CHADEMA fanyeni Maridhiano na wabunge 19 kama mnavyofanya na CCM, mtawashangaza maadui zenu

CHADEMA fanyeni Maridhiano na wabunge 19 kama mnavyofanya na CCM, mtawashangaza maadui zenu

Sir robby

JF-Expert Member
Joined
Jun 22, 2022
Posts
2,396
Reaction score
4,080
Hakika nimefurahishwa sana jinsi Rais Samia anavyofanya siasa zake. Hakika huyu mama anaijua siasa sana kuliko mtangulizi wake, hayati Rais Magufuli.

Kitendo cha kukubali kufanya maridhiano na Chama Kikuu cha Upinzani CHADEMA, wakati hayati Rais Magufuli aliombwa na Mbowe lakini alikataa, kinampa ushindi mkubwa huyu mama kuwa anaijua siasa. Hongera sana Rais.

Kwa upande wa CHADEMA, najua mpo kwenye maridhiano na CCM kutokana na yote yaliyotokea katika utawala katili wa Awamu ya 5, utawala uliowatisha na kuwarubuni wanachama wenu Halima Mdee na wenzake 18.

Binafsi, naamini kwa asilimia 100 kuwa ubunge wao wa viti maalum ulipewa na mtawala wa Awamu ya 5 kwa vitisho vikubwa ili kuwahadaa wahisani kutokana na bunge kutokuwa na kambi ya upinzani na kuidhoofisha CHADEMA, na sio Halima Mdee na wenzake 18 waliutafuta huo ubunge.

CHADEMA mnamjua vizuri mtawala wa Awamu ya 5. Hebu jiulizeni yule mwanachama aliyekuwa gerezani aliwezaje kutoka jela tena usiku na kwenda kuapa, kama sio agizo la mtawala?

CHADEMA, fanyeni maridhiano na Halima Mdee na wenzake 18 ili warudi kundini.

1646465721930.jpg
1652427482224.jpg
 
Binadamu ni kiumbe tata sana. Utata wake unafanya jamii kupata maendeleo zaidi.
 
Hakuna vitisho walivyopewa, sema tamaa ya pesa ambayo kila mwanamke anayo, ndio iliwaingiza huko hawa Covid 19.

CDM ikiwarudisha itahitaji nguvu nyingi sana kuwasafisha.

Hawa kwa sasa nawaona wapo CCM kimaslahi zaidi. Kuwachukua itakuwa ni kufanya fujo kama ile ya kumchukua Lowasa.

Lowassa hakuleta faida yoyote Chadema. Ongezeko la wabunge kipindi kile ni matokeo ya vuguvugu la Ukawa.

Ukawa ilikuwa na nguvu kubwa kiasi kwamba CCM ilijitafakari mara mbili. Na ndio iliyozima katiba mbovu isipite.
 
Hakuna vitisho walivyopewa, sema tamaa ya pesa ambayo kila mwanamke anayo, ndio iliwaingiza huko hawa Covid 19.

CDM ikiwarudisha itahitaji nguvu nyingi sana kuwasafisha.

Hawa kwa sasa nawaona wapo CCM kimaslahi zaidi. Kuwachukua itakuwa ni kufanya fujo kama ile ya kumchukua Lowasa.

Lowassa hakuleta faida yoyote Chadema. Ongezeko la wabunge kipindi kile ni matokeo ya vuguvugu la Ukawa.

Ukawa ilikuwa na nguvu kubwa kiasi kwamba CCM ilijitafakari mara mbili. Na ndio iliyozima katiba mbovu isipite.
VILIANZA VITISHO vya kuwatafutia KESI ndio ikaja TAMAA na yule wa Jela unadhani ilikuwaje?Alitishiwa kufungwa Milele Asipokubali JIWE alikuwa hana njia mbadala zaidi ya KUTISHA WATU
 
Back
Top Bottom