Kama ni hivyo basi yeyote anafaa kuwa kiongozi maana si mipango ya serikali ipo.Wanataka kusema maendeleo yanaletwa na mtu, na sio mipango sahihi ya serekali?
Hiyo ni kwa Tanzania tu? Ni ajabu imani zengine hizi.Kwa mbali naliona JENEZA la MWINYI 😹
Apumzike pema peponi 😹
Naunga mkono hoja.
Wajumbe wa Sekretarieti ya Kamati Maalum ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Zanzibar wamepitisha pendekezo la kuishauri Kamati Maalumu kuridhia kuongeza muda wa Rais wa Zanzibar, Dk Hussein Mwinyi kuongoza nchi katika muhula wake wa kwanza kwa kipindi cha miaka saba badala ya mitano.
Hayo yamesemwa na Naibu Katibu Mkuu wa CCM Zanzibar, Dk Mohamed Said Dimwa
wakati akifunga mkutano wa Baraza Kuu la Umoja wa Vijana (UVCCM) Wilaya Dimami kichama Zanzibar uliofanyika Ofisi za Wilaya hiyo Kiembesamaki.
Dk Dimwa amesema uamuzi wa kumuongezea muda wa kuongoza Dk Mwinyi unatokana na kuridhishwa na kasi yake ya kiutendaji katika kutekeleza Ilani ya CCM ya mwaka 2020-2025 kwa zaidi ya asilimia 100 ndani ya kipindi miaka mitatu na miezi kadhaa tangu aingie madarakani.
Katika maelezo yake, Dk Dimwa amesema CCM Zanzibar imeona Serikali kuingia katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2025 ni hasara na matumizi mabaya ya fedha za walipa kodi kwa kuwa ni wananchi wanahitaji maendeleo endelevu, hivyo Rais Mwinyi anafaa kuongezewa muda ili Zanzibar iwe nchi ya visiwa iliyoendelea kiuchumi katika ukanda wa Afrika mashariki.
"Wajumbe wa sektetarieti tumejadili na kutathimini kwa kina juu ya utendaji wa Rais Mwinyi, tukajiridhisha hakuna mbadala wake na anastahiki aongoze nchi kwa kipindi cha miaka saba ili apate muda mzuri wa kufanya Mapinduzi ya kimaendeleo katika nyanja za kiuchumi na kijamii,” amesema Dk Dimwa.
Kitendo Cha kupendekeza kihivyo tu! WAMEVUNJA KATIBA!Wajumbe wa Sekretarieti ya kamati maalum ya chama cha Mapinduzi Zanzibar wamependekeza kuongezeka Kwa kipindi cha utawala kwa Kwa Rais Hussein Mwinyi kutoka miaka mitano mpaka saba.
Je Kuna ubaya au inafaa?
Ewe mjenga nchi tiririsha maoni yako
let them freaking try it !Tujiandae na huku!! Janja janja imeanza
chuki dhidi ya MAGU,katibu kasema ameridhishwa na utendaji wa Mwinyi we unaleta hasira za vyeti feki hapa,mpango wenyewe hauendi kokote labda kama Mwinyi ndo anausimamia.Huu ulikuwa ni mpango wa dhalimu magu kabla Mungu hajaingilia kati, lakini mbegu matamanio yake imebaki hivyo inafanyiwa kazi.
Acha kupanick dogo.Wewe Mpuuzi tu Magu anaingiaje hapo? Pambana na Samia wako mpuuzi wewe!
Ndio inavyopaswa kuwa, labda useme kuna elimu inayosomewa ili kuwa rais.Kama ni hivyo basi yeyote anafaa kuwa kiongozi maana si mipango ya serikali ipo.
Jiwe angekuwepo angeendelea kutawala milele alishaanza harakati za kubadilisha katiba hata wabunge wa upinzani alikuwa hataki kabisa.Hii nchi ilikuwa inaelekea kuwa ya kifalme wakati ule,ule mshale tukaukwepa now umerudi kwa namna nyingine!Ngoja afariki kwanza ndio watakoma na kimbelembele chao hawajajifunza kwa marehemu jiwe na wapambe wao.
Kwanza nyie vichwa flat screen rais wenu anateuliwa dodoma kaeni kimya na flatscreen head zenu