CHADEMA kwa Magufuli mlilazimisha nchi iambiwe anaumwa nini ila kwa mwasisi wa chama chenu mnaheshimu haki ya usiri wa mgonjwa

CHADEMA kwa Magufuli mlilazimisha nchi iambiwe anaumwa nini ila kwa mwasisi wa chama chenu mnaheshimu haki ya usiri wa mgonjwa

comte

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2011
Posts
9,019
Reaction score
6,825
Mnyika amesema mzee Masinde pamoja na kutambua kuwa anaumwa ugonjwa huo lakini hakutaka ufahamike kwa familia na ndugu wa karibu ili kutozua taharuki na kuwafanya wakate tamaa.

===========
Akitoa salamu za rambirambi mbele ya familia ya marehemu, Mnyika amesema Masinde alifariki kwa ugonjwa wa saratani ya tezi dume aliougua kwa miaka mingi.

Mnyika amesema mzee Masinde pamoja na kutambua kuwa anaumwa ugonjwa huo lakini hakutaka ufahamike kwa familia na ndugu wa karibu ili kutozua taharuki na kuwafanya wakate tamaa.

"Wakati wote akiwa ospitalini alikuwa hataki kabisa tuzungumzie ugonjwa anaoumwa kwa sababu alijua kwamba umebainika ukiwa katika hatua ya mwisho. Hivyo alijua kwamba ni vigumu kutibika," amesema Mnyika.

Pia ameitaka familia, wanachama na viongozi wa chama hicho kumuenzi kiongozi huyo kwa kutimiza ndoto yake aliyoipambania kwa kipindi kirefu ya kujenga taasisi imara (Chadema), Katiba Mpya, Tume huru ya uchaguzi na kutumia maridhiano kuishinikiza serikali kufikia malengo hayo.

Mwananchi
 
..Magufuli alikuwa ni RAISI analishwa kwa kodi za umma.

..Kwa msingi huo Raisi ni mali ya nchi akiugua lazima wenye mali waelezwe.

..Hivyo ndivyo inavyofanyika ktk nchi zote zilizoendelea.

..Majuzi Mzee Biden alikwenda Hospitali kwa vipimo na Madaktari wake wakaeleza wananchi matokeo ya vipimo hivyo.
 
Mnyika amesema mzee Masinde pamoja na kutambua kuwa anaumwa ugonjwa huo lakini hakutaka ufahamike kwa familia na ndugu wa karibu ili kutozua taharuki na kuwafanya wakate tamaa...
Comte ni comte tu hata umpachike ubongo wa Albert Einstein bado atabaki na akili ile ya zaman!!! Tofautisha kati ya Rais na muasisi wa chama cha kisiasa!! Rais ni taasis kubwa world wide!!
 
Huyu sio rais wa nchi.

Taifa lolote lina maslahi na afya ya rais ndio maana watu wakata kujua kilicho msibu Magu.
 
Huko CCM, wengi hamnaga Akili?

Watu hawakutaka kujua JPM anaumwa nini, ila walitaka kujua yuko wapi.
Swadaktaaa!! Tuliambiwa haumwi yuko fit na anachapa kazi. Watanzania wakawa wakataka kujua yuko wapi? Maana alikuwa haonekani popote wala hafanyi chochote
 
Pole yao wafiwa... Mambo yao Chadema waachie wenyewe...
 
Back
Top Bottom