Pre GE2025 CCM Zanzibar wapendekeza Rais Mwinyi atawale kwa miaka 7, wasema kufanya uchaguzi 2025 ni hasara na matumizi mabaya ya fedha za umma

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Heshimuni katiba jmn waafrika sisi bora tungeendelea kutawaliwa na wazungu huenda tungekuwa mbali mno!Afrika hatuna akili ya kujiongoza zaidi ya kutanguliza matumbo mbele.Huyo Mzanzibar akipewa miaka miwili itamsaidia nini kama kwenye mitano ameshindwa.Sultani go bhna utaanza kuchosha watu muda si mrefu
 
Balaa kwa nchi yetu! Sasa kilichobaki, "if you can't fight them, join them, " But kill them slowly from inside"!
TZ imekuwa shamba LA chama tawala,ukitaka Mambo yako yaende, ama Uwe mfanyabiashara, usidungamane na upande, au, chukua kadi ya CCM, piga pesa
 
Kama wameridhishwa na utendaji wake wamchague tena mwakani lakini siyo kubadili kipindi kimoja kuwa miaka saba. Wacha wamchurie shauri yao,CCM wana upuuzi mwingi sana
Hutaki chura apige miaka 7❓
 
Hata huku tunaomba iwe hivyo,sio mitano tena kwa mama bali ni mikumi kabisa,nitapeleka hoja hii bungeni ijadiliwe kwa kina.

Mikumi tena kwa mama samia
 
Ndio inavyopaswa kuwa, labda useme kuna elimu inayosomewa ili kuwa rais.
Nachojua mimi hata ikiwepo mifumo ila bado kutakuwa na athari katika masuala ya uongozi wa nchi kutokana na aina ya rais aliyepo madarakani. Sasa hauwezi kusema yeyote tu anaweza kuwa rais.
 
Nachojua mimi hata ikiwepo mifumo ila bado kutakuwa na athari katika masuala ya uongozi wa nchi kutokana na aina ya rais aliyepo madarakani. Sasa hauwezi kusema yeyote tu anaweza kuwa rais.
Nasema yoyote anaweza, kwa maana hakuna mtu amezaliwa special wa kazi ya urais. Mifumo itamshepu atakayepata nafasi hiyo ili atakeleze majukumu yake kwa usahihi.
 
Nasema yoyote anaweza, kwa maana hakuna mtu amezaliwa special wa kazi ya urais. Mifumo itamshepu atakayepata nafasi hiyo ili atakeleze majukumu yake kwa usahihi.
Mifumo haimgeuzi mtu kuwa robot, ndio maana nasema pamoja na mifumo ila bado athari ya uongozi kutokana na aina ya rais aliyekuwepo madarakani lazima iwepo. Huko kwa wenzetu wana mifumo ila bado wakiona kiongozi wao anafanya wasiyotaka wanampiga chini na kuweka mwengine.
 
Sijawahi kuamini wazenji wana akili, unaswali sala tano mji mkongwe na kuchapa bakora makobe halafu mtu huyo huyo unaenda hoteli ya kitalii pwani mchangani kuwakaangia watalii wazungu nguruwe na kuserve whisky! huu ni ushahidi tosha.

Miaka mitano inatosha na kama Rais akitoboa uchaguzi anapewa mitano mingine na kutoka kumuachia mwingine ambae anaweza kuwa bora zaidi. Je rais alietoka angekaa madarakani miaka 7 times 2 = 14 huyu aliepo angepataje nafasi?

Katika miaka kumi ya urais huwa kuna makundi ya watu huwa yamebanwa kiuchumi , Rais akitoka akaja mwingine inakuwa zamu yao kula keki. Yaani huyu aliesema Rais aongezewe muda hataki uhondo, halua na tende viishe upande wake na wengine wapate kula!!

Kuruhusu jambo hilo ni mwanzo wa kuvuruga katiba na kitakachotokea ni fujo na vurugu maana sasa itakuwa kila Rais mzenji wa bara au visiwani anajiamulia atawale kama Mugabe hadi afie madarakani!!
 
Ndio maana nasema mifumo ndio inaamua kiongozi aweje, na akishindwa kwenda na mifumo anapigwa chini.
 
Naunga mkono uamuzi huo.Mwinyi yuko vizuri sana
 
Rais Hussein Mwinyi ni kijana anayeheshimika sana kwa utendaji na hata kwa maadili tena ni kwa watanzania wote kwa asilimia kubwa.Sidhani kama ataendekeza upuuzi na ujinga huu wa chawa wa CCM wa kuvunja katiba.Kwa maadili yake mema,AWAKEMEE HARAKA.Na Mwinyi asije akadhani wanampenda kwani zinaonekana ni mbinu za kumuangusha.Wajinga hawa wanajua hili litaleta tafrani na kumfanya adharaulike kupitia migongo yao.Sio watu hao Rais Mwinnyi.Wanavaa kijani tu lakini ni sawa sawa na wachawi tu.
 
Ndio maana nasema mifumo ndio inaamua kiongozi aweje, na akishindwa kwenda na mifumo anapigwa chini.
Kwahiyo tuseme uongozi wa Obama ulikuwa sawa tu na Trump naye Trump uongozi wake ulikuwa sawa tu na Biden?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…