Mimi nimetafakari sana kuhusu falsafa gani inaongoza Chadema hivi nikisema Chadema ina makundi na mikakati minne ya kimtazamo nitakosea. makundi hayo ni kundi la akina Lissu na Heche wanaoamini katika nguvu ya uanaharakati kuiondoa CCM madarakani,kundi la kina Mbowe,Mrema na Mnyika nk linaloamini kwenye siasa tulivu na diplomasia ili kuiondoa CCM,Kundi la akina Silaa na Askofu Mwanamapinduzi wanaoamini kwenye mtandao wa wananchi kuiangusha ccm,na kundi ls mwisho ni la wale wenye kuamini kwenye uasili wa Chadema enzi za Baregu,Marando nk Chadema ya kufanya utafiti sera na kujenga hoja,weledi kuitoa CCM. je kundi gani liko sahihi au yote yanahitaji kuunganisha nguvu na falsafa zao kuishinda CCM,yanahitaji uongozi imara na uratibu kuji compliment.