CHADEMA: Mzee Ali Kibao ametekwa na Vyombo vya Ulinzi na Usalama akiwa kwenye basi. Usalama wa Taifa waeleze alipo

CHADEMA: Mzee Ali Kibao ametekwa na Vyombo vya Ulinzi na Usalama akiwa kwenye basi. Usalama wa Taifa waeleze alipo

ukute mzee alijificha kwenye kichaka cha uongozi chadema kumbe mzee mafia au kazurumu alikuwa anakimbia
Kuna siri kwenye kukamata mhalifu? Jeshi hili hili la polisi linavyooenda sifa litashinswa kuita vyombo vya habar kujimwambafai kwamba wameweza....?
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika akizungumza na wanahabari mchana wa siku ya Jumamosi Septemba 7, 2024 Makao Makuu ya CHADEMA, Dar es Salaam amesema kuwa...

“Kwa aina ya bunduki walizokuwa nazo hao watu waliokuja kumchukua (Mzee Ally Mohamed Kibao ambaye ni mjumbe wa sekretarieti ya chama taifa (CHADEMA)) kwenye basi si bunduki ambazo kwa kawaida hutumiwa na Jeshi la Polisi, ni bunduki ambazo hutumiwa na Idara ya Usalama wa Taifa.

Wakati tukifuatilia taarifa zaidi na wakati tukijiandaa kuchukua hatua zaidi kuja kwenye vyombo vya habari kueleza tu kwamba kiongozi wetu na mwenzetu ametekwa na vyombo vya ulinzi na usalama, nitoe wito kwa IGP wa Jeshi la Polisi Mkuu wa Jeshi la Polisi kueleza iwapo Ally Kibao ametekwa na Jeshi la Polisi, waeleze sababu za kumteka, yupo wapi, na ana hali gani.

Kwa kawaida huwa tunajizuia sana kuzungumza kuhusu Idara ya Usalama wa Taifa lakini kwa sheria ya idara ya Usalama wa taifa kuna mtu mmoja tunaweza tukamtaja na tunaweza kumzungumza, Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa natoa wito kwake ajitokeze aeleze iwapo idara ya usalama wa taifa imemteka Mzee Ally Mohammed Kibao, yuko wapi?

Pia soma > John Mnyika: Kiongozi wa CHADEMA Mzee Ali Mohamed Kibao, adaiwa kushushwa kwenye Basi na kuchukuliwa
 
Unafiki wa vyombo vya habari umehirika Sasa
Yaani tunapata taarifa Kwa watu binafsi
Habari za kujiendekeza kizimkazi walijaa na wali report japo tulikuwa hatuhitaji
Yaani mnashindwa kutumia waandishi kufika hata mwananyamala hospital kufuatilia na kuleta habari za mwananchi kuuliwa mchana mpo kmy

Media Bado hazipo huru
 
Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) John Mnyika akizungumza na wanahabari mchana wa siku ya Jumamosi Septemba 7, 2024 Makao Makuu ya CHADEMA, Dar es Salaam amesema kuwa...

“Kwa aina ya bunduki walizokuwa nazo hao watu waliokuja kumchukua (Mzee Ally Mohamed Kibao ambaye ni mjumbe wa sekretarieti ya chama taifa (CHADEMA)) kwenye basi si bunduki ambazo kwa kawaida hutumiwa na Jeshi la Polisi, ni bunduki ambazo hutumiwa na Idara ya Usalama wa Taifa.

Wakati tukifuatilia taarifa zaidi na wakati tukijiandaa kuchukua hatua zaidi kuja kwenye vyombo vya habari kueleza tu kwamba kiongozi wetu na mwenzetu ametekwa na vyombo vya ulinzi na usalama, nitoe wito kwa IGP wa Jeshi la Polisi Mkuu wa Jeshi la Polisi kueleza iwapo Ally Kibao ametekwa na Jeshi la Polisi, waeleze sababu za kumteka, yupo wapi, na ana hali gani.

Kwa kawaida huwa tunajizuia sana kuzungumza kuhusu Idara ya Usalama wa Taifa lakini kwa sheria ya idara ya Usalama wa taifa kuna mtu mmoja tunaweza tukamtaja na tunaweza kumzungumza, Mkurugenzi wa Usalama wa Taifa natoa wito kwake ajitokeze aeleze iwapo idara ya usalama wa taifa imemteka Mzee Ally Mohammed Kibao, yuko wapi?

Pia soma > John Mnyika: Kiongozi wa CHADEMA Mzee Ali Mohamed Kibao, adaiwa kushushwa kwenye Basi na kuchukuliwa
Kutokana na hali mbaya kabisa ya kiusalama iliyopo hapa nchini hivi sasa, kuna kila sababu ya ku-declare the State of Emergency.

Siyo siri, hali ni mbaya sana.
Uhakika wa kufa leo hii ni mkubwa zaidi kuliko matumaini ya uwezekano wa kuiona kesho.
 
Ukisema vyombo vya ulinzi na usalama unakuwa umegusa vyombo kwa ujumla wake. Ulinzi ndio JWTZ. Hilo ni kosa ambalo wengi hawawezi kulitofautisha. Mnyika kama amesema hayo alitakiwa aseme tu vyombo vya usalama. Vyombo vya usalama ndio hivyo kuanzia Tiss, uhamiaji, magereza, polisi, zimamoto nk ndio vyombo vya usalama. Bila shaka Mnyika alimaanisha vyombo vya usalama.
 
Kuna tetezi kwamba LISU kagoma kuhudhuria mazishi Kwa tuhuma kwa Mbowe na Mnyika wanajua kilichomkuta Babu wa watu. Mwenye ukweli atujuze. Binafsi nahisi kama Mbowe siyo Mpinzani vile. Huko huki kwake CHADEMA akiona mtu yupo Serious kuipinga Serikali kama vile anamshughulikia. Najaribu tu kuunganisha dots kuanzia Kwa Chacha Wangwe, Ben Saanane na wengineo. Nahisi kama Ile hoja ya Rais Samia kwamba Mbowe ni gaidi kana ka ukweli Fulani. Sema tu inawezekana ni gaidi la system.

Nawaza tu huku nikiwa nimevimbiwa mihogo ya kuchemsha.
 
Ndugu zangu wapenda haki wote,Sijui nani atakayefuata baada ya hili tukio la kutekwa na kuuwawa kwa AlIy Muhamed kibao, kama tunavyoona jeshi la polisi limeshindwa kutulinda raia wake dhidi ya watekaji au wasiojulikana.Wanaweza kututeka mda wowote na saa yeyote na mahari popote,kama ilivyotokea kwa wahanga wangine waliotangulia,na ukitegemea wengi wanaotekwa ni wanachama wa upinzani wanaotokea chama cha Chadema.

Tungeomba Viongozi wetu wapate ujasiri wa kujisimamia wenyewe, siyo tena kushirikiana na Serikali iliyoshindwa kuwalinda wapinzani, ifike mda muanze kujilinda wenyewe dhidi ya watekaji
 
Hili swali kina Mwashambwa na ndugu zake wanalijua
 
Ndugu zangu wapenda haki wote,Sijui nani atakayefuata baada ya hili tukio la kutekwa na kuuwawa kwa AlIy Muhamed kibao, kama tunavyoona jeshi la polisi limeshindwa kutulinda raia wake dhidi ya watekaji au wasiojulikana.Wanaweza kututeka mda wowote na saa yeyote na mahari popote,kama ilivyotokea kwa wahanga wangine waliotangulia,na ukitegemea wengi wanaotekwa ni wanachama wa upinzani wanaotokea chama cha Chadema,
Tungeomba Viongozi wetu wapate ujasiri wa kujisimamia wenyewe, siyo tena kushirikiana na Serikali iliyoshindwa kuwalinda wapinzani, ifike mda muanze kujilinda wenyewe dhidi ya watekaji
polisiccm ni kero kubwa sana
 
Kuzurumu, au uwe jambazi hata kama ni gaidi bado sheria za ukamataji zipo pale pale mbona mashehe kibao walikamatwa wamekaa ndani miaka kibao lakini walipo kamatwa walijulikana wamepelekwa kituo gani na wamekamatwa kwa kosa gani. Huu ukamataji wa staili hii utakuja kuleta maafa siku moja. Kwa sabubu watu wakijua kuwa haea hawatu wakikamata watu kwa staili hii hawawapeleki POLISI watu watakuja kuleta resistance to siku moja na ndipo hapo maafa yatatoke. Aina hii ya ukamataji alikuwa anaifanya Idi Amini Dada rais wa uganda na ulikuwa ukikamatwa kwa staili hii hurudi
 
Back
Top Bottom