Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT-Wazalendo: Hoja saba zinazowafanya Watanzania wasiwe tayari kumwaga damu kwa maandamano

Uchaguzi 2020 CHADEMA na ACT-Wazalendo: Hoja saba zinazowafanya Watanzania wasiwe tayari kumwaga damu kwa maandamano

Stephano Mgendanyi

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2020
Posts
2,833
Reaction score
1,301
CHADEMA na ACT-WAZALENDO: Hoja 7 Zinazowafanya Watanzania Wasiwe Tayari Kumwaga Damu kwa Kuandamana.

Vyama vya CHADEMA na ACT- Wazalendo vimekutana na kuwaambia waandishi wa habari eti kuanzia jumatatu wataanza maandamano yasiokuwa na kikomo kwa kile walichodai eti kuibiwa kura katika Uchaguzi uliofanyika Oktoba 27-28, 2020.

Maandamano hayo yasiyo halali wamepanga kuyafanya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.

Makala hii baada ya kufanya utafiti katika pande mbili za Muungano, bara na visiwani, inafafanua sababu za watanzania kutojihusisha na maandamano ya CHADEMA na ACT- Wazalendo.

Hoja ya kwanza:
Watanzania ni watu wa amani
. Hawataki kupoteza amani iliyoasisiwa na wazee wa Taifa hili chini ya Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume.

Hoja ya pili:
Watanzania walishiriki kupiga kura
na kuchagua washindi wa uchaguzi kwa ngazi zote za urais, udiwani na ubunge kwa hiyo hawaoni kwa nini waandamane wakati wao ndio waliowachagua washindi.

Hoja ya tatu:
Maendeleo
. Watanzania wote kwa sasa wanaendelea na shughuli zao za maendeleo na maisha ya kila siku yanaendelea vizuri na kuwafanya wapate mkate wao wa kila siku. Kwa mantiki hii maandamano hayatawalisha chakula na walishamaliza uchaguzi.

Hoja ya nne:
Watanzania kwa sasa wameshajua
kuwa CHADEMA na ACT- Wazalendo wana ajenda za kuuza rasilimali za nchi kwa mabeberu kwa hiyo hawako tayari kuuzwa nchi yao na utu wao.

Hoja ya sita:
CHADEMA na ACT- Wazalendo kukosa wagombea wenye mvuto na sera za maendeleo. Wagombea kama Babu Seif na Tundu Lissu wote ni wachumia tumbo na makuwadi wa mabeberu. Hawa sio chaguo la Watanzania.

Hoja ya saba:
Watanzania wenyewe wameamua kuchagua maendeleo sio vurugu.
Baadhi ya maendeleo hayo ni upatikanaji wa maji, umeme, barabara na mengine mengi wameshayafaidi kwenye muhula wa kwanza wa Rais Magufuli. Kwa mantiki hiyo hawahitaji majaribio ya uongozi wakati asali wameanza kuiramba.

Badala ya CHADEMA na ACT- Wazalendo kuhamasisha umwagaji damu katika taifa huru la Tanzania, watumie muda huu kujitathimini kwa nini hawakuchaguliwa na wananchi. Waache mihemko kwani damu waliyopanga kuimwaga haitawaacha salama.

IMG-20201101-WA0026.jpg
 
Kwanini mnakibilia kumwaga damu?
Unafikiri jeshi litawaangalia tu bila kuwachukulia hatua?

Maana maandano ya vitu vingi sana vinavyoweza kujitokeza ikiwa ni pamoja na fujo katika maeneo mbalimbali yanayoweza kupelekea uharibifu wa mali za watu, wizi na uvunjifu wa amani.

Haba na haba hujaza kibaba.

Ni wazi kwamba wapinzani hawana sababu za msingi za kuandamana. Kama wameshindwa wanapaswa kukaa na kujipanga kwa uchaguzi ujao.

Wapinzani wanatakiwa kujua kwamba, wao siyo wa kwanza kushindwa.

Je, kila aliyeshindwa naye aandamane?
 
Tutaandamana. Kama mnataka kumwaga damu basi tayarisheni risasi na vifaru kama mlivyofanya kule Zanzibar. Sisi tutakuja na vitambaa vyeupe, ishara ya amani. Vitambaa vyeupe haviwezi kumwaga damu.
 
Mimi, bila hata kusoma "hoja" zako, nikiangalia kichwa cha mada yako pekee inatosha kutokuwa na shauku ya kusoma hizo hoja ulizoweka.

Ni hivi: Ni nani aliyekwambia kwamba "kufanya maandamano ni kumwaga damu"?

Hivi unaelewa maana ya kufanya maandamano?

Hili pekee linakuondolea sifa ya kuwa na uwezo wa kuweka mada zinazofikirisha hapa JF.

Kwa hayo uliyoandika hapa umelipwa kiasi gani, au ni katika juhudi za kujitangaza uonekane kwa wateuzi, kwa vile sasa kazi iliyobaki ni kuteuwa?

Watu aina yako ndio mnaojazana kwenye nafasi zinazotakiwa kuwatumikia waTanzania kwa uadilifu, badala yake mnapewa msiokuwa na sifa na kazi mnazopewa mzifanye.
 
Tutaandamana. Kama mnataka kumwaga damu basi tayarisheni risasi na vifaru kama mlivyofanya kule Zanzibar. Sisi tutakuja na vitambaa vyeupe, ishara ya amani. Vitambaa vyeupe haviwezi kumwaga damu.
Kadri demokrasia ya vyama vingi inavyozidi kuenea mataifa mbalimbali ni nani anayenufaika?
ii). Je,kwa kumjua mnufaika huoni unaikanyaga ardhi yako kupigania maslahi ya taifa la wenzio?
iii). Je, kwa kuujua werevu utajilazimisha kuendelea kuufanya ujinga?



MAGUFULI4LIFE.
 
CHADEMA na ACT-WAZALENDO: Hoja 7 Zinazowafanya Watanzania Wasiwe Tayari Kumwaga Damu kwa Kuandamana.

Mimi binafsi huwa natafuta uhusiano kati ya kuandamana na kumwaga damu, lakini siupati. Kila kimoja kinajitegemea, na kinaweza kutokea kwa sababu zinazojitegemea
 
Hujaambiwa kumwaga damu kuwa mwelewa kijana wa lumumba ni maandamano ya aman hakuna silaha wala vita hakuna panga wa kisu wa bunduki ni maandamano ya aman ya kudai haki ila polisi ndo watasababisha silaha zitumike lakin wakiachwa ujumbe wao ufike unakotakiwa utafika tu kwa aman bhasi
 
Polisi wanatakiwa kuwalinda pasiwe na vurugu tu na upigaji bhasi maandamano ni haki ya kila mtu pasipo kuvunja sheria
 
CHADEMA na ACT-WAZALENDO: Hoja 7 Zinazowafanya Watanzania Wasiwe Tayari Kumwaga Damu kwa Kuandamana.

Vyama vya CHADEMA na ACT- Wazalendo vimekutana na kuwaambia waandishi wa habari eti kuanzia jumatatu wataanza maandamano yasiokuwa na kikomo kwa kile walichodai eti kuibiwa kura katika Uchaguzi uliofanyika Oktoba 27-28, 2020.

Maandamano hayo yasiyo halali wamepanga kuyafanya Tanzania Bara na Tanzania Visiwani.

Makala hii baada ya kufanya utafiti katika pande mbili za Muungano, bara na visiwani, inafafanua sababu za watanzania kutojihusisha na maandamano ya CHADEMA na ACT- Wazalendo.

Hoja ya kwanza:
Watanzania ni watu wa amani
. Hawataki kupoteza amani iliyoasisiwa na wazee wa Taifa hili chini ya Mwalimu Julius Nyerere na Mzee Abeid Amani Karume.

Hoja ya pili:
Watanzania walishiriki kupiga kura
na kuchagua washindi wa uchaguzi kwa ngazi zote za urais, udiwani na ubunge kwa hiyo hawaoni kwa nini waandamane wakati wao ndio waliowachagua washindi.

Hoja ya tatu:
Maendeleo
. Watanzania wote kwa sasa wanaendelea na shughuli zao za maendeleo na maisha ya kila siku yanaendelea vizuri na kuwafanya wapate mkate wao wa kila siku. Kwa mantiki hii maandamano hayatawalisha chakula na walishamaliza uchaguzi.

Hoja ya nne:
Watanzania kwa sasa wameshajua
kuwa CHADEMA na ACT- Wazalendo wana ajenda za kuuza rasilimali za nchi kwa mabeberu kwa hiyo hawako tayari kuuzwa nchi yao na utu wao.

Hoja ya sita:
CHADEMA na ACT- Wazalendo kukosa wagombea wenye mvuto na sera za maendeleo. Wagombea kama Babu Seif na Tundu Lissu wote ni wachumia tumbo na makuwadi wa mabeberu. Hawa sio chaguo la Watanzania.

Hoja ya saba:
Watanzania wenyewe wameamua kuchagua maendeleo sio vurugu.
Baadhi ya maendeleo hayo ni upatikanaji wa maji, umeme, barabara na mengine mengi wameshayafaidi kwenye muhula wa kwanza wa Rais Magufuli. Kwa mantiki hiyo hawahitaji majaribio ya uongozi wakati asali wameanza kuiramba.

Badala ya CHADEMA na ACT- Wazalendo kuhamasisha umwagaji damu katika taifa huru la Tanzania, watumie muda huu kujitathimini kwa nini hawakuchaguliwa na wananchi. Waache mihemko kwani damu waliyopanga kuimwaga haitawaacha salama.

View attachment 1617068
Kwanini akili zenu zinakimbilia kumwaga damu?
Hakika nyie mmezoea damu, damu tupu mawazo yenu.
Mnanuka damu za watu.
Nyie siyo watanzania, na mtakuja kubainika. Mtanzania si mtu wa kuwaza kumwaga damu kama ndo suluhisho la matatizo yake. Hizi ni tabia za majirani zetu wahutu na watusi.

Watu wamesema wataandamana, tena kwa AMANI lakini wewe unapanga kumwaga damu za watu.
Ni mtanzania kweli wewe?
 
Unafikiri jeshi litawaangalia tu bila kuwachukulia hatua?

Maana maandano ya vitu vingi sana vinavyoweza kujitokeza ikiwa ni pamoja na fujo katika maeneo mbalimbali yanayoweza kupelekea uharibifu wa mali za watu, wizi na uvunjifu wa amani.

Haba na haba hujaza kibaba.

Ni wazi kwamba wapinzani hawana sababu za msingi za kuandamana. Kma wameshindwa wanapaswa kukaa na kujipanga kwa uchaguzi ujao.

Wapinzani wanatakiwa kujua kwamba, wao siyo wa kwanza kushindwa.

Je, kila aliyeshindwa naye aandamane?
Ukishindwa kwa haki hakuna atakaye andamana.
 
Unafikiri jeshi litawaangalia tu bila kuwachukulia hatua?

Maana maandano ya vitu vingi sana vinavyoweza kujitokeza ikiwa ni pamoja na fujo katika maeneo mbalimbali yanayoweza kupelekea uharibifu wa mali za watu, wizi na uvunjifu wa amani.

Haba na haba hujaza kibaba.

Ni wazi kwamba wapinzani hawana sababu za msingi za kuandamana. Kama wameshindwa wanapaswa kukaa na kujipanga kwa uchaguzi ujao.

Wapinzani wanatakiwa kujua kwamba, wao siyo wa kwanza kushindwa.

Je, kila aliyeshindwa naye aandamane?
Mbona CCM huwa wanaandamana kupongeza juhudi bila tatizo?
 
Mbona huzungumzii utafiti juu ya ukwapuaji wa masanduku siku ya tukio pia uwepo wa karatasi zilizowekewa vyema wagombea wa chama cha mezani zilizokamatwa nje ya kituo kwenye mabegi ya watu?
 

Mbona CCM huwa wanaandamana kupongeza juhudi bila tatizo?
Sababu za kuandamana ndiyo huwa zinaleta mashiko kwa watu kuwaunga mkono.

Waangalizi wengi wa uchaguzi kwa Afrika Mashariki (EAC), na SADC, na hata Waangalizi wa ndani wamekiri kuwa uchaguzi ulikuwa wa huru na haki. Maraisi wengi wametoa pongezi nyingi za ushindi wa JPM.
 
Back
Top Bottom