ZionGate
JF-Expert Member
- Oct 17, 2012
- 6,362
- 2,991
Baada ya kikosi cha Simba kurejea jijini Dar es Salaam jana, kwa sasa kinachosubiriwa kwa hamu na wapenzi wa soka nchini, hasa Wanamsimbazi, ni nini kitaendelea kuhusiana na kiungo wao, Jonas Mkude ambaye alidaiwa kukacha safari ya Kanda ya Ziwa walikokabiliwa na mechi mbili za Ligi Kuu Tanzania Bara dhidi ya Kagera Sugar na Biashara United.
Mkude alishindwa kuungana na wenzake kuelekea Bukoba, Jumatano iliyopita tayari kwa mechi dhidi ya Kagera Sugar waliyoshinda kwa mabao 3-0 Uwanja wa Kaitaba, kabla ya juzi kuichapa Biashara United mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Karume, mjini Musoma, Mara.
Mkude alikosekana katika mechi zote mbili, huku ikielezwa kuwa ni baada ya kuchelewa ndege, hivyo kuachwa jijini Dar es Salaam, japo yapo madai kuwa kiungo huyo aliikacha safari hiyo.
Inadaiwa kuwa muda mchache baada wachezaji wa Simba kuondoka Dar es Salaam kwenda Bukona na kubaini hali hiyo itamletea shida, kwa sababu tiketi yake ilikuwa imekatwa, Mkude anadaiwa kuomba kutumia fedha zake kupanda ndege kuwafuata wenzake, lakini aligomewa.
Taarifa ambazo BINGWA imezipata kutoka kwa mtu wa karibu na Mkude, aliyetia ngumu mchezaji huyo asijiunge na wenzake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Senzo Mazingiza.
Ikumbukwe kuwa siku ya mechi na Kagera Sugar, bosi huyo raia wa Afrika Kusini, alipanda ndege alfajiri kwenda kushuhudia mchezo huo na kuzungumza na wachezaji ili kuongeza chachu ya ushindi baada ya kupata fununu za uwepo wa hujuma.
Mtoa taarifa huyo alieleza kuwa kitendo cha Mkude kukosekana katika kikosi, kimemkasirisha bosi huyo ambaye ameahidi kushughulikia suala lake baada ya kurejea Dar es Salaam.
Alisema hata Mkude alipopiga simu kuomba kwenda hata katika mechi na Biasharabaada ya kukosa ile ya Kagera, bado Mazingiza aliendelea kushikilia msimamo wake na kumtaka amsubiri Dar es Salaam.
“Mkude amekiri kosa lake, alisema aliachwa baada ya kupitiwa na usingizi wakati wenzake wanaondoka, lakini amekataliwa kuungana na timu hadi akutane na CEO mpya, wazungumzie ishu yake.
"Bosi naona amekasirishwa sana na kitendo hicho, hii ishu haijaisha kabisa, Mkude anasubiri ni kitu gani ataambiwa na bosi wake, nadhani kuanzia kesho (leo), anaweza kuitwa,” kilisema chanzo hicho.
Alifafanua kuwa kinachomtia hofu Mkude, huenda akasimamishwa kuchezea timu hiyo kwa sababu anaweza kuambiwa ni kawaida yake, ukiangalia timu imecheza na kushinda bila hata uwepo wake.
Mkude alishindwa kuungana na wenzake kuelekea Bukoba, Jumatano iliyopita tayari kwa mechi dhidi ya Kagera Sugar waliyoshinda kwa mabao 3-0 Uwanja wa Kaitaba, kabla ya juzi kuichapa Biashara United mabao 2-0 kwenye Uwanja wa Karume, mjini Musoma, Mara.
Mkude alikosekana katika mechi zote mbili, huku ikielezwa kuwa ni baada ya kuchelewa ndege, hivyo kuachwa jijini Dar es Salaam, japo yapo madai kuwa kiungo huyo aliikacha safari hiyo.
Inadaiwa kuwa muda mchache baada wachezaji wa Simba kuondoka Dar es Salaam kwenda Bukona na kubaini hali hiyo itamletea shida, kwa sababu tiketi yake ilikuwa imekatwa, Mkude anadaiwa kuomba kutumia fedha zake kupanda ndege kuwafuata wenzake, lakini aligomewa.
Taarifa ambazo BINGWA imezipata kutoka kwa mtu wa karibu na Mkude, aliyetia ngumu mchezaji huyo asijiunge na wenzake ni Ofisa Mtendaji Mkuu wa klabu hiyo, Senzo Mazingiza.
Ikumbukwe kuwa siku ya mechi na Kagera Sugar, bosi huyo raia wa Afrika Kusini, alipanda ndege alfajiri kwenda kushuhudia mchezo huo na kuzungumza na wachezaji ili kuongeza chachu ya ushindi baada ya kupata fununu za uwepo wa hujuma.
Mtoa taarifa huyo alieleza kuwa kitendo cha Mkude kukosekana katika kikosi, kimemkasirisha bosi huyo ambaye ameahidi kushughulikia suala lake baada ya kurejea Dar es Salaam.
Alisema hata Mkude alipopiga simu kuomba kwenda hata katika mechi na Biasharabaada ya kukosa ile ya Kagera, bado Mazingiza aliendelea kushikilia msimamo wake na kumtaka amsubiri Dar es Salaam.
“Mkude amekiri kosa lake, alisema aliachwa baada ya kupitiwa na usingizi wakati wenzake wanaondoka, lakini amekataliwa kuungana na timu hadi akutane na CEO mpya, wazungumzie ishu yake.
"Bosi naona amekasirishwa sana na kitendo hicho, hii ishu haijaisha kabisa, Mkude anasubiri ni kitu gani ataambiwa na bosi wake, nadhani kuanzia kesho (leo), anaweza kuitwa,” kilisema chanzo hicho.
Alifafanua kuwa kinachomtia hofu Mkude, huenda akasimamishwa kuchezea timu hiyo kwa sababu anaweza kuambiwa ni kawaida yake, ukiangalia timu imecheza na kushinda bila hata uwepo wake.