benzemah
JF-Expert Member
- Nov 19, 2014
- 1,533
- 3,187
Chama cha Mapinduzi (CCM) kimesema hakitarudi nyuma kuhusu uwekezaji katika bandari kwa sababu uwekezai huo uko kwenye ilani ya chama hicho ya mwaka 2020-2025.
Katibu Mkuu wa chama hicho, Daniel Chongolo alibainisha hayo jana kwenye ziara yake ya kutoa elimu kwa wananchi kahusu uwekezaji katika Bandari ya Da es Salaam kati ya Tanzania na kampuni ya DP World kutoka Dubai jini Arusha jana.
Chongolo alisema kwa kuwa jambo la uwekezaji limepotoshwa kwa kiasi kikubwa hivyo ni bora wao kama chama chenye dhamana ya kuwaletea wananchi maendeleo kujitokeza na kuweka sawa suala hilo na kamwe CM haiko tayari kurudi nyuma kwenye suala hilo.
"CCM tuna dhamana kubwa ya kuhakikisha tunatatua changamoto za Watanzania na suala la bandari ni uwekezaji ambao umo kwenye ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025,"alisema.
Alisema suala la kuwaletea wananchi maendeleo linahitaji uthubu-tuna kutokubali kuyumbishwa na kama serikali haina vyanzo vizuri vya kukusanya mapato wananchi hawawezi kupata maendeleo.
"Rais wetu amekuwa na uthubutu kwa kufanya mambo makubwa likiwemo kuleta wawekezaji nchini na ili kutatua changamoto za watu lazima tuwe nafungu la kutosha," alisema.
Aliongeza kusema kwamba sasa hivi duniani kuna vita ya kiuchumi ambayo huwezi kuiona kwa macho akisema inaingia kwenye akili na mtu asipokuwa makini atakwama.
"Nchi yetu iko kwenye fursa ny-ingi, tusipofanya maamuzi magumu tutakwama, hii ni vita ya kiuchumi," alisema.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Kitila Mkumbo alisema serikali imefungua milango ya wawekezaji kwa ajili ya mapinduzi ya kiuchumi chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Kitila aliligusia suala la uwekezail katika Bandari ya Dares Salaam akisema kwamba mambo mengi
yamepotoshwa.
Alisema bandari nzima ya Dar es Salaam pamoja na bandari zake kavu ina hekta 667 wakati DP World wamepewa eneo lenye hekta 7.5 ambayo ni karibu asilimia nane ya eneo lote la bandari.
"Kwenye mkataba uliopo DP World watapewa kwa kukodishwa kwenye eneo dogo la asilimia nane tu," alisema.
Alisema uwekezaii wa kutumia mwekezaji kama DP World serikali kwa kutumia mapato yatokanayo na bandari pekee itakusanya kiasi cha Sh trilioni 26 kutoka Sh trilioni saba zinazokusanywa na
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Akimzungumzia mwekezaji DP World, Kitilya alisema serikali iko makini katika suala la uwekezaji na ilishawahi kuwashughulikia baadhi ya wawekezaji ambao wamevurunda nchini na kuwa hata
DP World wataondolewa kama 'watachemka'.
"Nasema hata hao DP World tutawaondoa mchana kweupe kama makampuni mengine ambayo tumewahi kufanya hivyo kama watashindwa," alisema.
Katibu Mkuu wa chama hicho, Daniel Chongolo alibainisha hayo jana kwenye ziara yake ya kutoa elimu kwa wananchi kahusu uwekezaji katika Bandari ya Da es Salaam kati ya Tanzania na kampuni ya DP World kutoka Dubai jini Arusha jana.
Chongolo alisema kwa kuwa jambo la uwekezaji limepotoshwa kwa kiasi kikubwa hivyo ni bora wao kama chama chenye dhamana ya kuwaletea wananchi maendeleo kujitokeza na kuweka sawa suala hilo na kamwe CM haiko tayari kurudi nyuma kwenye suala hilo.
"CCM tuna dhamana kubwa ya kuhakikisha tunatatua changamoto za Watanzania na suala la bandari ni uwekezaji ambao umo kwenye ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025,"alisema.
Alisema suala la kuwaletea wananchi maendeleo linahitaji uthubu-tuna kutokubali kuyumbishwa na kama serikali haina vyanzo vizuri vya kukusanya mapato wananchi hawawezi kupata maendeleo.
"Rais wetu amekuwa na uthubutu kwa kufanya mambo makubwa likiwemo kuleta wawekezaji nchini na ili kutatua changamoto za watu lazima tuwe nafungu la kutosha," alisema.
Aliongeza kusema kwamba sasa hivi duniani kuna vita ya kiuchumi ambayo huwezi kuiona kwa macho akisema inaingia kwenye akili na mtu asipokuwa makini atakwama.
"Nchi yetu iko kwenye fursa ny-ingi, tusipofanya maamuzi magumu tutakwama, hii ni vita ya kiuchumi," alisema.
Naye Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Mipango na Uwekezaji, Kitila Mkumbo alisema serikali imefungua milango ya wawekezaji kwa ajili ya mapinduzi ya kiuchumi chini ya Rais Samia Suluhu Hassan.
Kitila aliligusia suala la uwekezail katika Bandari ya Dares Salaam akisema kwamba mambo mengi
yamepotoshwa.
Alisema bandari nzima ya Dar es Salaam pamoja na bandari zake kavu ina hekta 667 wakati DP World wamepewa eneo lenye hekta 7.5 ambayo ni karibu asilimia nane ya eneo lote la bandari.
"Kwenye mkataba uliopo DP World watapewa kwa kukodishwa kwenye eneo dogo la asilimia nane tu," alisema.
Alisema uwekezaii wa kutumia mwekezaji kama DP World serikali kwa kutumia mapato yatokanayo na bandari pekee itakusanya kiasi cha Sh trilioni 26 kutoka Sh trilioni saba zinazokusanywa na
Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).
Akimzungumzia mwekezaji DP World, Kitilya alisema serikali iko makini katika suala la uwekezaji na ilishawahi kuwashughulikia baadhi ya wawekezaji ambao wamevurunda nchini na kuwa hata
DP World wataondolewa kama 'watachemka'.
"Nasema hata hao DP World tutawaondoa mchana kweupe kama makampuni mengine ambayo tumewahi kufanya hivyo kama watashindwa," alisema.