Cement gani nzuri kwa kufyatulia matofali?

Cement gani nzuri kwa kufyatulia matofali?

Hawafahamu wanachojua eti ukitumia 32.5N hata kwenye nguzo ni sawa kikubwa upunguze ratio ya mchanga, wakati kwenye nguzo inatakiwa iwe 42.5N yaani wanatuharibia ujenzi basi tu
32.5 inafaa kwa bimu, nguzo za nyumba za kawaida!
 
Hawafahamu wanachojua eti ukitumia 32.5N hata kwenye nguzo ni sawa kikubwa upunguze ratio ya mchanga, wakati kwenye nguzo inatakiwa iwe 42.5N yaani wanatuharibia ujenzi basi tu
Sio lazima boss.. Hio 32.5 inamaanisha maximum strength ambayo hio cement inaweza kuachieve after 28 days of curing ni 32.4N/mm2 the same kwa 42.5 so hio 32.5 unatumia vizuri kabisa
 
42.5R - rapid setting cement yaani ikitengenezwa zege inakakamaa fastafasta na kuwa jiwe(initial curing time ni ndogo)
42.5N - hiyo N inasimama badala ya NORMAL, setting time yake ni kawaida ,sio rapid (curring time kubwa) ,zote ni grade maana yake final strength ya zege la 42.5R na 42.5N Inafanana zinatofautiana kwenye curing time tu,42.5 R inakakamaa fastafasta
Hii 42.R Nadhani ndo inatumikaga kujenga coulms sehemu zenye maji
Bei zake zinakuwaje?
 
42.5R - rapid setting cement yaani ikitengenezwa zege inakakamaa fastafasta na kuwa jiwe(initial curing time ni ndogo)
42.5N - hiyo N inasimama badala ya NORMAL, setting time yake ni kawaida ,sio rapid (curring time kubwa) ,zote ni grade maana yake final strength ya zege la 42.5R na 42.5N Inafanana zinatofautiana kwenye curing time tu,42.5 R inakakamaa fastafasta
Hii 42.R Nadhani ndo inatumikaga kujenga coulms sehemu zenye maji
Si ndio nashangaa jamaa hapo juu atuingiza chaka N na R hii inahusiana na setting time (Cement kukauka haraka Raipd au Normal Time) Namba inaonyesha strength baada ya siku 28. Eg 32.5 itakuwa na strength ya 32.5 Mpa etc
 
Rapid strength ni initial curing time,yaani ukipika zege la R linakomaa fastafasta zege la N linakomaa lakini si KWA speed sawa na R japo mwisho wa siku baada ya Muda zege zote mbili zinakuja kuwa na strength sawa ,Sema R inakomaa fasta fasta baada ya kupikwa
Twiga ya 42.5 ina N au R sikumbuki ila inawahi kufanya hardening
 
Pamoja na maelezo ya mtoa maelezo hapo juu..

Hakikisha unatumia cement ambayo haijakaa store zaidi ya mwezi mmoja tokea siku yake ya kutoka kiwandani.

Inshort expire date yake isizidi mwezi mmoja.
Cemeng haina expire date ndugu, hapa uko wrong

Sent from my vivo 1611 using JamiiForums mobile app
 
Hivi hawa mafundi wetu huku mtaani wanafahamu chochote kuhusu huo utofauti wa cement na matumizi yake?
Mkuu fundi aliye pitia mafunzo katika vyuo vya ufundi hasa VETA anajua utofauti huo maana hiyo Ni topic kabisaa. Types of Cement.Wasio jua ni hao wanaojifunza kitaa kupandisha tofali na kuweka mortar kwenye kuunganisha tofali.
 
Hizo siyo aina za cement!
Hizo ni grades za cement, na hiyo N inamaanisha Normal strength, R ikiwa na maana ya rapid strength!
Aina za cement zipo nyingi tu, mfano ni kama hizi:-
Ordinary Portland Cement (OPC),Portland Pozzolana Cement (PPC), Rapid Hardening Cement, Extra Rapid Hardening Cement, Low Heat Cement, Sulfates Resisting Cement, Quick Setting Cement, Blast Furnace Slag Cement...n.k!

Kwa Tz aina kuu ya cement inayozalishwa na kutumika zaidi ni OPC na hata PPC, ambazo huwa zinazalishwa grades
32.5N/ 32.5R,(Cement daraja la chini)
42.5N /42.5R.(cement daraja la juu)
Lakini pia ipo 52.5N/52.5R (ambayoni cement daraja la juu zaidi, kwa tz hii bado haipo).
Cement ambayo ni grade 32.5N/32.5R hii inafaa zaidi kwa matumizi ya plaster na kazi ndogo ndogo ambazo hazihitaji kuhimili uzito mkubwa!
Cement ambayo ni grade 42.5N/42.5 au daraja la juu zaidi inafaa zaidi kwa kazi za zege kama nguzo, bimu, slabu, madaraja n.k kutokana na uimara wake kuwa mkubwa zaidi.

Maana ya herufi N, kama nilivyoeleza ni normal strengh, hii ina maana ili kufikia ubora wake baada ya matumizi huchukua muda kidogo tofauti na cement ambayo ni R-rapid strenght ambayo hii huwahi zaidi kufikia ubora wake baada ya matumizi! Kawaida ubora wake hufikiwa kuanzia siku 2-7.
Hivyo naamini kwa maelezo haya mafupi unaweza kuamua utumie cement yenye grades zipi kwa matumizi gani!
Salute mkuu
 
Tuambizane sasa kampuni ipi ndio ina 32 na ipi ina 42 Dangote au Twiga au SIMBA
 
Kampuni zote zinazalisha 32.5 na 42.5
42.5 ipo mara mbili N na R
Kama sikosei ni Dangote pekee anayezakisha 42.5 R, naye anataka ku i phase out kwa sababu ni cement inayokula malighafi nyingi , na hivyo kupelekea kuwa cement ghali kuteitengeneza
 
Back
Top Bottom