Elections 2010 CCM yaanza kuchota toka kwenye Ilani ya CHADEMA

Elections 2010 CCM yaanza kuchota toka kwenye Ilani ya CHADEMA

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Kwa watu ambao walimsikiliza Rais Kikwete jana huko Mwanza alianza kutoa ahadi ambazo haziko katika Ilani ya CCM bali ziko katika Ilani ya Chadema. Nimebahatika kupitia Ilani zote mbili nikiwa ni mdau maalum wa demokrasia. Kwa mujibu wa vyanzo vya kuaminika ni kuwa kwa kadiri Chadema wanaendelea kusua sua kutoa Ilani yao ambayo kama nilivyodokeza uko nyuma kuwa "inatisha" CCM toka J'pili wamekuwa wakiidadavua na kuanza kuingiza katika ahadi mbalimbali za Rais.

Ndani ya kampeni ya CCM ambapo mambo yale ambayo CCM hawakuyafikiria wanayarusha kwa kutumia hotuba za Rais ili Ilani ya Chadema itakapotoka (nadhani hadi J'mosi) CCM watadai kuwa mipango hiyo "ilikuwa tayari ndani ya ahadi zetu na Chadema ndio wameiiga)

Mbinu hii ambayo katika propaganda za siasa huitwa "political triangulation" imepangwa kutumiwa vizuri na CCM dhidi ya Chadema na hivyo kuneutralize mipango na kampeni ya Chadema.

Hata hivyo kucounter mipango hiyo ya CCM, Chadema nao wamefanyia marekebisho sehemu kidogo ya Ilani yao na hivyo kuikoleza munyu...


Tusubiri vitu... kabla hatujachelewa...
 
Nilijua mtaanza kunyoosheana vidole vya shutuma....siasa ni chaos tupu.
 
Mwanakijiji...
mimi CCM hata ukiwapa Ilani zooote za vyama kuanzia ile ya TLP,NCCR Mageuzi na hata ya CUF hawana cha kuuza, zaidi ya sura, wanchi[wanaccm] hawajadili tena JK anaongea nini, anaahidi nini , wala hawataki kujua ahadi zake....watu wanazungumzia uzuri wa mabango yake, wanazungumzia Tabasamu lake, watu wanazungumzia Bongo Flavor wanavyotumbiza mikutano yake.
JK, na CCM yake wamekiri wazi kuwa walishindwa kutimiza kile walichoahidi kwenye Ilani ya mwaka 2005, sasa wapenzi wake na mashabiki wao walipaswa kumuhoji Ilani ile ya 2005 itakamilika lini, shida hawana muda, hawana utashi wameridhika na kujadili upuuzi nilioonesha hapo juu.

CCM , wanatumia madhaifu ya watu wetu kujiuza, kwao sera sikitu na ndio maana 80% ya Ilani ya 2005 imewashinda kabisa.sasa hata wakidandia haya mazuri ya CHADEMA, kwakua wao hawawahitaji wale wanaohoji maswali ndo maaana wanawekeza kwenye Fulana, Kofia, kKagha, Pilau, kwa ajili ya wanachama wao.
 
tatizo ni kuwa hayo yaliyomo kwenye ilani ya Chadema CCM ikiyakumbatia tumekwisha!!!
 
tatizo ni kuwa hayo yaliyomo kwenye ilani ya Chadema CCM ikiyakumbatia tumekwisha!!!

nakuelewa sana, naelewa ilipo hofu yako na hofu ya wasomi wengine.
Nilikuwepo Mwanza wakati wakizindua kampeni zao, zaidi ya 89% ya wale waliowabeba na maroli na mabasi ya wadosi kutoka mawilayani ni kundi la waganga njaa, ni kundi ambalo kwa SERA, ELECTION MANIFESTO SI TIJA.
kwao wanahitaji mgombea ambae atawasaidia usafiri wakutoka vijijini kuja kutembea mjini, mtu ambae anawapa Fulana na Khanga, wanahitaji faraja japo za muda mfupi, hili kundi mwanakijiji limechoka , halijali utasema nini, kama huna bongoflava , hawaji.
CHADEMA, KUFIKIA jmosi SIKU YA UZINDUZI watakua hawajachelewa sana, by the way, hana ujasiri wakutekeleza yaliomengi ndani ya Ilani ile ya CHADEMA, inataka roho ngumu, atadodosa mepesi, yapo mambo mazito mle, kuyatekeleza atahitaji kutengana kina Rostam na mafisadi wa kariba hiyo.
otherwise naendelea kufikiri kwa mapana yake.
 
Mkuu MKJJ,

I think J1 si mbali sana. CCM hata uwape nini sasa hivi, hawana jipya.
 
Tatizo kubwa la ccm sii ilani na hutuba nzuri zilizonakshiwa kiuandishi bali utekelezaji. Wakumbuka jinsi walivyoidandia hoja ya chadema bungeni kuhusu ufisadi, lakini utekelezaji wake ndani ya ccm ukawa ni wakujilazimisha japo hawakupenda. Chedema ni chama makini na utekelezaji wa ilani yao ni makini Ref. Jimbo la Mbulu na Moshi mjini ndio utagundua kwamba chadema sii wazungumzaji zaidi ya utendaji.
 
Mwanakijiji,

Chadema watabadili ILANI yao ili kukoleza MUNYU siyo? Hahahaaaaa.. (munyu=chumvi).

Nimekupata Ng'wana mbati......... Ngoja tuvute pumzi kusubiri Jumamosi.

Fanyeni juu chini, hotuba nzima iwe kwenye YOUTUBE.

Ingelikuwa heri, watengeneze FILM moja ikionyesha Slaa akielezea ILANI ya uchaguzi na kuweka vielelezo vya picha na film kwa yale anayoyaelezea. Kwa mfano akisema MAFISADI, basi wanaweka picha zao. Akielezea migodi, wanaweka picha za walioathirika. Akielezea kuuza mbuga, anaweka picha za Wamasaai wa Loliondo etc etc.. Hizi zinaweza kuwa VSD ili iwe bei rahisi kucopy na watu waruhusiwe kuzicopy na kugawia wenzao.
 
Tatizo kubwa la ccm sii ilani na hutuba nzuri zilizonakshiwa kiuandishi bali utekelezaji. Wakumbuka jinsi walivyoidandia hoja ya chadema bungeni kuhusu ufisadi, lakini utekelezaji wake ndani ya ccm ukawa ni wakujilazimisha japo hawakupenda. Chedema ni chama makini na utekelezaji wa ilani yao ni makini Ref. Jimbo la Mbulu na Moshi mjini ndio utagundua kwamba chadema sii wazungumzaji zaidi ya utendaji.
Kiby
Ni Mbulu au Karatu?

Kama una maanisha Mbulu, nina imani mawaka huu CHADEMA itanyakua jimbo la Mbulu. Binafsi natarajia hivyo kwani mazingira ni mazuri kwa chadema kushinda kuliko CCM;

Ahsante kwa kutabiria CHADEMA kunyakua jimbo langu kutoa kwa mafisadi wa CCM;
 
nadhani J'mosi itakuwa ni siku ya kihistoria katika mahusiano kati ya watawala na watawaliwa, wapiga kura na wagombea, tulikotoka na tunakokwenda, tulichopewa na tunachotaka.
 
Mimi nadhani kuwa Ilani ni kitu ambacho hakina uzito sana ukilinganisha na ukweli kuwa CCM imeshindwa kuindeleza nchi na hivyo ni lazima miondolewe madarakani. Ni muhimu sana kwa CHADEMA kuwa makini na kuwaeleza wananchi kwa makini sana jinsi upungufu katika uongozi wa CCM ulivyosababaisha maisha ya wananchi yawe mabaya kuliko wanavyojielewa wenyewe. CHADEMA itumie mikakati mingine kama vile ya kusambaza video na kanda huko vijijini zenye kutoa mafunzo kuhusu ubovu wa maisha ya watanzania ukilinganisha na nchi nyingine zilizopata uhuru kipindi kama chetu na haziajawai kuwa na vita ye wenyewe kwa wenyewe ikiwa na raslimali nyingi kama zetu. Hata kama baadhi ya kanda na video hizo zitatatekwa na kuharibiwa CCM, wasichoke kusambaza nyingi kadri wawezavyo.


Wananchi wengi hata hawajui ni ilani ni nini kwa vile hawazisomi, na hata wakizisoma, imekuwa ni kawaida ya CCM kuwa baada ya uchaguzi ilani huishia jalalani, kwa hiyo hata CHADEMA wakija na ilani nzuri, wananchi wengi watakuwa wanelewa kuwa hiyo ni lugha ya kuombea kura tu.
 
tatizo ni kuwa hayo yaliyomo kwenye ilani ya Chadema CCM ikiyakumbatia tumekwisha!!!

CCM wameshasema USHINDI ni LAZIMA. Kwa hiyo, hakuna tena cha sera bali kushinda kama walivyozoea na kwa mbinu wanazozijua wao wenyewe.
 
CCM hata uwape ilani za dunia nzima hawawezi kutekeleza maana wanachoongea na kutenda ni tofauti...Hivi huyu JK yuko timamu kweli anatuambia mambo ya kununua mastering studio ya 50m na kuwalipia wasanii 7m pango la nyumba ...jamani hivi haya ndo mambo yaliyoko kwenye ilani yao!!!!!mi natamani kuzimia nikisikia watu wanapiga vigelegele kwa kushangilia mautumbo ya dizaini hii
 
nadhani J'mosi itakuwa ni siku ya kihistoria katika mahusiano kati ya watawala na watawaliwa, wapiga kura na wagombea, tulikotoka na tunakokwenda, tulichopewa na tunachotaka.

Ebana eeh wewe ni mmoja wa watunzi wa hiyo ilani nini? Knowing you....
 
Mimi nadhani kuwa Ilani ni kitu ambacho hakina uzito sana ukilinganisha na ukweli kuwa CCM imeshindwa kuindeleza nchi na hivyo ni lazima miondolewe madarakani. Ni muhimu sana kwa CHADEMA kuwa makini na kuwaeleza wananchi kwa makini sana jinsi upungufu katika uongozi wa CCM ulivyosababaisha maisha ya wananchi yawe mabaya kuliko wanavyojielewa wenyewe. CHADEMA itumie mikakati mingine kama vile ya kusambaza video na kanda huko vijijini zenye kutoa mafunzo kuhusu ubovu wa maisha ya watanzania ukilinganisha na nchi nyingine zilizopata uhuru kipindi kama chetu na haziajawai kuwa na vita ye wenyewe kwa wenyewe ikiwa na raslimali nyingi kama zetu. Hata kama baadhi ya kanda na video hizo zitatatekwa na kuharibiwa CCM, wasichoke kusambaza nyingi kadri wawezavyo.


Wananchi wengi hata hawajui ni ilani ni nini kwa vile hawazisomi, na hata wakizisoma, imekuwa ni kawaida ya CCM kuwa baada ya uchaguzi ilani huishia jalalani, kwa hiyo hata CHADEMA wakija na ilani nzuri, wananchi wengi watakuwa wanelewa kuwa hiyo ni lugha ya kuombea kura tu.

mzee kinyume na watu wanavyofikiria CCM inauza Ilani yake haiuzi maneno tu.. na msifikirie kuwa wananchi hawasomi au kufuatilia Ilani; watu wanasoma, wanazielewa na kuzikubali. CCM wanajua propaganda ya Ilani vizuri zaidi kuliko wapinzani. Labda kama mmesahau jinsi gani vitabu vya Ilani vilivyokuwa vinasambazwa kwenye maofisi ya CCM na vijijini miaka nenda rudi.
 
Mimi nadhani kuwa Ilani ni kitu ambacho hakina uzito sana ukilinganisha na ukweli kuwa CCM imeshindwa kuindeleza nchi na hivyo ni lazima miondolewe madarakani. Ni muhimu sana kwa CHADEMA kuwa makini na kuwaeleza wananchi kwa makini sana jinsi upungufu katika uongozi wa CCM ulivyosababaisha maisha ya wananchi yawe mabaya kuliko wanavyojielewa wenyewe. CHADEMA itumie mikakati mingine kama vile ya kusambaza video na kanda huko vijijini zenye kutoa mafunzo kuhusu ubovu wa maisha ya watanzania ukilinganisha na nchi nyingine zilizopata uhuru kipindi kama chetu na haziajawai kuwa na vita ye wenyewe kwa wenyewe ikiwa na raslimali nyingi kama zetu. Hata kama baadhi ya kanda na video hizo zitatatekwa na kuharibiwa CCM, wasichoke kusambaza nyingi kadri wawezavyo.


Wananchi wengi hata hawajui ni ilani ni nini kwa vile hawazisomi, na hata wakizisoma, imekuwa ni kawaida ya CCM kuwa baada ya uchaguzi ilani huishia jalalani, kwa hiyo hata CHADEMA wakija na ilani nzuri, wananchi wengi watakuwa wanelewa kuwa hiyo ni lugha ya kuombea kura tu.

hilo la kusambaza video na mikanda kwa sasa lina ugumu kwani ni vijiji vingapi vina umeme? si wanasema ni asilimia ndogo sana wanatumia umeme hapa TZ? ni swala ni nzuri sana ila lingeanza toka siku nyingi lingeeleweka kuliko sasa ukiangalia na muda uliobaki. labda lifanywe siku zijazo iwepo kampeni kubwa kuwaeleza wananchi namna mali zinavyoibwa nk
 
Hawa hawana lolote jipya. Unakumbuka hata zile ahadi za kupitia upya mikataba ya madini? Hivi ni nani aliyezurura dunia nzima kuwatafuta wawekezaji kwenye madini na kusaini mikataba hiyo? Leo mtu huyo huyo aje hapa adudanganye eti atapitia upya mikataba tuwe na win-win solution? Yalikuwa ni madai ya CHADEMA na CCM kujaribu kuzima moto wakaikwapua kama sera yao. Lakini sote tunajua kilichofanyika katika mikataba ya madini. Hawana jipya!
 
yani ccm wameanza ku-copy n paste ilani ya chadema? ngoma yao ngumu sana na huu ni mwanzo tu .
 
Back
Top Bottom