CHADEMA itumie sera za Magufulification kwenye mazuri yake ili ikamate dola

CHADEMA itumie sera za Magufulification kwenye mazuri yake ili ikamate dola

Justine Marack

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2014
Posts
612
Reaction score
1,698
Tunakubali Magufuli hakuwa mwema sana lakini hakuwa muovu kwa Kila kitu. Kama ilivyo Kila mwanadam anayo mabaya na mazuri katika amatendo yake.

Zile zama za kuungana na Mafisadi ya CCM kumtukana Magufuli Sasa imetosha. Tunahitaji Sasa kugeukia Yale mazuri ambayo aliyasamia.

Mnaweza kuyasema mabaya yake panapo bidi ili mmalize uko wa chuki zenu kwa Magufuli, lakini pia muyaseme mazuri yake panapo bidi. Inashangaza kuona CHADEMA na CCM kuungana kiitikadi. Inatia shaka sana kwamba kwanini muwe na adui mmoja? Je, matendo yenu pia yanafanana?

Katika kutumia Magufulification CHADEMA itaokoa rasilimali fedha na muda kwani jamii imekwisha amini juu ya sera za Magufuli na iko tayari kuendeleza sera hizo.

Hii itafanikiwa kama kweli lengo la CHADEMA ni kushika Dola.

Hakuna kipindi Chadema itakutana na mpinzani dhaifu kama 2025.

Fanyeni haya machache ya msingi.

1. Mrudisheni kundini Dr. Slaa
2. Pingeni maovu kwa kusimamia uzalendo wa kweli

CHADEMA imepitia vipindi vya maamuzi magumu katika historia yake.
Kama Chadema iliweza kubadili gia angani na Kumchukua Lowassa na wnanchi wakawaelewa, hakuna gumu zaidi.

Siasa ni dynamic kulingana na wakati.

Wananchi wanayo dukuduku kwa mambo mangi ya hovyo, tunahitaji atakae puliza kipenga ili mbungi ianze
 
Back
Top Bottom