Elections 2010 CCM yaanza kuchota toka kwenye Ilani ya CHADEMA

Elections 2010 CCM yaanza kuchota toka kwenye Ilani ya CHADEMA

Mwanakijiji,

Chadema watabadili ILANI yao ili kukoleza MUNYU siyo? Hahahaaaaa.. (munyu=chumvi).

Nimekupata Ng'wana mbati......... Ngoja tuvute pumzi kusubiri Jumamosi.

Fanyeni juu chini, hotuba nzima iwe kwenye YOUTUBE.

Ingelikuwa heri, watengeneze FILM moja ikionyesha Slaa akielezea ILANI ya uchaguzi na kuweka vielelezo vya picha na film kwa yale anayoyaelezea. Kwa mfano akisema MAFISADI, basi wanaweka picha zao. Akielezea migodi, wanaweka picha za walioathirika. Akielezea kuuza mbuga, anaweka picha za Wamasaai wa Loliondo etc etc.. Hizi zinaweza kuwa VSD ili iwe bei rahisi kucopy na watu waruhusiwe kuzicopy na kugawia wenzao.


Yeah, CHADEMA inatakiwa waje na kampeni zenye ubunifu wa hali ya juu, ambazo sisiem hawawezi iga kabisa, wazo lako ni zuri na inawezekana kabisa kuweka Screen kubwa na kuelezea mikakati mbali mbali huku wakionyesha picha.

Kwa mfano, atakapo fafanua orodha ya mafisadi papa na nyangumi picha inakuwa Displayed .... kwa mfano kwenye tovuti ya chadema Mafisadi 11 wametajwa na picha zao zimeambatanishwa, http://www.chadema.or.tz/tamko/tamko.php?id=16&pg=110
 
Kiby
Ni Mbulu au Karatu?

Kama una maanisha Mbulu, nina imani mawaka huu CHADEMA itanyakua jimbo la Mbulu. Binafsi natarajia hivyo kwani mazingira ni mazuri kwa chadema kushinda kuliko CCM;

Ahsante kwa kutabiria CHADEMA kunyakua jimbo langu kutoa kwa mafisadi wa CCM;

.
Nilikua namaanisha Karatu mkuu. Na kama mbulu kuna dalili za kunyakuliwa na chadema basi hizi ni habari njema pia masikioni mwa wapenda maendeleo.
 
Mwanakijiji...
mimi CCM hata ukiwapa Ilani zooote za vyama kuanzia ile ya TLP,NCCR Mageuzi na hata ya CUF hawana cha kuuza, zaidi ya sura, wanchi[wanaccm] hawajadili tena JK anaongea nini, anaahidi nini , wala hawataki kujua ahadi zake....watu wanazungumzia uzuri wa mabango yake, wanazungumzia Tabasamu lake, watu wanazungumzia Bongo Flavor wanavyotumbiza mikutano yake.
JK, na CCM yake wamekiri wazi kuwa walishindwa kutimiza kile walichoahidi kwenye Ilani ya mwaka 2005, sasa wapenzi wake na mashabiki wao walipaswa kumuhoji Ilani ile ya 2005 itakamilika lini, shida hawana muda, hawana utashi wameridhika na kujadili upuuzi nilioonesha hapo juu.

CCM , wanatumia madhaifu ya watu wetu kujiuza, kwao sera sikitu na ndio maana 80% ya Ilani ya 2005 imewashinda kabisa.sasa hata wakidandia haya mazuri ya CHADEMA, kwakua wao hawawahitaji wale wanaohoji maswali ndo maaana wanawekeza kwenye Fulana, Kofia, kKagha, Pilau, kwa ajili ya wanachama wao.
Ni kweli, ilani zilizoandikwa vizuri bila watendaji wazuri hazitusaidii sana. Sema tu kunakuwa na advanatage kubwa kwa chama chenye ilani nzuri na pia kinaonekana kuwa na mgombea bora/swaaafi!
 
CCM hata uwape ilani ya namna gani haitatekelezeka!

...na hili alishawahi kulisemea Mkapa miaka kadhaa hapo nyuma.
JK kaahidi watu wa kanda ya Ziwa meli kubwa zaidi ya ile iliyozama ya MV Bukoba, kabla hajaondoka madarakani.
 
Back
Top Bottom