CHADEMA ina "Options" gani kuhusiana na Mchakato wa Katiba Mpya?

CHADEMA ina "Options" gani kuhusiana na Mchakato wa Katiba Mpya?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Joined
Mar 10, 2006
Posts
33,771
Reaction score
41,027
Baadhi yetu tulikataa na tunaendelea kukataa kutambua mchakato huu wa Katiba Mpya. Tulianisha sababu za kufanya hivyo mapema kabisa Mwenyekiti wa CCM alipotangaza kuanzisha mchakato huu; na tuliweka zaidi bayana za kuukataa tulipopata tu mswada wa ile sheria ya kupitia mchakato wa Katiba. Tulionesha wakati ule kuwa Mkataba huu uko fundamentally biased and inherently flawed in favor of the ruling party.

Juzi nimeona Mtaalamu wa Katiba Prof. Maina naye amejia juu muundo wa baraza la kutunga Katiba ambapo wabunge wote na wajumbe wa BLW la Zanzibar ni wajumbe ( na hivyo kuipa CCM overwhelming majority) ndani ya mchakato huo. Tulipokataa mchakato huu kwa sababu zilizo wazi - kwamba umelengwa kuinufaisha CCM na kufanya matamanio ya watu kuhusu katiba mpya kuwa ya njozini zaidi. Wengine japo tuna michango mizuri tu kuhusiana na rasimu ya Katiba tumekataa kuitoa kwa sababu kutoa michango hii kwa tume ya Warioba ni kuipa uhalali ambao haina. Tulikataa tume na mchakato wenyewe kuwa vimepora mamlaka ya wananchi kuandika Katiba yao.

Hata hivyo chama kikuu cha upinzani ambacho ndicho kilikuwa kinapigania Katiba Mpya kwa muda mrefu kikarukia trela hili la "Katiba Mpya" huku viongozi wake wakitoa pongeza kuwa ni uamuzi mzuri. Na hata walipoonesha tatizo kidogo waliitwa wakawekwa sawa na baadaye kuukumbatia mchakato huu. Sasa mchakato umefika mahali ambapo tunaelekea kuunda Baraza la Kutunga Katiba wapinzani wanaanza kujia juu na wasomi wanaanza kuja juu - rejea jinsi watu wamelalamikia mabadiliko ya sheria hiyo kwa mara nyingine tena. Ni kana kwamba wapinzani walitegemea CCM na serikali yake watengeneze mchakato utakaowafurahisha wapinzani ili uwe halali!

Sasa inaonekana CCM haibadiliki na wala haitatarajii kubadilika; wapinzani walishavua nguo kuoga na sasa maji yanaanza kuwamwagikia wanataka kutoka bafuni! "Oh maji ya moto!"; kana kwamba hawakujua maji ni ya moto kwa sababu tunajua nani anayafungulia.

Maoni yangu ni kuwa CHADEMA imejiweka kwenye kona mbaya; kona ambayo sijui itatoka vipi:

a. Wameshakubali mchakato huu na wameupa uhalali kwa kushiriki kwao. Tayari wameshikiri kiasi cha kufikia kuunda mabaraza ya kupitia rasimu ya Katiba na kukusanya maoni. Kimsingi, CHADEMA wamekubali uhalali wa mchakato huu. Je sasa wanaweza kulalamika kuwa hauna haki? Je hawakujua kuwa hauna haki toka mwanzo? au walitarajia nini wakati toka mwanzo mchakato ulionekana - kisheria - kuipendelea CCM?

b. Wanalazimika kutumia nguvu ya ushawishi kwa wananchi ili waone matatizo na hakuna mahali pazuri pa kufanya hivyo kama Bungeni. Hata hivyo, tayari tumeshaona kuwa Bungeni nafasi hiyo hawapewi tena na hata wakipewa zinatumika kila mbinu kuzima hoja kama tulivyoshuhudia hivi karibuni. Kutumia Bunge kurekebisha mchakato huu ni zoezi gumu kulitekeleza.

c. Wanaweza kuamua kuendelea na mchakato na kutumia nguvu nyingi kuendesha kampeni wakati wa kura ya maoni kukataa Katiba Mpya. Kwa baadhi ya watu option hii inaonekana ni nzuri na yenye mantiki. Hata hivyo tatizo liko pale pale kama nilivyoonesha wakati mchakato huu unafukiziwa ubani Bungeni; sheria inasema rasimu ya katiba Mpya itapita kama itapata asilimia 50 au zaidi (simple majority) ya watu wa Zanzibar na Tanganyika ambao ni wapiga kura. Kimsingi, CCM haiitaji kura hata moja ya wapinzani kupitisha kwani wanahitaji kuhamasisha kura za wana CCM na walio watu huru (independents).

Hili pia lilikuwa tatizo kubwa kwangu kwa sababu fikiria kuwa kufanyia marekebisho Katiba ya sasa haiwezekani isipokuwa mpaka 2/3 ya wabunge wa bara na visiwani wakubali (yaani zaidi ya asilimia 66). Kwa maneno mengine ni vigumu kufanyia marekebisho kipengele cha Katiba ya sasa kuliko kuamua kupitisha Katiba mpya!

Ukiangalia sana utaona kuwa CHADEMA iko mahali pagumu sana; sijui ina options gani nyingi zaidi ya kukubali kwenda na mawimbi tu? Hawawezi kulazimisha mabadiliko ya sheria, hawawezi kuzuia mchakato kuendelea, na hawawezi kuzuia Katiba Mpya kupita! Sasa wafanye nini? wakubali tu matokeo ya kukubali mchakato huu. Sivyo?
 
Hivi, kwa akili yako, ulitarajia ni watu gani wawe majority kwenye kuwakilisha wenzao katika mchakato huu wa katiba mpya?

CCM ni chama ambacho kimepewa uhalali na watanzania walio wengi kutawala, ni wazi kuwa hata kwenye uwakilishi CCM itakuwa na wawakilishi wengi kuliko vyama vingine.

It pains, but learn to like it.
 
Mchakato wa Katiba haujaanzishwa na Mwenyekiti wa CCM. Umeanzashwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.

As usual, Mwanakijiji yuko katika ulaghai...
 
Ingetokea taasisi makini ikafanya tafiti kujua msimamo wa sasa wa Watanzania juu ya mchakato huu wa awali wa katiba mtashangazwa!!!

Sidhani kuna wanaojua kihalisia nini mtizamo wa wananchi sasa.Kibaya zaidi upepo wa kisiasa ndio unaoendesha mchakato.
 
Mchakato wa Katiba haujaanzishwa na Mwenyekiti wa CCM. Umeanzashwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.

As usual, Mwanakijiji yuko katika ulaghai...

Kwa hali ya sasa tusaidie kutenganisha kofia ya Mwenyekiti wa CCM na Rais wa Tanzania!
 
c. Wanaweza kuamua kuendelea na mchakato na kutumia nguvu nyingi kuendesha kampeni wakati wa kura ya maoni kukataa Katiba Mpya. Kwa baadhi ya watu option hii inaonekana ni nzuri na yenye mantiki. Hata hivyo tatizo liko pale pale kama nilivyoonesha wakati mchakato huu unafukiziwa ubani Bungeni; sheria inasema rasimu ya katiba Mpya itapita kama itapata asilimia 50 au zaidi (simple majority) ya watu wa Zanzibar na Tanganyika ambao ni wapiga kura. Kimsingi, CCM haiitaji kura hata moja ya wapinzani kupitisha kwani wanahitaji kuhamasisha kura za wana CCM na walio watu huru (independents).

Mzee wangu kumbe na wewe unatambua kuwa CCM haihitaji kura wapinzani kupata 50%+1? !!!

Uanaharakati wa CDM umeiponza sana CDM, kwa sasa wamebaki na option chache sana, mchakato unazidi kuyoyoma na muda unazidi kuisha, tatizo ni kuwa CDM haikuwa na na haina hoja za nguvu linapokuja swala la katiba, wamepumbazwa na serikali 3 wakapumbazika, CCM waka-pretend hawaitaki rasimu hii, CDM wakaingia kichwa kichwa kuipigia debe wakidhani wanaikomoa CCM kumbe wakasahau kuna kupigiwa kura, mabaraza ya katiba, bunge la katiba etc etc.

Narudia uanaharakati na kupumbazwa na matukio kumewaponza ndugu zako.

Nakumbuka sana kile kisa cha mbwa mlinzi na mwizi aliyekuja na kipande cha nyama............
 
Hii article imeandikwa as if Katiba ni ya vyama vya siasa.

Huu ni upotoshaji mkubwa unaodhamiria kuweka pembeni makundi mengine ya jamii.

Katiba sio ya CCM, NCCR, CUF, CHADEMA au TLP. Katiba ni ya wananchi WOTE hata wale wasio na vyama wala wasiopenda siasa.
 
Hii article imeandikwa as if Katiba ni ya vyama vya siasa.

Huu ni upotoshaji mkubwa unaodhamiria kuweka pembeni makundi mengine ya jamii.

Katiba sio ya CCM, NCCR, CUF, CHADEMA au TLP. Katiba ni ya wananchi WOTE hata wale wasio na vyama wala wasiopenda siasa.

yeah si ndio ulaghai wenyewe ulipo; CCM wanataka watu waamini kuwa ni mchakato wa wote! Inanikumbusha hadithi ya sungura na fisi ambapo walikuwa na "cha wote" na "cha wageni".
 
Kuungalia mchakato wa Katiba katika dirisha la vyama vya siasa na ushabiki wa kiitikadi za vyama vya siasa ni kukosa UZALENDO.

Katiba goes far beyond vyama vya siasa. Ni katiba ya watu wote wanaoishi sasa na vizazi vijavyo.

Chadema ni mdau mmojawapo tu kwenye katiba kama jinsi ilivyo timu ya mpira ya Coastal Union, SACCOS ya wabeba zege, NGO ya kulea watoto wanaoishi kwenye hali ngumu, Chama cha wavuvi Unguja, TLP, TAMWA, Kampuni ya IPP etc.

Chadema haistahili any special position zaidi ya wadau wengine. Watanzania WOTE wana haki sawa ya kutoa maoni na kuheshimiwa kwenye mchakato huu wa Katiba.
 
Mkuu mimi nawaungo mkono CHADEMA kwa ushiriano na ushiriki walioutoa. Jiulize tu kama wangekaa kando hali ingekuwaje.

Naomba nikuhakikishie kuwa kila kitu kinakwenda in favour ya CHADEMA na sisi wananchi.

Kwa kifupi sana mimi naona CCM wameshamaliza mchakato wao; kwa maana hii si ajabu watapita hadi kwenye baraza la katiba. NINA UHAKIKA HAWATAPITA KWENYE KURA ZA WANANCHI. Sema tu hapo wanafanya gamble kwa matarajio ya kuwa wataingia kwenye uchaguzi wa 2015 na katiba hii. HAPO PIA HAWANA GUARANTEE.
 
Kuungalia mchakato wa Katiba katika dirisha la vyama vya siasa na ushabiki wa kiitikadi za vyama vya siasa ni kukosa UZALENDO.

Katiba goes far beyond vyama vya siasa. Ni katiba ya watu wote wanaoishi sasa na vizazi vijavyo.

Chadema ni mdau mmojawapo tu kwenye katiba kama jinsi ilivyo timu ya mpira ya Coastal Union, SACCOS ya wabeba zege, NGO ya kulea watoto wanaoishi kwenye hali ngumu, Chama cha wavuvi Unguja, TLP, TAMWA, Kampuni ya IPP etc.

Chadema haistahili any special position zaidi ya wadau wengine. Watanzania WOTE wana haki sawa ya kutoa maoni na kuheshimiwa kwenye mchakato huu wa Katiba.

Ebu kwenye hoja yako weka CCM badala ya CHADEMA kama inafaa
 
Hapo tayari umeshaangalia mambo katika dirisha la Chadema na CCM. Katiba is beyond that...

Very good answer. Iweje sasa CCM wanatumia mabavu na mbinu chafu kukamindaza mawazo huru; kuzuia fursa ya sisi wengine tusio na chama kupata angalau maoni mbadala kuhusu katiba yetu? Uzingatie kuwa kuna waraka wa CCM umetekelezwa kikamilifu kutuengua baadhi yetu kwenye mchakato wa katiba.
 
Napata mashaka sana nakinacho endelea kwa kupima utayari wa wananchi wakawaida katika hili,japo kuwa kumekuwa na taarifa za ushirikishwaji wa mojakwamoja,naoana nguvu ya wanasiasa kuliko nguvu ya uhitaji wa wananchi wenyewe kutengenezewa nyumba ya kuishi bila kuainisha ni ya aina ipi na yenye ukubwa upi wanayo itaka,bali wamekuwa wakishauriwa na hawa wajenzi wenye manufaa yao binafsi kwamba kwa mpango huu hii nyumba huenda ikwa bora na ikawafaa...

Twende mbele turudi nyuma,nguvu ya wanasiasa bado inamwendesha mtanzania kutetea maslahi ya wanasiasa. Kwa mtaji huu sioni mwarobaini wa mabadilko ndani ya tanzania..
 
Kinachonisikitisha mimi ni mchakato huu wa Katiba mpya kuuvunja MUUNGANO. Hauwezi kuirudisha Tanganyika bila kuuvunja Muungano wetu.
 
Kaka haki inapiganiwa!Ikumbukwe ya kuwa muswada wa kwanza wa mabadiliko ya katiba ulikuwa na makosa mengi lakini ULIREKEBISHWA na mambo yakawa mazuri.Lakini sasa marekebisho haya ya pili yanaturudisha nyuma hatua 10.Sasa unataka chadema wafanye nini??!Wangekataa vipi tokea mwanzo wakati agenda ya katiba mpya ilianzishwa na Chadema.Kabla nikuelimishe ndugu yangu,kinachopingwa hapa ni marekebisho ya sheria ya katiba iliyoletwa na kupitishwa hivi majuzi.Ya kuwa muswada huo ulikuwa na makosa mengi ya msingi ikiwemo zanzibar kutoshirikishwa.Hivyo nakusihi uwe unafuatilia mambo kwanza badala ya kuandika mambo mengi yenye lengo la kuwahadaa watu.Unapojadili jambo kwenye public lazima uwe na ufahamu nalo kwa kina ndugu yangu.Otherwise,tunatafsiri ya kuwa hujaelewa mambo kama ulivyotakiwa kuelewa.
 
Mchakato wa Katiba haujaanzishwa na Mwenyekiti wa CCM. Umeanzashwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano.

As usual, Mwanakijiji yuko katika ulaghai...

jina lake ni jakaya kikwete , pamoja na urais alionao lakini pia ni mwenyekiti mtendaji wa ccm , ana kawaida ya kuweka maslahi ya chama chake mbele kwenye jambo lolote .
 
ushauri wangu kwa cdm ni kurudi kwa wananchi na kuwaelekeza kuupinga mchakato wa katiba kwa nguvu zote , haijapata kutokea mahali popote duniani kwa watu 10 kuushinda umati ! Takwimu nilizonazo ni kwamba wanachama wa ccm hawazidi mil 3 , hawa hata iweje hawawezi kuwashinda zaidi ya 40mil .
 
Very good answer. Iweje sasa CCM wanatumia mabavu na mbinu chafu kukamindaza mawazo huru; kuzuia fursa ya sisi wengine tusio na chama kupata angalau maoni mbadala kuhusu katiba yetu? Uzingatie kuwa kuna waraka wa CCM umetekelezwa kikamilifu kutuengua baadhi yetu kwenye mchakato wa katiba.

CCM haijatengua maoni ya mtu. CCM ingetaka kufanya hivyo hata rasimu isingekuwa na sura iliyo nayo.

Inachofanya CCM ni kushiriki mchakato kwa kutoa maoni yake kwa kutumia fursa waliyopewa na wananchi ya kuwawakilisha. Watanzania wengi wameipa CCM fursa ya kuwawakilisha kwa njia ya Bunge na mabaraza ya Halmashauri.

CCM kutokupigania maslahi ya wananchi hawa ni KUWATELEKEZA watu walioiamini.

Katika mchakato wa Katiba CCM ina jukumu la kipekee kwamba ndio chama chenye dhamana ya kuliongoza Taifa kuipata Katiba nzuri. mambo yakienda kombo, CCM inabeba lawama.
 
Kaka haki inapiganiwa!Ikumbukwe ya kuwa muswada wa kwanza wa mabadiliko ya katiba ulikuwa na makosa mengi lakini ULIREKEBISHWA na mambo yakawa mazuri.

WAkati mwingine unapoandika kitu uwe unasoma ili ujithibitishe umeandika kitu chenye mantiki; kama sheria ilikuwa na makosa mengi yakarekebishwa halafu mambo yakawa mazuri haya marekebisho ya sasa yanatoka wapi? Lakini la pili unataka watu waamini kuwa mapendekezo yaliyotolewa katika marekebisho ya kwanza yalichukuliwa yote! na hivyo sheria ikawa nzuri. Ukweli ni kuwa sheria nzima na mbovu na hata hayo marekebisho yaliyofanywa wakati ule hayakukidhi mahitaji ndio maana tumefika hapa.

Lakini sasa marekebisho haya ya pili yanaturudisha nyuma hatua 10.Sasa unataka chadema wafanye nini??!Wangekataa vipi tokea mwanzo wakati agenda ya katiba mpya ilianzishwa na Chadema.

Well, marekebisho ya sasa hayaturudishi mahali popote ambapo hatukuwepo tayari; yanatuthibitisha tu kuwa tupo tulipokubali kuwepo.

Kabla nikuelimishe ndugu yangu,kinachopingwa hapa ni marekebisho ya sheria ya katiba iliyoletwa na kupitishwa hivi majuzi.Ya kuwa muswada huo ulikuwa na makosa mengi ya msingi ikiwemo zanzibar kutoshirikishwa.

Sijui katika hili la Katiba Mpya una la kunielimisha. Makosa hayakuwemo juzi au hayakutumbukia tu humo ndani; sheria ya awali ilikuwa na makosa si kidogo; tukakubali kuendelea na mchakato huu pamoja na makosa yake na tukaona yalivyotuuma. Watu wengi (upinzani hasa) wamekubali rasimu ya Katiba si kwa sababu mchakato ni mzuri bali kwa sababu wanaamini matokeo ni mazuri. Hivyo, wameuhalalisha kwa sababu unaonekana kukidhi matakwa yao. Hata hivyo huko tunakokwenda mchakato huu utakuwa wazi zaidi kukidhi maslahi ya CCM na hapo wapinzani wataanza kusema mchakato una matatizo.

Hivyo nakusihi uwe unafuatilia mambo kwanza badala ya kuandika mambo mengi yenye lengo la kuwahadaa watu.Unapojadili jambo kwenye public lazima uwe na ufahamu nalo kwa kina ndugu yangu.Otherwise,tunatafsiri ya kuwa hujaelewa mambo kama ulivyotakiwa kuelewa.

Sidhani kama unafuatilia mambo vizuri kuliko mimi; na unavyochangia inanitisha kuwa unaamini huu mchakato ni halali. Hili ni tatizo kubwa zaidi la watu wanaounga mkono mchakato huu.
 
Back
Top Bottom