LGE2024 CHADEMA Simiyu wachukua fomu, wasema "Safari hii hatutakimbia, watakimbia wenyewe"

LGE2024 CHADEMA Simiyu wachukua fomu, wasema "Safari hii hatutakimbia, watakimbia wenyewe"

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024

KwetuKwanza

Member
Joined
Mar 13, 2023
Posts
82
Reaction score
150
Pazia la kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao utafanyika mwaka huu 2024 limefunguliwa Jana Oktoba 26, 2024 kwa mujibu wa TAMISEMI.

Zoezi hilo ambalo litafanyika kwa siku Saba, Hadi Novemba 1, 2024, litaambana na kurudisha fomu kwa wagombea mbalimbali.

Nafasi zinazowaniwa ni Mwenyekiti wa Kijiji, kitongoji, mtaa pamoja na wajumbe wa serikali za vijiji, na Miata.

Zoezi hilo linafanyika katika Ofisi za wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata na vijiji, ambapo wagombea mbalimbali walioteuliwa na vyama ndiyo wanaendelea kuchukua fomu hizo.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Wilaya ya Bariadi, kimekuwa Chama cha kwanza kwa wagombea wake kuchukua fomu hizo.

Katika Kata ya Malambo iliyoko Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Viongozi wa Chama hicho Wilaya wakiwa na wafuasi wao, wamewasindikiza wagombea katika uchaguzi huo kata ya Malambo kwenye kuchukua fomu ofsi za Kata hiyo.

Mamia ya wanachama hao, wakiwa na bendera, pikipiki, walifunga kwa muda mitaa ya Mji wa Bariadi, wakiwasindikiza wagombea wao kwenye kuchukua fomu hizo.

Zoezi la kuchukua fomu lilimalizika Salama, na wagombea hao wakaridhishwa jinsi walivyopokelewa na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi huo Kisha kuwahudumia na kuwapatia fomu hizo.

Mgombea nafasi ya Mwenyekiti wa mtaa wa Ngashanda amesema wamejipanga kuhakikisha fomu hizo zinajazwa mapema iwezekanavyo na kwa usahihi Kisha kuzirejesha.

Wamewaomba wasimamizi wa uchaguzi huo kutenda haki katika kuteua wagombea, lakini pia kutenda haki katika zoezi la kupiga kura ili wananchi waweze kuchagua viongozi wanaowataka.

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya, Martine Mogani, amesema kuwa mitaa yote na vijiji katika Wilaya hiyo, tayari wameweka wagombea na wote wameanza kuchukua fomu.

Soma Pia:
Amesema kuwa Chama hicho kitafanya kampeini za kistaarabu pamoja na Amani, lakini hakitasita kuchukua hatua ikiwa kitaingiliwa na watu katika kuvuruga Amani iliyopo.

Nimekuwekea video hapo chini kwa hisani ya Global tv.


Chanzo: Global tv.
 
Hawa nguruwe wa kijani wamehujumu zoezi la uandikishaji wakiamini kuwa Chadema watasusa sasa imekula kwao tutabanana hivyo hivyo hadi kieleweke
 
IMG_0225.jpeg
 
Pazia la kuchukua fomu za kugombea nafasi mbalimbali katika uchaguzi wa serikali za mitaa ambao utafanyika mwaka huu 2024 limefunguliwa Jana Oktoba 26, 2024 kwa mujibu wa TAMISEMI.

Zoezi hilo ambalo litafanyika kwa siku Saba, Hadi Novemba 1, 2024, litaambana na kurudisha fomu kwa wagombea mbalimbali.

Nafasi zinazowaniwa ni Mwenyekiti wa Kijiji, kitongoji, mtaa pamoja na wajumbe wa serikali za vijiji, na Miata.

Zoezi hilo linafanyika katika Ofisi za wasimamizi wasaidizi ngazi ya Kata na vijiji, ambapo wagombea mbalimbali walioteuliwa na vyama ndiyo wanaendelea kuchukua fomu hizo.

Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) katika Wilaya ya Bariadi, kimekuwa Chama cha kwanza kwa wagombea wake kuchukua fomu hizo.

Katika Kata ya Malambo iliyoko Halmashauri ya Mji wa Bariadi, Viongozi wa Chama hicho Wilaya wakiwa na wafuasi wao, wamewasindikiza wagombea katika uchaguzi huo kata ya Malambo kwenye kuchukua fomu ofsi za Kata hiyo.

Mamia ya wanachama hao, wakiwa na bendera, pikipiki, walifunga kwa muda mitaa ya Mji wa Bariadi, wakiwasindikiza wagombea wao kwenye kuchukua fomu hizo.

Zoezi la kuchukua fomu lilimalizika Salama, na wagombea hao wakaridhishwa jinsi walivyopokelewa na wasimamizi wasaidizi wa uchaguzi huo Kisha kuwahudumia na kuwapatia fomu hizo.

Mgombea nafasi ya Mwenyekiti wa mtaa wa Ngashanda amesema wamejipanga kuhakikisha fomu hizo zinajazwa mapema iwezekanavyo na kwa usahihi Kisha kuzirejesha.

Wamewaomba wasimamizi wa uchaguzi huo kutenda haki katika kuteua wagombea, lakini pia kutenda haki katika zoezi la kupiga kura ili wananchi waweze kuchagua viongozi wanaowataka.

Mwenyekiti wa Chadema Wilaya, Martine Mogani, amesema kuwa mitaa yote na vijiji katika Wilaya hiyo, tayari wameweka wagombea na wote wameanza kuchukua fomu.

Soma Pia:
Amesema kuwa Chama hicho kitafanya kampeini za kistaarabu pamoja na Amani, lakini hakitasita kuchukua hatua ikiwa kitaingiliwa na watu katika kuvuruga Amani iliyopo.

Nimekuwekea video hapo chini kwa hisani ya Global tv.



Chanzo Global tv.

Ahsante sana mkuu 'KwetuKwanza', kwa mchango wako huu katika kuliokoa taifa letu.

Lakini, hii taarifa imekuwepo hapa ukumbini kwa muda sasa.
Sasa tazama mwamko wa uchangiaji kwenye taarifa muhimu kama hii.

Chawa wote, kasoro huyo 'the baptist' wanapitia mbali kwa hofu kubwa. CHADEMA wao naona walisha achana na kuwa na watu wao haa JF; sana sana kabaki mkuu 'Erythro' na Mshana tu basi.

Hii ni taarifa ya kutia matumaini. Hali kama hii ikienea mikoa yote, CCM itabidi wakajipange upya; maanake hata wizi wa kura na mipango mingine haramu ya kupata ushindi itawawia ngumu sana.

Ngoja tusubiri tuone kama wataanza kununua hawa viongozi kwa hela za waarabu.
 
Safari hii watakiona cha moto
Pengine unajuwa usemalo. Mimi ni nani hadi nihoji?

Itapendeza sana, tena sana hali ikiwa hivi kwenye maeneo mengine nchi nzima; hasa hapo 2025.

Lakini inanilazimu niulize: mbona hizi mada muhimu sana hivi hazina msisimko hapa JF; kuna nini hasa!
Au chawa ndio wanao tawala kurasa hizi siku hizi?
 
Uchaguzi ukiisha utasikia wanasema hawashiriki tena mpka tume huru
 
  • Kicheko
Reactions: Tui
Back
Top Bottom