CHADEMA kwawaka Moto! Mbowe arudi Dar!

CHADEMA kwawaka Moto! Mbowe arudi Dar!

Status
Not open for further replies.
sasa nimechoshwa wazee, mie naenda kula thanksgiving bana maeneo ya 718,212,914 ! kama tutakutana basi tukutane huko !

natoka !
 
jamani sasa nadhani mambo ya kuattack member badala ya mada sio mchezo mzuri, inaeleweka kabisa kwamba kwenye siasa kuna mchezo mchafu so naomba huo mchezo usitumike hapa JF ili kueneza chuki, wee kama unaona kada anacopy habari na kupaste,ni either uchangie or you simply walk away, sipo hapa kuona mada niliyoanzsisha imesomwa mara ngapi, imejibiwa mara ngapi, AS LONG AS MESSAGE SENT am ok, hata kama mkichunia everything i post, THATS OK with me, as long as naweza kujiexpress what i feel, and my views and GOOD TO GO !

tuendeleeni na mada na sio kada !


KADA PUMBA eeeeehhhh
 
ni kweli naongea PUMBA !

wee unakoboa nafaka zote kuanzia PUMBA hadi MASHUDU !
 
nyinyi wooote mnaosema kada ni mnazi sijui anapendelea ccm, inaonekana kama mna uoga fulani, now guess what ? let me use your fear and your energy to reach out my issues !
wakati naongelea hapa suala la watu kuwa upande mmoja wakati huo naungana na madai mengi ya chadema mlikuwa wapi ? sasa nipo upande wa ccm ndio mnaanza kuona tatizo eeh ? je sikusema kwamba hili tuala la kuangalia upande mmoja sio mzuri ? of course nilisema, lakini mliziba maskio na kuniona mie ovyo, na wengine wakanikejeli na kusema kada kwa nini wee usifanye hivyo unavyofanya hata watu wasipotaka, and guess what ? i did it by switching sides peke yangu and later on watu wakaanza kuongezeka na sasa mnaona changes mnaanza kunilalamikia, je hii ni haki kweli ?? nilipokuwa napiga kelele siku zote mlikuwa wapi ??

anyway sitaki kuharibu mada, so lets keep the flow of the thread flowing !

Talking about flip flopin
 
jamani sasa nadhani mambo ya kuattack member badala ya mada sio mchezo mzuri, inaeleweka kabisa kwamba kwenye siasa kuna mchezo mchafu so naomba huo mchezo usitumike hapa JF ili kueneza chuki, wee kama unaona kada anacopy habari na kupaste,ni either uchangie or you simply walk away, sipo hapa kuona mada niliyoanzsisha imesomwa mara ngapi, imejibiwa mara ngapi, AS LONG AS MESSAGE SENT am ok, hata kama mkichunia everything i post, THATS OK with me, as long as naweza kujiexpress what i feel, and my views and GOOD TO GO !

tuendeleeni na mada na sio kada !


karibu to my world, the world you helped to create.. wenzio walisemaga mkuki huwa unanoga sana ukirushwa kwa nguruwe....
 
Kitila,
kwenye kamati kuu uyaseme hayo hayo, by the way kumbukeni CUF ilizorota kwa ubinafsi wao, sasa chama makini hakijajifunza yaliyotokea CUF, ambo kila linalofanywa na CCM ni baya. wananchi wakakiadhibu hakuna mbunge hata mmoja bara.

Kuhusu mwanakijiji lisikupe shida ni itikadi yake ni lazima uiheshimu.

Kilitime wananchi hawajawaadhibu CUF, ni system... ndio inayoamua nani wampe nani wasimpe...Hujapata kuwa ktk top Layer ya CCM ujue nani ni threat Kwao...tuache hio...mada hapa ni juu ya zitto na Kamati na Sintofaham iliyoibuka Chadema.. Nawatakia Kikao Chema chadema, by the way Chadema wata loss nini? Zitoo has been out in Parliament, and has lost some cash...so this sub-commitee will pop up his pocket..
 
ooh, yeah ! you can have it escalate @mwanakijeijei !
 
Vyama vya upinzani CUF, TLP vyajadili kuhusu Zitto
*Wawaasa Chadema wazungumzie hoja ya msingi
* Wasema mjadala ulenge katika rasilimali za nchi

*Makani ataka Zitto aingie jikoni kupakua ukweli


Na Waandishi Wetu


VYAMA vya CUF na TLP, vimewataka viongozi wa Chadema kuacha kujadili uteuzi wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe katika kamati ya kuangalia upya mikataba ya uchimbaji madini nchini na badala yake kisisitize mjadala katika hoja ya msingi.


CUF na TLP, vimesema wanachopaswa Chadema na jamii kwa jumla hivi sasa ni kukijadili kuhusiana na suala zima la ufisadi katika rasilimali za nchi, badala ya kumjadili Zitto.


Akizungumza na Mwananchi ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa TLP Taifa Augustine Mrema, alisema kuwa Chadema na jamii hawapaswi kumzungumzia Zitto, badala yake wanachotakiwa kukifanya ni kuzungumzia hoja ya msingi na kutokubali kutolewa nje ya hoja hiyo.


?Ikiwa jamii na viongozi wa Chadema watakubali kutolewa nje ya hoja ya msingi ya ufisadi na kuingizwa katika kumjadili Zitto watakuwa wamekosea,? alisema Mrema.


Alisema uteuzi wa Zitto katika kamati hiyo sio suala la kujadili kwani angeweza kuchaguliwa yeyote, bali linalopaswa kujadiliwa ni dhamira ya Rais Jakaya Kikwete ya kuunda kamati hiyo.


Naye Kaimu Mkurugenzi wa Haki za Bindamu na Mahusiano na Umma wa CUF, Mbaralah Maharagande, alisema maoni tofauti yanayotolewa na viongozi wa Chadema kuhusiana na uteuzi wa Zitto kwenye kamati hiyo, ni ya mtu mmoja mmoja na sio kauli ya pamoja.


Alisema kinachopaswa kujadiliwa hivi sasa, ni kuhusu ufisadi katika matumizi ya rasilimali za nchi, mikataba yenye utata ya uchimbaji wa madini, ikiwa ni sehemu moja tu ya ufisadi huo hapa nchini.


?Suala sio kujadili uteuzi wa Zitto katika kamati ya madini, tusikubali kuchezewa hisia zetu kwa kutolewa nje ya hoja kuu, suala ni kwamba kamati haiwezi kutoa matunda yaliyokusudiwa?, alisema Maharagande.


Hata hivyo, Maharagande alisema ushirikiano wa vyama vya upinzani, wanatarajia kufanya mkutano wa pamoja ambapo kupitia mkutano huo watatoa tamko la pamoja juu ya kamati ya madini na uteuzi wa Zitto katika kamati hiyo.


Hata hivyo, wakati viongozi wa CUF na TLP wakisema hayo, Makani ambaye pia ni mmoja wa waasisi wa Chadema alisema jana kuwa anaunga mkono uteuzi wa Zitto, lakini akasema ana wasiwasi na baadhi ya watu kuwamo katika kamati hiyo kwa kuwa walishiriki katika kuandika mikataba ya madini.


Aliwataja wanakamati hao kuwa ni pamoja na mjumbe kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na mwingine kutoka Wizara ya Nishati na Madini ambao alisema walipaswa kuwa mashahidi zaidi kuliko kuwa wanakamati.


"Kuna uwezekano wa watu hao kuitetea mikataba waliyoshiriki kuitayarisha," alisema Makani.


Hata hivyo, alisema dosari hiyo haiwezi kuwa ya msingi kiasi cha kuamua kuisusa kamati nzima kutokana na umuhimu wa madini hapa nchini.


Alisema suala la madini ambayo ni miongoni mwa rasilimali za nchi, si jambo la siasa au itikadi na kwamba, Ilani ya Chadema ilikwishaeleza mapema kwamba, mikataba ya uchimbaji madini ina matatizo na kwa sababu hiyo, ndiyo iliyomfanya Zitto aipeleke hoja hiyo bungeni kwa kuwa alikuwa anatekeleza Ilani ya chama chake.


"Alitimiza wajibu wake kama mbunge," alisema Makani.


Kutokana na hali hiyo, alisema anaunga mkono uteuzi wa mbunge huyo kwenye kamati hiyo kwa asilimia mia moja kwa kuwa utamwezesha kuwa karibu zaidi, kupambanua na kubainisha ukweli juu ya yote yatakayoshughulikiwa na kamati hiyo.


"Kufuatana na hayo, sina tatizo la uteuzi wa Zitto kwenye kamati hiyo, sina tatizo kabisa. Zitto aingie jikoni na kupakua kwa sababu anatetea maslahi ya nchi," alisema Makani na kuongeza:


"(Zitto) Akiona wanakamati wanakwenda kinyume na msimamo ambao hauna maslahi ya nchi, atakuwa huru kuandika ripoti ya kutofautiana na ripoti itakayokuwa imeandikwa na kamati.


Wengine ambao wameshatamka wazi kwamba wanamuunga mkono, Zitto kuwako katika kamati hiyo ni pamoja na mwasisi wa Chadema, Edwin Mtei. Pia Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amenukuliwa na vyombo vya habari vya nje, akisema yeye binafsi haoni tatizo kwa Zitto kuwako katika kamati hiyo.


Tayari Mbowe, ameitisha kikao cha Kamati Kuu ambacho kinatarajiwa kufanyika Jumamosi kujadili pamoja na mambo mengine uteuzi wa Zitto katika kamati ya kupitia upya madini.


Novemba 13, Mwaka huu, Rais Kikwete alitangaza kuundwa kwa Kamati ya kupitia mikataba na sheria za madini na kuwateua wajumbe wa kamati hiyo iliyojumuisha wajumbe kutoka kambi ya upinzani akiwemo Zitto wa Chadema na Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP) ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo.


Tangu Rais Kikwete aunde kamati hiyo na kumteua Zitto kuwa mmoja wa wajumbe wake (kamati hiyo), baadhi ya watu, wakiwamo wafuasi wa chama hicho wakiongozwa na Mbunge wa Tarime (Chadema), Chacha Wangwe, wameripotiwa na vyombo vya mawasiliano na jamii wakipinga uteuzi huo wa Zitto kwa madai kwamba, unadhoofisha hoja za wapinzani na kujenga usaliti baina yao kuhusiana na suala la madini nchini.


Kamati hiyo yenye wajumbe 12, iko chini ya uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mstaafu, Jaji Mark Bomani.


Wengine wanaounda kamati hiyo, ni Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk Harrison Mwakyembe.


Wajumbe wengine, ni Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, PriceWaterHouseCoopers, David Tarimo ambaye ni mtaalamu wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo.


Imeandaliwa na Muhibu Said, Elizabeth Suleyman, Salim Said na Mwanaid Omary wa MUM.
 
Vyama vya upinzani CUF, TLP vyajadili kuhusu Zitto
*Wawaasa Chadema wazungumzie hoja ya msingi
* Wasema mjadala ulenge katika rasilimali za nchi

*Makani ataka Zitto aingie jikoni kupakua ukweli


Na Waandishi Wetu


VYAMA vya CUF na TLP, vimewataka viongozi wa Chadema kuacha kujadili uteuzi wa Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe katika kamati ya kuangalia upya mikataba ya uchimbaji madini nchini na badala yake kisisitize mjadala katika hoja ya msingi.


CUF na TLP, vimesema wanachopaswa Chadema na jamii kwa jumla hivi sasa ni kukijadili kuhusiana na suala zima la ufisadi katika rasilimali za nchi, badala ya kumjadili Zitto.


Akizungumza na Mwananchi ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Mwenyekiti wa TLP Taifa Augustine Mrema, alisema kuwa Chadema na jamii hawapaswi kumzungumzia Zitto, badala yake wanachotakiwa kukifanya ni kuzungumzia hoja ya msingi na kutokubali kutolewa nje ya hoja hiyo.


?Ikiwa jamii na viongozi wa Chadema watakubali kutolewa nje ya hoja ya msingi ya ufisadi na kuingizwa katika kumjadili Zitto watakuwa wamekosea,? alisema Mrema.


Alisema uteuzi wa Zitto katika kamati hiyo sio suala la kujadili kwani angeweza kuchaguliwa yeyote, bali linalopaswa kujadiliwa ni dhamira ya Rais Jakaya Kikwete ya kuunda kamati hiyo.


Naye Kaimu Mkurugenzi wa Haki za Bindamu na Mahusiano na Umma wa CUF, Mbaralah Maharagande, alisema maoni tofauti yanayotolewa na viongozi wa Chadema kuhusiana na uteuzi wa Zitto kwenye kamati hiyo, ni ya mtu mmoja mmoja na sio kauli ya pamoja.


Alisema kinachopaswa kujadiliwa hivi sasa, ni kuhusu ufisadi katika matumizi ya rasilimali za nchi, mikataba yenye utata ya uchimbaji wa madini, ikiwa ni sehemu moja tu ya ufisadi huo hapa nchini.


?Suala sio kujadili uteuzi wa Zitto katika kamati ya madini, tusikubali kuchezewa hisia zetu kwa kutolewa nje ya hoja kuu, suala ni kwamba kamati haiwezi kutoa matunda yaliyokusudiwa?, alisema Maharagande.


Hata hivyo, Maharagande alisema ushirikiano wa vyama vya upinzani, wanatarajia kufanya mkutano wa pamoja ambapo kupitia mkutano huo watatoa tamko la pamoja juu ya kamati ya madini na uteuzi wa Zitto katika kamati hiyo.


Hata hivyo, wakati viongozi wa CUF na TLP wakisema hayo, Makani ambaye pia ni mmoja wa waasisi wa Chadema alisema jana kuwa anaunga mkono uteuzi wa Zitto, lakini akasema ana wasiwasi na baadhi ya watu kuwamo katika kamati hiyo kwa kuwa walishiriki katika kuandika mikataba ya madini.


Aliwataja wanakamati hao kuwa ni pamoja na mjumbe kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (AG) na mwingine kutoka Wizara ya Nishati na Madini ambao alisema walipaswa kuwa mashahidi zaidi kuliko kuwa wanakamati.


"Kuna uwezekano wa watu hao kuitetea mikataba waliyoshiriki kuitayarisha," alisema Makani.


Hata hivyo, alisema dosari hiyo haiwezi kuwa ya msingi kiasi cha kuamua kuisusa kamati nzima kutokana na umuhimu wa madini hapa nchini.


Alisema suala la madini ambayo ni miongoni mwa rasilimali za nchi, si jambo la siasa au itikadi na kwamba, Ilani ya Chadema ilikwishaeleza mapema kwamba, mikataba ya uchimbaji madini ina matatizo na kwa sababu hiyo, ndiyo iliyomfanya Zitto aipeleke hoja hiyo bungeni kwa kuwa alikuwa anatekeleza Ilani ya chama chake.


"Alitimiza wajibu wake kama mbunge," alisema Makani.


Kutokana na hali hiyo, alisema anaunga mkono uteuzi wa mbunge huyo kwenye kamati hiyo kwa asilimia mia moja kwa kuwa utamwezesha kuwa karibu zaidi, kupambanua na kubainisha ukweli juu ya yote yatakayoshughulikiwa na kamati hiyo.


"Kufuatana na hayo, sina tatizo la uteuzi wa Zitto kwenye kamati hiyo, sina tatizo kabisa. Zitto aingie jikoni na kupakua kwa sababu anatetea maslahi ya nchi," alisema Makani na kuongeza:


"(Zitto) Akiona wanakamati wanakwenda kinyume na msimamo ambao hauna maslahi ya nchi, atakuwa huru kuandika ripoti ya kutofautiana na ripoti itakayokuwa imeandikwa na kamati.


Wengine ambao wameshatamka wazi kwamba wanamuunga mkono, Zitto kuwako katika kamati hiyo ni pamoja na mwasisi wa Chadema, Edwin Mtei. Pia Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amenukuliwa na vyombo vya habari vya nje, akisema yeye binafsi haoni tatizo kwa Zitto kuwako katika kamati hiyo.


Tayari Mbowe, ameitisha kikao cha Kamati Kuu ambacho kinatarajiwa kufanyika Jumamosi kujadili pamoja na mambo mengine uteuzi wa Zitto katika kamati ya kupitia upya madini.


Novemba 13, Mwaka huu, Rais Kikwete alitangaza kuundwa kwa Kamati ya kupitia mikataba na sheria za madini na kuwateua wajumbe wa kamati hiyo iliyojumuisha wajumbe kutoka kambi ya upinzani akiwemo Zitto wa Chadema na Mwenyekiti wa United Democratic Party (UDP) ambaye pia ni Mbunge wa Bariadi Mashariki, John Cheyo.


Tangu Rais Kikwete aunde kamati hiyo na kumteua Zitto kuwa mmoja wa wajumbe wake (kamati hiyo), baadhi ya watu, wakiwamo wafuasi wa chama hicho wakiongozwa na Mbunge wa Tarime (Chadema), Chacha Wangwe, wameripotiwa na vyombo vya mawasiliano na jamii wakipinga uteuzi huo wa Zitto kwa madai kwamba, unadhoofisha hoja za wapinzani na kujenga usaliti baina yao kuhusiana na suala la madini nchini.


Kamati hiyo yenye wajumbe 12, iko chini ya uenyekiti wa Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mstaafu, Jaji Mark Bomani.


Wengine wanaounda kamati hiyo, ni Mwanasheria wa Wizara ya Nishati na Madini, Salome Makange, Kamishina wa Sera Wizara ya Fedha, Mugisha Kamugisha, Mkurugenzi Msaidizi Idara ya Makazi Wizara ya Ardhi, Edward Kihundwa na Mbunge wa Kyela (CCM), Dk Harrison Mwakyembe.


Wajumbe wengine, ni Mbunge wa Msalala (CCM), Ezekiel Maige, Peter Machunde kutoka Soko la Hisa, Dar es Salaam (DSE), Mkaguzi wa Mahesabu kutoka Kampuni ya Kimataifa ya Ukaguzi wa Mahesabu, PriceWaterHouseCoopers, David Tarimo ambaye ni mtaalamu wa masuala ya kodi na Mkurugenzi wa Madai na Sheria za Kimataifa, Wizara ya Katiba na Sheria, Maria Kejo.


Imeandaliwa na Muhibu Said, Elizabeth Suleyman, Salim Said na Mwanaid Omary wa MUM.


Source: Mwananchi
 
alifunua madudu mengi sana ambayo tusingeyajua kama asingekuwepo ikiwemo EL kumpigia simu Mengi kumpa taarifa za kuhongwa kwa kamati.

Nimesoma maoni yote kuhusu ushiriki wa Zitto kwenye hii forum na kwenye magazeti; sijaona hata mtu moja akitueleze kinagaubaga athari za ushiriki wa Zitto katika kamati hii kwa maslahi ya nchi. Yaani, tuelezeni jamani ni namna nchi, chadema na Zitto wataathirika kwa huyu mbunge machachari kushiriki katika hii kamati. Ebu msizunguke, wekeni pint, 1,2, 3..plainly.

PS: Mwanakijiji nimesoma makala yako ile ndefu kwenye Tanzania Daima, pamoja na uzuri wa makala hiyo sijaona kabisa makala yako ikijibu hizo dukuduku zangu hapo juu: taifa, chadema na Zitto wataathirikaje kwa Zitto kushiriki katika kamati hii?

Kitila Mkumbo,

Kuna Maswali ya msingi ambayo yanaulizwa kama:


  • 1. Nini kimeundwa - kuna watu wanadai kamati, wengine tume, na wengine wanaaiita tume teule.

    2. Kazi na mamlaka ya tume ni nini?

    3. Nguvu ya kisheria ya tume ni ipi. Wakijua kuna uovu na wizi, je watafanya nini?

    4. Kama hii ni tume kama nyingine nyingi zilizopita ambazo hazikuzaa chochote zaidi ya kula mapesa ya wananchi, kuna sababu gani ya hii tume kuundwa?

    5. Imejulikana kuwa kamati ya bunge ina nguvu kuliko tume za rais, kwa nini upinzani wasipush kwa kamati huru ya huru bunge?

    6. Nini kazi ya Machunde, Mama Kejo, na Mwakyembe kwenye hii kamati/tume/usanii - hasa ukichukulia historia za hao wawili?


Maswali haya na baadhi ya yanayoulizwa hapa ni part ya demokrasia na nivizuri Chadema na wadau wengine wakubaliane namna ya kulinda maslahi ya nchi maana inaonekana ccm wanauza nchi na hawatoi nafasi ya mijadala kwenye chama chao.

Mimi ninapinga uundwaji wa hii ... hata sijui jina lake ila sina uwezo wa kumuamulia Zitto cha kufanya.

Ukweli ni kuwa, kama Zitto akienda huko na akazidiwa nguvu na spin master -Mwakyembe na akapitisha mambo yasiyofaa kwa nchi, namuhakikishia from the begining kuwa asitegemee ize ride hapa JF na kutoka vyombo vya habari vya kweli vya nyumbani.
 
Mheshimiwa Spika, utata huu ambao umegubika sekta hii ya madini unaweza kufafanuliwa na Bunge lako Tukufu kupitia Kamati Teule. Kamati Teule ya Bunge ichunguze upitiaji wa mikataba hii na kuona kama kuna vitendo vyovyote vya uvunjaji wa sheria za nchi na kupotea kwa mapato ya Serikali na ufisadi.
Mheshimiwa Spika, suala hili ni suala la kitaifa. Halina hata chembe ya itikadi za kivyama. Naamini Wabunge wataamua kwa maslahi ya Taifa letu. Uundwaji wa Kamati Teule ya Bunge kuchunguza mapitio ya mikataba ya madini na mazingira ya kusainiwa kwa mkataba mpya wa Buzwagi utatoa msaada mkubwa kwa azma ya Rais wetu, Ndugu Jakaya Mrisho Kikwete ya kuona rasilimali za madini zinafaidisha nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, ninaomba kutoa hoja.

Hiki ndicho alichokitaka Zitto Bungeni, swali je ndicho alichokipata?
 
heheee, nimeifumani na hii tena !


Zitto ageuka mada




na Irene Mark



UAMUZI wa Rais Jakaya Kikwete kumteua Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, kuwa mjumbe wa kamati ya kuhakiki madini, umezidi kuchukua sura mpya, zinazotofautiana kila kukicha.
Hali hiyo imejidhihirisha tangu baadhi ya makundi ya watu wenye ushawishi, kuanza kuhoji kile kilichosababisha kuwamo kwa mwanasiasa huyo wa upinzani ndani ya kamati hiyo, Tanzania Daima imebaini.

Taarifa zilizokusanywa na gazeti hili kutoka vyanzo mbalimbali vya habari huru na vile vyenye masilahi tofauti katika suala hili, zinaonyesha kwamba, hoja hiyo sasa ndiyo inayogusa hisia za makundi yenye ushawishi katika jamii.

Aidha, mwenendo huo wa mambo, ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) anakotoka Zitto, umesababisha kuibuka na kuendelea kuimarika kwa makundi yenye mtazamo na mwelekeo unaopingana.

Hali hiyo ya mambo ambayo imepewa tafsiri tofauti na watu na vyombo mbalimbali vya habari, sasa imesababisha CHADEMA ilazimike kuchukua hatua za haraka kudhibiti mwelekeo wa mambo ambao kwa hakika unakiweka chama hicho katika hatari ya kuyumba, na kama hali isipodhibitiwa, kwenda kule ilikokwenda NCCR-Mageuzi miaka takriban 10 iliyopita.

Msimamo wa wanasiasa kadhaa ndani ya chama hicho unaoonyesha hali ya kutoaminiana na kupingana waziwazi, sasa umesababisha uongozi wa juu wa chama hicho, ukiongozwa na Mwenyekiti wake wa taifa, Freeman Mbowe, kuamua kuingilia kati ili kurejesha utulivu na mshikamano.

Habari kutoka ndani ya chama hicho ambazo zimethibitishwa na Mbowe na Katibu Mkuu wake, Willbrod Slaa, zinaeleza kuwa kwa siku nzima jana viongozi wote wakuu wa CHADEMA walitumia siku nzima kuwasiliana na kuwekana sawa kuhusu kimbunga cha kisiasa kinachoonekana kukikumba chama chao.

Wakati viongozi hao wakitafakari hatima ya chama hicho, wanahabari wa ndani na wale wa mashirika ya kimataifa ya habari kama lile la Uingereza (BBC) na la Ujerumani (DW) walikuwa wakihaha kuwasaka viongozi wakuu wa chama hicho ambao wamesambaa katika maeneo mbalimbali.

Miongoni mwa viongozi ambao walikuwa wakisakwa kwa udi na uvumba, ni Mbowe ambaye sasa yuko masomoni Uingereza akisomea siasa, uchumi na filosofia katika Chuo Kikuu cha Hull.

Kutokana na hali hiyo tete, Mbowe jana aliihakikishia Tanzania Daima kuwa, alikuwa amelazimika kurejea nyumbani na kuitisha kikao cha Kamati Kuu ya dharura ya chama hicho, lengo likiwa ni kufikia uamuzi wa pamoja utakaomaliza mzozo wa maneno kuhusu uteuzi huo wa Zitto.

Kikubwa kilichosababisha kurejea kwa Mbowe, ni kuibuka kwa mvutano wa mawazo ndani ya chama hicho yakihusisha makada wenye majina makubwa ndani ya CHADEMA ambao ama wanamuunga mkono Zitto au wanamtaka ajitoe katika kamati hiyo.

Akizungumza katika mahojiano kwa njia ya simu jana, Mbowe hakuwa tayari kutoa maoni yake kuhusu suala hilo zaidi ya kusema kwamba, chama hicho kilikuwa kikitarajia kutoa tamko lake rasmi Jumamosi wiki hii.

Mjumbe mmoja wa Kamati Kuu ya CHADEMA aliieleza Tanzania Daima kwamba, uamuzi wa kuitisha kikao hicho umekuja baada ya kubaini kuwapo kwa mpango mahususi kutoka kwa mahasimu wao wa kisiasa unaolenga kukisambaratisha chama chao, ambacho katika siku za hivi karibuni kimejijengea umaarufu mkubwa machoni mwa wananchi.

"Tunafahamu kwamba, hawa mahasimu wetu wanataka kutugombanisha kwa kutumia uteuzi huu wa Zitto. Ni jambo la bahati mbaya kwamba na sisi tumeingia katika mtego wao na tunacheza ngoma ya kujimaliza wenyewe," alisema kada huyo wa CHADEMA.

Akizungumzia mwenendo na misimamo ya baadhi ya wana CHADEMA, muasisi wa chama hicho, Edwin Mtei, alisema hakuna sababu ya Zitto kujiondoa ndani ya kamati hiyo, na akasisitiza kuwa chama hicho kinapaswa kutumia nafasi hiyo kuwasilisha maoni yake serikalini.

Alisema, CHADEMA ni mkusanyiko wa watu wengi, hivyo mawazo ya watu yanapokewa na kujadiliwa kwa mtazamo mpana zaidi, ili kuifikisha nchi kwenye maendeleo yanayotakiwa.

Alionya kuwa ni vigumu kuendesha nchi kwa kususia, badala yake aliwataka walio kwenye makundi kutoa mawazo ndani ya kamati husika za chama kwa ujasiri na uwazi.

"Tangu tulipounda chama tunaamini katika uwazi na ukweli lakini ‘view' zetu zinakuwa ‘recorded' huwezi kurekodi kama tunasusa, ni vizuri kwamba Zitto amekubali kushiriki na kushawishi.

"Endapo mawazo yake yatakubalika, atakuwa ame-influence policy ya nchi yetu na kama atapuuzwa, anaweza akatoa minority report. Mchango wetu uwe ni wa kuchangia na si wa kususia," alisema Mtei.

Alisema: "Wanaosema kuna ‘vested interest' ni lazima wajue kuwa masilahi ya kwanza ni nchi yetu…kama kuna mtu anaogopa ‘views' zake zitakuwa influenced, hana msimamo."

Hata hivyo aliweka wazi kwamba amempelekea Zitto mawazo yake na hadidu rejea na akamtaka aendelee kupigania masilahi ya taifa ndani ya kamati.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa alikiri kuwa uongozi wa chama utakutana mwishoni mwa wiki kutoa msimamo kuhusu kamati ya madini iliyoteuliwa na Rais Kikwete.

"Kamati Kuu ya CHADEMA itakutana mwishoni mwa wiki kujadili suala la Zitto, lakini kubwa zaidi ni muundo mzima wa kazi za kamati ya madini iliyoteuliwa na Rais," alisisitiza Dk. Slaa ambaye msimamo wake kuhusu kamati hiyo umeacha maswali mengi.

Aidha, Mwenyekiti wa CHADEMA wa Mkoa wa Kigoma, Jaffari Kasisiko, aliupongeza uamuzi wa Rais Kikwete na kuongeza kuwa matokeo ya kamati hiyo yatawaongezea imani wananchi kutokana na mchanganyiko wa wajumbe wake.

"CHADEMA Kigoma, inapongeza uamuzi wa Rais Kikwete kwa sababu unaleta heshima kwa wapinzani…tumemshauri Zitto kutoa ushirikiano wa kutosha kwenye kamati hiyo bila kujiengua kama anavyoshauriwa na baadhi ya watu," alisema mwenyekiti huyo.

Naye, Jussa Ismail, kutoka Chama cha Wananchi, amewataka wanaomshauri Zitto kujitoa kwenye kamati hiyo waache, badala yake wajenge siasa za kistaarabu.

Alisema, iwapo wataendelea kumshinikiza kujiondoa kwenye kamati watamwathiri kisaikolojia na kumfanya ashindwe kutekeleza majukumu yake ndani ya kamati hiyo.

"Umefika wakati wa kujenga siasa za kistaarabu, haya yanayotokea yanawachanganya wananchi, kwani lengo letu tangu mwanzo ni kuundwa kwa kamati ya kuchunguza mikataba ya madini na kurekebisha sheria zinazohusu madini.

"Leo hii tukimwambia Zitto asiingie kwenye kamati ile ni kumchanganya. Kufanya hivyo ni kujishushia hadhi wapinzani na jamii itashindwa kutuelewa, tutaonekana tunayumba," alisema Ismail.

Aidha, amemtaka Zitto kuendelea na shughuli mbalimbali ndani ya kamati hiyo na si kuufanya uteuzi wake kuwa wa kisiasa, badala ya masilahi ya taifa.
 
Vita vya panzi furaha ya mwewe! I must take my hat off JK on this! Look at how Upinzani and us Wananchi are at each other's throat about Utezi wa Kabwe, while CCM and mafisadi wakipeta!

We have lost it guys! We do not know what we want anymore ila ulalamishi, kelele 500 na kuzunguka boma kama mbuzi wanaotaka kupata UHURU!

No one goes back and ask, the sole purpose of Kamati, its capabilities, the strategies or timeline! Kila kitu ni Zitto Kabwe, Maria Kejo, Mwakyembe etc.

CUF, TLP, CHADEMA are spending little money they have to have vikao vya Kamati Kuu na NEC kutafakari UTEUZI wa Kabwe!

GET A LIFE PEOPLE! Ripoti ya BOT karibu kumalizika nad everyone will forget about it while focusing on Uteuzi wa Kabew!

How about asking Ikulu for clarification on what will Kamati/Tume do? will it review all the past contracts? someone told me this is not the first time kuna Kamati za Madini! where is the report from General Mboma?

Let's ask the President what is the purpose of Kamati/TUme? is it to review the whole mining industry past, present and future or to review the contracts that exists? what powers does Kamati have? Does it have parliamentary Powers to subpoena anyone it needs to grill?

Or it is Kamati ya kula na kunywa?
 
UAMUZI wa Rais Jakaya Kikwete kumteua Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Kabwe Zitto, kuwa mjumbe wa kamati ya kuhakiki madini, umezidi kuchukua sura mpya, zinazotofautiana kila kukicha.
Hali hiyo imejidhihirisha tangu baadhi ya makundi ya watu wenye ushawishi, kuanza kuhoji kile kilichosababisha kuwamo kwa mwanasiasa huyo wa upinzani ndani ya kamati hiyo, Tanzania Daima imebaini.

Taarifa zilizokusanywa na gazeti hili kutoka vyanzo mbalimbali vya habari huru na vile vyenye masilahi tofauti katika suala hili, zinaonyesha kwamba, hoja hiyo sasa ndiyo inayogusa hisia za makundi yenye ushawishi katika jamii.

Aidha, mwenendo huo wa mambo, ndani ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) anakotoka Zitto, umesababisha kuibuka na kuendelea kuimarika kwa makundi yenye mtazamo na mwelekeo unaopingana.

Hali hiyo ya mambo ambayo imepewa tafsiri tofauti na watu na vyombo mbalimbali vya habari, sasa imesababisha CHADEMA ilazimike kuchukua hatua za haraka kudhibiti mwelekeo wa mambo ambao kwa hakika unakiweka chama hicho katika hatari ya kuyumba, na kama hali isipodhibitiwa, kwenda kule ilikokwenda NCCR-Mageuzi miaka takriban 10 iliyopita.

Msimamo wa wanasiasa kadhaa ndani ya chama hicho unaoonyesha hali ya kutoaminiana na kupingana waziwazi, sasa umesababisha uongozi wa juu wa chama hicho, ukiongozwa na Mwenyekiti wake wa taifa, Freeman Mbowe, kuamua kuingilia kati ili kurejesha utulivu na mshikamano.

Habari kutoka ndani ya chama hicho ambazo zimethibitishwa na Mbowe na Katibu Mkuu wake, Willbrod Slaa, zinaeleza kuwa kwa siku nzima jana viongozi wote wakuu wa CHADEMA walitumia siku nzima kuwasiliana na kuwekana sawa kuhusu kimbunga cha kisiasa kinachoonekana kukikumba chama chao.

Wakati viongozi hao wakitafakari hatima ya chama hicho, wanahabari wa ndani na wale wa mashirika ya kimataifa ya habari kama lile la Uingereza (BBC) na la Ujerumani (DW) walikuwa wakihaha kuwasaka viongozi wakuu wa chama hicho ambao wamesambaa katika maeneo mbalimbali.

Miongoni mwa viongozi ambao walikuwa wakisakwa kwa udi na uvumba, ni Mbowe ambaye sasa yuko masomoni Uingereza akisomea siasa, uchumi na filosofia katika Chuo Kikuu cha Hull.

Kutokana na hali hiyo tete, Mbowe jana aliihakikishia Tanzania Daima kuwa, alikuwa amelazimika kurejea nyumbani na kuitisha kikao cha Kamati Kuu ya dharura ya chama hicho, lengo likiwa ni kufikia uamuzi wa pamoja utakaomaliza mzozo wa maneno kuhusu uteuzi huo wa Zitto.

Kikubwa kilichosababisha kurejea kwa Mbowe, ni kuibuka kwa mvutano wa mawazo ndani ya chama hicho yakihusisha makada wenye majina makubwa ndani ya CHADEMA ambao ama wanamuunga mkono Zitto au wanamtaka ajitoe katika kamati hiyo.

Akizungumza katika mahojiano kwa njia ya simu jana, Mbowe hakuwa tayari kutoa maoni yake kuhusu suala hilo zaidi ya kusema kwamba, chama hicho kilikuwa kikitarajia kutoa tamko lake rasmi Jumamosi wiki hii.

Mjumbe mmoja wa Kamati Kuu ya CHADEMA aliieleza Tanzania Daima kwamba, uamuzi wa kuitisha kikao hicho umekuja baada ya kubaini kuwapo kwa mpango mahususi kutoka kwa mahasimu wao wa kisiasa unaolenga kukisambaratisha chama chao, ambacho katika siku za hivi karibuni kimejijengea umaarufu mkubwa machoni mwa wananchi.

“Tunafahamu kwamba, hawa mahasimu wetu wanataka kutugombanisha kwa kutumia uteuzi huu wa Zitto. Ni jambo la bahati mbaya kwamba na sisi tumeingia katika mtego wao na tunacheza ngoma ya kujimaliza wenyewe,” alisema kada huyo wa CHADEMA.

Akizungumzia mwenendo na misimamo ya baadhi ya wana CHADEMA, muasisi wa chama hicho, Edwin Mtei, alisema hakuna sababu ya Zitto kujiondoa ndani ya kamati hiyo, na akasisitiza kuwa chama hicho kinapaswa kutumia nafasi hiyo kuwasilisha maoni yake serikalini.

Alisema, CHADEMA ni mkusanyiko wa watu wengi, hivyo mawazo ya watu yanapokewa na kujadiliwa kwa mtazamo mpana zaidi, ili kuifikisha nchi kwenye maendeleo yanayotakiwa.

Alionya kuwa ni vigumu kuendesha nchi kwa kususia, badala yake aliwataka walio kwenye makundi kutoa mawazo ndani ya kamati husika za chama kwa ujasiri na uwazi.

“Tangu tulipounda chama tunaamini katika uwazi na ukweli lakini ‘view’ zetu zinakuwa ‘recorded’ huwezi kurekodi kama tunasusa, ni vizuri kwamba Zitto amekubali kushiriki na kushawishi.

“Endapo mawazo yake yatakubalika, atakuwa ame-influence policy ya nchi yetu na kama atapuuzwa, anaweza akatoa minority report. Mchango wetu uwe ni wa kuchangia na si wa kususia,” alisema Mtei.

Alisema: “Wanaosema kuna ‘vested interest’ ni lazima wajue kuwa masilahi ya kwanza ni nchi yetu…kama kuna mtu anaogopa ‘views’ zake zitakuwa influenced, hana msimamo.”

Hata hivyo aliweka wazi kwamba amempelekea Zitto mawazo yake na hadidu rejea na akamtaka aendelee kupigania masilahi ya taifa ndani ya kamati.

Kwa upande wake, Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk. Willbrod Slaa alikiri kuwa uongozi wa chama utakutana mwishoni mwa wiki kutoa msimamo kuhusu kamati ya madini iliyoteuliwa na Rais Kikwete.

“Kamati Kuu ya CHADEMA itakutana mwishoni mwa wiki kujadili suala la Zitto, lakini kubwa zaidi ni muundo mzima wa kazi za kamati ya madini iliyoteuliwa na Rais,” alisisitiza Dk. Slaa ambaye msimamo wake kuhusu kamati hiyo umeacha maswali mengi.

Aidha, Mwenyekiti wa CHADEMA wa Mkoa wa Kigoma, Jaffari Kasisiko, aliupongeza uamuzi wa Rais Kikwete na kuongeza kuwa matokeo ya kamati hiyo yatawaongezea imani wananchi kutokana na mchanganyiko wa wajumbe wake.

“CHADEMA Kigoma, inapongeza uamuzi wa Rais Kikwete kwa sababu unaleta heshima kwa wapinzani…tumemshauri Zitto kutoa ushirikiano wa kutosha kwenye kamati hiyo bila kujiengua kama anavyoshauriwa na baadhi ya watu,” alisema mwenyekiti huyo.

Naye, Jussa Ismail, kutoka Chama cha Wananchi, amewataka wanaomshauri Zitto kujitoa kwenye kamati hiyo waache, badala yake wajenge siasa za kistaarabu.

Alisema, iwapo wataendelea kumshinikiza kujiondoa kwenye kamati watamwathiri kisaikolojia na kumfanya ashindwe kutekeleza majukumu yake ndani ya kamati hiyo.

“Umefika wakati wa kujenga siasa za kistaarabu, haya yanayotokea yanawachanganya wananchi, kwani lengo letu tangu mwanzo ni kuundwa kwa kamati ya kuchunguza mikataba ya madini na kurekebisha sheria zinazohusu madini.

“Leo hii tukimwambia Zitto asiingie kwenye kamati ile ni kumchanganya. Kufanya hivyo ni kujishushia hadhi wapinzani na jamii itashindwa kutuelewa, tutaonekana tunayumba,” alisema Ismail.

Aidha, amemtaka Zitto kuendelea na shughuli mbalimbali ndani ya kamati hiyo na si kuufanya uteuzi wake kuwa wa kisiasa, badala ya masilahi ya taifa.

Hapa ndipo CHADEMA wanaonyesha namna walivyoimara katika demokrasia. Hakuna mambo ya ndio mzee au kupitisha kila kitu kivyama bila kuwa na debate kali.

Kama ccm wangekuwa na debates kama hizi ndani ya vyama basi nina hakika nchi isingekuwa inaliwa na wachache every other day.

This is what I predicted. Hatimaye hata Zitto akiingia huko basi atajua kabisa kuwa wananchi wanataka vitendo na sio kuburuzwa.

I like this democracy. CHADEMA endelezeni debate ili mambo yote msingi yakubaliwe kabla ya kuuingia mkenge wa spinner Mwakyembe
 
Wana forum kwa mara nyingine tuko pamoja,kada mpinzani tunashukuru kwa kuiposti mada hii hapa jf ili iweze kujadiliwa.Nimechelewa kidogo,ila nimefanikiwa kufuatlia maendeleo ya mada hii.Binafsi mpaka sasa naungana na MWAFRIKA WA KIKE kwa namna ambayo ameweza kuchangia mada hii na kulenga pointi muhimu ambazo zinaonyesha ukomavu wa hali ya juu wa namna ya kutafakari bila kufuata mkumbo.Ameosha kuwa ni "MWAFRIKA WA KIKE MWENYE PRINCIPLE"
Naunga mkono wanachadema kufanya kikao chao cha dharura kujadili mwenendo mzima wa hili sakata la hi...(nakubaliana na mwafrika wa kike kuwa hatujui kama ni tume,kamati,nk.)ILA SASA WAKATI NAKWENDA KWENYE POINT INABIDI NIZUNGUMZE KWA HERUFI KUBWA;
1)KWANZA HII KAMATI NI YA NINI?EVERYBODY KNOWS KWAMBA SHERIA ZA MIKATABA YA MADINI NI MBOVU,ILO LIKO WAZI!SASA HII KAMATI NI YA NINI?KAMA NI YA KUREKEBISHA HIZO SHERIA THEN HILO LIWE WAZI!
2)KABLA YA KUUNDWA KWA KAMATI HIYO SUALA LA MSINGI HALIKUWA SHERIA ZINAZOLINDA MIKATABA,BALI SUALA LA MSINGI LILIKUWA NI PERSONAL INETEREST WAKATI WA UTIAJI SAINI WA MIKATABA HIYO,KWA MAANA HALISI NA AMMARUFU HIVI SASA "UFISADI"KAMA UPINZANI NA SRIKALI KWA UJUMLA WAMEAMUA KUBADILSHA AMA KUZIPITIA HIZO SHERIA THEN WAWEKE WAZI KUWA SASA WAKO PAMOJA NA HIVYO TUSAHAU MAMBO YA UFISADI,KWANI NIMESOMA MAKALA MOJA IKIDAI KUWA KAMATI HII SI YA KUTAFUTA WACHAWI NDIO MAANA IMEWASHIRIKISHA WATU AMBAO AWALI WALIKUWA WAKIHUSISHWA NA KASHFA HIZO,AMA WENYE UHUSIANO NA WALIOHUSISHWA.HILO SIO SHIDA,TUNATAKA IWEPO KAULI YA WAZI KUTOKA SERIKALINI KWAMBA WAMEKUBALI KUBEBA LAWAMA ZA MIKATABA YOOTE MIBOVU,NA SASA WANAUNDA KAMATI YA KUIPITIA MIKATABA HIYO ILI KUTOA MAPENDEKEZO YA MAREKEBISHO.
3)KUTOKANA NA POINTI YANGU NAMBA MBILI NI WAZI KUWA HATA ZITTO MWENYEWE AMEKUBALI KUWA TATIZO HALIKUWA WAKINA KARAMAGI,BALI NI SHERIA ZILIZOTUNGWA TOKA MIAKA YA SABINI.ZITTO ANATAKIWA ALIWEKE HILO WAZI MBELE YA WANANCHI,WANACHAMA NA WAPENZI WAKE ILI KAMA ALIVYOSEMA MWAFRIKA WA KIKE "KISIJE KIKAMGEUKA"
4)KWASABABU SASA CHADEMA IMESHAINGIA KWENYE HUO MTEGO THEN NI MUHIMU SANA WAELEKEZE NGUVU ZAO KWENYE KIKAO HICHO CHA JUMAMOSI NA NINAWAPONGEZA CHADEMA NA MBOWE KWA UAMUZI HUO;ILA WATAKACHOJADILI SASA NDIO CHA KUZUNGUMZIA,BINAFSI NAFIKIRI NI MUHIMU AJENDA ZAO ZIKACONTAIN POINTI ZOTE ALIZOZITAJA MWAFRIKA WA KIKE,NA PIA NINA NYONGEZA;
a)JE HITIMISHO LA KAMATI HIYO LITAKUWA NA IMPACT GANI KWA CHAMA CHAO NA ZITTO KWA UJUMLA?
b)JE TUHUMA NA UFUATILIAJI WA SAKATA LA UFISADI LITAFIFISHWA NA SIASA ZA KAMTI HII?
c)NI MAMLAKA GANI KAMATI HII ILIYONAYO,JE ZITTO ANA UHURU KIASI GANI NDANI YA KAMATI HIYO,NANI MWENYEKITI,NANI NI NANI KWENYE KAMATI HIYO?
d)LASTLY;BINAFSI NAFIKIRI ZITTO HANA NJIA ZAIDI YA KUBAKI HUMO KAMATINI,UKITAKA KUSHINDA MATOPENI NI LAZIMA UCHEZE MATOPENI.ZITTO YUKO MATOPENI,ATEGEMEE UTELEZI,UCHAFU,UTEPETEPE NA HALI NYINGINEZO NYINGI TU UNAZOKUTANA NAZO MATPOPENI.CHA MUHIMU NI ASITETEREKE,ASIMAME IMARA,NA HISTORIA ITAMKUWA UPANDE WAKE.PENGINE ITAKUWA PIA NDIO MWANZO WA RAIS KUWEZA KUWASHIRIKISHA WADAU WA NCHI HII BILA KUJALI ITIKADI ZAO!ILA KIKWETE AMECHEZA DUME WALA SIO SIRI!
 
Kilitime wananchi hawajawaadhibu CUF, ni system... ndio inayoamua nani wampe nani wasimpe...Hujapata kuwa ktk top Layer ya CCM ujue nani ni threat Kwao...tuache hio...mada hapa ni juu ya zitto na Kamati na Sintofaham iliyoibuka Chadema..
Chuma,

Wakati tunaliacha hili, ukumbuke kwa kura walizopata CUF ni wa pili baada ya CCM lakini hawana Mbunge hata mmoja Tanzania Bara, hiyo system ya kuwaambia watu wasichague mbunge wa CUF naomba unimegee kidogo niifahamu maana hata TLP walikuwa/wana na at least Mbunge mmoja.

Ningeona ni jambo ya maana sana kama CHADEMA ingeweka agenda ya Zitto kama tu moja ya agenda zake kwenye vikao vya kamati kuu!!!

Lakini at kuitisha kikao cha kamati kuu kwa ajili ya issue ya Zitto, kwa maoni yangu ni wastage of resources, na sio hivyo tu bali kama kweli kuna uhuru wa maoni unaheshimiwa hapo CHADEMA si ndio hivyo tena kila mmoja ana wazo lake,,,kwa nini kutisha kikao ili kulazimisha mawazo yawe ya namna moja, kila mmoja aachwe aendelee na mawazo yake, maana hamna kanuni ya katiba ya CHADEMA imekiukwa!!! kama kungekuwa na kanuni ya katiba imekiukwa hili ndio ingekuwa misconduct ya kuitisha kikao... Na nadhani kwa chama tawala hili wako makini kutumia kanuni zao sana... kuliko kutumia utashi na hata ukitaka kutumia utashi unaelekezwa kwenye kanuni as well.

I smell something wrong somewhere, but you can polish as much as you can!!!
 
Hapa ndipo CHADEMA wanaonyesha namna walivyoimara katika demokrasia. Hakuna mambo ya ndio mzee au kupitisha kila kitu kivyama bila kuwa na debate kali.

Kama ccm wangekuwa na debates kama hizi ndani ya vyama basi nina hakika nchi isingekuwa inaliwa na wachache every other day.

This is what I predicted. Hatimaye hata Zitto akiingia huko basi atajua kabisa kuwa wananchi wanataka vitendo na sio kuburuzwa.

I like this democracy. CHADEMA endelezeni debate ili mambo yote msingi yakubaliwe kabla ya kuuingia mkenge wa spinner Mwakyembe
Mwafrika wa kike,
Heshima yako dada,hebu msaidie kupanua uwezo wake wa kufikiri huyu.
Hajui ni demokrasia gani ambayo tunaizungumzia.Huko kwao hawajazoea.And yet wanadai kutupa uhuru na demokrasia.Sijui utampa vipi mtu kitu usichokijua na usionacho.

Hawa wamezoea kuongoza kimazingaombwe ndio maana wakiona Tuna-debate wanaona tunagombana.
 
Tumshukuru Mungu kwa Zitto kuchaguliwa na tuombee afanye kazi yake kwa uaminifu na ushujaa. Tukianza kumshtumu atapoteza komfo. Ila cha muhimu ni kusubiria afanye utumbo ndio tuanze kumpa dozi. Kwa sasa tumkague, ni wakati bora wa kumkagua huyu mheshimiwa.
 
Ila lakini hawa jamaa wa CCM tukumbuke ni wajanja sana, hivyo Zitto apaswe kulitambua hilo. Manake kwa fununu nasikia wameplan kuanza na mkataba wa Buzwagi, if yes, then tujue kuwa wanatafuta kitu cha kummaliza kisiasa. So, he better be very careful kwa kila step na neno. Ajue anaowakagua, wasijemuonyesha mkataba feki kisha akatangaza kuwa alikosea kuishutumu CCM bungeni. Itakuwa ni aibu ya millenia na atajimaliza kisiasa kabisa. Hivyo awe makini, atambue ni mkataba upi feki na real. These guys are smart, si wajinga kiasi cha kumuweka kwenye kamati if hawajajiandaa cha kutosha.

Zitto my friend, be careful. Play karata zako kwa umakini wa hali ya juu. This is the golden chance ya wewe kuprove kuwa upinzani si kambi ndogo ya CCM kujipatia umaarufu.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom