kusisitiza kuwa halmashauri kuu ya CCM mkoani inamuunga mkono mwenyekiti wa taifa, Kikwete kuwa ni mgombea pekee wa nafasi hiyo.


Alisema mmoja wa wabunge hao anayedaiwa kutaka kugombea urais ni mjumbe wa halmashauri ya CCM ya mkoa ambayo imetoa tamko la kumuunga mkono Kikwete kugombea urais peke yake kupitia chama hicho.


Pia halmashauri hiyo imewataka wanachama wa CCM wote kutomdhihaki Kikwete kwa kuwa ndiye anayesimamia ilani waliyoiweka wenyewe na kwamba kama wanayo maoni ama matatizo watumie vikao vya chama hicho.


Lakini Shibuda alisema hapingi vikundi vya watu kutamka hadharani kuwa vinamuunga mkono Rais Kikwete.


"Kwa mujibu wa taratibu za kidemokrasia, matamko ya namna hiyo ni ishara ya ukosefu wa elimu ya uraia kwa wanaoyatoa," alisema Shibuda, mmoja wa wabunge machachari ndani na nje ya Bunge.


Shibuda alisema kuwa hakuhudhuria kikao cha halmashauri kuu ya mkoa na wala hana taarifa za kufikiwa uamuzi wa kumtangaza Kikwete kuwa mgombea pekee wa urais.


CCM pia imeunga mkono hotuba ya rais ya kuuaga mwaka 2009 na kuukaribisha mwaka 2010 ambayo ilitahadharisha dhidi ya kauli zinazotolewa na baadhi ya wanasiasa na viongozi wa taasisi za kiraia, hasa za kidini, akisema kuwa zina mwelekeo wa kuligawa taifa.


Katibu huyo wa CCM mkoa alisema kauli za watu hao zinaonyesha kuwa ni vipofu wa macho na mioyo na kwamba kuna uwezekano mkubwa wakawa na chuki binafsi.


Katibu huyo alisema wanaccm wana amini kuwa kukosoa na kukosolewa kwa kufuata taratibu ni msingi wa kuimarishana lakini kudhalilishana na kubezana ni msingi wa kuvunjana moyo na kwamba vitendo hivyo vinaweza kusababisha viongozi wa awamu zote za serikali zikapimwa kwa kuangaliwa mtu na hivyo nchi kupoteza mwelekeo.

.......................................................

Nashindwa kuelewa hawa viongozi kama Mbonde huwa wanasoma katiba ya chama chao au la. Sijaona mahala popote (I stand to be corrected) kwenye katiba ya CCM panaposema kuwa Rais atakaa madarakani miaka kumi.
 
Back
Top Bottom