CHADEMA mmejipangaje na wabunge 19 wa viti maalumu kutorudi bungeni tena mwaka 2025/26?

CHADEMA mmejipangaje na wabunge 19 wa viti maalumu kutorudi bungeni tena mwaka 2025/26?

Chama cha Demokrasia na Maendeleo hakina ubavu wa kuwakataa hawa wabunge wao.

Kwanza, kuna viashiria kila mahali kwamba wako bungeni kufuatia nia, mchakato, na baraka za chama.

Pili, itaibuka hoja tunapoelekea kwenye ngwe za uchaguzi mwakani, kwamba kama walipokelewa mapapa wa mafisadi kama akina Lowassa, Sumaye na Lazaro Nyalandu, wakasafishwa, wakasifiwa na kugombea, seuze akina Halima Mdee?

Hii hoja moja tu inatosha kutuliza hali ya hewa na kuleta mtangamano Chademani.

Isitoshe, mwenyekiti atadai, kama anavyodaigi kila mwaka, kwamba hii ni fursa ya pekee kuunganisha nguvu zote za peponi na motoni za wafuasi watiifu na wasaliti ili kuingia Ikulu kwa kishindo, au kama wao waitavyo - mafuriko!

Mwisho, siasa hainaga maadui wala marafiki wa kudumu. Ndiyo maana juzi Zitto Kamwe alikuwa Msisiemu, jana akatimkia Chadema, leo yuko siti ya mbele kabisa Eisitii, na, nani ajuaye, huenda kesho akapokelewa kwenye chama cha Republican Marekani!
Tatizo unaongea tu, kikatiba Baraza kuu ndilo lenye uwezo wa kuwaburudisha sio mwenyekiti. Halafu pia mahakama kuu ilibariki maamuzi ya kamati kuu kuwafukiza uanachama, ndio maana akina halima Mdee wamekata Rufaa. Soma kwanza kabla ya kuandika.
 
CDM wanacheka na Ruzuku zinazotokana na hao wabunge yaani wanajitekenya na kucheka wenyewe,Msigwa unajua utamu wa Ruzuku.
Unajua Ruzuku inapatiakanaje?. Hata Chaumma anapata Ruzuku lakini Hana mbunge.
 
Tatizo unaongea tu, kikatiba Baraza kuu ndilo lenye uwezo wa kuwaburudisha sio mwenyekiti. Halafu pia mahakama kuu ilibariki maamuzi ya kamati kuu kuwafukiza uanachama, ndio maana akina halima Mdee wamekata Rufaa. Soma kwanza kabla ya kuandika.
Bila shaka huu mchezo hujui namna unavyochezeshwa na wenye mamlaka yao.
 
Umeuliza maswali muhimu sana mleta mada, lkn wasioona mbali wanakushambulia.

CCM inaweza kufanya chochote muda wowote na kupelekea haya unayoyahofia yakafanyika.
Wafanye tu. Mbona wamefanya na wameishia kufukuzana bungeni wenyewe CCM. Mambo mengine unaiachia Karma. Halafu akina Halima wamekata Rufaa mahakama ya Rufaa Ina maana maamuzi ya mahakama kuu yalibariki kamati kuu kuwafukiza, hivyo mpaka Sasa sio wanachama.
 
Tatizo watu hawafuatilii hata hukumu ya mahakama kuu. Kasomeni hukumu ile ndio mtajua kwanini akina Halima Mdee wamekata Rufaa mahakama ya Rufaa. Wale wanalindwa na huyo Spika Kilaza aitwaye.
 
dk-slaa-pic.jpg
mwabukusi-pic.jpg

Haya Majembe muhimu ili Timu ikamilike ✌️✌️✌️
 
CHADEMA mna mkakati wowote wa kuwazuia wabunge wa viti maalumu waliopo bungeni wakati huu kutorudi bungeni wakati na baada ya uchaguzi wa mwaka 2025?

Mtawazuiaje ikiwa mtaona wao ndio wamepewa fursa ya kugombea na wanapeperusha bendera ya CHADEMA katika uchaguzi wa mwaka 2025?

Mtawazuiaje ikiwa mtawaona wao ndio wabunge wa viti maalumu tena baada ya uchaguzi?


Watagombea vipi wakati sio wanachama🙉
 
HAKUNA WATU WAJINGA KAMA WATANZANI!


Wewe unauliza CHADEMA wamejipangaje wakati unaelewa kabisa hao si wabunge wa CHADEMA na walifukuzwa tangu zamani kwenye CHAMA CHAO,Hao wanaendelea kutumia kodi Kibwena za Walipa kodi halafu wewe Unakuja kuueleza umma wa Watanzania "CHADEMA MMEJIPANGAJE"

Nilitegemea hadi muda huu ungekuja na hoja ya namna ulivyowashitaki mahakamani wabunge wasiokuwa na Chama badala yake unauliza maswali ya kipumbavu!


By the way :

TANZANIA NDO NCHI INAONGOZA KWA KUWA NA NG'OMBE WENGI BARANI AFRIKA!
 
Back
Top Bottom