CCM wangependa CHADEMA wasusie chaguzi

CCM wangependa CHADEMA wasusie chaguzi

Kujipanga kwa ushindi katika hali yoyote nako hakuwezi kuwa impossible.

Hata hivyo itataka kusugua vichwa kweli kweli.
Mkuu 'Brazaj', naiona mada yako hii kuwa ni juhudi tu za kutafuta michango ya mawazo ni nini hasa wanachotakiwa kufanya CHADEMA ili kukomesha uharamia wa CCM kubaki madarakani.

CHADEMA kama chama cha siasa, sioni chochote wanachoweza kunufaika nacho kwa kususia uchaguzi wowote tokea hapa kwenda mbele.
Mchango wangu katika hili ni kuwa, CHADEMA ni lazima wawe tayari kabisa kuweka wagombea wao katika nafasi zote za uchaguzi, bila kukosa hata moja, toka ngazi ya shina hadi juu kabisa. Kazi ya kuwaandaa watu hawa ni sasa hivi, wakati huu na siyo baadae. Mgombea yeyote kuenguliwa katika nafasi ya kugombea kwa sababu za kizembe au hila za CCM kama ilivyokuwa huko nyuma iwe ni mwiko kabisa. Na hili lisiwe swala la kujaza nafasi za wagombea tu, ni lazima wawe wagombea wenye sifa na uwezo wa kuongoza.

Pili, umegusia swala na "wenye vifua", nikidhani una maana ya "matumizi ya nguvu za Dola" katika uharamia wa CCM kuchafua chaguzi. Hili tulishalijadili huko nyuma, kama unakumbuka.
Huu ni "uhalifu" wanaofanya CCM, na wananchi wanajua ni uhalifu, ila hawana uongozi unaowaweka pamoja kuukataa uhalifu huo. Kazi iliyopo na ambayo ingepashwa iwe tayari inafanyika, ni kwa CHADEMA kuweka mikakati ya kuukataa uvunjaji huu wa sheria.
CHADEMA wanatakiwa kuzijua njia zote zinazotumika katika uhalifu huo, na kuandaa mipango ya kuizuia katika kila ngazi.
Siyo kazi ngumu kujua wanayofanya CCM. Kwa mfano, angalia tu sasa hivi wanavyojipanga kutumia njia zilezile! Umeangalia hizi ziara za hivi karibuni za Mwenyekiti wa Chama hicho, akitumia kofia ya URais wake? Soma vizuri mikusanyiko hiyo na mbinu zote tokea huko. Huyo huyo Mwenyekiti, anaunda serikali yenye madhumuni yaleyale wakati wa chaguzi zinazokuja. Kwa nini CHADEMA wasiyasome yote haya na kuyaelewa vizuri, na kujiandaa kuyaaangusha?

CCM hawana njia mpya watakazozitegemea kubaki madarakani, na mbaya zaidi kwao, hata hali ya kisiasa ya kawaida tu haiwapi nafuu yoyote, sasa CHADEMA watashindwa vipi kupambana na hawa majambazi?
 
Ni vyema hali ya uwanja ikawa wazi kwetu na kwao. Ukweli hautaacha kuwa mchungu.

Kususia uchaguzi itakuwa ni SAWA na kususia fisi bucha. Wanapaswa kujua kususa hakupo!

Kujipanga kwa ushindi katika hali yoyote nako hakuwezi kuwa impossible.

Hata hivyo itataka kusugua vichwa kweli kweli.

Ikumbukwe wenye vifua vyao wanayo kila sababu ya kufanya yao.
Hali ya kuwa chama cha upinzani cha kweli kwenye nchi kama yetu ni mtihani mkubwa sana.

Maana sioni kuna siku ccm watakubali kuweka uwanja sawa wa kiushindani.

Ccm wanaelewa kabisa kuwa wamechokwa na watanzania walio wengi.
 
Ukweli ni kwamba ccm imekwisha
Imekwisha kwenye mioyo ya watanzania wanaojitambua ila tukiingia kwenye uwanja wa mapambano ccm watatumia ulaghai kutokana na mapungufu makubwa yaliyopo kwenye tume ya uchaguzi na katiba ya nchi yetu.
 
Tatizo ni kwenye kuukwamisha mpira wavuni ila chenga twawala ..
Hilo lipo wazi sana mkuu.
Ebu tazama uchaguzi wa zenji maana kila mwaka huwa wanapigwa sana lkn mwisho kina Jecha wanaamua nani atawale.
 
Ni ujinga sana kwa vidole viwili kugomea uchaguzi, maana mafisiem yanafurahi na kujikita zaidi. Before marehemu vijana kibao walisimama na kujenga hoja za msingi wakashinda majimbo, wanapaswa kupigania angalau turudi zama za kabla ya marehemu, demokrasia ni finyu tz, lakini maamuzi mgando sana kuwasusia kijani msosi.

Hawashtuki wale ndo kwanza wanakomba vizuri. Kwasasa ni mawazo potofu sana kuamini kutakuwa na katiba mpya anytime soon. Mechi ni hii hii, ingia uwanjani kacheze game, kama ni daluga ukipigwa piga, kila mmoja akizidiwa mtacompromise mbele ya safari maana kila mtu anaumia. This was the way to go 2015 and before.
Inawezekana vyama vya upinzani vikapata ushindi kwenye baadhi ya majimbo.

Ila lazima tujitoe mhanga bila kuogopa kuswekwa magerezani maana ccm hawatakubali kuwapatia wapinzani nafasi hata moja ya jimbo.

Ni muhimu kulazimisha kuzilinda kura kwa moyo Safi na nia thabiti.
 
Then tukubali kuwa ccm itakuwa imefanikiwa kuendeleza ushindi wao wa hila.
Mabalozi wa Nchi za magharibi wanafuatilia kwa karibu sasa viongozi wa CHADEMA ndio wanatakiwa wapigilie msumari ili pressure iongezwe kwa huyo Mama.
 
Mkuu 'Brazaj', naiona mada yako hii kuwa ni juhudi tu za kutafuta michango ya mawazo ni nini hasa wanachotakiwa kufanya CHADEMA ili kukomesha uharamia wa CCM kubaki madarakani.

CHADEMA kama chama cha siasa, sioni chochote wanachoweza kunufaika nacho kwa kususia uchaguzi wowote tokea hapa kwenda mbele.
Mchango wangu katika hili ni kuwa, CHADEMA ni lazima wawe tayari kabisa kuweka wagombea wao katika nafasi zote za uchaguzi, bila kukosa hata moja, toka ngazi ya shina hadi juu kabisa. Kazi ya kuwaandaa watu hawa ni sasa hivi, wakati huu na siyo baadae. Mgombea yeyote kuenguliwa katika nafasi ya kugombea kwa sababu za kizembe au hila za CCM kama ilivyokuwa huko nyuma iwe ni mwiko kabisa. Na hili lisiwe swala la kujaza nafasi za wagombea tu, ni lazima wawe wagombea wenye sifa na uwezo wa kuongoza.

Pili, umegusia swala na "wenye vifua", nikidhani una maana ya "matumizi ya nguvu za Dola" katika uharamia wa CCM kuchafua chaguzi. Hili tulishalijadili huko nyuma, kama unakumbuka.
Huu ni "uhalifu" wanaofanya CCM, na wananchi wanajua ni uhalifu, ila hawana uongozi unaowaweka pamoja kuukataa uhalifu huo. Kazi iliyopo na ambayo ingepashwa iwe tayari inafanyika, ni kwa CHADEMA kuweka mikakati ya kuukataa uvunjaji huu wa sheria.
CHADEMA wanatakiwa kuzijua njia zote zinazotumika katika uhalifu huo, na kuandaa mipango ya kuizuia katika kila ngazi.
Siyo kazi ngumu kujua wanayofanya CCM. Kwa mfano, angalia tu sasa hivi wanavyojipanga kutumia njia zilezile! Umeangalia hizi ziara za hivi karibuni za Mwenyekiti wa Chama hicho, akitumia kofia ya URais wake? Soma vizuri mikusanyiko hiyo na mbinu zote tokea huko. Huyo huyo Mwenyekiti, anaunda serikali yenye madhumuni yaleyale wakati wa chaguzi zinazokuja. Kwa nini CHADEMA wasiyasome yote haya na kuyaelewa vizuri, na kujiandaa kuyaaangusha?

CCM hawana njia mpya watakazozitegemea kubaki madarakani, na mbaya zaidi kwao, hata hali ya kisiasa ya kawaida tu haiwapi nafuu yoyote, sasa CHADEMA watashindwa vipi kupambana na hawa majambazi?


Twende kwenye uchaguzi tukiwa tumedhamiria kushinda na pia tukiwa tumedhamiria kukataa kuibiwa.

Dhamira zetu zilizothabiti machoni Pao zitatuvusha.

Tukae chini kukubaliana tunayodhamiria Kila mtu akiwamo wao ayajue.
 
Ni vyema hali ya uwanja ikawa wazi kwetu na kwao. Ukweli hautaacha kuwa mchungu.

Kususia uchaguzi itakuwa ni SAWA na kususia fisi bucha. Wanapaswa kujua kususa hakupo!

Kujipanga kwa ushindi katika hali yoyote nako hakuwezi kuwa impossible.

Hata hivyo itataka kusugua vichwa kweli kweli.

Ikumbukwe wenye vifua vyao wanayo kila sababu ya kufanya yao.
Yaani uko correct vibaya sana. Huwa nasikia watu wakipiga kelele eti Chadema wasishiriki uchaguzi mkuu ujao. Hili ni kosa kubwa sana. Itakachofanya CCM ni kupanga deal na vibaraka kama kina Zitto, halafu wampe majimbo ya Pemba yote kama ilivyokuwa inashinda CUF zamani plus majimbo kadhaa huku kwetu Tanganyika. Wanaweza kuwapa na vyama vingine kama CUF majimbo machache sana halafu watasifu uchaguzi ulikuwa huru na wa haki, na ambaye hakushiriki alipenda mwenyewe. Kuanzia hapo CCM (b) a.k.a. mazambarao, watakuwa chama kikuu cha upinzani wakiongozwa na Abel Muzorewa wa Tanzania yaani Zitto. Hapo sasa watatengeneza katiba fake na mbovu kuliko hata hii ya hivi sasa ili 2030, wachukuwe tena nchi kiulaini. Chadema wana alternative moja tu: Kushiriki uchaguzi hivyo hivyo na katiba ya sasa, lakini nguvu wawekeze kwenye kuwaambia wapiga kura kuwa CCM akiiba kura basi wakiwashe na kudai haki kwa nguvu. Japo kuna uwezekano kuwa watanzania bado ni waoga lakini huwezi kujua.... siku zote siyo Jumamosi..
 
Bila marekebisho ya Katiba ya 77 kwenda kwenye uchaguzi ni kupoteza muda au labda tufanye nae makubaliano ya serikali ya "nusu mkate"
Uko sahihi kabisa. Lakini nako kususia ni mbaya zaidi. Ni bora wawatayarishe wananchi kupiga na kulinda kura kwa gharama yoyote. Wengi wa polisi na hata wanajeshi sasa hivi huwa wanasema wananchi wakijitokeza kwa wingi wala hawatakuwa kizuizi. Wanachotaka tu ni wananchi wajitokeze wengi ili ionekane kuwa wamezidiwa nguvu.
 
Uko sahihi kabisa. Lakini nako kususia ni mbaya zaidi. Ni bora wawatayarishe wananchi kupiga na kulinda kura kwa gharama yoyote. Wengi wa polisi na hata wanajeshi sasa hivi huwa wanasema wananchi wakijitokeza kwa wingi wala hawatakuwa kizuizi. Wanachotaka tu ni wananchi wajitokeze wengi ili ionekane kuwa wamezidiwa nguvu.
Lakini Samia aliwahi kusema nyie pigeni kura lakini CCM ndio watakaotangazwa
 
Lakini Samia aliwahi kusema nyie pigeni kura lakini CCM ndio watakaotangazwa
Ni kweli kabisa. Na naweza kusema 2025 watafanya kila njia kuiba kwa sababu kuna mikataba ya kipigaji wameingia na wanapanga kuingia hivyo watalazimisha kuilinda. Pia wanaogopa akiingia rais mwingine anaweza kuibua machafu mengi yaliyofanyika. Yaani kwa kifupi watafanya kila namna ili kuiba. Ila sasa kususia kutafanya mambo yao yawe rahisi zaidi. Maoni yangu ni kuwa Chadema washiriki huwezo kujua muujiza wa wananchi kukataa wizi wa kura unaweza kutokea.
 
Ni vyema hali ya uwanja ikawa wazi kwetu na kwao. Ukweli hautaacha kuwa mchungu.

Kususia uchaguzi itakuwa ni SAWA na kususia fisi bucha. Wanapaswa kujua kususa hakupo!

Kujipanga kwa ushindi katika hali yoyote nako hakuwezi kuwa impossible.

Hata hivyo itataka kusugua vichwa kweli kweli.

Ikumbukwe wenye vifua vyao wanayo kila sababu ya kufanya yao.
Ninachowaomba CHADEMA chonde chonde wasifanye kosa la kususia uchaguzi. Majimbo yenu mengi yanawasubiri!
 
Kama waliweza kuiba Zanzibar mpaka Maalim kuja na strategy ya kupiga kura kwa wingi ili kuwa overwhelm wakaamua kumtuma JECHA avuruge mchakato.

CHADEMA tukitumia hiyo njia ya kupiga kura kwa wingi watavuruga tu.
 
Chadema wana alternative moja tu: Kushiriki uchaguzi hivyo hivyo na katiba ya sasa, lakini nguvu wawekeze kwenye kuwaambia wapiga kura kuwa CCM akiiba kura basi wakiwashe na kudai haki kwa nguvu. Japo kuna uwezekano kuwa watanzania bado ni waoga lakini huwezi kujua.... siku zote siyo Jumamosi..
Mkuu 'macho', hapa ndipo wanapotakiwa kuwekeza juhudi kubwa sana hawa CHADEMA.

Njia zote za uharamia wa CCM zinajulikana, na hakuna njia mpya hata moja inayoonekana wanaiandaa kuhujumu chaguzi zijazo.

CHADEMA hawahitaji waTanzania milioni sitini na ushee, kukataa ujinga unaofanywa na CCM kila mara. Wanachohitaji, sana sana ni kama watu hamsini hivi kila kituo cha kura kuhakikisha kuwa hakuna upuuzi unaoweza kufanywa kuharibu kura za wananchi.

CHADEMA sasa hivi, wanao wanachama wa kutosha kila sehemu ya nchi kuhakikisha kuwa CCM hawafanyi uchafu wowote, hata bila ya kuhusisha vyombo vya dola.

Swala muhimu, ni kuandaa mkakati madhubuti kukabiriana na hawa CCM, ili kuzuia uhalifu waliozoea kuufanya katika kila chaguzi.

Kwa hiyo, hapa siyo swala la waTanzania kuwa waoga, ni swala tu la kuwaeleza uhalifu unaofanyika na njia sahihi za kuzuia uhalifu huo, basi.
Watu watatekeleza wajibu wao pasipo haja ya kuogopa chochote.
 
Inawezekana vyama vya upinzani vikapata ushindi kwenye baadhi ya majimbo.

Ila lazima tujitoe mhanga bila kuogopa kuswekwa magerezani maana ccm hawatakubali kuwapatia wapinzani nafasi hata moja ya jimbo.

Ni muhimu kulazimisha kuzilinda kura kwa moyo Safi na nia thabiti.
Hao kina Sugu, Professor J and the like walipataje, tunaact as if before Magufuli hakukuwa na hiyo fursa. Chadema warudi tu kwenye mapambano waliyoyaweza zamani. Ni as if wamekata tamaa na kusahau vurugu kubwa ilikuwa tu kwenye uchaguzi uliopita. Halafu acheni ujinga wa kuwapinga ACT, the real threat ni chama tawala, hao purple mnawapinga as if wana impact kwenye harakati zenu.
 
Back
Top Bottom