Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Civilians will never understand why and how military think about their lives.
Maswala yaulinzi magumu rudia tenaSamahani Mkuu....nimetafuta point kwenye hoja yako ila nimeambulia patupu!
Hii ndio point.. kuna watu wanalipwa mamilioni sababu ya haya mambo.. sisi tule maisha tu na tutimize majukumu yetuVitu vingine hata visikuumize kichwa mzee, kula maisha.
mwisho kabisa ya makala yake kuna point labda kama hujssomaSamahani Mkuu....nimetafuta point kwenye hoja yako ila nimeambulia patupu!
kichwa chako ni MB moja lazima haiwezi kukopi msg hii
Nimeelewa point yako unayotaka kusema lakini nadhani umeshindwa pia kuelewa tofauti ya security na secrecy. Hata kwenye computer unaambia kutumia password imara kama security, at the same time unaambiwa kuwa usimwambie mtu mweingine kuhusu password yakpo; hapo kuna security na secrecy. Secuirty ni ulinzi dhidi ya adversaries, halafu secrecy ni kuwanyima adversaries information za ndani zinazokuhusu.Salam wana JF.
Leo ningependa tujadili lawama anazopewa CDF General Mabeyo baada ya kuonekana kama ameleeza mengi yaliyo paswa kuwa siri kuhusu ujenzi wa Makao Makuu Ya Jeshi la Wnanchi (JWTZ) kule Dodoma.
Katika kutoa maelezo yake ilionekana kama amefichua sehemu za kimkakati ambazo zitakuwa na vifaa nyeti vya kiulinzi na usalama ndani ya kambi na kuzunguka eneo husika kwenye landmarks tofauti kama milima n.k.
Katika hali ya kuonekana Mheshimiwa Raisi kujaribu kufuta makosa hayo aliongea maneno flani ambayo ni kama alijaribu kuficha au kupoza maelekezo ya kina ya CDF kuhusu hivyo vitu nyeti.
Kuna msemo wa kiingereza wa wamarekani unasema "Loose lips sink ships" ambao ndio unaweza kuwa msingi wa woga au tahadhari ya wanaomlaumu CDF.
Lakini inasemekana msemo huu uliwekwa makusudi wakati wa vita kuu ya pili ya dunia huko Marekani kwa lengo la kuwapa tahadhari waeneza taarifa au tetesi kama habari za uongo au za kweli bila tahadhari, kwani zinaweza kuondoa au kushusha hari(molari) au kusababisha taharuki miongoni mwa askari wao wapambanaji.
Mimi najaribu kumtetea CDF kama ambavyo wapo wengi walio tangulia kumtetea, kwamba ulimwengu wa sasa unao tawaliwa kila kitu na teknolojia tena ya tehama basi ni ngumu sana kuficha ramani, vifaa na miundombinu mingine ya kiulinzi ili kujiweka ktk hali ya usalama.
Watu wa Usalama katika Tehama (Cyber Security) wana msemo unaotumika mara nyingi ktk mijadala ya usalama nao ni Obscurity through Security is discouraged.
Wanasema Usalama wa kitu sio kuficha kiko wapi bali kuweka vitu madhubuti vya kuzuwia watu wasifanikiwe kuvishambulia na kuvishinda. Kwa kuweka wazi vifaa vyako vya ulinzi unakuwa makini kutumia mbinu nzuri kujilinda au kuvilinda vifaa husika.
Mfano wake ni kama vile kila mtu anajua kwenye ATM mashine kuna fedha lakini ulinzi uliowekwa kuzuwia usifanikiwe kuchua pesa ndio bora zaidi.
Mfano wa ulinzi ni kama vile Safe la kuhifadhia pesa la ATM lipo ndani ya strong room, huku milango ya strong room ikiwa imara na kuwekwa kufuli(lock) lenye combination ngumu kuitengua, au kuvunja.
Huko nje ya strong room kuna askari imara wanalinda na silaha za moto.
Kama usalama wa fedha za kwenye ATM ungetegemea kuficha mahali ilipo hiyo pesa kwa maana ya chumba gani hata zikiwa zimehifahiwa ktk chombo dhaifu basi ATM zingekuwa zinaibiwa sana pesa, maana watu wangepeleleza pesa inafichwa wapi.
Kuficha mitambo au vyumba maalum ni kama kuchimbia kiroba cha pesa chini ya mti ukitegemea wezi hawajui umeficha wapi, ikitokea mtu akajua basi hakuna kitu cha kumzuwia asiibe, lakini ukihifadhi pesa kwa njia imara kama vile wanavyofanya kwenye ATM au Bank Strong rooms sio rahisi kuibiwa ingawa kila mtu anajua pesa zipo wapi au chumba gani.
Ukiweka mitambo yoyote yenye chuma, au ya kielektroniki ni rahisi sana mtu kutumia vifaa vya kisasa vya kielektroniki na vya mionzi kujua kuna kitu kimefichwa mahala hapo.
Na ndio maana mifumo ya kuzuwia ndege isitunguliwe haijajikita kuzuwia isionekane kwa macho bali imejikita ktk kuficha heat signature (hii ni mionzi) kuzuwia eaves dropping (mivujo ya signal za kielekroniki) ya mawasialiano ya kwenye ndege, na mwendokasi wa vifaa.
Kwa mfano huwezi kuficha kituo kikubwa cha rada au yalipo makombora au vifaru bali unaweza kuweka vifaa vya kuilinda rada isishambuliwe na makombora au na watu kwa kuweka mitambo ya ulinzi kama ya kutungulia makombora au ndege na kuweka watu wenye silaha pale kwenye rada au mizinga.
Kwa kutumia vipima mwimbi ya sauti za binadamu, satellite heat map, pamoja na seismic measuring instruments (A seismograph, or seismometer ), x-ray na laser beam unaweza kujua vyumba vilivyopo kwenye kambi husika, na ndani kuna vifaa gani na idadi gani ya binadamu na wana silaha gani na wamesima au wanatembea.
Mnakumbuka Operation Geronimo jinsi US Seals walivyojua chumba alichokuwa anaishi Osama? Walijua idadi ya watu waliopo ndani ya nyumba yake, jinsia zao, umri na kukisia urefu wake(Osama) kwanza kupitia teknolojia nilizo sema hapo juu, kisha ndio wakatuma mpelelezi wao yule daktari kuchukua DNA sample kwa uthibitisho zaidi.
Tena hapo Osama alijitahidi kukwepa vifaa vya teknolojia ya mawasiliano kukwepa hiyo Eaves-Dropping.
Inavyo onekana Osama alijiamini sana kuishi makazi ya watu akiwa na ulinzi mdogo akidhania usiri wa kujulikana alipo utamsaidia. Siku siri ilipovuja kwa adui wake yakamkuta yale yaliyo tokea. Angetegemea ulinzi mkubwa basi kazi ya kumuungamiza isingekuwa rahisi kwa kikosi cha Seal toka marekani.
Kitu kingine ambacho kipo wazi kabisa ramani zote za kambi za kijeshi na mpangilio wa vitu unajulikana duniani kote, na unafanana kwa kiasi kikubwa hasa kama sisi nchi masikini tunaopenda kutumia mbinu tulizosoma kwa wenzetu au vile tunavyo penda kutumia misaada na teknolojia toka kwa rafiki zetu wachina au nchi zingine.
Si tuna waona wachina pale kambi flani karibu wanaporusha mwewe wetu wa kazi za ulinzi?
Si tunajua wanakuja kufanya ukarabati kwenye kambi kadhaa ambako kuna teknolojia yao?
Kuna sehemu miaka iliyopita tulifungiwa hadi taa za umeme hizi tube lights au kitaalamu Fluorescent Lamps kutoka kwao, tunajuaje kama zilikuwa zinakusanya taarifa hizi taa kama vile inavyo daiwa wachina wanakusanya taarifa kwenye Jengo la AU walilotujengea kule Ethiopia?
Kwa mfano hivi tunavyo wakazia kwenye rasilimali zetu, maradi wa SGR na mradi wa bandari ya bwaga moyo hawawezi kuuza siri hizo kwa adui wetu jirani kama tukiiingia vitani?
NOTE:
Mimi sio muajiriwa wa serikali na sijui chochote kuhusu majeshi na ulinzi au Usalama kiujumla, nimeleta mjadala tuujadili tu tunaweza kusaidia jambo au kupunguza shinikizo (pressuare) kwa wenye dhamana.
Nukuu toka mtandaoni
"Security through obscurity would be burying your money under a tree. The only thing that makes it safe is no one knows it's there. Real security is putting it behind a lock or combination, say in a safe. You can put the safe on the street corner because what makes it secure is that no one can get inside it but you. " By Rex-M ( From stackoverflow.com)
Pitia na mjadala huu CDF alipotoka, Magufuli akasahihisha ni zamu ya TCRA kufuta clip
Ahsante kwa kutuongezea maarifa mkuu.Nimeelewa point yako unayotaka kusema lakini nadhani umeshindwa pia kuelewa tofauti ya security na secrecy. Hata kwenye computer unaambia kutumia passowrd imara kama security, at the same time unaambiwa kuwa usimwambia mtu mweingien kuhusu passowrd yakpo; hapo kuna security na secrecy. Secuirty ni ulinzi dhidi ya adversaries, halafu secrecy ni kuwanyima adversaries information za ndani zinazokuhusu.
Kwa mfano, sote tunajua white house ya Marekani ilipo na vile vile ina ulinzi kiasi kuwa huwezi kuingia pale kirahisi, lakini vile vile hatujui muundo wa ndani wa jumba lile na mahandaki yaliyomo mle ndani. Sote tunajua ilipo Pentagon yaani makao makuu ya jeshi la malekani, na vile vile kuna maeneo mengi sana ya siri ambako raia hawafiki na huko ndiko wanatunzia siri za jeshi. Mifano michache ni kama Area 51 huko Nevada ambako ndiko wanatunzia siri za jeshi la anga. Huko Pennsylvania maporini kuna maeneo ambayo hayana hata majina kwa ajili ya jeshi la nchi kavu; ukiingia pale simu inakata mawasiliano yenyewe, hata google maps haionyeshi chochote kuhusu maeneo hayo; hiyo ndiyo secrecy.
Hapana mkuu mimi raia tu, msomaji mzuri wa mambo mengi.