CCM vyeo wanagawiana familia zao na uongozi wanapeana wao kwa wao; je wanachama wengine ni wapagazi wa kubeba nyundo na majembe?

CCM vyeo wanagawiana familia zao na uongozi wanapeana wao kwa wao; je wanachama wengine ni wapagazi wa kubeba nyundo na majembe?

Mikopo Consultant

JF-Expert Member
Joined
Oct 28, 2024
Posts
529
Reaction score
1,150
download (1).png


Tukiwa katikati ya mtanange mkali wa kidemokrasia wa CHADEMA ambao umetoa usawa na fursa kwenye kugombea nafasi mbalimbali hivo kuibua vipaji vipya vya uongozi; CCM waliibuka na wao Dodoma kwenye mchakato wao wa kutafuta makamu mwenyekiti wa chama.

Kwa mbwembwe za msururu wa magari mapya (vinyulaa) yaliowabeba wajumbe wa CCM wakiambatana na viongozi wazito wa chama hicho, tulijua kuna jambo kubwa linaenda kutokea Dodoma ambalo halijawahi kutokea.

Kwa masikitiko makubwa, kimetokea kihoja Dodoma; mbali na nafasi ya makamu kupatikana pasipo misingi ya demokrasia ya kugawa fursa za kuchaguana kwa wote, CCM wamekuja na mzee asiyeendana na nyakati za kileo na mabadiliko makubwa ya kisiasa yanayotokea.

Nimepata huruma sana kwa wana CCM wengine ambao wao hawatoki kwenye familia za vigogo wala hawana ushawishi wowote kwenye chama; je hao watapewa lini fursa za kuonesha vipaji vyao vya uongozi kama bado kuna misingi ya demokrasia za majina ya mfukoni?

Au hawa wana CCM wengine wataishia kuwa wapagazi wa kuwabebea ma 'giants' wa CCM majembe na manyundo mpaka wanazeeka, huku wakisindikizwa na wapiga madebe akina Tlaatlaah ChoiceVariable na kamanda asiyechoka kububujika machozi Lucas Mwashambwa ?

Hii inahitaji tafakari sana, CCM msidhani kwamba kushangilia kwenu ukosefu wa misingi ya demokrasia nchini kunawanufaisha kwa chochote. Kwa misingi iliyopo ndani ya CCM wengi mtaishia kuwa wapagazi, wapambe na machawa mpaka mzeeke.

What a waste of life.
 
Nina mshikaji wangu huyu bwana
1. Ni HR wa Halmashauri X
2. Ana Masters ya MBA in HR
3. Mpiga kazi balaa

Sasa bwana kwenye chama cha CCM ...
1. Yeye kila mwaka ana jezi mpya
2. Hakuna event ya CCM ya mkoa au wilaya asihudhurie
3. Kaenda mara kibaoo kwenye mikutano ya Chama Dodoma

Ila sasa ....
Sio kiongozi yoyote, huwa namwambiaga kuwa "braza huko unapotea na kupoteza muda, CCM ina wenyewe na walio wenyewe ni hawa wenye koo za VIP au wanaojuana na hizo koo"" ila Haelewagi

Namuoneaga huruma sanaa huyu kijana wangu.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
 
Nina mshikaji wangu huyu bwana
1. Ni HR wa Halmashauri X
2. Ana Master ya MBA in HR
3. Mpiga kazi balaa

Sasa bwana kwenye chama cha CCM ...
1. Yeye kila mwaka ana jezi mpya
2. Hakuna event ya CCM ya mkoa wa wilaya asiudhurie
3. Kaenda mara kibaoo kwenye mikutano ya Chama Dodoma

Ila sasa ....
Sio kiongozi yoyote, huwa namwambjaga kuwa "braza huko unapotea na kupoteza muda, CCM ina wenyewe na walio wenyewe ni hawa wenye koo za VIP au wanaojuana na hizo koo"" ila Haelwagi

Namuoneaga huruma sanaa huyu kijana wangu.

#YNWA
#YANGA_BINGWA
Inahuzunisha ila ndo ukweli, na mimi nawajua watu CCM kindaki ndaki wana mpaka ma Phd ila hola bila bila na wanakomaa sana ilaa wapii
 
Observe kwa makini, ni Pyramid. Waliochini watabaki humo humo tu na wajuu ndo wapogo hapo milele.

Wasira akichoka kabisa kabisa, atampa pasi mwanae..
Mwanaye yupi sasa?

Halafu kumbuka mambo ya chama yanafuata katiba ya chama husika, unaweza kuamua ukajitoa, ila serikali ndio unaweza kulalamikia maamuzi kama hayo, kwasababu ni ya wote, chama ni hiyari ya wanachama.
 
Kwani Lucas Mwashambwa hajapewa hata Uenyekiti wa Bawacha?

Nyiee!!! Na kububujikwa kote kule hajaambulia lolote?

Naagiza Lucas apewe ukatibu wizara ya maliasili.

Hili litekelezwe mara moja.
Bila bila kama Yanga na Mc Algers. Ila with time, ninachoamini gradually wapagazi wa CCM wataanza kuchoka tu siku moja baada ya kuutambua ukweli kwamba hawana chao kwenye chama
 
Mwanaye yupi sasa? Halafu kumbuka mambo ya chama yanafuata katiba ya chama husika, unaweza kuamua ukajitoa, ila serikali ndio unawwza kulalamikia maamuzi kama hayo, kwasababu ni ya wote, chama ni hiyari ya wanachama.
Lugha ya picha hiyo, simaanishi mwanae ila ni kwamba watapeana wao kwa wao.
 
View attachment 3205616

Tukiwa katikati ya mtanange mkali wa kidemokrasia wa CHADEMA ambao umetoa usawa na fursa kwenye kugombea nafasi mbalimbali hivo kupata vipaji vipya vya uongozi; CCM waliibuka na wao Dodoma kwenye mchakato wao wa kutafuta makamu mwenyekiti wa chama.

Kwa mbwembwe za msururu wa magari mapya (vinyulaa) yaliowabeba wajumbe wa CCM wakiambatana na viongozi wazito wa chama hicho, tulijua kuna jambo kubwa linaenda kutokea Dodoma ambalo halijawahi kutokea.

Kwa masikitiko makubwa, kimetokea kihoja Dodoma; mbali na nafasi ya makamu kupatikana pasipo misingi ya demokrasia ya kugawa fursa za kuchaguana kwa wote, CCM wamekuja na mzee asiyeendana na nyakati za kileo na mabadiliko makubwa ya kisiasa yanayotokea.

Nimepata huruma sana kwa wana CCM wengine ambao wao hawatoki kwenye familia za vigogo wala hawana ushawishi wowote kwenye chama; je hao watapewa lini fursa za kuonesha vipaji vyao vya uongozi kama bado kuna misingi ya demokrasia za majina ya mfukoni?

Au hawa wana CCM wengine wataishia kuwa wapagazi wa kuwabebea ma 'giants' wa CCM majembe na manyundo mpaka wanazeeka, huku wakisindikizwa na wapiga madebe akina Tlaatlaah ChoiceVariable na kamanda asiyechoka kububujika machozi Lucas Mwashambwa ?

Hii inahitaji tafakari sana, CCM msidhani kwamba kushangilia kwenu ukosefu wa misingi ya demokrasia nchini kunawanufaisha kwa chochote. Kwa misingi iliyopo ndani ya CCM wengi mtaishia kuwa wapagazi, wapambe na machawa mpaka mzeeke.

What a waste of time.
Wewe ni Mwana CCM? Kama sio shida ni nini? Na kama wewe ni mwana CCM na hupendi hayo kwanini bado upo CCM?
 
Back
Top Bottom