CECAFA KAGAME CUP 2011 Finals in Tanzania

Hongereni wa-tanzania kwa timu zetu mbili kuingia ''semi-final'' , sasa jukumu letu sasa kwa timu zetu mbili kuziunga mkono kwa kuziombea dua ili zikutane ''final'' kila laheri Simba kila laheri Yanga..
 
Si unajua TFF na CECAFA wanataka yanga na simba wacheze fainali ili wajaze uwanja, no wonder mpira east africa haukui Gumbo na Asamoah walikosa penati
 

Ni jambo la muhimu sana kila mtu kuwa na principle, ikiwa ni mbaya ama nzuri haijalishi sana muhimu ni wewe kuwa na principle tena unapokuwa kiongozi ndio muhimu zaidi.

Kwa aina ya wachezaji wetu wa kitanzania kujifanya mafaza na kujipangia utaratibu wao wa mazoezi kinyume na mpango wa mwalimu bora asipangwe hadi mashindano yaishe ili ashike adabu.

ufaza unawamaliza wachezaji wa kibongo ndio maana kila wakienda nje trials wanashindwa na kurudi hapa kula chips dume huku wenzao wa kenya na uganda wakifika huko hakuna kurudi kinaeleweka.
 

Atupatie kombe kwanza......Hao wachezaji atawajaribu wwakati wa kujiandaa na VPL
 
CECAFA imeonyesha udhaifu mkubwa sana. Ushindi wa Yanga wa matuta ni scandal! Mshika kibendera alionyesha wazi kuwa alikuwa na maelekezo ya kuhakikisha Yanga inaingia semi final. Alikanyanyua kibendera chake kwa penati mbili ambazo Yanga walikosa kwa kisingizio kuwa kipa alikuwa ame-move kabla ya kupigwa. Lakini cha ajabu ni kwamba kipa yule wa Red Sea ali-Move hata kwenye penati hizo mbili ziliporudiwa lakini akakubali kwamba ni magoli. Shame on you CECAFA! Shame on you MUSONYE/TENGA. Ndio maana ukanda wa CECAFA unaendelea kuburuza mkia kwenye viwango wa soka vya FIFA.
 
Nimemsikia TIMBE kupitia cloud FM alipokuwa ana hojiwa live na supersport, badala ya kusema RED SEA anasema ST GEORGE??
 
Wakuu
Ngoja niongee ya kwangu pia.
Kwanza sijafurahia hata kidogo the way Yanga walivyofuzu semi final, lakin sina budi kuikubali maana imeshatokea.
Ukweli ni uungwana siku zote, najua wanazi wa Simba SC wataanza kuleta ubishi ili ionekane mechi ya leo Yanga alibebwa.
Ni kawaida kwa timu pinzani kuombea mabaya mwenzake, na kwa wengine watatetea hata uongo ili hayo mabaya waliyoomba yatimie na wapate cha kuongea. Ndio wanachofanya washabiki wa Simba sasa.

Red Sea pamoja na kuizuia Yanga isiwafunge kwenye dk 90, walionekana kutumia "Udogo wao" kushinikiza wanaonewa na maamuzi ya refa. Na uliona mambo yanaanza tangu kwenye kuchagua goli la kupigia penati. Replays zinaonyesha wazi wazi kipa alikuwa akitoka golini kabla ya penati kupigwa, na kama vile haitoshi kibendera kilikuwa juu hata kabla ya penati kupigwa.

Kumalizia tu niseme, Red Sea haikuwa na uwezo wa kuitoa Yanga hata kidogo. Mpira waliocheza unaonyesha kila kitu. Walikuwa wanachelewesha sana mpira, wanajiangusha sana, na hata staili yao ya kupaki basi nyuma ilionyesha walijiandaa kulinda goli tu. Sijaona shuti hata moja walilopiga hawa Red Sea kipindi cha pili.

Tukubaliane tu kwamba Yanga hawakucheza vizuri kabisa leo, wariboronga sana, na vile vile Red Sea hawakuwa na uwezo wowote wa kuifunga Yanga. Mechi ilichezeshwa kwa haki kabisa, sema tu ushindi wa Yanga kuitoa Red Sea kwa njia hii ni aibu kwa Yanga. Lakin wameshinda kihalali kabisa.
 
Yanga ndivyo tulivyo

Tunatumia pesa nyingi sana kusajili lakini ukija kuangalia kinachofanyika uwanjani unashindwa kuelewa kabisa

Huku kwenye soka nako kuna virada vingi sana msimu wa usajili.

Yanga wana characteristics za u-champions.....winning while playing ugly.

Walipochukua hichi kikombe kule Kampala mara mbili miaka ya huko nyuma, walikuwa wanacheza hovyo kama hivi kwenye mechi za awali.
Naam, ndiyo sifa ya ma-champion wote duniani!
 
Aaai wapi! utatusikilizia bombani....leo mtu anakula 11 goli....hadi kipa wetu mpya lazima afunge!
We Mentor, njo uchukue zawadi, umebashiri ukapatia, yanga 6+5 ya red c=11, hongeraaaaaa!!!!
 
Nilishamwambiaga mapema dogo TEGETE cheza mpira kwanza,acha dharau na malingo kwa mpira wa bongo bado hujatoka na utaaribu kipaji chako,bora hizo dharau ungefanya kama ungekuwa majuu lakini hakutaka kusikia,dharau nyingi kwa kocha na wachezaji pamoja na kujisikia baada ya kuona yeye ndio mfungaji bora.....sasa naona kocha kaamua ku pay back baada ya kumvumilia......
 
Nasikitika kuwatangazia ndugu zetu, watani wetu wapinza, na mahasimu wetu dar young africans kuwa hata wafanyaje leo kufa lazima....
dah! Yahaya bin sheh alikufa na utabiri wake, waliobaki wote ni wagonjwa wa akili, vichaa na matahira
 
Kwa hiyo tusimlaumu kocha jamani anafanya kazi yake jinsi inavyotakiwa......mchezaji lazima uwe na nidhamu kwa kila mtu.....
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…