SI KWELI CCM yatoa barua inayohusu kuhujumiwa na Watendaji Serikali za Mitaa

SI KWELI CCM yatoa barua inayohusu kuhujumiwa na Watendaji Serikali za Mitaa

Baada ya kuitathmini taarifa hii, tumebaini kuwa si ya kweli.
Source #1
View Source #1
Source #2
View Source #2
Baada ya mipango yao ya kuandikisha watoto kufeli leo Chama cha Mapinduzi kimesema kinahujumiwa na viongozi na mawakala wao na watendaji wa serikali za mitaa.

1000163332.jpg

 
Tunachokijua
Chama Cha Mapinduzi (CCM) ni chama tawala ambacho kilianza rasmi Februari 5, 1977 kutokana na kuunganishwa vyama vya Tanganyika African National Union (TANU) kilichokuwa chama tawala Tanzania Bara, kikiongozwa na Rais wa Kwanza wa Tanzania, Mwalimu Julius Kambarage Nyerere na Chama cha Afro-Shirazi Party (ASP) kilichokuwa chama tawala Zanzibar kikiongozwa na Rais wa kwanza wa Zanzibar Sheikh Amaan Abeid Karume.

Kuelekea uchaguzi wa serikaliza mitaa utakaofanyika mwezi Novemba 2024, CCM ni moja kati ya vyama vingi ambavyo vitashiriki uchaguzi huo huku kadri siku zinapokwenda kumekuwepo na taarifa nyingi zinazohusiana na uchaguzi huo ambapo pamoja na uwepo wa taarifa za kweli lakini kuwekuwepo na taarifa nyingi zisizo za kweli na zenye lengo la kupotosha.

Kumekuwepo na barua ambayo imekuwa ikisambaa mtandaoni na kudaiwa kuwa imetolewa na Chama Cha Mapinduzi (CCM), barua ambayo inahusishwa na harakati za kuelekea uchaguzi wa serikali za mitaa.

Uhalisia wa barua kutolewa na CCM upoje?
Ufuatiliaji uliofanywa na JamiiCheck umebaini kuwa barua hiyo si ya kweli na haijatolewa na Chama Cha Mapinduzi CCM kwani haijachapishwa katika kurasa rasmi za mitandao ya kijamii ya CCM.

Aidha JamiiCheck imebaini mapungufu kadhaa yanayodhihirisha kuwa barua hiyo barua hiyo haijatolewa na CCM, Moja ya mapungufu hayo ni kutofautiana kwa mwandiko (fonts) ambapo barua hiyo imeandikwa kwa mwandiko tofauti na ule ambao umekuwa ukitumiwa na CCM katika barua zake rasmi.

Aidha kupitia kurasa wake wa mtandao wa X CCM imeikanusha barua hiyo na kwamba si ya kweli na kuutaka umma kuipuuza barua hiyo.

1729251359550-jpeg.3128677

Barua hiyo imehifadhiwa hapa na hapa.
wakuu salaam, bila shaka ni wazima wa afya.
Katika pitapita zangu huko mtandaoni Nimekutana na barua hii inayodaiwa kutolewa na CCM, hii uhalisia wake ni upi wakuu?
Screenshot 2024-10-18 142230.png
 
Baada ya mipango yao ya kuandikisha watoto kufeli leo Chama cha Mapinduzi kimesema kinahujumiwa na viongozi na mawakala wao na watendaji wa serikali za mitaa.
Upinzani tumieni hii kufungua kesi
Wekeni zuio mahakamani

mnaishia kulalamika wamewasaidia sana fanyeni kweli.

Kule kujiandikisha ki digital kulikuwa na faida kweli? Kwa nini kuandikishana kwenye daftari
Sensa ina faida gani?

Uchaguzi usimame tuanze upya.
 
simba odds 3
YYanga2.57
sijiuko
 
Nazurula zurula huku na kule, naona ona sehemu chache watu wamevaa kijani...ndo hizo sehemu watu wanajiandikisha?

Kijijini hapa, tunachangishana ili tuchonge barabara, hatuna maji salama, ni visima vya jamaa wanaojiweza, zile mvua zilikata daraja, tuanzunguka km14 zaidi ili kufika sehemu ile ile.
- Wakasema mkandarasi atakuwa field early August, vijana wameamua kuchonga njia kutupunguzia kero ya km 14 zaidi.

Panya road walitutiririsha, wananchi tunaambiwa tujilinde, tulipie sungusungu au tujiunge polisi jamii.

Tuna migogoro ya ardhi kuanzia vijijjni huku, hakuna anayeweza kumaliza hiyo shida.

Watoto wanakaa chini shuleni, wao mtu mmoja anatembelea gari ya milioni 600 kwenda kazini umbali wa km 6 toka kwake.

MNATAKA KUCHAGUA NINI SASA? KWAAJILI YA NINI? ILI WAFANYE NINI?
 
Back
Top Bottom