Chadema na usimamizi wa fedha zake; mgongano wa maslahi?

Chadema na usimamizi wa fedha zake; mgongano wa maslahi?

Mzee Mwanakijiji

Mfumo wa CHADEMA umeweka check and balance ili kudhibiti hali hii; na hata yameelekezwa katika taratibu za fedha(finnancial regulations) ambazo zimepitishwa na vikao vyama chama.

Mnyika.. hoja yangu inashambulia moja kwa moja huo mfumo wa chama. Kama umepitishwa na vikao vya chama haufanyi kuwa sahihi bali unauhalalisha tu. Dhana ya mgongano wa maslahi inapata nguvu pale ambapo mtu ambaye ana maslahi binafsi (deni) anapata nafasi ya kusimamia kile ambacho ni cha umma (public funds) ambapo maslahi yake binafsi pia yamo.

Daktari licha ya utaalamu wote alionao inapendekezwa mara nyingi asimtibu ndugu yake wa karibu isipokuwa kama ni lazima kweli hii ni katika kumsaidia kuwa objective katika kazi yake. Hivyo daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake mke wake anapopata matatizo ya ujauzito anaenda kwa daktari mwingine.

Vivyo hivyo majaji; kesi ya ndugu yake wa familia inapokuja mbele yake anatakiwa kujitoa ili kuhakikisha kuwa hata mwonekano wa mgongano wa maslahi hauwezi kutokea. Hata kama huyo ndugu yake waligombana miaka iliyopita na hawazungumzi. Hawezi kusema "naweza kusikiliza kesi hii kwa sababu huyu ndugu yangu hatuzungumzi". Akiruhusiwa na akamkuta ndugu yake hana hatia.. watu watasema "kamuachilia ndugu yake".

Sasa, Mbowe anaidai Chadema milioni 42; Sasa hilo la kukiposhesha chama mimi sina tatizo nalo hata kidogo. Ni haki ya mtu yeyote mwanachama au mtu mwingine kukikopesha chama kwa taratibu zilizopo na kwa makubalianao. Lakini hapa pia kuna maswali mengine.

a. Je amekikopesha kwa riba na ni riba ya kiasi gani? Matumaini yangu ni kuwa hakuna riba at all. Lakini kama kuna riba, tutaingia kwenye tatizo jingine kabisa ambalo naweza kuliona kama ukungu kutoka mbali.

b. Kama Mbowe ni mshiriki wa mijadala ya matumizi ya fedha za chama na mipango ya chama kuhusu fedha mbalimbali je anashiriki katika mijadala ya kiasi gani kitumike kulipa madeni ya wadeni wa chama? Kama ndiyo, tatizo jingine liko wazi.

c. Kama chama kinapanga matumizi ya fedha zake, Mbowe kama Mkopeshaji ana nafasi gani ya kuelekeza (steer) fedha za chama katika kulipa madeni wakati yeye ni mdeni mkuu?

Sasa, hapa ninachozungumzia ni mwonekano wa mgongano wazi wa maslahi.

Mbowe ajitoe kwenye kutia sahihi za matumizi ya fedha za chama na asihusishwe katika maamuzi (anaweza kushiriki mijadala lakini bila ya kuwa na nguvu ya kura) hadi pale atakapolipwa deni lake. Hili la mwisho linamhusu Ndesa vile vile.
 
Kwa mujibu wa kanuni za fedha za chadema, Mwenyekiti wa chama ni moja wa signatories wa account za chama katika kundi moja, wakati Katibu Mkuu ni moja wa signatories katika kundi lingine. Ndivyo ilivyokuwa wakati wa Mzee Mtei chama kilipoanza, ndivyo ilivyokuwa wakati wa Bob na ndivyo ilivyo kwa Mbowe na ndivyo itakavyokuwa kwa Mwenyekiti yeyote ajaye huko mbele unless Kamati Kuu na Vikao vingine katika chama viamue vinginevyo.

Kuchangia harakati za mabadiliko, tuma neno CHADEMA kwenda 15710 (kwa mitandao ya Vodacom na Zain pekee)

Kitila, kuna kanuni nzuri na kuna kanuni mbovu; kanuni kuwa Mwenyekiti ni signatory ni kanuni nzuri; kanuni kuwa mkopeshaji ni signatory ni kanuni mbaya! Sina tatizo na Mwenyekiti kuwa mtia sahihi; nina tatizo na mkopeshaji kuwa mtia sahihi. The difference is not that subtle.
 
- Kushinda uchaguzi wa US na ku-maintain au kuanzisha chama cha siasa Tanzania ni vitu viwili tofauti, au?

Respect.

FMEs!

Mtu kama anatoa michango ya Chama ni wazi atakitolea hata wakati wa uchaguzi. Mimi sitakurupuka tu kukichangia CUF kipindi cha uchaguzi lazima niwe nakipenda kwanza.Chama kupendwa ni wajibu wa viongozi, kama ni chama cha watu kitapata popularity kama ni cha 'small grop' kitabaki dormant na hii ndio sura tunayoiona kwa vyama vyetu hivi vitukufu vya upinzani!
 
Mbona haya maneno ya kutaka ushahidi kwa ufisadi niliwahi kusikia akisema Mkapa, makamba na Rostam zamani kidogo...mhhhh.

Slaa anajua kukariri sana...eh...mafisadi kwa kuomba ushahidi kama njia ya kukimbia ukweli kunakuwa hakuna tofauti na kina CCM yetu macho..
 
Mbona haya maneno ya kutaka ushahidi kwa ufisadi niliwahi kusikia akisema Mkapa, makamba na Rostam zamani kidogo...mhhhh.

Slaa anajua kukariri sana...eh...mafisadi kwa kuomba ushahidi kama njia ya kukimbia ukweli kunakuwa hakuna tofauti na kina CCM yetu macho..

teh teh teh teh

Ndio inaona kabisa chadema ni subset ya ccm.

Kanuni zile zile,muundo uleule taratibu zilele ufisadi uleule.
 
Hapana, hii logic yako haiwezi ku-apply kwa vyama vya siasa, hasa vya upinzani Tanzania. Duniani kote vyama vya siasa hujiendesha kwa michango ya wanachama. Hapa kwetu ni tofauti sana. Kwetu vyama vya siasa vya upinzani vinaendeshwa kwa kiasi kikubwa na michango ya viongozi wake wa juu. Hapa kwetu kama viongozi wa chama cha siasa wapo hoi kiuchumi na hawana ruzuku ya kutosha kutoka serikalini hicho chama lazima kidode na kiloe. Na mifano ipo tele hapa kwetu ambapo vyama vya siasa kati ya karibu 20 vilivyopo ni vyama visivyozidi 5 ambavyo angalau vipo kwenye lime light. CHADEMA tunabahati kwamba tangu kianze kimekuwa kikipata viongozi ambao wana uwezo na wana moyo wa kutumia uwezo wao kifedha kuendesha chama.

Unavyoongea wewe ni kama vile chadema walipanga kikatiba kumkopa Mbowe kama ambavyo wameweka katika kanuni zao kwamba mwenyekiti wa chama atakuwa signatory wa cheque. Na unaongea kana kwamba kukopa ni harusi. Ndugu yangu unakopa kwa sababu una shida. Sasa mwenyekiti hawezi kukosa sifa ya kuwa signatory kwa sababu tu eti amekisaidia chama chake. This is simply bad logic, lakini ni vigumu kuelewa kwa sababu umesema hadi ashuke malaika kutoka mbinguni ndio akuelewesha.

Kwa mujibu wa kanuni za fedha za chadema, Mwenyekiti wa chama ni moja wa signatories wa account za chama katika kundi moja, wakati Katibu Mkuu ni moja wa signatories katika kundi lingine. Ndivyo ilivyokuwa wakati wa Mzee Mtei chama kilipoanza, ndivyo ilivyokuwa wakati wa Bob na ndivyo ilivyo kwa Mbowe na ndivyo itakavyokuwa kwa Mwenyekiti yeyote ajaye huko mbele unless Kamati Kuu na Vikao vingine katika chama viamue vinginevyo.

Kuchangia harakati za mabadiliko, tuma neno CHADEMA kwenda 15710 (kwa mitandao ya Vodacom na Zain pekee)


Sasa nimeelewa kwa nini "wazee" wa Chadema walimuengua Zitto kugombea Uenyekiti. Kumbe mpaka uwe na mshiko ndio utapata nafasi ya kuongoza Chadema.

Mngesema mapema unatakiwa kuwa na kiasi gani "ku qualify" kuwa Mwenyekiti wa Chadema ili akina Zitto na wengine wakujue mapema kuwa suala sio uwezo tu wa kuongoza bali na mshiko pia.
 
Kitila, kuna kanuni nzuri na kuna kanuni mbovu; kanuni kuwa Mwenyekiti ni signatory ni kanuni nzuri; kanuni kuwa mkopeshaji ni signatory ni kanuni mbaya! Sina tatizo na Mwenyekiti kuwa mtia sahihi; nina tatizo na mkopeshaji kuwa mtia sahihi. The difference is not that subtle.

There you are talking, kwamba inaweza ikawa kanuni...

Hata hivyo, hii inamaanisha kuwa yeyote atakayekuwa signatory wa account za chama hapaswi kukikopesha chama na yeyote atakayekikopesha chama kamwe isitokee akawa signatory. Is this what you are trying to say?

Ninachojua mimi ni kwamba ukiwa wewe ni signatory na malipo yakawa yanakuhusu hupaswi kuidhinisha voucher au kusaini hundi ya malipo. Ningeona ni tatizo kama cheque ilikuwa imeandikiwa jina la Mbowe kama mlipwaji na yeye huyohuyo asaini hiyo cheque, which is not the case here-in fact angefanya hivyo hata benki hawawezi kukubali achukue hiyo cheque.
 
Sasa nimeelewa kwa nini "wazee" wa Chadema walimuengua Zitto kugombea Uenyekiti. Kumbe mpaka uwe na mshiko ndio utapata nafasi ya kuongoza Chadema.

Mngesema mapema unatakiwa kuwa na kiasi gani "ku qualify" kuwa Mwenyekiti wa Chadema ili akina Zitto na wengine wakujue mapema kuwa suala sio uwezo tu wa kuongoza bali na mshiko pia.

Wewe spinning huiwezi....kachukue shule kwanza kwa wenzako then uje. Kamuuliza angalau Makamba namna ya ku-spin, hii ya kwako ni nyeupe mno....
 
Kitila nimekuuliza maswali yangu hujayajibu Dr. Nategemea jibu zuri na la kitaalam form you.Post no.18
 
Pole sana Dr.Kitila

Kwa hiyo unakiri wazi kabisa kuwa wenye fedha ndio wanaanzisha vyama

1. Kwa nini vyama hivi vinakosa michango ya watu?
2. Je ni mpaka lini Vyama hivi vitaendelea kuwategema viongozi tu wenye fedha , je wakifilisika chama ndio kimekufa?
3. badala ya kusema tu kuwa 'mnawategema viongozi kifedha' je mmefanya juhudi gani kuepuka tegemezi hizi za viongozi? Obama ansema walichangiwa mpaka dola 1 na watoto wa shule ili washinde uchaguzi

4. Je kama mnategema fedha za viongozi, lengo lao na dhumuni lao ni nini? maana kwa namna hii
(a) Chama kinakuwa hakina demokrasia
(b)kuwapinga kama wakikosea ni kazi..YES si watazira na kuondoka na fedha zao

5.Hivi hao viongozi hizo fedha wanazokopesha wanapolipwa wanalipwa na Interest?


6. Is this project of opposition parties is viable? to you?

Kama mpaka leo ni miaka zaidi ya 15 bado hamjaweza kuwa na uhakika wa michango ya wanachama wanaokipenda, hauoni CHADEMA SIO CHAMA CHA WATU.. CHAMA CHA WAJASIRIAMALI WACHACHE WHICH IS WRONG!

7.Ili nishike nafasi ya Mbowe ninatakiwa kuwa na Capital ya shiling ngapi Dr.??

Siasa ni mapambano, usifikiri ni longolongo. Watu wameanza, tena kwa kasi kabisa, wanakimbia. The opposition project is very viable, tough as it may be. Being in the opposition is a struggle and you have to have a longterm vision,not a butter and bread project! It took Abdulah Wade 35 years for his party to win an election. The message is simple: Yes, it is tough but doable and it is an obligation anyway. Would you be very happy if everybody belonged to CCM?

Join the struggle-tuma neno CHADEMA kwenda 15710
 
tusilaumu vyama kukopa kwa viongozi. inabidi tujiulize je sisi tunao
utamaduni wa kuchangia vyama vya siasa? ndio vyama vya siasa kwani
harusi tunachangia (labda kwa sababu tunatarajia kushiriki katika matunda
ya uchangiaji wetu katika muda mfupi tofauti na tukichanga kwenye vyama).

That is the point.Watanzania tuna tatizo inapokuja katika kuchangia mambo ya maendeleo, sio vyama vya siasa tu. Watu wanachangiana harusi hadi wanakufuru, waombe mchango wa mwanao umekwama ada ya shule au chuo uone wanavyokuangalia na kukujadili.

Lazima tubadilike; vyama vya siasa ni taasisi muhimu kama tunataka nchi zetu za Africa zianze safari ya maendeleo. Lakini vyama hivi haviwezi kuimarika kama tunafikiri ni jukumu la watu fulani tu waliovianzisha.

Tuanze, tumeni neno CHADEMA kwenda namba 15710
 
There you are talking, kwamba inaweza ikawa kanuni...

Hata hivyo, hii inamaanisha kuwa yeyote atakayekuwa signatory wa account za chama hapaswi kukikopesha chama na yeyote atakayekikopesha chama kamwe isitokee akawa signatory. Is this what you are trying to say?

In the strictest sense yes; lakini zaidi ni katika kujenga mtazamo wa chama haipaswi kuwapa wakosoaji sababu ya kukosoa. Yaani, Chadema inapokuja katika mfumo na muundo wake wa kiutendaji ni lazima iwe juu ya petty politics. Haiwezi kufanana na CCM bali lazima ijipe standard ya juu zaidi ya CCM.

Ninachojua mimi ni kwamba ukiwa wewe ni signatory na malipo yakawa yanakuhusu hupaswi kuidhinisha voucher au kusaini hundi ya malipo.

Hilo ni sawa; lakini katika mfumo wa chama suala siyo kulipa voucher tu bali kuangalia matumizi na mapato yote na kushiriki mijadala ya fedha za chama ambazo wewe mwenyewe una maslahi nazo. Ingekuwa ni kulipa vouchers tu.. hilo ni rahisi kwani unamwambia mtu "usijilipe"!

Ningeona ni tatizo kama cheque ilikuwa imeandikiwa jina la Mbowe kama mlipwaji na yeye huyohuyo asaini hiyo cheque, which is not the case here-in fact angefanya hivyo hata benki hawawezi kukubali achukue hiyo cheque.

It is the appearance of pecuniary interest Dr Kitila that bothers me.
 
Kitila Mkumbo,
Sijui Bongo lakini hapa mimi naweza kujiandikia Chque na ikapita maadam inatoka kwa kampuni yangu na payee ni jina langu na kuna siahihi yangu.. Ndivyo navyochukua petty cash yangu siku zote, nachokataliwa ni kuchukua cash toka counter teller pasipo kuandika Cheque.
Kifupi kama nilivyokwisha sema Mbowe ni mshikaji na namuamini sana isipokuwa kulingana na Principal za Uhasibu sii vizuri kabisa Taasisi na hasa Chama ( a legal entity by itself) kuwa na msaini ambaye ndiye mdai mkubwa wa chama hicho...Mbowe anatakiwa kuwa katika kamati nyingine zote iwe za upitishaji matumizi na mipango ya maendeleo ya chama lakini sii mweka sahihi.. Hili halina Ubishi mkuu wangu, inaleta picha mbaya ya kuwa ni NGO kama Taasisi iloanzishwa na mtu binafsi...Nitaliacha hili maadam imepitishwa (mmeamua) na chama kuwa hivyo..
 
Join the struggle-tuma neno CHADEMA kwenda 15710

Nilifikiri unatipa jibu kuwa miaka 10 iliyopita Chadema ilikuwa na wanachama xxxx na michango kutoka kwa wanachama ilikuwa yyyy. Leo 2008 tuna wanachama zzzz na michango tunayoipata ni wwww.

Mtazamo wangu ni kuwa Chama hakina influence kwa watu na ndio maana hampati michango.

Kwa nini nisiamini kuwa economic crisis imewafanya viongozi wenu wasipate faida kwenye biashara na ndio mmeanzisha ''TUMA NENO CHADEMA'' ina maana viongozi wako OK kabisa na hili swala la kutopata michango kutoka kwa wanachama na NDIO NIKAKUULIZA LENGO LAO NI NINI??
 
That is the point.Watanzania tuna tatizo inapokuja katika kuchangia mambo ya maendeleo, sio vyama vya siasa tu. Watu wanachangiana harusi hadi wanakufuru, waombe mchango wa mwanao umekwama ada ya shule au chuo uone wanavyokuangalia na kukujadili.

Lazima tubadilike; vyama vya siasa ni taasisi muhimu kama tunataka nchi zetu za Africa zianze safari ya maendeleo. Lakini vyama hivi haviwezi kuimarika kama tunafikiri ni jukumu la watu fulani tu waliovianzisha.

Tuanze, tumeni neno CHADEMA kwenda namba 15710

Kitila if we can not answer the question WHY is that,then I doubt many things....

Kweli tuna matatizo makubwa sana ya watu kuchangia mamilioni ya shilings kwenye harusi na sio kwenye siasa....why?

Tatizo ni watu au ni vyama kutowainfluence watu.Imagine mwaka '95 Mrema alikuwa na influence sana , and I thought ule moto ungesambaa na kuongezeka hata kwa vyama vingine.Just Imagine 14yrs later bado hakuna aliyefikia ule moto,watu wale wale, Tanzania ile ile. Kilichobadilika ni maendeleo ya sayansi na Teknolojia ambayo tulitegemea ndio yangeongeza moto wa mawasiliano na kuwaweka kwenye wakati mgumu CCM!

Watu wanabadilika, hatuwezi tukakaa chini na kusema tukubali hali iliyopo eti kwa sababu watu hawachangii basi viongozi lazima wajitolee tu! halafu still wapiga kura wanatoka kwenye hao hao mnaowalaumu wanachangia sana harusi! thats why I asked is this project viable?

Kama hali halisi ya wananchi iko hivyo na baada ya tafiti zenu zinaonyesha hawatabadilika ...kwa nini kuna ulazima basi wa kuwa na vyama vya upinzani particulary Chadema-Lengo lenu ni nini wakati wananchi wenyewe hawana muda na nyie wanachangia harusi na kufurahia maisha??? can't you see??.Maana sura ya chama sasa hivi sio ya kitaifa..bali group la watu ambao kwa sababu wame invest basi wakishika nchi MAJIBU YENU YATAKUWA HAYO HAYO KUWA ''KWANZA HAMKUCHANGIA CHAMA HIKI MPAKA KINAPATA KUTAWALA''!!

Kama unakiri kuwepo kwa hii hali,hali mkijua, basi lengo lenu ni lingine na sio kuwakomboa hawa wachangia harusi!!
 
hivi Chadema wamefanya nini kiasi cha kuwafanya watu waone wanastahili kuchangiwa? Nililiuliza hili swali huko nyuma kwani jibu lake ni zito sana. Sijauliza wamesema nini!
 
hivi Chadema wamefanya nini kiasi cha kuwafanya watu waone wanastahili kuchangiwa? Nililiuliza hili swali huko nyuma kwani jibu lake ni zito sana. Sijauliza wamesema nini!

Labda kwa sababu wameshiriki kikamilifu katika kupambana VITA dhidi ya Ufisadi(kwa kuanzia na ile list of shame).......kingine sikioni so far kinachoweza kunifanya niwachangie,nina wasiwasi hela nitakazowachangia zaweza kutumika kulipa madeni kwa Mbowe na Ndesa(nisieleweke vibaya hapa)..Cha msingi CHADEMA muwe wabunifu katika kuanzisha miradi/vyanzo vya mapato badala ya kutegemea kukopa kutoka kwa akina Mbowe&Co..Pia muliangalie kwa umakini hilo suala la Mwenyekiti kuwa signatory(ambalo limeleta msuguano mkubwa dani ya chama na ninaamini litaendelea kuleta msuguano lisipofanyiwa ufumbuzi wa haraka) na mjithidi kuwa na utulivu ndani ya chama hasa katika kipindi hiki kigumu cha kuelekea uchaguzi mkuu...
 
Labda kwa sababu wameshiriki kikamilifu katika kupambana VITA dhidi ya Ufisadi(kwa kuanzia na ile list of shame).......kingine sikioni so far kinachoweza kunifanya niwachangie,nina wasiwasi hela nitakazowachangia zaweza kutumika kulipa madeni kwa Mbowe na Ndesa(nisieleweke vibaya hapa)..Cha msingi CHADEMA muwe wabunifu katika kuanzisha miradi/vyanzo vya mapato badala ya kutegemea kukopa kutoka kwa akina Mbowe&Co..Pia muliangalie kwa umakini hilo suala la Mwenyekiti kuwa signatory(ambalo limeleta msuguano mkubwa dani ya chama na ninaamini litaendelea kuleta msuguano lisipofanyiwa ufumbuzi wa haraka) na mjithidi kuwa na utulivu ndani ya chama hasa katika kipindi hiki kigumu cha kuelekea uchaguzi mkuu...

Heshima mkuu, umesema bila woga wala kumung'unya maneno

Ujasiri waliouonyesha kwa kuanzia list of shame ni mkubwa na utakuwa kwenye historia siku nyingi zijazo.Je wangapi wameenda jela na wangapi wamerudisha pesa zetu? mwaka wa tatu sasa! Chadema walitakiwa kwenda mbali zaidi na kama wameshindwa kujua namna gani basi hawakutakiwa kuitoa ile list!.Je hao mawaziri mafisadi hawawezi kufikishwa mahakamani? Chadema hawawezi kuwashtaki (mtikila style)angalau kwa hili hata wangemtafuta mmoja tu mnyonge! wangetangaza michango ya kuwapeleka hao jamaa mahakamani Chadema igekuwa wapi leo? -kama si jukumu lao kuwapeleka mahakamani lilikuwa jukumu lao kutangaza list of shame? tunapoanza mission tuzimalize.Nilichoona ni kuwa jamaa wamerelax na hapa ndio maswali yanaanzia what makes them to relax? au matajiri wanaogopa kupoteza fedha mahamakani? kama wanaogopa basi hata hizi fedha wanazozitoa chamani wanapata faida! thats give alarm! Tuna wapinzani kweli?? lakini ilikuwa rahisi kabisa kuomba michango kwa watu tena ingetolewa kwa hamasa! watu hawashirikishwi na hapa pia kuna mswali, kwa nini?

Pili umesema vyema mkuu, hakuna kitu kinachoboa kama kujua natoa mchango kwa sababu namlipa Mbowe na Ndesa.Kwa nini haya mambo basi yasiwe siri? Hii inasababisha hao matajiri kuogopwa, kuheshimiwa sana, kutopingwa, na kuyazima mambo mengi ya kidemokrasia.Bavicha juzi wametangaza tuzo ya Freeman Mbowe, nyuma ya pazia ni aidha Bavicha wanajikomba kwa Mbowe kwani ndiye tajiri, au Mbowe anajijengea himaya zaidi! unafikiri mtu akitaka kugombea uenyekiti si lazima atoe fedha nyingi zaidi ya Mbowe! Tunachokimbia CCM na kukipigia kelele ni ishu za rushwa na Takrima.....wenye fedha CCM ndio wana reign, so as in Chadema what is the difference between these two parties anyway!

Hamna haja ya wao kufanya uchaguzi mwakani mpaka waweke foundation inayotakiwa.Kipindi hiki unachosema Kigumu wamejitakia wenyewe! after all kura awape nani wakati wao wanasema watu wanawaza harusi!!!

Let us be Honest Chadema kuna watu potential wengi sana, ila misingi imeshakosewa!

"If the facts don't fit the theory, change the facts." --Albert Einstein
 
inawezekana sababu za watu kuchangia/kuwekeza kwenye harusi
badala ya kuchangia vyama vya siasa inatokana na yafuatayo

- kipindi cha kuwekeza kwenye harusi ni kifupi (unachanga na matokea
unayaona muda si mrefu) tofauti na kwenye siasa.

- mara nyingi (sio zote) mchangiaji wa harushi anakuwa mshiriki wa moja kwa moja kwenye harusi. yaani anajumuika kwa kula, kunywa na burudani inayoambatana na shughuli hizo.

- anaimani kwamba kwa kiasi kikubwa mchango aliotoa utafanya shughuli iliyodhamiriwa yaani kufanikisha harusi. tofauti na kwenye vyama vya siasa ambako shutuma za ubadhirifu nyingi tuu

- michango ya harusi sio haijirudii, yaani ukishamchangia mtu mara moja ndio imetoka haji tena mwakani kukuomba mchango kwa ajili ya harusi nyingine (ingekuwa hivi nadhani watu wachache wangekuwa tayari kuchangia hizo harusi). kwenye vyama michango inatakiwa mara kwa mara na wakati mwengine hata kabla mchangiaji hajaona matokea ya mchango wake wa awali
n.k.
 
Mnyika.. hoja yangu inashambulia moja kwa moja huo mfumo wa chama. Kama umepitishwa na vikao vya chama haufanyi kuwa sahihi bali unauhalalisha tu. Dhana ya mgongano wa maslahi inapata nguvu pale ambapo mtu ambaye ana maslahi binafsi (deni) anapata nafasi ya kusimamia kile ambacho ni cha umma (public funds) ambapo maslahi yake binafsi pia yamo.

Daktari licha ya utaalamu wote alionao inapendekezwa mara nyingi asimtibu ndugu yake wa karibu isipokuwa kama ni lazima kweli hii ni katika kumsaidia kuwa objective katika kazi yake. Hivyo daktari bingwa wa magonjwa ya wanawake mke wake anapopata matatizo ya ujauzito anaenda kwa daktari mwingine.

Vivyo hivyo majaji; kesi ya ndugu yake wa familia inapokuja mbele yake anatakiwa kujitoa ili kuhakikisha kuwa hata mwonekano wa mgongano wa maslahi hauwezi kutokea. Hata kama huyo ndugu yake waligombana miaka iliyopita na hawazungumzi. Hawezi kusema "naweza kusikiliza kesi hii kwa sababu huyu ndugu yangu hatuzungumzi". Akiruhusiwa na akamkuta ndugu yake hana hatia.. watu watasema "kamuachilia ndugu yake".

Sasa, Mbowe anaidai Chadema milioni 42; Sasa hilo la kukiposhesha chama mimi sina tatizo nalo hata kidogo. Ni haki ya mtu yeyote mwanachama au mtu mwingine kukikopesha chama kwa taratibu zilizopo na kwa makubalianao. Lakini hapa pia kuna maswali mengine.

a. Je amekikopesha kwa riba na ni riba ya kiasi gani? Matumaini yangu ni kuwa hakuna riba at all. Lakini kama kuna riba, tutaingia kwenye tatizo jingine kabisa ambalo naweza kuliona kama ukungu kutoka mbali.

b. Kama Mbowe ni mshiriki wa mijadala ya matumizi ya fedha za chama na mipango ya chama kuhusu fedha mbalimbali je anashiriki katika mijadala ya kiasi gani kitumike kulipa madeni ya wadeni wa chama? Kama ndiyo, tatizo jingine liko wazi.

c. Kama chama kinapanga matumizi ya fedha zake, Mbowe kama Mkopeshaji ana nafasi gani ya kuelekeza (steer) fedha za chama katika kulipa madeni wakati yeye ni mdeni mkuu?

Sasa, hapa ninachozungumzia ni mwonekano wa mgongano wazi wa maslahi.

Mbowe ajitoe kwenye kutia sahihi za matumizi ya fedha za chama na asihusishwe katika maamuzi (anaweza kushiriki mijadala lakini bila ya kuwa na nguvu ya kura) hadi pale atakapolipwa deni lake. Hili la mwisho linamhusu Ndesa vile vile.

Mwanakijiji Hoja yako ya kusaini cheque mbona haina uzito sana. Hujui kusign check kwa makampuni mengi yenye sheria safi za kihasibu siyo part ya internal control.

Kwa taarifa yako yako makampuni mengi sana sasa wala hizo cheque haziwi signed na binadamu bali zinakuwa printed na kupewa watu wanaodai. Pia kuna makampuni mengi tu amabayo wanafanya bank transfers (BAC System) na hakuna cheque kabisa. Hivyo sasa control inakuwa wapi? Control inakuwa kwa watu waliopewa madaraka ya kuapprove au authorise payment na hawa huwa wanaelezwa wazi kwenye standing orders na huwa wanapewa kuapprove certain amount kutokana na majukumu yake

Ningekuelewa kama ungesema kuwa mbowe kwa sababu anakidai chama basi asiruhusiwe ku approve/authorise payament yake mwenyewe (ambavyo ni kawaida kabisa kwa makampuni yenye utaratibu mzuri mtu hawezi kuapprove/authorise payment yake) na siyo ku sign cheque

Mimi nimestuka na maelezo ya mwanyika kwani sikutegemea kama wana financial system iliyo robust kama hiyo kwa mtizamo wangu kama kweli wanafuata basi wako katika khli nzuri.

Halafu mijitu huku inapiga kelele kuhusu signatories kwani Mkapa alipiga sahii yoyote kwenye pesa za EPA? lakini zilitoka kwa nini ? kwa sababu alihizinisha
 
Back
Top Bottom