CHADEMA kwawaka Moto! Mbowe arudi Dar!

CHADEMA kwawaka Moto! Mbowe arudi Dar!

Status
Not open for further replies.
Nono,

Ninazidi kusema, hebu sisi tuna vichwa gani hivi tusiosikia hata tukiguswa na Muumba wetu?

Ni lini tutatumia akili kidogo ili kukabiliana na changa moto zilizo mbele yetu?

Hebu kweli sisi watanzania ni Mazezeta kiasi hiki jamani?

Tusipoangalia tutaendelea kuwasindikiza CCM mpaka tutakapozikwa hiki kizazi, haiwezekani tukose mikakati na maandalizi ya 2010, tunazidi kupiga soga na wakati unazidi kusonga

Maswari ya kujiuliza :

(a) Ni kweli tumejiandaa 2010 kupambana na hawa Mafisadi CCM?


(B) Watanzania watakuwa tayari kuumpa M/kiti wetu kura ili aiongoze inchi hii? na kwa kuwa hawa mafisadi wameanza kampeni za kumchafua, ni kwa nini tusiwe na mkakati ndani ya chama kwa maslahi ya Taifa?

Ninazidi kusema, upenzi na ushabiki usiozingatia Maslahi ya Taifa ni jambo la kipuuzi sana, tunaomba watanzania wenzetu tuwe na mikakati ya 2010, hii ni pamoja na kuwapata wabunge wa upinzani wa kutosha.

Naomba mtambue hivi, CCM mikakati yao ni kuona wanayarudisha Majimbo yote ya Upinzani huku Tanzania bara, na hiyo ndiyo itapelekea kuua upinzani, tutie akili jamani.

Lakini naona kama ajenda yako ikowazi nayo ni kuiangamiza CHADEMA. Sio kweli kuwa una mikakati yakuipatia ushindi. Kwani CHADEMA imefikia hapa ilipo wakati gani?

Maslahi ya taifa unayozungumzia ni yepi? ni ya kuififisha CHADEMA, ili CCM ikose mtu wa kuikosoa na kuihoji. Vyama vinavyoitwa vya siasa Tanzania vipo vingi.

Mimi nadhani ungekuwa na hoja za msingi zingeweza kujadilika kuliko ajenda imbayo unaitumia kama vile unazungumzia maslahi ya mageuzi Tanzania kumbe kuyadhoofisha.

Mbowe kama binadamu kama wewe anamapungufu yake na pia ana strength zake, na siku zote watu wanapimwa kwa weekness zao na stregth zao. Kwanini Mbowe leo aonekane kuwa kiongozi asiyetakiwa kwenye Mageuzi wakati huu ambapo CHADEMA wanaendelea kupata nguvu na kukubalika zaidi. Kwani Mbowe ameshika nafasi ya Mwenyekiti kwa kipindi kirefu kuliko nani kati viongozi wa vyama vya siasa, achilia mbali Kikwete. Tangu amepokea CHADEMA, ni mafanikio gani yaliyoonekana.

Ndio maana nikasema katika post iliyopita kuwa naamini kuwa CHADEMA kama chama watayatafakari misukosuko kama hii unayojaribu kuudanga umma ndani ya vikao vyao, lakini sio kuja kutafuta kuungwa mkono kwa hoja isiyokuwa na nguvu kwa maslahi ambayo yako dhahiri kuwa ni against CHADEMA.

Naamini Mbowe hana sababu yoyote ya kujiuzulu. Muda wake ukiisha vikao halali vya chama vitampima kama anafaa kuendelea na kama mwenyewe atakuwa ameomba, lakini sio kwa kupandikiziwa chuki za kuidhoofisha CHADEMA. Ndio mimi sio mwanachama wa CHADEMA lakini mtizamo wangu katika mada yako ni kuwa unamikakati ile ile ya kuisukasuka ili iporomoke kisiasa.
 
Hapa tusiwe na jasiba ndugu zangu, lengo letu ni kukifanya chama hiki chenye nguvu kwa sasa Tz bara kizidi kuwa na mwelekeo.
Na kwa kuwa jana muungano wa vyama vya upinzani (CUF, TLP NA NCCR) wamekanusha yale Zitto aliyokanusha kuwa Tarime hakukuwa na fujo badala yake wapinzani hao kwa pamoja wamesema kuwa kulikuwa na fujo, basi tunaweza kusema vyama hivi havina nia njema na CHADEMA, Na kwa kuwa mafisadi tayari wameshajipanga kufanya wanavyoweza kukipiga chini chama hiki, sasa basi naona ni vema Mbowe akatangaza kuwa amejiuzulu ili waendelee na uchunguzi wao

LENGO LENU WEWE NA NANI?
Hivi ina maana JF ni taasisi ya chadema? nifananulieni jamani nisije kuwa nimeingia choo cha kiki/kiume kwa kujiunga humu.

Kwa ufupi bila kujali itikadi yangu na wafuasi wangu nwasiokufungamana na upande wowote, nadhani kujiuzuRu ni kushindwa vita na sio ushauri mzuri kwa wapiganaji na watarajiwa.
NI HAYO TU
 
LENGO LENU WEWE NA NANI?
Hivi ina maana JF ni taasisi ya chadema? nifananulieni jamani nisije kuwa nimeingia choo cha kiki/kiume kwa kujiunga humu.

Kwa ufupi bila kujali itikadi yangu na wafuasi wangu nwasiokufungamana na upande wowote, nadhani kujiuzuRu ni kushindwa vita na sio ushauri mzuri kwa wapiganaji na watarajiwa.
NI HAYO TU

Subiri tuwe wasindikizaji 2010............

Ninazidi kusema tumpate mtu atakae leta changamoto 2010......,

Najua nikisema hivyo akina halisi, na wengine wengi wenye mtizamo hasi mioyo inataka kuchomoka.

Ila kwa kufanya hivyo ndipo tunaweza kufika tunapotaka kwenda.
 
Hapa tusiwe na jasiba ndugu zangu, lengo letu ni kukifanya chama hiki chenye nguvu kwa sasa Tz bara kizidi kuwa na mwelekeo.
Na kwa kuwa jana muungano wa vyama vya upinzani (CUF, TLP NA NCCR) wamekanusha yale Zitto aliyokanusha kuwa Tarime hakukuwa na fujo badala yake wapinzani hao kwa pamoja wamesema kuwa kulikuwa na fujo, basi tunaweza kusema vyama hivi havina nia njema na CHADEMA, Na kwa kuwa mafisadi tayari wameshajipanga kufanya wanavyoweza kukipiga chini chama hiki, sasa basi naona ni vema Mbowe akatangaza kuwa amejiuzulu ili waendelee na uchunguzi wao

Watu hawana jazba,problem thread haina nyama za kutosha.Mafisadi gani? hiyo sio sababu au wewe CCM nini? una uhakika gani kuwa vyama hivyo kuwa vina nia mbaya na chadema,tuna taka analysis zenye mashiko.Vina nia mbya na chadema kama chama au mtu(Mbowe).Mbowe aki resign then? wewe kwa maoni yako badala ya mbowe tumuweke nani?
 
Kumbukeni MBOWE siyo CHADEMA,Na CHADEMA siyo MBOWE! Chadema ni chama na Mbowe ni kiongozi aliyechaguliwa tu,Wala siyo alijitolea madaraka!!A
 
Kumbukeni MBOWE siyo CHADEMA,Na CHADEMA siyo MBOWE! Chadema ni chama na Mbowe ni kiongozi aliyechaguliwa tu,Wala siyo alijitolea madaraka!!Akijiuzulu leo tukakuchagua wewe kuwa Mwenyekiti mathalani muono wako ni upi wa kukifanya CHADEMA kishinde uchaguzi na kushika uongozi wa Tanzania 2010?Kama unalo jibu linalojitosheleza basi nakushauri utakapofika wakati wa uchaguzi ndani ya CHADEMA ukachukue fomu.Eleza sera zako kama zina mafanikio basi CHADEMA kama chama cha maendeleo na Demokrasia kitakupa fursa ya kurusha karata yako.
Ama la basi ukiache chama na viongozi wake waliochaguliwa kihalali watimize malengo kama yalivyoainishwa kwenye katiba yao.

IsayaMwita mambo ya Tarime yana nafasi ndogo tu katika kukiongoza chama kama CHADEMA,Kumbuka Tarime ni sehemu ndogo sana ya Tanzania.
 
Hakika umenishangaza sana, unadhani kuwa mimi ni ccm, pole sana, CHADEMA ni chama cha kitaifa kwa sasa, chama chenye nguvu Tanzania bara, na hivyo mimi kutoa mawazo yangu kuwa Mbowe AJIUZULU NI Ili hao ccm wakose Mshiko, na si vinginevyo.

Usisahau wasomi wote wenye mlengo wa kushoto wote wanakiona CHADEMA kama mkombozi wao.

Ni kweli Mbowe amefanya makubwa sana hasa kukuza Demokrasia hapa nchini na kweli anakubalika sana ila kwa kuwa vijikashifa hivi vimeanza kumuandama ni bora sasa yeye akae pembeni akiache chama kisipate mtikisiko.
IsayaMwita,
Nami pia nitashukuru kupata ushauri wako uliouita wa Bure. Ili uwe ushauri ni vema ujitosheleze:
i) Utueleze kwa kina kujua hizo kashfa zinazomwandama ni zipi, ili kwanza zifanyiwe kazi kama zipo, kabla ya kutaka ajiuzulu. Ni ustaarabu tu, mtu anayetuhumiwa na yeye apewe nafasi ya kujitetea, kwa kuwa kumtaka ajiuzulu ni kumhukumu bila kumpa nafasi ya kujitetea jambo ambalo ni kinyume na Natural Justice.
ii) Kama wewe ni mpenzi wa Chadema, ningetegemea sana, ushauri huo uufikishe ofisini, angalau kwa mtu unayemwamini ili tujue hao maadui wetu ambao kwa bahati wewe umepata nafasi na fursa ya kuwafahamu ni kina nani. Si vema tukaogopa kivuli, na unapomfahamu adui yako una uwezo wa kujipanga vizuri. Kama uko mbali basi ni vema ukatafuta namna ya kutufikishia "nyeti" hizo, ili tuweze kuzifanyia kazi. Hapo nami na chama kizima tutakuchukua kama shujaa wetu, tutakupenda na kukuheshimu. Jambo zito kama hilo kwa manufaa ya Chama na Watanzania kwa ujumla, kama unavyosema unaamini Chadema ni chama mbadala unataka kukiokoa, sina shaka utatafuta njia sahihi ya kufikisha ujumbe huo mzito mahali panapostahili, na wala hutaishia hapa. Kama ukipenda kuyaweka yote JF au hadharani kwa njia nyingineyo utakayoona inafaa wala hatuna kipingamizi, kwani Chadema tumekwisha kutangaza kuwa hatuna tunachokificha. You will indeed take as a mile further in our struggle for Transparency in the National Institutions.
iii) Ni kutokana na hatua yako hiyo Wanachadema makini wataona umuhimu wa ushauri wako. Iwapo utatupa kwa njia ya siri sisi tutawafahamisha ili wapenzi wetu wasije wakaachwa tu kwenye mataa, na kama utaona ni siri isitoke nje, tutatafuta namna ya kuwajulisha bila kuathiri usiri huo. Nawatakia mjadala mwema, wala sina nia ya kufunga mjadala, bali nilitaka kutoa mwelekeo wenye tija wa mjadala. Thanks
 
LENGO LENU WEWE NA NANI?
Hivi ina maana JF ni taasisi ya chadema? nifananulieni jamani nisije kuwa nimeingia choo cha kiki/kiume kwa kujiunga humu.

Kwa ufupi bila kujali itikadi yangu na wafuasi wangu nwasiokufungamana na upande wowote, nadhani kujiuzuRu ni kushindwa vita na sio ushauri mzuri kwa wapiganaji na watarajiwa.
NI HAYO TU

Dhahiri hauhitaji hata kujitetea wewe CCM (nifananulieni jamani nisije kuwa nimeingia choo cha kiki/kiume kwa kujiunga humu) confirmes you mengine ni porojo tu ila undani wako uko hapo
 
Ndugu zangu wanaJF sisi sote tunafahamu kuwa sasa jamaa wameamka, wamecharuka kwa njia yoyote wanataka kufanya lolote lile ili kutokomeza upinzani Tanzania, na kwa kuwa Mbowe sasa anatazamwa kwa jicho la husuda na wapinzani wenzake na pia *** sasa ushauri wa bure mbowe akae pembeni ili chama kipone

JF mnalitazamaje hili?

We IsayaMwitaMaraanyaaa una yako binafsi kumutima. Inaonekana kama vile baadhi ya wanachama wa CHADEMA kutoka Mkoa wa Mapanga Shyaaaa wana ajenda zao za siri kuhusu Mbowe. Hivyo hizi ni propaganda za kumchafulia jina tu.

Hasira yenu kwa Mbowe bado haijaisha??? Mbona mna capacity kubwa ya kutunza hasira kwa muda mrefu hivyo???? Acheni kukigawa chama...lasivyo kitashindwa kutimiza malengo yake.

Nawashauri mkamwone daktari awaondolee capacity ya kutunza hasira kwa muda mrefu na badala yake ainstall capacity ya kupooza mambo yakawa shwari (baridi) kama makontainer ya barafu ili muwe na amani....hahahahaha....ukijinijibu..nakugecha.....
 
Kumbukeni MBOWE siyo CHADEMA,Na CHADEMA siyo MBOWE! Chadema ni chama na Mbowe ni kiongozi aliyechaguliwa tu,Wala siyo alijitolea madaraka!!Akijiuzulu leo tukakuchagua wewe kuwa Mwenyekiti mathalani muono wako ni upi wa kukifanya CHADEMA kishinde uchaguzi na kushika uongozi wa Tanzania 2010?Kama unalo jibu linalojitosheleza basi nakushauri utakapofika wakati wa uchaguzi ndani ya CHADEMA ukachukue fomu.Eleza sera zako kama zina mafanikio basi CHADEMA kama chama cha maendeleo na Demokrasia kitakupa fursa ya kurusha karata yako.
Ama la basi ukiache chama na viongozi wake waliochaguliwa kihalali watimize malengo kama yalivyoainishwa kwenye katiba yao.

IsayaMwita mambo ya Tarime yana nafasi ndogo tu katika kukiongoza chama kama CHADEMA,Kumbuka Tarime ni sehemu ndogo sana ya Tanzania.

kimatire;

My brother pole sana na fikra zako hizi zilizochakaa, najua wewe ni mpiga kelele usiyekuwa mtizamo chanya, hii inadhihilika tu mara tu baada ya kuchangia maada hii. Ninajua wewe ni kipenzi wa upinzani pasipozingatia yajayo, yaani unataka tuonekane kama ilivyokuwa 1995? Tulionekana kama tunanguvu kisha vikabuniwa vinjia kwa kuua upinzani vikafanyika kisha ndiyo tukaona wakina Mrema wakiwayawaya? Unamkumbuka Marando? Unamkumbuka Tambwe Hiza? wako wapi sasa?

Mimi sitamsahau Kabulu, Namkumbuka sana tena sana Da aaaaa!!!!!!!! Hebu yuko wapi?

Sikiliza kimatire; sisi ni wazelendo wenye uchungu na nchii hiii, hatuogopi kuwa sadaka hata kesho, wewe kalia hako kamkate ka wanawo na sisi tutaendelea kushauri na kuonyesha Mifano.

kimatire; kwa udhibitisho hou tungoje 2010 kama CCM hapa Mkoani (mara) watapata chochote,


Wenzenu wana Mara tutadhihirisha HILO 2010 na Mungu atusaidie.
 
IsayaMwita,
Nami pia nitashukuru kupata ushauri wako uliouita wa Bure. Ili uwe ushauri ni vema ujitosheleze:
i) Utueleze kwa kina kujua hizo kashfa zinazomwandama ni zipi, ili kwanza zifanyiwe kazi kama zipo, kabla ya kutaka ajiuzulu. Ni ustaarabu tu, mtu anayetuhumiwa na yeye apewe nafasi ya kujitetea, kwa kuwa kumtaka ajiuzulu ni kumhukumu bila kumpa nafasi ya kujitetea jambo ambalo ni kinyume na Natural Justice.
ii) Kama wewe ni mpenzi wa Chadema, ningetegemea sana, ushauri huo uufikishe ofisini, angalau kwa mtu unayemwamini ili tujue hao maadui wetu ambao kwa bahati wewe umepata nafasi na fursa ya kuwafahamu ni kina nani. Si vema tukaogopa kivuli, na unapomfahamu adui yako una uwezo wa kujipanga vizuri. Kama uko mbali basi ni vema ukatafuta namna ya kutufikishia "nyeti" hizo, ili tuweze kuzifanyia kazi. Hapo nami na chama kizima tutakuchukua kama shujaa wetu, tutakupenda na kukuheshimu. Jambo zito kama hilo kwa manufaa ya Chama na Watanzania kwa ujumla, kama unavyosema unaamini Chadema ni chama mbadala unataka kukiokoa, sina shaka utatafuta njia sahihi ya kufikisha ujumbe huo mzito mahali panapostahili, na wala hutaishia hapa. Kama ukipenda kuyaweka yote JF au hadharani kwa njia nyingineyo utakayoona inafaa wala hatuna kipingamizi, kwani Chadema tumekwisha kutangaza kuwa hatuna tunachokificha. You will indeed take as a mile further in our struggle for Transparency in the National Institutions.
iii) Ni kutokana na hatua yako hiyo Wanachadema makini wataona umuhimu wa ushauri wako. Iwapo utatupa kwa njia ya siri sisi tutawafahamisha ili wapenzi wetu wasije wakaachwa tu kwenye mataa, na kama utaona ni siri isitoke nje, tutatafuta namna ya kuwajulisha bila kuathiri usiri huo. Nawatakia mjadala mwema, wala sina nia ya kufunga mjadala, bali nilitaka kutoa mwelekeo wenye tija wa mjadala. Thanks


Dr.W.Slaa;

Mweshiwa Dr.W.Slaa; hakika nakuheshimu sana tena sana, hakika Tanzania hii na ijayo itaendelea kukumbuka na jinsi gani umeifanya Demokrasia kukua hapa Tanzania, nitakuwa mwizi wa fadhira kama sitawashukuru wabunge wate mnaoshirikiana katiak vita hii iliyo mbele yenu.

Dr.W.Slaa;ni kweli kuwa nimekuwa kila kukicha nikishauri Ndugu yetu Mbowe ajiweke Pembeni na kisha tumpate mtu Mbadala atakeye weza kuleta changamoto katika kinyang'anyiro 2010.

Dr.W.Slaa; najua unaweza kudhani huenda nina utindio wa ubongo ila haya ni mawazo yangu, na kama tutayaheshimu hakika tutakuwa na mshiko 2010. nimesoma mchango wako na ninauzingatia vlivyo, katika yote nuliyoyasema hapo mimi sipo, kuna vigezo viwili vitakavyomfanya mweshimiwa Mbowe 2010 chama kitakapompitisha kusimama nafasi ya urais ashindwe kufanya vizuri.

1. Elimu aliyonayo hakika kwa sasa haikidhi haja na hii itasababisha upungufu wa kura 2010.
2. Mweshimiwa Mbowe ni mfanya biashara, nadhani hapa hata kama atapata furusa ya kuwa Rais kuna uwezekano wa kutenganisha utawala na biashara zake,(comflict of interest)

Hizi ni baadhi ya sababu tu ,kwa kuwa chama hiki kwa sasa kina wasomi wengi sana na kwa kuwa kina sura ya kitaifa kwa sasa ni vema Mweshimiwa akapisha nafasi hiyo na ninyi viongozi wa juu mkatupa mtu mwenye haiba na mvuto kwa watanzania. Pia ni vema akawa na uwezo na akawa mbunifu ili chama hiki kikaendelea kukua.

Najua 2010 kama tutajipanga vema hakika tutafanya vizuri

Mungu ibariki Tanzania, Mungu kiimarishe chama hiki cha CHADEMA.
 
Dr Slaa,
Nimeona unachungulia kwenye hii thread. Nitakushangaa sana kama utaendelea kumjibu huyu isaya.
 
Dr Slaa,
Nimeona unachungulia kwenye hii thread. Nitakushangaa sana kama utaendelea kumjibu huyu isaya.

Hilo linatosha kukutambua kuwa haujua 2015 itakuwaje, hauelewi utashi wa mtu na pia sikuhukumu kwa lolote Mkuu.

Ninaelewa kuwa hisia zako zinakutuma kuwa mimi ni wa upande wa pili asante, ila ujue ni vema kutoainisha msimamo wako bila tija.
 
Isaya , nimegundua kuwa ulijiandikia bila kujua unataka kusema kitu gani maana unasema MBOWE ajiuzulu ili kukinusuru chama , wakati huo huo ulipotakiwa kuonyesha kashfa ambazo zinamwandama unakuja na sababu nyingine za kitoto sana ,

Ujumbe wako ulikuwa kuna kashfa sasa hapa unajifanya kuwa Sheikh Yahaya kutabiri eti itakuwa vigumu kutenganisha bioashara za Mbowe na Ikulu.

Jibu kashfa unazosema , ila kama unaendelea kupiga ramli inawezekana unalakwako jambo.

Kama huna majibu ni bora hii ikawekwa kwenye historia , kwani heading yako ukiisoma inavutia kweli eti kukinusuru chama wakati huna hoja .

Kama kweli wewe ni wa Tarime inawezekana siku unaandika ulikuwa tayari umeshaipata ile ya KIBASUKA.
 
Isaya , nimegundua kuwa ulijiandikia bila kujua unataka kusema kitu gani maana unasema MBOWE ajiuzulu ili kukinusuru chama , wakati huo huo ulipotakiwa kuonyesha kashfa ambazo zinamwandama unakuja na sababu nyingine za kitoto sana ,

Ujumbe wako ulikuwa kuna kashfa sasa hapa unajifanya kuwa Sheikh Yahaya kutabiri eti itakuwa vigumu kutenganisha bioashara za Mbowe na Ikulu.

Jibu kashfa unazosema , ila kama unaendelea kupiga ramli inawezekana unalakwako jambo.

Kama huna majibu ni bora hii ikawekwa kwenye historia , kwani heading yako ukiisoma inavutia kweli eti kukinusuru chama wakati huna hoja .

Kama kweli wewe ni wa Tarime inawezekana siku unaandika ulikuwa tayari umeshaipata ile ya KIBASUKA.

Mpaka Kieleweke;

Nashukuru sana mkuu kwa majibu yako mema yaliyo jaa hasira na chuki dhidi yangu, pia naomba utambue hii maada ilianza siku nyingi na ilianza tu baada ya kifo cha .... na baada ya hapo maada hii ilipotea hapa jamvini,

Mpaka Kieleweke;maada hii inarudi ikiwa na upya kwa maana ya kusisitiza yale niliyoyabaini hapo juu, ninajua hakika umeonesha msimamo wako na nia yako thabiti,ukiangalia kama tungekuwa karibu basi roho yangu ungeichukua.

Mpaka Kieleweke;naomba upunguze jazba kisha ufikiri kama ninayoyasema hayana mshiko basi unishauri tuifunge post hii na hii imenitia shaka sana hata kudhani kuna nini hadi ujibu kwa uchungu nanma hii?

Mpaka Kieleweke;Lakini usisahau kuwa chama hiki ni chetu sote tunaweza kushauri na kutoa mapendekezo sasa kama Mpaka Kieleweke; wewe baada ya kunihoji nini kifanyika na wewe unasimama nyuma ya muhusika hakika unanitia shaka.

Mpaka Kieleweke; wenzako hujibu kwa busara, nimefurahi kuwa wewe umetambua kuwa siku nabandika hapa hii post yangu nilikuwa tayari nimeshapata kabasuka, asante mkuu.
 
Dr Slaa,
Nimeona unachungulia kwenye hii thread. Nitakushangaa sana kama utaendelea kumjibu huyu isaya.
Gagnija,
Nakushukuru sana kwa ushauri wako. Hata hivyo, kwa vile kwenye jamvi hili sote tunaheshimiana nadhani ni vema tumejadili sana hoja hii. Tumesubiri Kashfa alizotaja mwenzetu kumtaka Mhe. Mbowe ajiuzulu. Sisi wengine tulikuwa tayari kuzipokea. Sembuse, ameisha kutujibu, na jibu lakehalionyeshi kama kuna kashfa kwani Elimu, ndogo au kubwa haiwezi kuwa Kashfa. Isipokuwa kwamba mwenzetu hajafanya utafiti wa kina na kutosha, tunafahamu sote, viongozi duniani walioendesha nchi zao, na kiwango chao cha elimu.
Naamini ni ustaarabu wa kawaida, kama IsayaMwita atahitimisha hoja yake sasa kwa kutueleza, baada ya kukosa hoja na kushindwa kufafanua kashfa anaeleza nini WanaJF?
 
Gagnija,
Nakushukuru sana kwa ushauri wako. Hata hivyo, kwa vile kwenye jamvi hili sote tunaheshimiana nadhani ni vema tumejadili sana hoja hii. Tumesubiri Kashfa alizotaja mwenzetu kumtaka Mhe. Mbowe ajiuzulu. Sisi wengine tulikuwa tayari kuzipokea. Sembuse, ameisha kutujibu, na jibu lakehalionyeshi kama kuna kashfa kwani Elimu, ndogo au kubwa haiwezi kuwa Kashfa. Isipokuwa kwamba mwenzetu hajafanya utafiti wa kina na kutosha, tunafahamu sote, viongozi duniani walioendesha nchi zao, na kiwango chao cha elimu.
Naamini ni ustaarabu wa kawaida, kama IsayaMwita atahitimisha hoja yake sasa kwa kutueleza, baada ya kukosa hoja na kushindwa kufafanua kashfa anaeleza nini WanaJF?

Dr.W.Slaa;

Dr.W.Slaa; nashukuru kwa ushauri wako ulioainisha hapo juu, na tena kwa moyo wa dhati napenda kuujulisha huu umma wa hapa jamvini kuwa naufunga mjadala huu kwa shingo upande, lakini nategemea kuwa mwenyekiti wetu ni msikivu.

Dr.W.Slaa;naomba utambue kuwa neno kujiuzulu huenda lilitumika vibaya na jinsi nilivyotaka kufikisha ujumbe kwa hadhira wangu, lakini sijui ni neno gani lingefaa hapa ili kuweza kumshauri Mweshimiwa Mbowe akajiweka pembeni.

Dr.W.Slaa; Ni kweli hoja yangu imekosa mshiko na hivyo naomba wanajamii forums waichukue hii maada kama changamoto kwetu na pia nadhani imekuwa ikifanya nikomae ktk hili ninaloliamini.

Maada hii ilipoanza ilionekana kama SHUBILI, walioichangia walikuwa waoga sana huku wakijipendekeza kwa muhusika bila kujali hoja iliyopo mezani

Mwisho nasema mUNGU IBARIKI TANZANIA
 
SISI makamanda wa CHADEMA tuko makini na tuna imani na Mbowe, hao wanaodai mbowe anatazamwa kwa jicho baya wa wapinzani...aaah mpinzani mwenyewe mbatia, tangu awe mwenyekiti chama hajawahi kushinda jimbo la uchaguzi, au mrema , huyu kaisha au unamaana ya kina Lipumba aah huyu msomi lakini siasa kwake sihasa.
Daima mbele Mbowe, daima mbele CHADEMA.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom