CEO Simba Sc: Tulitaka kuwaalika Yanga Simba Supercup lakini wakakosa vigezo

CEO Simba Sc: Tulitaka kuwaalika Yanga Simba Supercup lakini wakakosa vigezo

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Dar es Salaam. Ofisa Mtendaji Mkuu wa Simba, Barbara Gonzalez amesema walikuwa na wazo la kuishirikisha Yanga katika mashindano yao ya wiki moja ya ‘Simba Super Cup’.

Mashindano hayo ya Simba yanayoshirikisha timu tatu pekee yanatarajiwa kuanza kesho kwa wenyeji kuwaalika TP Mazembe, kabla ya wageni hao kucheza na Al Hilal na kisha kumaliza na Simba kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa, Dar es Salaam.

Barbara alisema walikuwa na wazo la kuwashirikisha mahasimu wao hao, Yanga katika michezo hiyo, lakini baada ya majadiliano ya kama watakubali au la, wakaamua kuahirisha.

Kiongozi huyo wa juu wa Simba alisema wazo hilo lilikuwa kwa nia njema, kwani kwao hawakuwa wakihitaji kuonyeshana ubabe kwa upinzani walionao, bali kutumia kama njia mojawapo ya kujiandaa kimataifa.“Ni kweli, tulikuwa na wazo la kuiandikia barua kabisa Yanga kushiriki Super Cup, lakini tulifikiria mara mbili kama wanaweza kutujibu na kushiriki kwa wakati huu, ama wataelewa vinginevyo.

“Baada ya majadiliano ya muda tukaona tuliahirishe wazo hilo hadi wakati mwingine. Tunataka kufanya mashindano haya kufanyika kila mwaka na inawezekana kabisa wakati mwingine tukawaandikia wenzetu wa Yanga kushiriki,” alisema Gonzalez.

Simba inashiriki mashindano ya Ligi ya Mabingwa Afrika na imeanza mazoezi juzi kwa ajili ya kujiandaa na mzunguko wa pili lakini pia mashindano hayo ya kimataifa mwezi ujao.
 
walijua yanga lazima wawafilimbe hahahaha wakaogopa wakaamua alika wazembe wazembe

alicho kifanya tuisila kwa onyango wanakikumbuka hahahahaha
Unachekesha wewe jamaa.
Apo kuna timu imechukua kombe la Africa mara mbili mfululizo wewe ambae hata robo ujawai kunusa unawaona wazembe?

Nyinyi ata uwanja wa mazoezi tu hamna,mishahara ya wachezaji pia hamna,mnasijili wachezaji miezi sita sita.
 
Mkuu weka fact kusupport utopolo uliouweka kwenye kichwa cha habari
Fact ya nini tena?
Uto awana sifa na vigezo vya kushiriki aya mashindano ya wababe wa Africa full stop.
 
Unachekesha wewe jamaa.
Apo kuna timu imechukua kombe la Africa mara mbili mfululizo wewe ambae hata robo ujawai kunusa unawaona wazembe?

Nyinyi ata uwanja wa mazoezi tu hamna,mishahara ya wachezaji pia hamna,mnasijili wachezaji miezi sita sita.
1998 ulicheza wewe siyo?
 
Tatizo pesa. Mbongo mpe dili bado atataka mgawane pasu kwa pasu.
 
Hii ndio imekuwa wimbo utadhani mlishinda mechi. Inakuwa kama mlivyokuwa mnasherehekea goli la Morrisson kila mwezi, matokeo yake mkaja kupigwa goli 4-1
Mashabiki ya utopolo hayajielewi. Kwenye hiyo mechi Tuisila alitengeneza faulo ambayo haikustahili kuwa penati ila Onyango alifunga goli, lakini yanamwimba Tuisila utafikiri alipiga hat trick.
 
Back
Top Bottom