CHADEMA kwawaka Moto! Mbowe arudi Dar!

Status
Not open for further replies.
Zitto lazima aende ktk kamati ili alitumikie taifa, muhimu kwake ni kuwa makini na muadilifu kwa taifa. Kwa kujitoa itakuwa kama mchezo wa kina zembwela tu!!!

Akiona kuna uzushi hapo ndipo anatakiwa ajitoe na kuweka mambo hadharani!! nafikiri hiyo ndio move inayohitajika! si mwakumbuka hata mzee ndesa aliachia ngazi!!!
 
kikwete is politician and zitto is just underground,from my point of view there is one winner on this...time will tell
 

Kama serikali haitaaanza longo longo mikataba na siri kibao za serikali zikivuja na kuanikwa hapa JF kama kawaida, basi Zitto inabidi aingie humo kwenye hiyo ...... hata sijui jina lake
 
..Terms of Reference za hiyo Tume ni nini?

..Tume hii ina tofauti gani na Tume ya Dr.Jonas Kipokola?

..Mabere Marando aliteuliwa na Mwinyi kuingia kwenye Tume ya Nyalali. Kumbukumbu zangu zinaniambia alikataa. Nadhani Mabere hakukubaliana na terms of reference walizopewa na Raisi Mwinyi.

..Suala la kuangalia hapa ni kama Zitto anakubaliana na terms of reference za Tume hii ya Jaji Bomani.

..Zitto ana deni la kutueleza terms of reference ktk tume hii ni zipi na kama anakubaliana nazo.

..Maria Kejo Ndosi,Andrew Chenge ni mwanasheria tu. Hawa siyo wanaopanga royalty, kodi, na mambo mengine yanayohusu fedha na mapato ktk migodi.

..Mimi nalia na aliyekokotoa na kuja na formula ya kuuza madini kwa bei ya kutupa. Nina hakika mtu/mtaalamu huyo si mwanasheria.

NB:
 

Mzee Ndesa alipata faida gani, na uamuzi wake uliisaidia vipi Kamati hiyo?
 
habari za wakati huu salamu na amani iwe juu yenu.

Binafsi sioni sababu ya Zitto kujitokea kwenye kamati kwa sababu siioni mantiki hiyo ila kila mmoja ana mawazo yake na lazima mawazo hayo yaheshimiwe na wengine ambapo mimi ni mmoja wao ambaye nitaheshimu mawazo ya wengine lakini kwa mawazo yangu naona hakusa haja ya kujitoa.

Naomba nitoe mfano mmoja: mimi nikiwa namshutumu mwanamke fulani kwamba nyumba yake ni chafu na kuna vitendo vibaya ndani ya nyumba hiyo vinafanywa lakini pamoja na shutuma hizo sijawahi kuingia ndani ya nyumba hiyo kuthibitisha niliyosema mwanamke mwenyewe akanisikia ninavyomshutumu na akanambia kwamba shutuma ninazompa ni uongo mtupu na kama kweli basi akanitaka niingie ndani ya nyumba hiyo ili mwenyewe nithibitishe. sasa jee mimi nikatae kuingia ndani ya nyumba wakati mwenyewe ameniruhusu? naona hakuna sababu ya kukataa kwanza nitajifunza mengi niingiapo ndani ya nyumba hiyo pia nitapata kujua kwamba shutuma zile ni kweli au uongo? na kama kweli mimi nitajua kwamba nilisema kweli na kama uongo basi nitajua nijifunze kuchunguza jambo kabla ya kulisema.

lakini pia nitafahamu namna watu wanavyoishi ndnai ya nyumba ile na jinsi wanavyokaribisha wageni wao kutoka nje vipi wanawakirimu na vipi wanawapuuza nk. mengi tu si unajua tena kwenye nyumba kuna siri nyingi?

kwanza Zitto ni miongoni mwa wabunge wenye kuwa na wasi wasi na mikataba kwa maana hiyo akiwemo katika kamati hiyo itampatia nafasi ya kuondosha wasi wasi wake aliokuwa nao.
stonetowner
 
Mzee Ndesa alipata faida gani, na uamuzi wake uliisaidia vipi Kamati hiyo?

alifunua madudu mengi sana ambayo tusingeyajua kama asingekuwepo ikiwemo EL kumpigia simu Mengi kumpa taarifa za kuhongwa kwa kamati.

Nimesoma maoni yote kuhusu ushiriki wa Zitto kwenye hii forum na kwenye magazeti; sijaona hata mtu moja akitueleze kinagaubaga athari za ushiriki wa Zitto katika kamati hii kwa maslahi ya nchi. Yaani, tuelezeni jamani ni namna nchi, chadema na Zitto wataathirika kwa huyu mbunge machachari kushiriki katika hii kamati. Ebu msizunguke, wekeni pint, 1,2, 3..plainly.

PS: Mwanakijiji nimesoma makala yako ile ndefu kwenye Tanzania Daima, pamoja na uzuri wa makala hiyo sijaona kabisa makala yako ikijibu hizo dukuduku zangu hapo juu: taifa, chadema na Zitto wataathirikaje kwa Zitto kushiriki katika kamati hii?
 
Kitila,
kwenye kamati kuu uyaseme hayo hayo, by the way kumbukeni CUF ilizorota kwa ubinafsi wao, sasa chama makini hakijajifunza yaliyotokea CUF, ambo kila linalofanywa na CCM ni baya. wananchi wakakiadhibu hakuna mbunge hata mmoja bara.

Kuhusu mwanakijiji lisikupe shida ni itikadi yake ni lazima uiheshimu.
 
Mhh Kutawaka moto mwaka huu...ama kweli mwaka wa Shetani sio sisiemu wala Chadema
 
Kidumu Chama cha Chadema!

Wanaoneana wivu nini kwa "ulaji" wa Zitto?! kwi kwi kwiiiiii
Kumbe kuna Ulaji? Chadema wamesema wanafanya mkutano wao Jmosi.....wale wanachama walioko humu wanaweza wakatupa brief.Kuteuliwa kwa Zito si sawa na kama angeteuliwa Mwafrika wa Kike,Kada Mpinzani,Mchambuzi kwenye Tume ile? mbona imekuwa big deal saaana?
 

je nimekiuka sheria za JF ???? basi you will just have to deal with it !
Lunyungu angalau saa nyingine unaonega point lakini hapa akili zako nimeziona fupi mno, wee umesikia members hapa wanabishana na kada ama wanabishana na mada ??halafu inaelekea una chuki fulani hivi, etihabari za kucopy na paste, kwani hizo majority za habari zinatoka wapi ? sisemi zote, nasema majority, au ndio umemuona kada tu ? mimi sio mwandishi wa habari kukaa kuandika what i think, bali kama kitu kimeshaandikwa na magazeti mengine will it make sense to you mimi kuandika the same shyt again ?am doing what i can, not what you want me to do!
 

nyinyi wooote mnaosema kada ni mnazi sijui anapendelea ccm, inaonekana kama mna uoga fulani, now guess what ? let me use your fear and your energy to reach out my issues !
wakati naongelea hapa suala la watu kuwa upande mmoja wakati huo naungana na madai mengi ya chadema mlikuwa wapi ? sasa nipo upande wa ccm ndio mnaanza kuona tatizo eeh ? je sikusema kwamba hili tuala la kuangalia upande mmoja sio mzuri ? of course nilisema, lakini mliziba maskio na kuniona mie ovyo, na wengine wakanikejeli na kusema kada kwa nini wee usifanye hivyo unavyofanya hata watu wasipotaka, and guess what ? i did it by switching sides peke yangu and later on watu wakaanza kuongezeka na sasa mnaona changes mnaanza kunilalamikia, je hii ni haki kweli ?? nilipokuwa napiga kelele siku zote mlikuwa wapi ??

anyway sitaki kuharibu mada, so lets keep the flow of the thread flowing !
 

kibaya gani nilichokosea ??
 

inalekea wee mgeni hapa forum lakini kama ungekuwa pande gani nilikuwa from the beginning usingesemahaya unayosema sasa hivi ! usiband wagon mambo kwa kuwa fulani kasema hivi na wewe unafuata tu, jua nini nilichokuwa nasimamia from the beginning na utanielewa zaidi !
 


Hongera kwa kazi ngumu na ya kuonesha mfano!! sikujua ulifanya mambo haya peke yako... it must be very lonely and hard sometimes.. but keep on fighting!!
 

i said the same thing, sijui watu wanaogopa nini ! kama mie wananiona ni mnazi basi waache niwe hivyo maana i cant be who they want to be cuz am simply not that and vice versa !

watu wanaogopa mawazo tofauti ya watu, wanaogopa mambo chungu mzima !hata saa nyingine nashindwa kuelewa nini haswa wanaogopa !
 
Hongera kwa kazi ngumu na ya kuonesha mfano!! sikujua ulifanya mambo haya peke yako... it must be very lonely and hard sometimes.. but keep on fighting!!

asante, lakini pia hongera kama hii anastahili kupewa zitto baada ya yeye kuamua kubaki kwenye kamati ingawa wengi hawataki awemo ! shukrani !
mwanakijiji unajua ilikuwaje kipindi kile na nadhani wengi wageni hapa hupata wakati mgumu kuelewa kwa nini nipo hivi, lakini mnyonge mnyongeni haki yake mpeni, kama utaweza waeleze nilikuwa vipi !
 
 
jamani sasa nadhani mambo ya kuattack member badala ya mada sio mchezo mzuri, inaeleweka kabisa kwamba kwenye siasa kuna mchezo mchafu so naomba huo mchezo usitumike hapa JF ili kueneza chuki, wee kama unaona kada anacopy habari na kupaste,ni either uchangie or you simply walk away, sipo hapa kuona mada niliyoanzsisha imesomwa mara ngapi, imejibiwa mara ngapi, AS LONG AS MESSAGE SENT am ok, hata kama mkichunia everything i post, THATS OK with me, as long as naweza kujiexpress what i feel, and my views and GOOD TO GO !

tuendeleeni na mada na sio kada !
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…