CHADEMA kutohudhuria hafla fupi ya kukabidhi taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020

CHADEMA kutohudhuria hafla fupi ya kukabidhi taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Mwaka 2020

Mwaka jana kulikuwa na wizi wa kishamba sana wa kura,Ni mjinga pekee anayeweza kufanya uchaguzi kwa style ile
 
Hiyo hafla inagharamikiwa na nani? Kwa fedha zipi?
TOZO pumbavu zao.. wanatamba wanatukamua mpaka ”NGAMA ”na hakuna tunachowafanya. MaCCM watayalipa mateso wanayowapatia watanzania siku moja.
 
  • Thanks
Reactions: PNC
CDM wanavyojitunisha unaweza kudhani ni Republicans, ODM or Labour party! Kumbe chama chenyewe kimeshajifia zamani, yamebaki mabaki machache jf na Twitter
 
CDM wanavyojitunisha unaweza kudhani ni Republicans, ODM or Labour party! Kumbe chama chenyewe kimeshajifia zamani, yamebaki mabaki machache jf na Twitter
Kama hujui hasara ya mambo haya muulize Magufuli kilichomfanya atumie mabilioni ya hela kununua Halima Mdee na wenzake
 
nasubiri kumuona prof lipumba akihudhuria ripoti ya ubakwaji wa demokrasia
 
Tumepokea mwaliko kutoka Kwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kwa ajili ya Mwenyekiti Taifa, Katibu Mkuu, aliyekuwa mgombea urais na aliyekuwa mgombea wa umakamu wa urais kuhudhuria hafla fupi ya kukabidhi kwa Rais taarifa ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Chama kupitia barua ya Katibu Mkuu kimemjulisha Mkurugenzi wa uchaguzi kuwa hatutashiriki hafla iliyopangwa kufanyika Ikulu tarehe 21 Agosti 2021 kwa sababu zifuatazo:

1. Hakukuwa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2020; kulikuwa na "Uchafuzi Mkuu" uliohusisha uporaji wa ridhaa ya wananchi kuchagua viongozi wao na ukiukwaji mkubwa wa sheria na haki. Kwa sababu ya kukosa uhuru kama taasisi, Tume ya Uchaguzi ilishiriki moja kwa moja katika kuharibu mchakato wa Uchaguzi Mkuu na kusababisha kuwa na "Uchafuzi Mkuu".

Sisi hatuwezi kushiriki kwenye tukio lolote litakalohalalisha Uchafuzi Mkuu huo mbele ya macho ya jamii ndani ya Tanzania na kimataifa.

2. Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe amepewa kesi ya kubambikiza ya ugaidi kwa sababu ya chuki za kisiasa dhidi yetu. Tunaelekeza nguvu na muda tulionao kufanya jitihada za kuhakikisha Mwenyekiti wetu na viongozi na wanachama wengine waliokamatwa kwa uonevu na wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wanaachiliwa huru.

3. Aliyekuwa mgombea urais wetu na Makamu Mwenyekiti wa chama Bara , Mheshimiwa Tundu Lissu, 'alilazimishwa kukimbilia nje ya nchi ' kwa sababu ya vitisho dhidi ya maisha yake vilivyofanywa na vyombo vya usalama au kwa ushiriki au baraka za vyombo hivyo.

Alikamatwa na Jeshi la Polisi akiwa nje ya Ubalozi wa Ujerumani, na isingekuwa wanadiplomasia wa Ofisi ya Ubalozi wa Ujerumani kuingilia kati angeweza kudhuriwa na Jeshi la Polisi.

Aidha, Mkuu wa Jeshi la Polisi amesema hadharani kwamba Mheshimiwa Lissu hatapatiwa ulinzi wowote wa polisi licha ya ukweli kwamba aliponea chupu chupu jaribio la mauaji la tarehe 7 September 2017, jaribio ambalo halijawahi kuchunguzwa na hatua stahiki kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

Bila kuhakikishiwa usalama na uhuru wake, ikiwemo kufutiwa kesi za uongo alizofunguliwa mahakamani kati ya 2016 na 2017, Mheshimiwa Lissu hajioni kuwa atakuwa salama kuweza kurudi nyumbani kushiriki kwenye shughuli za kisiasa za nchi yetu ikiwemo kushiriki kwenye tukio hili.

4. Tume ya Taifa ya Uchaguzi haijajibu mpaka sasa barua ya Katibu Mkuu ya tarehe 25 Novemba 2020 yenye kumb. Na. C/HQ/ADM/20/TU/05/14 ambapo alitaka maelezo ni nani alisaini barua na fomu za waliotangazwa kuwa wabunge wa viti maalum na kutupatia nakala ya nyaraka husika kwa ajili ya kuchukua hatua kwa kuzingatia kuwa Kamati Kuu haijawahi kufanya uteuzi wala Katibu Mkuu hajawahi kuwasilisha orodha ya majina katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

5. Kwa sasa na kwa siku zijazo, agenda kuu ya chama chetu ni kuhakikisha tunapata Katiba Mpya itakayotengeneza mfumo huru na wa kidemokrasia wa uchaguzi kwa nchi yetu. Kushiriki katika mialiko na shughuli za Tume isiyokuwa huru ni kuipa baraka za kisiasa Tume hiyo, na kupunguza nguvu na ari ya jitihada za kufanya mabadiliko yanayohitajika katika nchi yetu.

Kutokana na sababu tajwa hapo juu Chama hakitatuma mwakilishi katika hafla hiyo na badala yake tutaendeleza nguvu kutetea Uhuru,Haki,demokrasia na Maendeleo ya watu.

Imetolewa Leo Ijumaa tarehe 20 Agosti,2021

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya NjeView attachment 1899771View attachment 1899772
Habari ndiyo hiyo,anyepingana na hizo hoja atakuwa mchawi wa nchi hii.Uzuri huwa hawakawii na hawajifichi.Watakuja kusema CHADEMA wametumwa na mabeberu na wanapinga kila kitu ilhali CCM ikipinga hoja mujarab za CHADEMA na wapinzani wengine zenye maslahi ya Wananchi kwa kudai siyo vipaumbele vyao.Mifano IPO mingi na mkubwa mojawapo ni Mchakato wa kuandika Katiba.Tulitumia fedha nyingi za walipa kodi maskini(wanyonge) ambazo hazipungui 100Billion halafu wanadai so kipaumbele chao?
Kama siyo kipaumbele cha CCM ni kipaumbele chetu sisi Watanzania.
 
Tumepokea mwaliko kutoka Kwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kwa ajili ya Mwenyekiti Taifa, Katibu Mkuu, aliyekuwa mgombea urais na aliyekuwa mgombea wa umakamu wa urais kuhudhuria hafla fupi ya kukabidhi kwa Rais taarifa ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Chama kupitia barua ya Katibu Mkuu kimemjulisha Mkurugenzi wa uchaguzi kuwa hatutashiriki hafla iliyopangwa kufanyika Ikulu tarehe 21 Agosti 2021 kwa sababu zifuatazo:

1. Hakukuwa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2020; kulikuwa na "Uchafuzi Mkuu" uliohusisha uporaji wa ridhaa ya wananchi kuchagua viongozi wao na ukiukwaji mkubwa wa sheria na haki. Kwa sababu ya kukosa uhuru kama taasisi, Tume ya Uchaguzi ilishiriki moja kwa moja katika kuharibu mchakato wa Uchaguzi Mkuu na kusababisha kuwa na "Uchafuzi Mkuu".

Sisi hatuwezi kushiriki kwenye tukio lolote litakalohalalisha Uchafuzi Mkuu huo mbele ya macho ya jamii ndani ya Tanzania na kimataifa.

2. Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe amepewa kesi ya kubambikiza ya ugaidi kwa sababu ya chuki za kisiasa dhidi yetu. Tunaelekeza nguvu na muda tulionao kufanya jitihada za kuhakikisha Mwenyekiti wetu na viongozi na wanachama wengine waliokamatwa kwa uonevu na wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wanaachiliwa huru.

3. Aliyekuwa mgombea urais wetu na Makamu Mwenyekiti wa chama Bara , Mheshimiwa Tundu Lissu, 'alilazimishwa kukimbilia nje ya nchi ' kwa sababu ya vitisho dhidi ya maisha yake vilivyofanywa na vyombo vya usalama au kwa ushiriki au baraka za vyombo hivyo.

Alikamatwa na Jeshi la Polisi akiwa nje ya Ubalozi wa Ujerumani, na isingekuwa wanadiplomasia wa Ofisi ya Ubalozi wa Ujerumani kuingilia kati angeweza kudhuriwa na Jeshi la Polisi.

Aidha, Mkuu wa Jeshi la Polisi amesema hadharani kwamba Mheshimiwa Lissu hatapatiwa ulinzi wowote wa polisi licha ya ukweli kwamba aliponea chupu chupu jaribio la mauaji la tarehe 7 September 2017, jaribio ambalo halijawahi kuchunguzwa na hatua stahiki kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

Bila kuhakikishiwa usalama na uhuru wake, ikiwemo kufutiwa kesi za uongo alizofunguliwa mahakamani kati ya 2016 na 2017, Mheshimiwa Lissu hajioni kuwa atakuwa salama kuweza kurudi nyumbani kushiriki kwenye shughuli za kisiasa za nchi yetu ikiwemo kushiriki kwenye tukio hili.

4. Tume ya Taifa ya Uchaguzi haijajibu mpaka sasa barua ya Katibu Mkuu ya tarehe 25 Novemba 2020 yenye kumb. Na. C/HQ/ADM/20/TU/05/14 ambapo alitaka maelezo ni nani alisaini barua na fomu za waliotangazwa kuwa wabunge wa viti maalum na kutupatia nakala ya nyaraka husika kwa ajili ya kuchukua hatua kwa kuzingatia kuwa Kamati Kuu haijawahi kufanya uteuzi wala Katibu Mkuu hajawahi kuwasilisha orodha ya majina katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

5. Kwa sasa na kwa siku zijazo, agenda kuu ya chama chetu ni kuhakikisha tunapata Katiba Mpya itakayotengeneza mfumo huru na wa kidemokrasia wa uchaguzi kwa nchi yetu. Kushiriki katika mialiko na shughuli za Tume isiyokuwa huru ni kuipa baraka za kisiasa Tume hiyo, na kupunguza nguvu na ari ya jitihada za kufanya mabadiliko yanayohitajika katika nchi yetu.

Kutokana na sababu tajwa hapo juu Chama hakitatuma mwakilishi katika hafla hiyo na badala yake tutaendeleza nguvu kutetea Uhuru,Haki,demokrasia na Maendeleo ya watu.

Imetolewa Leo Ijumaa tarehe 20 Agosti,2021

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya NjeView attachment 1899771View attachment 1899772
 
Tumepokea mwaliko kutoka Kwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kwa ajili ya Mwenyekiti Taifa, Katibu Mkuu, aliyekuwa mgombea urais na aliyekuwa mgombea wa umakamu wa urais kuhudhuria hafla fupi ya kukabidhi kwa Rais taarifa ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Chama kupitia barua ya Katibu Mkuu kimemjulisha Mkurugenzi wa uchaguzi kuwa hatutashiriki hafla iliyopangwa kufanyika Ikulu tarehe 21 Agosti 2021 kwa sababu zifuatazo:

1. Hakukuwa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2020; kulikuwa na "Uchafuzi Mkuu" uliohusisha uporaji wa ridhaa ya wananchi kuchagua viongozi wao na ukiukwaji mkubwa wa sheria na haki. Kwa sababu ya kukosa uhuru kama taasisi, Tume ya Uchaguzi ilishiriki moja kwa moja katika kuharibu mchakato wa Uchaguzi Mkuu na kusababisha kuwa na "Uchafuzi Mkuu".

Sisi hatuwezi kushiriki kwenye tukio lolote litakalohalalisha Uchafuzi Mkuu huo mbele ya macho ya jamii ndani ya Tanzania na kimataifa.

2. Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe amepewa kesi ya kubambikiza ya ugaidi kwa sababu ya chuki za kisiasa dhidi yetu. Tunaelekeza nguvu na muda tulionao kufanya jitihada za kuhakikisha Mwenyekiti wetu na viongozi na wanachama wengine waliokamatwa kwa uonevu na wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wanaachiliwa huru.

3. Aliyekuwa mgombea urais wetu na Makamu Mwenyekiti wa chama Bara , Mheshimiwa Tundu Lissu, 'alilazimishwa kukimbilia nje ya nchi ' kwa sababu ya vitisho dhidi ya maisha yake vilivyofanywa na vyombo vya usalama au kwa ushiriki au baraka za vyombo hivyo.

Alikamatwa na Jeshi la Polisi akiwa nje ya Ubalozi wa Ujerumani, na isingekuwa wanadiplomasia wa Ofisi ya Ubalozi wa Ujerumani kuingilia kati angeweza kudhuriwa na Jeshi la Polisi.

Aidha, Mkuu wa Jeshi la Polisi amesema hadharani kwamba Mheshimiwa Lissu hatapatiwa ulinzi wowote wa polisi licha ya ukweli kwamba aliponea chupu chupu jaribio la mauaji la tarehe 7 September 2017, jaribio ambalo halijawahi kuchunguzwa na hatua stahiki kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

Bila kuhakikishiwa usalama na uhuru wake, ikiwemo kufutiwa kesi za uongo alizofunguliwa mahakamani kati ya 2016 na 2017, Mheshimiwa Lissu hajioni kuwa atakuwa salama kuweza kurudi nyumbani kushiriki kwenye shughuli za kisiasa za nchi yetu ikiwemo kushiriki kwenye tukio hili.

4. Tume ya Taifa ya Uchaguzi haijajibu mpaka sasa barua ya Katibu Mkuu ya tarehe 25 Novemba 2020 yenye kumb. Na. C/HQ/ADM/20/TU/05/14 ambapo alitaka maelezo ni nani alisaini barua na fomu za waliotangazwa kuwa wabunge wa viti maalum na kutupatia nakala ya nyaraka husika kwa ajili ya kuchukua hatua kwa kuzingatia kuwa Kamati Kuu haijawahi kufanya uteuzi wala Katibu Mkuu hajawahi kuwasilisha orodha ya majina katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

5. Kwa sasa na kwa siku zijazo, agenda kuu ya chama chetu ni kuhakikisha tunapata Katiba Mpya itakayotengeneza mfumo huru na wa kidemokrasia wa uchaguzi kwa nchi yetu. Kushiriki katika mialiko na shughuli za Tume isiyokuwa huru ni kuipa baraka za kisiasa Tume hiyo, na kupunguza nguvu na ari ya jitihada za kufanya mabadiliko yanayohitajika katika nchi yetu.

Kutokana na sababu tajwa hapo juu Chama hakitatuma mwakilishi katika hafla hiyo na badala yake tutaendeleza nguvu kutetea Uhuru,Haki,demokrasia na Maendeleo ya watu.

Imetolewa Leo Ijumaa tarehe 20 Agosti,2021

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya NjeView attachment 1899771View attachment 1899772
Mbeleko hiyo ya wanakijani ijibebe yenyewe au ibebwe na wanakijani kwani walikuwa mstari wa mbere kufanikisha uchafuzi mkuu na uchafuzi wa mitaa.
 
Ila uamuzi huo wa cdm umenifurahisha sana tena wamepinga kushiriki hafla hiyo kwa hoja mujarabu .Big up sana na mubarikiwe sana[emoji16][emoji16]
 
Tumepokea mwaliko kutoka Kwa Mkurugenzi wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Kwa ajili ya Mwenyekiti Taifa, Katibu Mkuu, aliyekuwa mgombea urais na aliyekuwa mgombea wa umakamu wa urais kuhudhuria hafla fupi ya kukabidhi kwa Rais taarifa ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020.

Chama kupitia barua ya Katibu Mkuu kimemjulisha Mkurugenzi wa uchaguzi kuwa hatutashiriki hafla iliyopangwa kufanyika Ikulu tarehe 21 Agosti 2021 kwa sababu zifuatazo:

1. Hakukuwa na Uchaguzi Mkuu mwaka 2020; kulikuwa na "Uchafuzi Mkuu" uliohusisha uporaji wa ridhaa ya wananchi kuchagua viongozi wao na ukiukwaji mkubwa wa sheria na haki. Kwa sababu ya kukosa uhuru kama taasisi, Tume ya Uchaguzi ilishiriki moja kwa moja katika kuharibu mchakato wa Uchaguzi Mkuu na kusababisha kuwa na "Uchafuzi Mkuu".

Sisi hatuwezi kushiriki kwenye tukio lolote litakalohalalisha Uchafuzi Mkuu huo mbele ya macho ya jamii ndani ya Tanzania na kimataifa.

2. Mwenyekiti wa Chama Taifa Mheshimiwa Freeman Mbowe amepewa kesi ya kubambikiza ya ugaidi kwa sababu ya chuki za kisiasa dhidi yetu. Tunaelekeza nguvu na muda tulionao kufanya jitihada za kuhakikisha Mwenyekiti wetu na viongozi na wanachama wengine waliokamatwa kwa uonevu na wanashikiliwa na Jeshi la Polisi wanaachiliwa huru.

3. Aliyekuwa mgombea urais wetu na Makamu Mwenyekiti wa chama Bara , Mheshimiwa Tundu Lissu, 'alilazimishwa kukimbilia nje ya nchi ' kwa sababu ya vitisho dhidi ya maisha yake vilivyofanywa na vyombo vya usalama au kwa ushiriki au baraka za vyombo hivyo.

Alikamatwa na Jeshi la Polisi akiwa nje ya Ubalozi wa Ujerumani, na isingekuwa wanadiplomasia wa Ofisi ya Ubalozi wa Ujerumani kuingilia kati angeweza kudhuriwa na Jeshi la Polisi.

Aidha, Mkuu wa Jeshi la Polisi amesema hadharani kwamba Mheshimiwa Lissu hatapatiwa ulinzi wowote wa polisi licha ya ukweli kwamba aliponea chupu chupu jaribio la mauaji la tarehe 7 September 2017, jaribio ambalo halijawahi kuchunguzwa na hatua stahiki kuchukuliwa dhidi ya wahusika.

Bila kuhakikishiwa usalama na uhuru wake, ikiwemo kufutiwa kesi za uongo alizofunguliwa mahakamani kati ya 2016 na 2017, Mheshimiwa Lissu hajioni kuwa atakuwa salama kuweza kurudi nyumbani kushiriki kwenye shughuli za kisiasa za nchi yetu ikiwemo kushiriki kwenye tukio hili.

4. Tume ya Taifa ya Uchaguzi haijajibu mpaka sasa barua ya Katibu Mkuu ya tarehe 25 Novemba 2020 yenye kumb. Na. C/HQ/ADM/20/TU/05/14 ambapo alitaka maelezo ni nani alisaini barua na fomu za waliotangazwa kuwa wabunge wa viti maalum na kutupatia nakala ya nyaraka husika kwa ajili ya kuchukua hatua kwa kuzingatia kuwa Kamati Kuu haijawahi kufanya uteuzi wala Katibu Mkuu hajawahi kuwasilisha orodha ya majina katika Tume ya Taifa ya Uchaguzi.

5. Kwa sasa na kwa siku zijazo, agenda kuu ya chama chetu ni kuhakikisha tunapata Katiba Mpya itakayotengeneza mfumo huru na wa kidemokrasia wa uchaguzi kwa nchi yetu. Kushiriki katika mialiko na shughuli za Tume isiyokuwa huru ni kuipa baraka za kisiasa Tume hiyo, na kupunguza nguvu na ari ya jitihada za kufanya mabadiliko yanayohitajika katika nchi yetu.

Kutokana na sababu tajwa hapo juu Chama hakitatuma mwakilishi katika hafla hiyo na badala yake tutaendeleza nguvu kutetea Uhuru,Haki,demokrasia na Maendeleo ya watu.

Imetolewa Leo Ijumaa tarehe 20 Agosti,2021

John Mrema

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya NjeView attachment 1899771View attachment 1899772
Hongereni sana Chadema.
Chama cha siasa kinapaswa kusimama kwa miguu yake na maono yake. Wakati wanaandaa mikakati ya hujuma walisahau kuwa ipo siku watawahitaji
 
Back
Top Bottom