CHADEMA amsheni watu kwa kauli za kina Chalamila kwa mjamzito kwamba kama hatoi Shs 50,000 arudi nyumbani mume wake amkate kwa kisu na mkasi ajifungue

Chadema kitengo Cha propaganda kimekufa hizi kauli ni mtaji mkubwa kisiasa.
Umeona eeh? Zipo nyingi sana kauli mtaji toka CCM lakini hawazitumii. Yaani sijui niombe kazi ya kuwa consultant wao wa propaganda, maana kuna kauli nyingi sana za CCM wanajiua wenyewe, kuwahemusha wananchi ni rahisi sana!

Kifo ni kifo!
Hata Marekani watu wanatekwa!
Kula urefu wa kamba yako!
Msile hadi kuvimbiwa!

Some very short sighted statements ambazo ni political suicide
 
masikini amepata,,,tunasikia sauti ya matako yake tu. Ila ipo siku watatafuta pa kuficha sura zao
 
Hauna uelewa mpana kuhusiana na neno kodi. Japo umenisikitisha kiasi, kwamba serikali iwachaji wananchi wake pesa ya gloves? Au wewe unashauri wananchi waache kuzaa then nchi ikose rasilimali watu?
 
Hauna uelewa mpana kuhusiana na neno kodi. Japo umenisikitisha kiasi, kwamba serikali iwachaji wananchi wake pesa ya gloves? Au wewe unashauri wananchi waache kuzaa then nchi ikose rasilimali watu?
Zaa kama unaweza kulea mkuu usije zaa panyarodi, vibaka na dada poa wakaanza kuongeza mzigo Kwa serikali kuajiri police

Uzazi sio ajali mkuu tujiandae mapema tusije Anza sumbua watu
 
 

Attachments

  • 5938169-3f8437b06df44d0a7c8b8e175f481762.mp4
    23 MB
Yaani mtu yupo Dar es salaam hapa hapa anataka kujifungulia bure?
 
Chalamila aonywe ameteleza ila ni Kiongozi mzuri.Atoke Hadharani aombe radhi.
Katoka hadharani lakini badala ya kuomba radhi kajikanganya katika maelezo yake na kukanusha akieleza kuwa kanukuliwa vibaya na vyomba vya habari. Hayo aliyoyasema hapo awali akiwa mubashara kabisa tumeyaona na kuyasikia. Waandishi wa habari hawakunukuu aliyoyasema bali yote mwenyewe anaonekana akiyaongea hayo maneno yake na suala la kunukuliwa vibaya halipo. Muungwana haropoki na akivuliwa nguo huchutama. Huyu jamaa badala ya kuchutama kaendelea kusimama na kuacha vitu vyake hadharani.
 
Huyu hafikirii, anakariri neno nimenukuliwa vibaya, eti wrong context. Hili sio suala la kumnukuu, bali la kumsikiliza! Watu wamereact kutokana na kitu walichosikia toka mdomonimwake sio walichosoma kilichoandikwa na waandishi wa habari!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…