CHADEMA: Matamanio ya IGP Sirro anayosema amejifunza Rwanda kuhusu Polisi kuingia Misikitini na Makanisani na kuandaa mitaala ni kinyume na Katiba

Huu ndio utofauti wa CCM na CHADEMA. CHADEMA kila anayeongea hutoa hoja zenye uzito na mantiki.

Siro huko aliko atakuwa amepata shule ambayo hakuitarajia. Na hakika si Siro wala polisi yeyote atakayeenda msikitini au kanisani eti kwenda kuangalia mitaala.
 
Mtu anayevunja katiba na sheria za nchi kwa makusudi hafai ni lazima kutangaza mgogoro nae hamna namna
 

Nilidhani ungefurahi kuwa mpinzani wako sasa hana uongozi na haeleweki. Badala yake inakuuma sana kuona hata hakuna wanaotilia shaka hatma ya chama.

Nikukumbushe hili - itikadi huwa sio swala la kiongozi tu. Buddha, Mtume Mohamad, Yesu Kristu na hata OBL hawako tena lakini walichoacha kimesimama!!
 
Swadakta
 
Aiiiseeeeee!

SIRRO alikwenda Rwanda kujifunza njia za kuwakandamiza wapinzani kama polisi wa huko walivyofanikiwa kuwafanyia wapinzani wa Rwanda?

Maana ya ziara ile kumbe ilikuwa ni nzito kiasi hiki!
Kaenda kujifunza maovu ya wa italahamwe. Kamanda ni mtu hatari sana.

Umri alionao hata miaka 10 mbele hafikishi. Badala atengeneze na Mungu anazidi kuwa mtu wa Ibilisi.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…