CCM ya Magufuli ni ya kijima kweli kweli: Hivi unamkataje Stephen Masele, Makamu wa Kwanza wa Rais Bunge la Pan-African, chombo muhimu cha AU?

Professor Majalalaa mtoa macho awamu hii amekuwa promoted. Next...
 
Afisa wa TISS uyo
 
Zamaza sura zile zile imeshaita.sasa ivi ni mwendo wa sura mpya na mawazo mapya...
 
Maselle Ni Afisa Kipenyo Huyo wanajuana wenyewe kwà wenyewe nyie tafuteni Ngawila tu mle na Familia zenu Haya masuala yatawachosha tu
Mambo ya twiter unayaamini?
Kigogo unamwamini?
 
Eti "kioo cha siasa". Kioo cha siasa rushwa zote hizo?! Labda choo cha siasa. Kioo cha siasa my foot.
Throw back Edward lowassa 2015.

Kijana Tulia Akili yàko Ni nyeupe Sana Huwezi kunielewa.
 
Masuala ya kidiplomasia ni dynamic na sio static, mfano; kipindi cha Nyerere hatukuwa na mahusiano mazuri na taifa la Israel hadi kupelekea kutokuwa na mahusiano ya kibalozi, leo hii katika utawala wa Magufuli kupitia Mahiga tulifungua ubalozi wetu pale Jerusalem na wala sio Tel Aviv.

Mfano mwingine, kipindi cha Nyerere EAC ilikufa, kipindi cha mkapa ikafufuliwa, kipindi cha kikwete ikayumba, mpaka sasa inayumba.

Mfano mwingine, kipindi cha Obama, Marekani walisaini maridhiano na Iran, leo hii Potus katupilia mbali makubaliano yote na sanctions zinawekwa kila siku, vp kuhusu mahusiano yao na China kipindi hiki?

Leo hii UAE wanasaini makubaliano na Israel na hakuna cha kushangaza, hakuna mahusiano ya kidiplomasia ya kudumu au ugomvi wa kudumu, whatever can happen in between.

Mahusiano ya Rwanda na Uganda unayaonaje kwa sasa licha ya urafiki wa muda mrefu baina ya Kagame na Museveni?

Usipotoshe, hakuna mtu aliyeteuliwa kimataifa alafu Magufuli akabana, kama yupo tutajie.

Mwisho, chama chochote hakipangiwi taratibu, kinajiwekea taratibu zake chenyewe na wanachama wanaridhia. Huyo Masele analielewa hilo na anajua huko AU asingefika bila mwamvuli wa chama, sasa kama baadae akakengeuka na kujiona kama mkubwa kuzidi chama, mkubwa kajionyesha, imekula kwake.
 
Jitahidi kujisomea na kufuatilia mambo ya nchi na dunia kwa ujumla, utaboresha uelewa wako. Licha ya kwamba nilifahamu mapema lakini pia nimefika Jerusalem na Tel Aviv nchini Israel. Ni kwamba ubalozi wa Tanzania hauko Jerusalem bali uko Tel Aviv. Nchi zenye ubalozi Jerusalem mpaka kufikia muda huu ni United States na Guatemala pekee. Nchi nyingine zote zenye uhusiano mzuri na Israel balozi zao ziko Tel Aviv.

Mapungufu haya kwenye hoja yako tayali yanaonesha ulivyo mvivu wa kujisomea na kuandika kishabiki zaidi kuliko uhalisia wa mambo.
 
Usikimbie point ya msingi, hayo mapungufu nimeyapokea, pointi ya msingi ni Tanzania kuwa na Ubalozi Israel wakati hapo awali hatukuwa na mahusiano mazuri ya kidiplomasia.
 
Usikimbie point ya msingi, hayo mapungufu nimeyapokea, pointi ya msingi ni Tanzania kuwa na Ubalozi Israel wakati hapo awali hatukuwa na mahusiano mazuri ya kidiplomasia.
Nimekuelewa, ni kweli diplomasia ya nchi hubadilika kulingana na wakati, lakini si kwa kiwango cha kumfitini mzawa ili akose vyote, maana si kwamba unamkomoa yeye tu bali ni hasara kubwa kwa nchi.

Masele ni kijana mwelewa na anasikiliza wazee, ikiwa wanaona aliwakosea kibinafsi ni kiasi cha kumuita tu na kumweleza ajirekebishe, lakini kutumia interest binafsi kuangamiza taifa nao ni uhujumu uchumi na si utawala bora kwa nchi.
 
Sijamfuatilia in details huyu jamaa kwa hiyo siwezi ongelea zaidi suala lake, nilichoongelea mimi ni general concept ya flexibility ya diplomasia, anything can happen at anytime.

Chukulia mfano leo hii marekani kujitoa kufund WHO, apparently,wamarekani wengi ambao wanaajira za moja kwa moja kupitia hiyo hiyo organization watakwenda kuathirika. Kwa hiyo ni uamuzi nchi imefanya na unamwenda kuwaathiri raia wake kwa namna fulani lakini ndio hivyo tena, mambo ya diplomasia yalivyo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…