CHADEMA wafahamu kuwa suala la kutaka Tanzania iwekewe vikwazo ni usaliti mkubwa kwa wapiga kura wake

Kwanza wakiiwekea vikwazo serekali hii haramu iliyokosa utu na huruma kwa wananchi watakuwa wameihurumia sana,inatakiwa ing'olewe kabisa isiwepo kama shetani alivyotupwa kutoka mbinguni na uharamu wake.
 
Siyo Chadema tu. Wananchi tulio wengi sasa tunataka intervention ya jumuiya ya kimataifa katika mazingira haya ambayo polisi ndiyo wanahakikisha chama kimoja ndicho kinashinda kwa heri au kwa shari.

Kumbuka kauli chafu ya yule polisi kule Hai dhidi ya Mbowe - ule ni ushahidi tosha. Kumbuka Halima Mdee alikwenda kuripoti polisi juu ya uhalifu aliotaka kufanyiwa lakini mapolisi walimgeuzia kibao. Ipo mifano mingi tu.
Hii haikubaliki asilani na kwa namna hii hakuna namna bali ni lazima tupate msaada wa watu wengine ili kubalansisha mambo.

CCM waache kutumia polisi kukaa madarakani. Bila ya ridhaa ya sisi wananchi, intervention ya jumuiya ya kimataifa haikwepeki!
 
Kwani tunahitaji misaada ya mabeberu?
 
Anayeleta matatizo kwa Nchi ni CCM kwa kuubaka kuunajisi kuulawiti uchaguzi mkuu kwa njia haramu za kishetani, chanzo cha tabu yote ni CCM siyo vinginevyo
 
Msaliti ni yule tu aliyeiba kura maana huyo ndiyo chanzo. KAMA angekubali tu kuwa watu hawamkubali na hawamuhitaji tusingekuwa tunafikiria vikwazo sasa hivi.
 
Anatufutwa mchawi, acheni akili za kipuuzi. Wahisani si watu wa kushawishiwa wala kuambiwa, ni watu wanaofanya maamuzi yao kwa kutumia vigezo vyao walivyojiwekea. Kumbukeni izo fedha mnazopewa misaada ni fedha za kodi za wananchi wa nchi nyengine ambao kwa huruma zao huona kuna umuhimu wa kusaidia nchi za wanyonge.

Sidhani kama wananchi wao wanafurahi wakiona au kusikia fedha zile zimetumika kununua silaha za kupiga na kufanya mauji kwa wapemba! Mtu huvuna alichokipanda, nadhani watafanya maamuzi ya msingi kuondoa hii misaada. Pia ni kheri ili Tanzani iweze kujitegemea 😉
 
Sisi wafuasi wa chadema wenyewe tunataka nchi ipigwe vikwazo vya hatari ili misukule ya ccm ifunguke akili
 
Msaliti ni yule tu aliyeiba kura maana huyo ndiyo chanzo. KAMA angekubali tu kuwa watu hawamkubali na hawamuhitaji tusingekuwa tunafikiria vikwazo sasa hivi.
Vikwazo vinaletwa na CCM kwa kuendekeza vitendo haramu vya kishamba na kishetani
 
Sisi wafuasi wa chadema wenyewe tunataka nchi ipigwe vikwazo vya hatari ili misukule ya ccm ifunguke akili
Watesi CCM wanajua kuwatesa kuwaonea kuwabambikia kesi kuwapiga risasi wapinzani tu lakini wakisikia vikwazo wanaanza kuchachawa
 
Viongozi wa Chadema hawana akili na ndiyo maana kila uchaguzi wanazinguana wenyewe kwa wenyewe na kuchanganya akili wafuasi wako
 
Mlivyoambiwa mmeingia uchumi wa kati mlifurahi...mtoto umeshakuwa kajitegemee unalialia nini...
Hata wasiposwma tutaenda juu kwa nguvu na juhudi zetu tu,
Waseme wasiseme sawa kwani watatushusha?
 
Viongozi wa Chadema hawana akili na ndiyo maana kila uchaguzi wanazinguana wenyewe kwa wenyewe na kuchanganya akili wafuasi wako
Post zote 34 za waliotangulia kuchangia wamepingana na mleta mada!Wewe wa 35 ndiye umeungana na mleta mada!
Hii inamaana watanzania hawapendezwi na ukandamizwaji wa haki unaofanya na serikali ya CCM kwa kutumia dola!Wakulaumiwa hapa ni serikali ya CCM!
Mmetugawa sana wananchi,mnapandikiza chuki katika jamii!
 
Hata wasiposwma tutaenda juu kwa nguvu na juhudi zetu tu,
Waseme wasiseme sawa kwani watatushusha?
Uzi huu unatoa tafsiri fulani!Post zote 34 za kwanza zimempinga mleta mada!
Hii ni wazi mmeleta mgawanyiko baina ya watanzania,ama kweli haki huinua utaifa na kinyume chake!
 
CCM imewasaliti sana watanzania kwa kunajisi demokrasia na hivyo kupelekea nchi kuwekewa vikwazo na jumuia ya kimataifa!
 
Kaka sijui ulitaka sasa waende kwa Siro? au Tume ya Uchaguzi ya Mahera? toa suruhisho acha kulalamikatu . Kumbuka kuwa Chadema hawawapangii Wahisani adhabu ya kutoa kwa wachafuzi wa uchaguzi, kumbuka Demokrasia haikuletwa na Chadema bali imeletwa na hao hao wahisani ambao wengine wapo Belgium pia. Kwa hiyo kama tulikubali demokrasia na masharti yake lazima tuyaishi.Hakuna namna nyingine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…