CCM yaachwa solemba

CCM yaachwa solemba

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
CCM ina msimamo wake rasmi juu ya Rasimu ya Katiba mpya.Msimamo huo unahusu hasa kupinga kwa nguvu zote uwepo wa Serikali Tatu. Msimamowa cahama chetu ni kutaka Serikali mbili. Si tatu kama Rasimu inavyopendekeza.

Pamoja na kutoa msimamo kichama,CCM inategemea makada wake walioko kwenye Tume ya Katiba iliyochini ya Jaji Joseph Sinde Warioba ili kuchukua msimamo huo wa chama kama'maoni ya wananchi wengi'. Mambo sasa ni tofauti. Wajumbe karibu wote wa Tume ya Warioba wanaupinga hadharani msimamo wa CCM-wa Serikali mbili na kutetea Serikali tatu.

Ningetarajia wengine wote waunge mkono 'usaliti' kwa chama lakini si Prof. Palamagamba J. A. M. Kabudi. Lakini jana,Prof.Kabudi,akiwa Kisarawe, amesema wazi kuwa Serikali tatu hazikwepeki. Naujua msimamo dhabiti wa Prof.Kabudi katika utetezi wa sera na misimamo ya chama na Serikali yake. Mfano wa hivi karibuni ni kuunga mkono katazo la mgombea huru katika kesi ya Mwanasheria Mkuu dhidi ya Mchungaji Christopher Mtikila iliyokuwa na kuamuliwa na Mahakama ya Rufani Tanzania.

Huu wa jana ni mpya. Naye ameamua kuicha solemba CCM.Ameikatalia. Prof.Kabudi amesema kitu pekee kitakachosaidia kuwapo kwa maridhiano kati yetu kama watanzania ni Serikali tatu tu. Si vinginevyo. Baada ya hapo,Wajumbe karibu wote wa Baraza la Katiba Wilaya ya Kisarawe walikubaliana naye.

Wakabadili msimamo wao.Wakalaumu 'kulishwa kasa' kwa mambo muhimu kama haya;tena na chama tawala.Wajumbe hao wakaendelea kuchangia Rasimu kwa bashasha na utulivu.Wakauweka msimamo wa CCM kando. Wakaupuuza. Prof.Kabudi apaswa kwenda kwinginepo pia kuisambaratisha picha isiyovutia ya msimamo wa CCM.

Mzee Tupatupa wa Lumumba,Dar es Salaam
 
Serikali tatu muhimu ili tubaki na tanganyika yetu.
Muungano ulishakufa siku nyingi..
Mzee tupatupa huogopi wangoao kucha na meno??
Utueleze pia kwa nini mnawanyima uhuru watangazaji wa TBC kutupa taarifa za mrengo wa vyama vyote.
 
vuta nikuvute,

una siku ya ngapi hujala??
njaa inayokusumbua ni hii ya kawaida au ipo nyingine?? kwann unaficha maradhi??
 
Usitake kuharalisha hoja yako kwa kujinasibisha kama wewe ni mwanaCCM na unafanya kazi ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM, Lumumba.

Kila mara unaleta uwongo na uzandiki hapa JF kutaka kuwaaminisha wanaJF.

Tunakufahamu vizuri sana ila sheria za JF hazituruhusu kuwambia wanaJF uhalisia wako.

Uwongo siyo nguzo imara na uwongo mara nyingi huwa ni siraha ya muda mfupi.

Endelea kuwadanganya wanaJF.
 
mtu mfupi huwa na mawazo mafupi wewe na dr slaa nani mkubwa kwa mwenzake.
 
Msimamo wa ccm ni serikali mbili
pemba wanataka muungano wa mkataba wa serikali tano
unguja wanataka serikali nne
machadema yanataka serikali tatu wakishirikiana na cuf
sio dhambi kwa ccm kama taasisis kutoa maoni ya katiba waitakayo, tatizo la mleta mada ni mtindio tu wa ubongo
 
vuta nikuvute,

una siku ya ngapi hujala??
njaa inayokusumbua ni hii ya kawaida au ipo nyingine?? kwann unaficha maradhi??
Masalia jenga hoja, msimamo wenu ni serikali mbili, wakati umeshafika wa kuitambua Tanganyika yetu... tunaiona ile inakuja...
 
vuta nikuvute,

una siku ya ngapi hujala??
njaa inayokusumbua ni hii ya kawaida au ipo nyingine?? kwann unaficha maradhi??

huyu ni mmoja wa wanaosaini hizo elfu saba unazopewa , jaribu kuwa na heshima , Alaaah !
 
Msimamo wa ccm ni serikali mbili
pemba wanataka muungano wa mkataba wa serikali tano
unguja wanataka serikali nne
machadema yanataka serikali tatu wakishirikiana na cuf
sio dhambi kwa ccm kama taasisis kutoa maoni ya katiba waitakayo, tatizo la mleta mada ni mtindio tu wa ubongo
Mkuu hii si mada.Hii ni habari
 
Usitake kuharalisha hoja yako kwa kujinasibisha kama wewe ni mwanaCCM na unafanya kazi ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM, Lumumba.

Kila mara unaleta uwongo na uzandiki hapa JF kutaka kuwaaminisha wanaJF.

Tunakufahamu vizuri sana ila sheria za JF hazituruhusu kuwambia wanaJF uhalisia wako.

Uwongo siyo nguzo imara na uwongo mara nyingi huwa ni siraha ya muda mfupi.

Endelea kuwadanganya wanaJF.
Jadili hoja Mkuu. Utabaki kunijua hivyo hivyo tu. Tena,yawezekana nimekupokea chamani wewe
 
Usitake kuharalisha hoja yako kwa kujinasibisha kama wewe ni mwanaCCM na unafanya kazi ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM, Lumumba.

Kila mara unaleta uwongo na uzandiki hapa JF kutaka kuwaaminisha wanaJF.

Tunakufahamu vizuri sana ila sheria za JF hazituruhusu kuwambia wanaJF uhalisia wako.

Uwongo siyo nguzo imara na uwongo mara nyingi huwa ni siraha ya muda mfupi.

Endelea kuwadanganya wanaJF.

Unaleta mikwara jf ! Kwani alichoandika ni uongo ? Haya tuletee ukweli unaoufahamu .
 
Serikali tatu muhimu ili tubaki na tanganyika yetu.
Muungano ulishakufa siku nyingi..
Mzee tupatupa huogopi wangoao kucha na meno??
Utueleze pia kwa nini mnawanyima uhuru watangazaji wa TBC kutupa taarifa za mrengo wa vyama vyote.
Ni wajibu wako kutoa maoni yako ya serikali tatu hata tano ukitaka, naheshimu sana mawazo yako. mimi maoni yangu ni serikali mbili tu, hakuna sababu ya kuwa na miserikali miiingi, huo ni uroho wa madaraka na ni mzigo kwa walipa kodi
 
Usitake kuharalisha hoja yako kwa kujinasibisha kama wewe ni mwanaCCM na unafanya kazi ofisi ndogo ya makao makuu ya CCM, Lumumba.

Kila mara unaleta uwongo na uzandiki hapa JF kutaka kuwaaminisha wanaJF.

Tunakufahamu vizuri sana ila sheria za JF hazituruhusu kuwambia wanaJF uhalisia wako.

Uwongo siyo nguzo imara na uwongo mara nyingi huwa ni siraha ya muda mfupi.

Endelea kuwadanganya wanaJF.

shikamoo MwanaDiwani
 
Last edited by a moderator:
Asante kwa taarifa mkuu , magamba yote yatapukutika hata kwa upepo , Poor Magamba !
 
Masalia jenga hoja, msimamo wenu ni serikali mbili, wakati umeshafika wa kuitambua Tanganyika yetu... tunaiona ile inakuja...
utakoma na ujinga wako. msimamo wenu ni serikali nyingi, sisi tunasiamamia kwenye serikali mbili. twendeni kwenye hoja.
 
huu uongo wala haukusaidii kitu zaidi ya kujifariji na bavicha wenzako.
 
i have dream that iko siku moja ambapo tutakuwa na Tanganyika yetu iliyopata uhuru 9/12/1961.Mungu bariki iwe hivyo.
nina ndoto kuwa kutakuwa na Muungano bora wa Tanzania ambao watu watakuwa na umoja na pili kutakuwa hakuna kero za muungano tena

oh lord help us to live to see
 
tunajua chadema wanataka serikali tatu ili moja iwe inatumikia wachaga tu hii nyingine ndiyo iwe ya wote hiki ni chama cha ajabu kabisa.
 
Back
Top Bottom