LGE2024 CHADEMA: Baada ya Waziri wa TAMISEMI kusema Wagombea walioenguliwa wakate rufaa, tumepokea taarifa ofisi za Mitaa, Vitongoji na Vijiji zimefungwa

LGE2024 CHADEMA: Baada ya Waziri wa TAMISEMI kusema Wagombea walioenguliwa wakate rufaa, tumepokea taarifa ofisi za Mitaa, Vitongoji na Vijiji zimefungwa

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Roving Journalist

JF Roving Journalist
Joined
Apr 18, 2017
Posts
3,984
Reaction score
13,760
TAARIFA KWA UMMA

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa jana Novemba 08, 2024 akizungumza Waaandishi wa Habari jijini Dodoma alisema kuwa wagombea walioenguliwa wakate rufaa na kuwa rufaa hizo zitasikilizwa kwa haki.

Baada ya kauli hiyo ya Waziri jana, leo Novemba 09, 2024 tunapokea taarifa kuwa ofisi za watendaji wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji zimefungwa kuanzia Bukoba Vijijini, Dar es salaam, Simiyu, Solwa, Bariadi na maeneo mengine nchini.

Mosi, tunaitaka TAMISEMI ielekeze Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wawepo ofisini ili kupokea mapingamizi yetu.

Kupata habari za Uchaguzi Serikali za Mitaa kimkoa bofya hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Pili, TAMISEMI ifungue mlango mwingine wa kupokea mapingamizi ikiwa watendaji wataendelea kukaidi amri ya kuwa ofisini. Hii ikifanyika itatuthibitishia kuwa kufunga ofisi ni maelekezo ya TAMISEMI kwa watendaji hao.

Tatu, tunataka kuona hatua za kinidhamu zikichukuliwa dhidi ya Watendaji na Wasimamizi wote ambao wanaharibu Uchaguzi Kwa makusudi huku wakijua kufanya hivyo kunaweza kulitumbukiza Taifa kwenye machafuko.

Nne, kuna Wasimamizi wa Uchaguzi ambao wameondolewa kwenye nafasi zao baada ya kufanya uteuzi jana, kama Buhigwe, Kigoma wameshushwa vyeo na kuteuliwa wasimamizi wapya.

Tunataka kujua sababu za kuondolewa kwao, kwani huu ni uthibitisho kuwa TAMISEMI inaelekeza hivyo. Tunawataka Wanachama, Wagombea na Viongozi wetu wa maeneo yote walioenguliwa, wakate rufaa na kwenda kuziwasilisha kwenye ofisi za watendaji na kama zimefungwa ofisi hizo wakae hapo mpaka ofisi zitakapofunguliwa na watendaji kupokea mapingamizi yetu.

Imetolewa leo Jumamosi tarehe 09 Novemba, 2024

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya nje.
1731139670091.jpeg
Wagombea walioenguliwa, Wameenda kukata rufaa, Wakukuta Milango imefungwa
 
TAARIFA KWA UMMA

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa jana Novemba 08, 2024 akizungumza Waaandishi wa Habari jijini Dodoma alisema kuwa wagombea walioenguliwa wakate rufaa na kuwa rufaa hizo zitasikilizwa kwa haki.

Baada ya kauli hiyo ya Waziri jana, leo Novemba 09, 2024 tunapokea taarifa kuwa ofisi za watendaji wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji zimefungwa kuanzia Bukoba Vijijini, Dar es salaam, Simiyu, Solwa, Bariadi na maeneo mengine nchini.

Mosi, tunaitaka TAMISEMI ielekeze Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wawepo ofisini ili kupokea mapingamizi yetu.

Kupata habari za Uchaguzi Serikali za Mitaa kimkoa bofya hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Pili, TAMISEMI ifungue mlango mwingine wa kupokea mapingamizi ikiwa watendaji wataendelea kukaidi amri ya kuwa ofisini. Hii ikifanyika itatuthibitishia kuwa kufunga ofisi ni maelekezo ya TAMISEMI kwa watendaji hao.

Tatu, tunataka kuona hatua za kinidhamu zikichukuliwa dhidi ya Watendaji na Wasimamizi wote ambao wanaharibu Uchaguzi Kwa makusudi huku wakijua kufanya hivyo kunaweza kulitumbukiza Taifa kwenye machafuko.

Nne, kuna Wasimamizi wa Uchaguzi ambao wameondolewa kwenye nafasi zao baada ya kufanya uteuzi jana, kama Buhigwe, Kigoma wameshushwa vyeo na kuteuliwa wasimamizi wapya.

Tunataka kujua sababu za kuondolewa kwao, kwani huu ni uthibitisho kuwa TAMISEMI inaelekeza hivyo. Tunawataka Wanachama, Wagombea na Viongozi wetu wa maeneo yote walioenguliwa, wakate rufaa na kwenda kuziwasilisha kwenye ofisi za watendaji na kama zimefungwa ofisi hizo wakae hapo mpaka ofisi zitakapofunguliwa na watendaji kupokea mapingamizi yetu.

Imetolewa leo Jumamosi tarehe 09 Novemba, 2024

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya nje.
View attachment 3147690Wagombea walioenguliwa, Wameenda kukata rufaa, Wakukuta Milango imefungwa
Ukimchekea nyani lazima uvune mabua. Unamchekea mwizi anayekuibia ataona huo wizi wake ni sawa tu.
 
Yaani uchaguzi unasimamiwa na mwanachama wa chama kimoja wapo kinachoshiriki kinyang'anyiro tena ni mkwe wa mwenyekiti wa chama hicho.

Unatakiwa uwe na matatizo ya akili kushiriki ujinga huo.
 
Kuna wagombea wa CCM walio enguliwa pia??
 
Hivi Hawa wanasikia kinachoendelea Msumbiji? Wasitiletee balaa
 
Hakuna uchaguzi hapo, jiondoeni mapema ili msije kulalamika tena. Bora waachiwe wenyewe(ccm) huku nyie mkiendelea kujitafakari na kutafuta njia nyingine ya kudai haki au kuipigania, lakini kwa maigizo haya ya CCM, kila siku hamtaacha kulalamika. Chukueni hatua
 
Laana ya kushangilia kifo cha Magufuli
 
CCM hawataondoka madarakani kwa kura kwani wanajua kuwa watashindwa vibaya wameamua kuendela kubaki madarakani kwa nguvu ya majeshi ni dhahiri wanatakaitumike nguvu hiyo hiyo kuwaondoa, swali je JW lina wazalendo wa kuweza kuwaondoa hawa wakoloni na makaburu weusi CCM ?
 
Kwenye huu uchaguzi mkwe kacheza kama Pele kawasafishia CCM njia.
 
CHADEMA haya yanayotokea mliyataka wenyewe hivyo acheni kulia lia
 
Chadema hamkujiaandaa na uchaguzi msitafute visingizio.
Waliokuwa hawakujiandaa na uchaguzi ni ccm inayotumia nguvu kubwa kukubalika na kutaka kupita bila kupingwa kwa sababu inajua bila ya hivyo haiwezi kushinda.
 
TAARIFA KWA UMMA

Waziri wa TAMISEMI Mhe. Mohamed Omary Mchengerwa jana Novemba 08, 2024 akizungumza Waaandishi wa Habari jijini Dodoma alisema kuwa wagombea walioenguliwa wakate rufaa na kuwa rufaa hizo zitasikilizwa kwa haki.

Baada ya kauli hiyo ya Waziri jana, leo Novemba 09, 2024 tunapokea taarifa kuwa ofisi za watendaji wa Mitaa, Vijiji na Vitongoji zimefungwa kuanzia Bukoba Vijijini, Dar es salaam, Simiyu, Solwa, Bariadi na maeneo mengine nchini.

Mosi, tunaitaka TAMISEMI ielekeze Wasimamizi Wasaidizi wa Uchaguzi wawepo ofisini ili kupokea mapingamizi yetu.

Kupata habari za Uchaguzi Serikali za Mitaa kimkoa bofya hapa: LGE2024 - Special Thread: Orodha ya Mijadala ya Mikoa yote Tanzania Bara inayoshiriki katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

Pili, TAMISEMI ifungue mlango mwingine wa kupokea mapingamizi ikiwa watendaji wataendelea kukaidi amri ya kuwa ofisini. Hii ikifanyika itatuthibitishia kuwa kufunga ofisi ni maelekezo ya TAMISEMI kwa watendaji hao.

Tatu, tunataka kuona hatua za kinidhamu zikichukuliwa dhidi ya Watendaji na Wasimamizi wote ambao wanaharibu Uchaguzi Kwa makusudi huku wakijua kufanya hivyo kunaweza kulitumbukiza Taifa kwenye machafuko.

Nne, kuna Wasimamizi wa Uchaguzi ambao wameondolewa kwenye nafasi zao baada ya kufanya uteuzi jana, kama Buhigwe, Kigoma wameshushwa vyeo na kuteuliwa wasimamizi wapya.

Tunataka kujua sababu za kuondolewa kwao, kwani huu ni uthibitisho kuwa TAMISEMI inaelekeza hivyo. Tunawataka Wanachama, Wagombea na Viongozi wetu wa maeneo yote walioenguliwa, wakate rufaa na kwenda kuziwasilisha kwenye ofisi za watendaji na kama zimefungwa ofisi hizo wakae hapo mpaka ofisi zitakapofunguliwa na watendaji kupokea mapingamizi yetu.

Imetolewa leo Jumamosi tarehe 09 Novemba, 2024

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya nje.
View attachment 3147690Wagombea walioenguliwa, Wameenda kukata rufaa, Wakukuta Milango imefungwa
mnapataje taarifa za upotoshaji badala muende physically ofisini hapo?

mnahijumiana wenyewe mnakimbilia kushtaki mitandaoni. huruma za mitandaoni hakitawasaidia chochote ndrugo zango wachadema 🐒
 
Yaani uchaguzi unasimamiwa na mwanachama wa chama kimoja wapo kinachoshiriki kinyang'anyiro tena ni mkwe wa mwenyekiti wa chama hicho.

Unatakiwa uwe na matatizo ya akili kushiriki ujinga huo.
Ukishiriki ni kama mvua ikinyesha ndipo utaona panapovuja kwenye nyumba. Bila kushiriki uchaguzi hivi vituko vya sasa visingejulikana. Kuhusu Mkwe wa Rais kusimamia uchaguzi Sheria zetu hazizuii ila ilitakiwa tu busara itumike kama ambapo Jaji kusimamia kesi ya Mwanae ni ngumu hukumu ya kesi kuaminika.
 
Nchi maskini zimegeuza uchaguzi kuwa njia rahisi Sana ya kuwaingiza madarakani wezi, wauaji Na wachumia tumbo.

Hizi sarakasi Dawa yake ingelikuwa inawezekana Ni sie wananchi kugawana majengo ya serikali Na kila mmoja afe Na wake
 
Back
Top Bottom