CHADEMA: Khamis Omary amepatikana akiwa kituo Cha Polisi Chato, ambako awali Polisi walisema hawajamshikilia katika kituo hicho

Khamis Omary Khamis amepatikana akiwa kituo Cha Polisi Chato, ambako awali polisi walisema hawajamshikilia katika kituo hicho.

Bila maandamano na mbinyo wa kisawa sawa serikali ya chama dola kongwe CCM haiwezi kusikia sauti za umma.

Taratibu serikali inaanza kuitikia madai ya umma, lakini bado tuendelee kuichagiza CCM na serikali yake iwaachie wafungwa wote wa kisiasa waliopo katika mahabusu ya kundi la watu wasiojulikana.


Khamis Omary Khamis amepatikana akiwa kituo Cha Polisi Chato
 
laana na aibu kubwa sana hii " panya kaloa " na bado utamona mtu kwenye press akihamasisha wananchi kama sie yeye anae husika, aisee kuna watu hawamuogopi Mungu, hawana aibu wala soni na hawana ubinadamu kabisa
Kuteka, kutesa na kuua mdomo koma
 
Kuteka, kutesa na kuua ukimaliza hapo unapitia kibunda chako unaenda kula na familia pesa za damu, watoto wanajua baba karudi kazini kumbe karudi kuua mdomo koma JF watakulima ban
 
Tanzania hamna polisi ,kuna genge la vibaka na wauaji walipewa leseni na sare na ccm
 
Yaani! Hivi hii mission lengo lake ni nini haswa, na hata baada ya mission hiyo wanategemea nini, maana kila wanaeruka nae wanatokea wengine kadhaa, ina saidia nini, na sasa imekua too much yaani too much
Uchaguzi unakaribia, take out wale wapinzania ambao ni vikwazo kwa harakati zao
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…