Chadema Wajikite kwenye Katiba Mpya suala la DP World limeshashughulikiwa na Waraka wa TEC pamoja na akina Mwabukusi!

johnthebaptist

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2014
Posts
97,869
Reaction score
171,716
Mkutano wa Chadema pale Shinyanga Mjini haukuwa na msisimko kwa sababu mambo waliyoongea yalikuwa yanajirudia

Mambo ya DP World yameshawasilishwa kwa Wananchi kwa upana sana kupitia Waraka wa TEC ambao TV Imaan na hata BASUTA wameufanyia rejea

Ni vema sasa Chadema mkajikita kwenye kudai Katiba Mpya

Nawatakia Sabato Njema πŸ˜„
 
wacha waendelee na ndp world watakuja kushtukia 2025 hawajauza sera zao tena sasa hivi wauze sera siyo matusi wananchi waanashindwa kuwaelewa
 
Issue ya DPW haitakiwi kupoa.

Ikiwezekana itungiwe na nyimbo
 
Mkuu. johnthebaptist Mimi nina maoni tofauti kidogo kwa hilo jambo.
Kwa sababu yote ni mambo mawili tofauti lakini yenye maslahi mapana kwa taifa letu.

Katiba mpya ni muhimu kuelekea uchaguzi mkuu wa 2025.
Pia la DP-WORLD halipaswi kuachwa lipowe kwa sababu likipoa tayari mafisadi hawa wataendelea na mikakati yao na hatimae kulikamilisha.

Pia kupitia siasa za majukwaani,kule kunakuwa na watu wa madhehebu yote sambamba na wapagani pia.

Na pia hizo ndio agenda ambazo hukipa chama kitu inaitwa
"Political Mileage."
Kwa hiyo Chadema waachwe waendelee na huo moto wao.
 
Inashangaza sana kuwa hata wewe johnthebaptist huwezi kuelewa connection ya matatizo ya nchi hii ikiwemo hii skendo ya mkataba wa bandari/DP World kuwa ni Kwa sababu ya udhaifu wa katiba tuliyonayo..

Ndo kusema, skendo ya mkataba wa bandari na DP World imeinogesha na kuiongezea nguvu agenda ya umuhimu kuandika katiba mpya Tanzania.

Ni kwa mantiki hii kuwa, huwezi kuongelea katiba mpya bila kuihusisha na majanga mengi na makubwa ya nchi hii likiwemo hili skendo ya mkataba wa bandari/DP World pamoja na mapungufu makubwa ya muungano wa Tanganyika & Zanzibar..

Ingekuwa ni mwalimu anafundisha darasani tunasema, mkataba wa bandari na bubwasha linaloitwa DP World ni zana ya kufundishia (teaching aid) ya mada inayoitwa UMUHIMU WA KATIBA MPYA...

Kwa hiyo CHADEMA wako sawasawa kabisa. Na Tundu Lissu alisema, skendo ya mkataba wa bandari kwao ni agenda ya kisiasa. And they are damn right..!
 
DPW itaongezea sana ushawishi na credibility ya TEC. TEC wameamua kuwa upande sahihi wa historia. Muda utadhihirisha haya.
 
Nimekuelewa Lakini waje na mbinu mpya ya ufundishaji
 

Nimekuelewa Lakini waje na mbinu mpya ya ufundishaji
Wewe ni nani wa kuwapangia? Unaonaje ukija na hiyo mbinu wewe?
 
Nimekuelewa Lakini waje na mbinu mpya ya ufundishaji
Hiyo wanayoenda nayo na kutumia ndiyo mbinu sahihi ya kufundisha somo la UMUHIMU WA KATIBA MPYA na wapinzani wao wakuu - CCM wanaelewa kabisa kuwa walilikoroga wenyewe na inawawia ngumu sana kudhibiti uharibifu huo waliokwisha kuufanya wenyewe..

Mimi nawafuatilia vyema CHADEMA hatua kwa hatua (Operesheni yao sasa iko kanda ya Serengeti yenye mikoa ya Shinyanga, Simiyu & Mara) na Jana walianzia Shinyanga mjini...

Honestly, kwa namna wanayokutana na wananchi na namna wanavyowasilisha agenda ya Katiba Mpya + Okoa Bandari Zetu reference ikiwa ni mkataba wa bandari - DP World, ni kwa umaridadi mkubwa sana na wenye kueleweka kirahisi kwa wananchi..

Narudia Tena kusema, hapo waliposhika na kupapiga ni penyewe. Hakuna kuachia..
 
wanasiasa makini wanaweza kuufanyia kazi ushauri huu, lakini wanaharakati Lazima wakushukie kama mwewe na matusi juu 😳
 
wanasiasa makini wanaweza kuufanyia kazi ushauri huu, lakini wanaharakati Lazima wakushukie kama mwewe na matusi juu 😳
Nyingi wote ni vichwa maji tu! Unaona issue ya bandari ni ndogo wakati unahusu mapato na mapato ndo uhai wa nchi! Acheni propaganda za ukada!
 
Kuna sheria inakubana wewe kuyafanya hayo wasio yafanya wao?
 
Limeshughulikiwaje? Hebu thibitisha.
 
Kwani kulikuwa na tatizo katika Hilo? Hebu yaeleze...kama yalikuwepo au yapo..
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…