Uchaguzi 2020 CHADEMA kwa sera hii, mtakomba kura zote za wafanyakazi wa nchi hii, na haya ndio maneno tunayotaka kuyasikia yatayomuangusha Magufuli na CCM yake

Salary Slip

Platinum Member
Joined
Apr 3, 2012
Posts
49,390
Reaction score
152,301


Ushauri wangu:CHADEMA waandae na wasambaze kwa wingi vipeperushi vyenye sera hizi kuanzia kwenye madaladala,mabasi ya mikoani,sokoni,kwenye mabaa, na sehemu nyingine zozote zile zenye mikusanyiko ya watu wakati wa kampeni ukifika.

Msisahau pia swala la kupunguza PAYE pamoja na swala la kupunguza kama sio kufuta kabisa makato ya Bodi ya Mikopo.

Mkiondoa au kupunguza mashangingi serikalini,kufuta mbio za mwenge, na hata kupunguza au kuondoa kabisa sitting allowance za wabunge na mambo mengine, mnaweza pata fedha za kusomesha watoto wa masikini wa nchi bila kuwabagua kwa madaraja au kutokana na uwezo mzuri wa kifamilia kwa wale wanaotoka katika famila zinazojiweza/zenye unafuu wa kipato.

Sera nyingine ni kama hizi:





CCM must go!!
 
Ajira pia,ni pigo kubwa kwa serikali iliyopo madarakani,wanasisitiza viwanda,wakati vyuoni hasa vyuo vya kati na vyuo vikuu wanazalisha walimu wa sanaa na sayansi ambao hawaajiriwi viwandani.
 
Sijui ni kwanini Mimi ninaamini kwenye matumizi ya nguvu kuiondoa ccm kuliko hizi sera zenu? Hivi Kati yenu nani anaamini 2015 Magu alishinda uchaguzi? Chadema hawajaanza kuwa na sera nzuri leo, elimu bure pia ilikuwa sera ya chadema
 
Sijui ni kwanini Mimi ninaamini kwenye matumizi ya nguvu kuiondoa ccm kuliko hizi sera zenu? Hivi Kati yenu nani anaamini 2015 Magu alishinda uchaguzi?
Mashaka na hofu ya kuibiwa kura hata sisi wengine tunayo,ila ili uweze kudai kutangazwa mshindi au kuandamana kutaka alieshinda atangzawe mshindi,ni lazima kwanza uwe umepata kura nyingi kumshinda mpinzani wako(umeshinda uchaguzi) ndio unaweza kuwa na uhalali wa kutumia njia mbadala kudai haki yako.
 
Sijui ni kwanini Mimi ninaamini kwenye matumizi ya nguvu kuiondoa ccm kuliko hizi sera zenu? Hivi Kati yenu nani anaamini 2015 Magu alishinda uchaguzi? Chadema hawajaanza kuwa na sera nzuri leo, elimu bure pia ilikuwa sera ya chadema
alipata kura mil 3 unusu tu dhidi ya kura mil 10 alizopata mgombea wa UKAWA , haya Lowassa aliyajua na alitamka hadharani lakini baadaye akaufyata , bali usitegemee ujinga kama huo kutoka kwa Lissu , akidhulumiwa kibwege ni lazima pachimbike , hilo halina mjadala
 
Katika nchi ambayo matokeo ya urais yaliyotangazwa na tume hayapingwi mahakamani unatafuta uhalali wa nini? Kumbuka Chadema na wapinzani wengine wanakabiliana na serikali si ccm,katika mazingira ambayo serikali inafanya kazi za chama fulani,bila nguvu kutumika haiwezekani kubadiri huo mfumo
 
Mimi CCM ing'olewe kivyovyote vile,siwezi kufadhaishwa kwasababu kuwepo kwake madarakani sioni ninachofaidika zaidi ya kuona wengine wanafaidika.Hao wanaofaidika ndiyo waitetee ikiwezekana hata kifo.
 
Ili upate uhalali wa kutumia nguvu kama unavyosema, ni lazima kwanza uwe na uhakika umeibiwa kura vinginevyo kila mtu atakushangaa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…