comte
JF-Expert Member
- Dec 11, 2011
- 9,019
- 6,825
Mnyika amesema mzee Masinde pamoja na kutambua kuwa anaumwa ugonjwa huo lakini hakutaka ufahamike kwa familia na ndugu wa karibu ili kutozua taharuki na kuwafanya wakate tamaa.
===========
Akitoa salamu za rambirambi mbele ya familia ya marehemu, Mnyika amesema Masinde alifariki kwa ugonjwa wa saratani ya tezi dume aliougua kwa miaka mingi.
Mnyika amesema mzee Masinde pamoja na kutambua kuwa anaumwa ugonjwa huo lakini hakutaka ufahamike kwa familia na ndugu wa karibu ili kutozua taharuki na kuwafanya wakate tamaa.
"Wakati wote akiwa ospitalini alikuwa hataki kabisa tuzungumzie ugonjwa anaoumwa kwa sababu alijua kwamba umebainika ukiwa katika hatua ya mwisho. Hivyo alijua kwamba ni vigumu kutibika," amesema Mnyika.
Pia ameitaka familia, wanachama na viongozi wa chama hicho kumuenzi kiongozi huyo kwa kutimiza ndoto yake aliyoipambania kwa kipindi kirefu ya kujenga taasisi imara (Chadema), Katiba Mpya, Tume huru ya uchaguzi na kutumia maridhiano kuishinikiza serikali kufikia malengo hayo.
Mwananchi
===========
Akitoa salamu za rambirambi mbele ya familia ya marehemu, Mnyika amesema Masinde alifariki kwa ugonjwa wa saratani ya tezi dume aliougua kwa miaka mingi.
Mnyika amesema mzee Masinde pamoja na kutambua kuwa anaumwa ugonjwa huo lakini hakutaka ufahamike kwa familia na ndugu wa karibu ili kutozua taharuki na kuwafanya wakate tamaa.
"Wakati wote akiwa ospitalini alikuwa hataki kabisa tuzungumzie ugonjwa anaoumwa kwa sababu alijua kwamba umebainika ukiwa katika hatua ya mwisho. Hivyo alijua kwamba ni vigumu kutibika," amesema Mnyika.
Pia ameitaka familia, wanachama na viongozi wa chama hicho kumuenzi kiongozi huyo kwa kutimiza ndoto yake aliyoipambania kwa kipindi kirefu ya kujenga taasisi imara (Chadema), Katiba Mpya, Tume huru ya uchaguzi na kutumia maridhiano kuishinikiza serikali kufikia malengo hayo.
Mwananchi