CHADEMA imfukuze Lissu sasa

Wamfukuze kwa kosa gani? Na ni nani atamfukuza? Wajumbe hao hao wanaopaswa kumfukuza ndiyo hao hao wanaomkubali na ndiyo wataokwenda kumpigia kura ya kuwa mwenyekiti.
Lissu is here to stay.
Kila aliyewahi kutaka kuwa mwenyekuti basi wapambe husema ni msaliti
 
Kosa la kumfukuza ni lipi?

Maana hueleweki ni kama umekurupushwa kuandika na hujaweka kinachofanya afukuzwe.
 
Wewe uko CCM...
Ya CHADEMA waachie wenyEwe.
 
Kimpumu ya Mbalizi hii.
 
Weka vitu mkuu.
 
Tuondolee kifaduro chako hapa pimbi wewe
 
Nakuunga mkono asee hivi lissu anajikuta yeye nani mwenyekiti atabaki mmoja tu na ni mbowe lisu hatumtambui

Over
 
Na bado
 
Huo ndio mpango wa TAL.
Wafinyiane kwenye port la ugali wakizidiwa wapige kelele na kumfukuza na hiki ndicho anachohitaji zaidi. Kinyume chake ni kutomnyang'anya ushindi.
 
Huna hoja Mzee
Nyie mnajiita Chama cha Demokrasia mnataka nini sasa.
Tulieni Hivyo hivyo hamjashika anchi mnakuwa na Kisiran cha Kike.
Lisu sio Mzuri lakini Nibora Zaid ya Mbowe Mara 1000
Kama kweli mnahitaji Upinzani walau wakuwasumbua Majani Huyo ndio Anafaa
 
Kumfukuza Lisu wakati huu ni kuzidi kuichafua CHADEMA na kumpa Lisu nguvu ya kusema mengi Kuhusu CHADEMA na kumuhusu Mbowe,sanduku la Kura litaamua lenyewe.
Chama cha siasa hakikosi minyukano,na minyukano yenye mashiko ustawisha chama.
Mbowe na Lissu watia nia wanaanza kusogea ulingoni.
Hili litakuwa pambano kubwa la kihistoria raundi 15 na si 12. Limeanza kuwavutia watu wengi vyama vya kisiasa ikiwemo CCM.
Sheria za pambano watakao shindwa wawaunge mkono timu ushindi.Na hiyo ndio ukomavu wa demokrasia ndani ya chama.
Labda pambano hili linairudisha Chadema kwenye pick ya 2015.
 
Kile ambacho CCM mnatamani kiwakute kibaya CDM muda sio mrefu kuanzia Machi 2025-Jul 2025 uhuni utakuwa umetamalaki Lumumba hadi mtafikiana hatua ya kuuana kwa njia ya sumu. kuzushiwa maovu yasiyomithilika, kupangiwa ajali na kutengenezewa tuhuma za kihalifu.

Rejea: Katibu wa CCM Kilolo Iringa auwawa kwa kupigwa risasi-makada na viongozi watatu wa CCM wahusishwa na kukamatwa
 
Yupo tunayetaka kumfukuza kwanza kabla ya unayeshauri
 
Wote hakuna kitu
 
Kweli ni muda muafaka wa huyu jamaa kuitwa mbele ya kamati ya maadili ya chama kujibu tuhuma zote alizozitoa kwa ushahidi.- wamemuacha huru mno akiendelea kubwabwaja.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…