Chadema na dharau kwa amri ya mahakama.

Chadema na dharau kwa amri ya mahakama.

hata kuibia unashiinfwa? Hapatatizo liko. Wapi mbona unatokwa na povu kohivp?. Jifunze kutafsiri maagizo upunguze. Udivision 5

pingine ujamsoma vyema lissu na dr slaa.

Mkuu hizi kashifa zako hazini yumbishi kabisa.

Tudulissu anasema zitto anaendelea kuwa mwana chama kwa sababu ya mahakama tuu.

Ukimsoma hapo vyema utagundua amesema kuwa walisha mjadili zitto na kumfukuza. Soma kwa makini hizi kejeli si chochote kwangu.
 
Chadema obviously walikuwa wamejipanga kumvua Zitto uanachama na wamezuiwa na mahakama dakika za mwisho....Walilolifanya ni kuchukua tahadhari based on this new development i.e. hawawezi kumfukuza kwa sababu ya mahakama, lakini inabidi wamwekee restrictions kwa kadri wanavyoweza (kwani obviously anaweza akafanya uharibifu zaidi kwa sababu naye anajua anaondoka).....Sasa kama wewe hizo restrictions (ambazo hajawekewa yeye), ila CDM imeshawishi wanachama wake wengine kutohudhuria mikutano yake, wewe ndio unaita wamemjadili na kumvua uanachama endelea kuamini hivyo !

Hata hivyo kama unasema unasema CDM wamemjadili na kumvua uanachama....mahakama itahitaji official doc. au official statement inayoonyesha wamemvua uanachama kama unavyodai.....Itakuwa ni kituko mahakamani ukaibuka ukasema kwamba proof ni kuwashawishi wanachadema wengine wasihudhurie mikutano yake.....

Nadhani kwa hili hatutakubalina, hivyo naomba tukubaliane kutokubalina............


tundu lissu anasema zitto anaendelea kuwa mwana chama wa chadema kwa sababu ya mahakama tuu, akimanisha wao kama wao walisha ujadili uanachama wake na wakamvua na ndio maana dr slaa amenukuliwa akiwasihi wana chadema wasi hudhurie mikutano ya zitto akijua fika hiyo ni haki ya mtu ambaye bado ni mwanachama.

Ukiyasoma vyema maneno ya lissu na dr slaa utagundua waliujadili uanachama wa zitto kinyume na maagizo ya mahakama na wanacho fanya ni kucheza na akili za watu tuu.
 
Upuuzi Mtupu!!!!! Dah!!!!! SMDH!!!!

Post nyingine bhana!Aarrgghh,kwani ni lazima?by the way umetekeleza kazi ya leo ok wahi B7 yako lumumba.
 
Chadema ni chama chenye ndoto za kushika dola na kilitegemewa kiwe chama cha kwanza kuheshimu amri za vyombo vya dola ikiwemo mahakama.

Sote tuna fahamu zitto kabwe aliweka zuio mahakamani dhidi ya kamati kuu ya chadema kujadili uanachama wake na kutokana na mwenendo wa shauri hilo mahakami, mahaka iliagiza chadema kutojadili uanachama wa mh zitto kabwe hadi mwisho wa shauri yani hukumu.

Siku ya ijumaa John Mnyika alionekana kwenye vyombo vya habari akisema hawatojadili uanachama wa zitto kutokana na agizo la mahakama na shauri linalo endelea.

Lakini cha ajabu leo kwenye kikao cha chadema na waandishi wa habari kilicho kuwa na lengo la kutoa na kueleza maazimio ya kamati kuu, wameonesha wazi kuwa wame kahidi agizo la mahakama na kuya dharau na ni wazi walijadili uanachama wa zitto.
Kurugenzi ya Habari imenukuu maneno yaliyo somwa na dr slaa ya kionesha kamati kuu imejadili uanachama wa zitto.
Na nukuu
" chama kina wataka wanachama wote na wapenzi wote kuto shiriki mikutano ,ama shughuli zozote za kisiasa zitakazo andaliwa na zitto kabwe na washirika wake kwa jina la chadema"

kwa hayo maneno hapo juu haihitaji kuwa profesa kuelewa kuwa chadema wamemjadili zitto pamoja na uanachama wake hivyo wame kahidi maagizo ya mahakama na kuyasigina kabisa kama hawatambui uwepo wake.


Hayo maneno yaliyo somwa na dr slaa leo yanaonesha kabisa chadema kuto heshimu mamlaka za nchi.

Wananchi wanatakiwa kujua hawa chadema mambo yanapo kwenda kombo kwa upande wao ndio huwa wa kwanza kusema wanaonewa.

Nimejiuliza kilicho wafanya chadema kuto subiri jumatatu baada ya hukumu ndio wajadili uanachama wa zitto?

Hivi kwanini mh Tundu Lissu unashindwa kuwa mshauri mzuri kwa chama chako?

Chadema kwa hili la leo ni dharau kubwa kwa mahakama.

Karibuni wana jamvi.
Mimi kwa mtazamo wangu,sioni namna gani Chadema imekiuka agizo la mahakama la kutojadili uanachama wa Zitto.

Kwa kuwa kilichoagizwa na mahakama ni kutojadili uanachama wa Zitto,ndiyo maana waliotimuliwa uanachama wa Chadema ni Dr Kitilya Mkumbo na Samson Mwigamba,na Zitto uanachama wake umebaki pale pale,ingawa hao watatu ndiyo waliokuwa na zile ID za MM, M1,na M2.

Kwa maana hiyo kama Chadema ingetaka kupuuzia amri ya mahakama, ZZK naye jana angekuwa keshatolewa kwa kadi nyekundu!!

Kuhusu kauli ya Dr Slaa kusema kuwa Zitto kwa sasa haruhusiwi kuitisha mikutano ya kwa jina la CDM,naamini yupo sahihi kwa asilimia 100,kwa sababu CC ya Chadema ndiyo chombo cha juu kabisa cha maamuzi ndani ya chama,na kwa kuwa chombo hicho kilishamvua nyadhifa zote ndani ya CDM,na kwa kuwa Zitto kaamua kulipeleka shauri lake mahakamani,maamuzi ya CC ya kumvua nyadhifa zote ndani ya CDM yabaendelea kuwa halali,hadi pale mahakama itakapoamua vinginevyo kutokana na shauri alilololipeleka ZZK mahakamani hapo!
 
Last edited by a moderator:
Atakayetimuliwa CHAMANI atakuwa ndo failure

Vice Verse is True that atakayebaki CHAMANI ndio mshindi???

Sidhani kama uko sahihi kama mtazamo wako ndio huu. Mimi nadhani tulipaswa hapa tubishane kuwa Je ni halali watu kuandaa mkakati wa ushindi ndani ya chama au hapana? maana yake kama chama kitafika kitakubali kuwa wanachama wanaotaka kumpinga mwenyekiti wako huru kujiandaa na kufanya hivyo basi tunasema kweli chama chetu kina nia ya dhati ya kukuza na kustawisha demokrasia na kama KK itapiga chini mtu yeyeyote kuanza mkakati wa kuchukua mdaraka basi tunasema chama chetu ni Conservative.
 
Hahahahahaha lol!!!! Mambo ya ndani ya CHADEMA yanakuhusu nini!? Unatumia nguvu nyingi sana kumtetea huyu fisadi, ndio ameshafukuzwa rasmi uanachama wake umebaki kupitia mahakama na mahakama hata siku moja haiwezi kukilazimisha chama chochote cha siasa nchini kuendelea kuwa na mwanachama ambaye hatakiwi na chama hicho.

yani Tundu Lissu anasema zitto ni mwana chama lakini papo hapo tamko lao linaonesha haki za zitto kama mwana chama wa chadema amepokonywa.

Ni wazi wameujadili uanachama wa zitto na hapo ndipo walipo kahidi amri ya mahakama.
 
Acha uzuzu wewe.Zito kabwe hakujadiliwa kwenye cc ya chadema.Acha upotoshaji.

Yametimia; wapenzi wa ZZK yawapasa kukubali matokeo, hamkumshauri vizuri .Ni chungu kumeza lakini ndio hali halisi.Muda wa ku team up na kujenga chama kipya bado upo msaidiane kuanzisha wenzenu hawawataki wameshtuka.Kesho kitaeleweka mbivu na mbichi
 
zitto ni mwanachama wa chadema. Kumjadili zitto ni kujadili uanachama wake. Unawezaje kumtenganisha zitto na uanachama wake. Ndani ya chadema they are like chicken and eggs. You can't separate them Mpaka zitto atoke chadema. Think twice. Mahakama Pse react on this.
Tatizo la Watanzania ndo maana hatuna maendeleo, Mahakama ilizuia kujadili uanachama wa Zito na si matendo ya Zito katika Chama, Uanachama una maana ya kuendelea kuwa mwanachama au kuondolewa kwenye chama . kitu ambacho CHADEMA haikufanya. Hii haizuii kumchambua Zito kama mwenzao katika matendo na kukusanya ushahidi kuhusu mwenendo wake ili baada ya kesi kwisha uamuzi ufikiwe kukiwa na ushahidi madhubuti dhidi yake kama huu wa Mkono.
 
kwa hiyo unataka kusema kwamba cdm haina uwezo wa kuwaambia wanachama wake wasihudhurie mikutano itakayoitishwa na mwanachama mwingine yeyote wa cdm ? (kama wakitaka kufanya hivyo). Zitto ni mbunge anaweza kwenda jimboni kwake akaitisha mikutano na kuongea na wapiga kura wake na cdm hawana uwezo wa kumzuia kuitisha mkutano kama huo. Lakini wana uwezo na haki ya kuwashawishi wanachama wao kutohudhuria mikutano yake wakitaka kufanya hivyo.....

Hilo wanaweza kulifanya kwa mwanachama yeyote including zitto, unless unataka kutuambia kwamba mahakama imetoa amri kwamba zitto awe na status tofauti na wanachama wengine ndani ya cdm !
hebu niambie maneno aliyo sema dr slaa na lissu bado yana maanisha kuwa zitto bado ni mwanachama kutokana kuwa na shauri mahakamani?

Ukiyasoma maneno ya hao wawili vema utagundua kuwa zitto amevuliwa uanachama leo pamoja na shauri kuwa mahakamani.
 
Mhaya kweli wewe au jina la bandia? Maana hata speling zake zinaonyesha wasi wasi huo. Kinachothibitisha ni mtazamo wako!
 
Huwezi kujadili tuhuma dhidi ya Kitila na Mwigamba bila kumtaja Zitto au M2, kwa sababu wote ni sehemu ya issue moja, hivyo in one way or another Zitto anatajwa.....

Lakini mashtaka yanayomhusu moja kwa moja kama yeye sidhani kama yalijadiliwa.....In case Chadema wakishinda mahakamani kesho, Zitto ataitwa kujieleza kabla ya kutoa hukumu kwake (ambayo wote tunajua itakuwa vipi i.e. atapigwa chini).

Kamati kuu inawezwa kuitwa kwa dharura....nadhani hata hichi kikao kilichopita kilikuwa cha dharura !



Anachomaanisha Tundu Lissu ni kuwa CHADEMA imeshamfukuza Zitto Uanchama wake na yeye amebaki kuwa mwanachama wa CHADEMA kwasababu ya kesi iliyopo Mahakamani. Maana yake nini? ni kuwa KK ilijadili ajenda ya Uanachama wa Zitto na kutolea maamuzi. Na hii inawezekana, kwa mujibu wa katiba toleo la 2006 KK inakutana mara 4 kwa mwaka, sasa kwa Quarter hii KK imeshakutana, Kama KK isingejadili suala la Zitto maana yake suala lake libaki mpaka itakapokuja kukutana tena Baada ya mwezi wa 3. na kutokana na hasira za baadhi ya wajumbe wa KK walizonazo dhidi ya ZZK wasingependa kuona kuwa ZZK anabaki kuwa mwanachama wa CHADEMA baada ya kesi. Hivyo basi walilazimisha KK kujadili na kufikia maamuzi, Ili baada ya kesi kama watashinda Kesi hawana haja ya kuiita KK tena bai ni Mheshimiwa ZZK anapewa barua ya kuvuliwa uanachama wake moja.

Pia ushahidi unaonyesha wazi kuwa kulikuwa na mjadala kuhusiana na uanachama wa Zitto, kama kusingekuwa na mjadala maelezo ambayo ni ushahidi wa ushiriki wa Zitto katika Waraka wa Mabadiriko 2013 yasingetamkwa ndani ya Kikao. Maelezo kuwa ZZK aliwasiliana na mtu anayefahamika kwa jina la CHADEMA mpya yasingetolea, Maelezo ya kuwa Kitila Alikiri kuwa alimpa briefing ZZK kuhusiana na waraka yasingetolewa. It is Obvious kuwa KK ya CHADEMA walipuuza maagizo ya Mahakama
 
Hahahahahaha lol!!!! Mambo ya ndani ya CHADEMA yanakuhusu nini!? Unatumia nguvu nyingi sana kumtetea huyu fisadi, ndio ameshafukuzwa rasmi uanachama wake umebaki kupitia mahakama na mahakama hata siku moja haiwezi kukilazimisha chama chochote cha siasa nchini kuendelea kuwa na mwanachama ambaye hatakiwi na chama hicho.

Mi hata sielewi kwa nini Zitto kaenda mahakamani. Lengo lake ni nini hasa? Kwa nini anang'ang'ania kuendelea kuwa mwanachama wa CHADEMA wakati CHADEMA ni dhahiri hawamtaki? Simwelewi kabisa aisee. Si aondoke tu mwenyewe..

He needs to stop being such a prima donna.
 
Misukule ya Zitto inatapatapa sasa.....Haina pa kwenda wala kula...Subirini Zitto aanzishe chama chake muwe huko.....
 
Uelewa Mkuu Nyani Ngabu!!!! Mie nilidhani huyu shule aliyoenda imemuelimisha kumbe hajaelimika hata kidogo anafanya maamuzi kama hajawahi kukanyaga darasani kabisa.

Mi hata sielewi kwa nini Zitto kaenda mahakamani. Lengo lake ni nini hasa? Kwa nini anang'ang'ania kuendelea kuwa mwanachama wa CHADEMA wakati CHADEMA ni dhahiri hawamtaki? Simwelewi kabisa aisee. Si aondoke tu mwenyewe..

He needs to stop being such a prima donna.
 
Last edited by a moderator:
pingine ujamsoma vyema lissu na dr slaa.

Mkuu hizi kashifa zako hazini yumbishi kabisa.

Tudulissu anasema zitto anaendelea kuwa mwana chama kwa sababu ya mahakama tuu.

Ukimsoma hapo vyema utagundua amesema kuwa walisha mjadili zitto na kumfukuza. Soma kwa makini hizi kejeli si chochote kwangu.

Umebaki unatapatapa msukule wewe....Zitto.hajao kwahiyo huenda akakuposa na kukuoa....

Zitto habari yake imekwishaaaaaaaa!!!!!!
 
Back
Top Bottom