Uchaguzi 2020 CHADEMA wanajipa matumaini hewa

Uchaguzi 2020 CHADEMA wanajipa matumaini hewa

Kwanza kabisa me sio mpenzi wa vyama vya Siasa ila nimekuwa mfuatiliaji wa siasa za Tanzania. Nimefatilia mchakato mzima wa chama Cha Chadema na wote tumejua wagombea wa uraisi watakao chuana na Dr. John Magufuli niwe mkweli katika hai wagombea wote sijaona hata mmoja atakayepata kura kuanzia 40% kuendelea dhidi ya Magufuli, keep it in your mind.

Nimeona humu jamvini wapenzi wa Chadema wakiaminishana watashinda uchaguzi mkuu. Niwaambie kitu: Hakuna Jambo zuri kama kukubali hali halisi kuliko kujipa matumaini hewa.

Kuwa rais wa nchi sio jambo jepesi kama wanavyoaminishana wanaChadema. Kuna vitu vingi vinavyo determine mtu kuwa raisi Kama ifuatavyo:

1. Financial capability
Uwezo wa mgombea kuwa na uwezo mkubwa wa kifedha au Chama kinachomsimamisha wa kufanya kampeni kwenye maeneo mengi ya Tanzania.Ukiangalia wagombea wa chadema hawana uwezo mkubwa wa kifedha. Lowassa aliweza kupata kura around 6 million; haikuja kwa urahisi ali-invest sana hela. Kwanza alinunua baadhi ya vipindi vya television ikiwemo ITV kuwafikia Watanzania wengi, ndio mgombea pekee aliyewahi kutokea wa upinzani ambaye aliyofanya kampeni maeneo mengi ya Tanzania n.k

2. Strong group support
Hapa tuna angalia makundi yenye nguvu Magufuli ana support kubwa ya viongozi wa dini zote na amecheza karata zake vizuri amejenga misikiti na amekuwa karibu Sana na viongozi wa kiislamu karibia shughuli zote pia ana support ya viongozi wa kikristo hata wale waliokuwa wanampinga sasa wapo upande wake kama mchungaji wangu Maksai wa kanisa la Korogwe huyu alikuwa ni Team Lowassa na alimpigia sana kampeni kanisani ila nowdays ni Team Magufuli na amekuwa anampaisha sana kanisani. Kuna Lusekelo, kuna Gwajima n.k Kuna magroup mengine ila naomba niishie hapo wakati Chadema haina mahusiano mazuri na viongozi wa dini.

3. 99.9% of artists support CCM
Wasanii wote wenye influence kubwa kwenye Jamii wanaisapoti CCM Kama vile Diamond and WCB in general ambao Wana wafuasi wengi sana kwa jina la "Team WCB" Kuna Alikiba, Harmonize, Mwana fa n.k

4. Kuwekeza kwenye majimbo aliyokosa kura
Hii Ni sababu itakayompa ushindi mnono Magufuli mf. Jimbo la Arumeru Arusha lilikuwa na tatizo sugu Sana la ukosefu wa Maji ila chini ya Magufuli ameleta mradi mkubwa wa Maji lakini pia walikuwa wanasumbuliwa na tatizo la Umeme tangu aingia Magufuli ameweza kupunguza tatizo la Umeme kwa kiasi kikubwa Sana. Kuimarisha usafiri wa treni Moshi, la tatu ni kuweka Dar kajenga flyover na miundombinu ya Barabara lakini uko kwetu kimara kulikuwa na tatizo maji kwa kiasi kikubwa na nikilio kikubwa kwa wakazi wa Ubongo, Kimara na Mbezi Magufuli amelitatua kwanza kwa kuaweka mabomba maeneo yote bure na wanatoa maji karibia wiki nzima. Suala mgao wa Umeme ulikuwa unaboa Sana na ilikuwa Ni tatizo kuu sana kwa dar ila now day inaweza kuchukua miezi hata 6 Umeme usikatike na hata ukikatika unarudi mapema tofauti na kipindi Cha nyuma.

NB: Kama nilivyotoa analysis yangu kwa kifupi Chadema hata kupata Asimilia 40 ya kura itakuwa ngumu kupata huo ndio ukweli wenyewe.Na bahati nzuri nyuzi zinabaki humu Kama kumbukumbu tutajionea.
Kwa maoni yako haya hukutaka uchaguzi ufanyike ?!. Au lengo ni nini, Magufuli asipingwe ?!.

Nikukumbushe kitu kimoja . Wakati Magufuli anachukuwa fomu za kuomba kazi aliyonayo Leo, hakuwa na nguvu kama kina Lowassa, Membe na hata Sitta. Lakini leo ni Rais na si hao waliokuwa ma giants.

Kitu muhimu ungesema tume tulionayo si tume huru ya uchaguzi . Lakini ukisema swala la kukubalika, huwezi kujiamini mambo ya kura za siri.
 
Mzee hapa nimechambua kutokana na siasa ilivyo sio kwasababu ya hisia zangu hatuwezi kumezeshana uongo wahati ukweli unaonekana.Kuhusu kupenda au kutopenda kwa CCM kuendelea madarakani nazani hiyo ipo kwa wafia chama hata hao chadema unao wahabudu sioni wanatofautiana Nini na CCM
Nimewauliza wanaccm wengi swali hili; kwanini mnaichagua ccm? majibu yake ni yale yale kama yakwako; Hakuna sababu ya msingi...ni hatari.
 
Kwa maoni yako haya hukutaka uchaguzi ufanyike ?!. Au lengo ni nini, Magufuli asipingwe ?!.

Nikukumbushe kitu kimoja . Wakati Magufuli anachukuwa fomu za kuomba kazi aliyonayo Leo, hakuwa na nguvu kama kina Lowassa, Membe na hata Sitta. Lakini leo ni Rais na si hao waliokuwa ma giants.

Kitu muhimu ungesema tume tulionayo si tume huru ya uchaguzi . Lakini ukisema swala la kukubalika, huwezi kujiamini mambo ya kura za siri.
Magufuli alipata nguvu kwa sababu ya ndio alikuwa mgombea mkuu wa CCM pili baada ya makosa mengi aliyofanya Lowassa baada ya kuwa akipiga kampeni dakika 5 karibia maeneo mengi pia kuchafuliwa kwa kashifa ya ufisadi.
 
Nimewauliza wanaccm wengi swali hili; kwanini mnaichagua ccm? majibu yake ni yale yale kama yakwako; Hakuna sababu ya msingi...ni hatari.
Sitakuja kupenda chama chochote Cha siasa Cha Tanzania by any means atanikikuuliza wewe kwanini unakipenda chama Cha Chadema wewe ujanijibu Nini?
 
Sitakuja kupenda chama chochote Cha siasa Cha Tanzania by any means atanikikuuliza wewe kwanini unakipenda chama Cha Chadema wewe ujanijibu Nini?
Nataka madiliko baada ya miaka 60 ya ccm. Nchi zilizoendelea zote ambazo tunawapigia magoti kuomba hela wanabadilisha chama kila baada ya miaka 4 au 8. Na sisi tunashangaa kwanini tunawakimbilia kuomba hela; tunapenda hela yao lakini hatupendi wanachofanya kupata hela hiyo.
 
Magufuli alipata nguvu kwa sababu ya ndio alikuwa mgombea mkuu wa CCM pili baada ya makosa mengi aliyofanya Lowassa baada ya kuwa akipiga kampeni dakika 5 karibia maeneo mengi pia kuchafuliwa kwa kashifa ya ufisadi.
Nimekuuliza sasa lengo lako ni nini ?! Hutaki apingwe kwenye uchaguzi ?!. Au ulitaka chama gani kimuwekee mgombea wa kumpinga !!
 
Nimekuuliza sasa lengo lako ni nini ?! Hutaki apingwe kwenye uchaguzi ?!. Au ulitaka chama gani kimuwekee mgombea wa kumpinga !!
Nashangaa unaniuliza swali la kipuuzi Kama Hili au kichwa nikigumu kuelewa kusoma kote thread yangu na umeshindwa kujua Nini nimelenga any way nilichoandika hapo Ni mtazamo au maono yangu ya uchaguzi wa mwaka Huu.
 
Nataka madiliko baada ya miaka 60 ya ccm. Nchi zilizoendelea zote ambazo tunawapigia magoti kuomba hela wanabadilisha chama kila baada ya miaka 4 au 8. Na sisi tunashangaa kwanini tunawakimbilia kuomba hela; tunapenda hela yao lakini hatupendi wanachofanya kupata hela hiyo.
Je unavyoona wewe Chadema ndio itaisaidia hii iwe Tajiri?
 
Niambie Ni kwanini?
Mfumo wa ccm ni wa zamani tangu mwaka 1954. Watu wengi waliokulia kwenye mfumo huu walikuwa na lengo la kupigania uhuru wa nchi miaka ya 1960. Wengi chini ya Nyerere walikuja kuwa wajamaa. Huu ni mfumo maskini sana na mataifa waliyochukua mfumo huu walijikuta wakiwa maskini wakubwa e.g. Msumbiji, na nchi kadhaa za America ya Kusini.

Watu hawa kwenye mfumo wa ccm wamejenga himaya au genge lenye lengo la kujilinda wao wenyewe. Ukiwaunga mkono wanakupa nafasi kwenye genge lao. Wamezoea kutawala na kupata fedha kirahisi kwa njia ya madili ya serikalini. Hawajui biashara wala hawana ujuzi wa mikakati mbalimbali. Hawajui namna ya kujituma na kufanya kazi kwa maarifa, wamezoea kufanya mambo ili mradi wao wanafaidika haijalishi.

Ona jinsi viwanda vyote walivyoacha wakoloni vilivyokufa chini ya Mwalimu. Ona mashirika mbalimbali yaliyokuwepo, ni mengi sana siyataji hapa yalivyokufa, shirika la ndege, shirika la meli, mashamba ya mkonge, kahawa, hata korosho ona zinavyokosa soko, tumbaku, n.k. Watu kama akina Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli, hawajawahi kufanya biashara na hawajui biashara, unafikiri mtu kama huyu atasimamia mgawanyo mzuri wa dili au mkataba wa madini? Kenya marais waliopita walikuwa watu wenye mashamba makubwa, mahoteli n.k, wanajua uchumi ni nini.

Chadema ina watu wanaojua uchumi na wao wenyewe wamewahi kufanya kazi nje ya siasa sio kama wana ccm ambao ni watu wa mtandao wa ccm tangu kuzaliwa wanapiga siasa tu. Usitegemee mtu huyo aweze kuleta mabadiliko na kunyanyua kilimo na biashara nchini, atakuwa mtu wa kukwapua tu vilivyo tayari mezani. Ndivyo walivyo ccm na hivyo tunahitaji akili mpya.
 
Umeandika vitu vya ukweli kabisa
Zile kura million 6 za lowasa sio za Chadema ni za ukawa
Ukitaka upate uhalisia subiri October CDM wakipata kura mil 3 wafanye sherehe kabisa

2015 vijana wengi walikuwa na hamasa ya kufanya mageuzi bila kujali mgombea ni nani?
Yule mkwele alifanya makosa mengi na ya wazi kabisa
Hadithi za EPA, KAGODA, RICHMOND, ESCROW, GES YA MTWARA,
mikataba ya IPTL, AGRECO,
KUKATIKA UMEME OVYO OVYO
MAJI HAKUNA
MAWAZIRI WAPIGAJI
RAIS MKWELE KUWA KAMA VASCO DAGAMA
BUNGE LA 2010 / 2015 Kutawaliwa na hoja za nguvu za upinzani
Haya yote yaliwatia hasira wananchi wakataka kufanya mageuzi
Mbowe akaja kuhalibu kabisa mageuzi
Tulipata kura mil 6 za hasira
Lakini uchaguzi huu 2020
Kwanza Rais ameshajulikana iwe isiwe
Pili upinzani umepararaizi
Vijana awana tena ile hamasa
Msije kushangaa kusikia wapiga kula wa 2020 awazidi mil 10


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mfumo wa ccm ni wa zamani tangu mwaka 1954. Watu wengi waliokulia kwenye mfumo huu walikuwa na lengo la kupigania uhuru wa nchi miaka ya 1960. Wengi chini ya Nyerere walikuja kuwa wajamaa. Huu ni mfumo maskini sana na mataifa waliyochukua mfumo huu walijikuta wakiwa maskini wakubwa e.g. Msumbiji, na nchi kadhaa za America ya Kusini.

Watu hawa kwenye mfumo wa ccm wamejenga himaya au genge lenye lengo la kujilinda wao wenyewe. Ukiwaunga mkono wanakupa nafasi kwenye genge lao. Wamezoea kutawala na kupata fedha kirahisi kwa njia ya madili ya serikalini. Hawajui biashara wala hawana ujuzi wa mikakati mbalimbali. Hawajui namna ya kujituma na kufanya kazi kwa maarifa, wamezoea kufanya mambo ili mradi wao wanafaidika haijalishi.

Ona jinsi viwanda vyote walivyoacha wakoloni vilivyokufa chini ya Mwalimu. Ona mashirika mbalimbali yaliyokuwepo, ni mengi sana siyataji hapa yalivyokufa, shirika la ndege, shirika la meli, mashamba ya mkonge, kahawa, hata korosho ona zinavyokosa soko, tumbaku, n.k. Watu kama akina Mwinyi, Mkapa, Kikwete, Magufuli, hawajawahi kufanya biashara na hawajui biashara, unafikiri mtu kama huyu atasimamia mgawanyo mzuri wa dili au mkataba wa madini? Kenya marais waliopita walikuwa watu wenye mashamba makubwa, mahoteli n.k, wanajua uchumi ni nini.

Chadema ina watu wanaojua uchumi na wao wenyewe wamewahi kufanya kazi nje ya siasa sio kama wana ccm ambao ni watu wa mtandao wa ccm tangu kuzaliwa wanapiga siasa tu. Usitegemee mtu huyo aweze kuleta mabadiliko na kunyanyua kilimo na biashara nchini, atakuwa mtu wa kukwapua tu vilivyo tayari mezani. Ndivyo walivyo ccm na hivyo tunahitaji akili mpya.
Naona umemezeeshwa propaganda Sana unaweza ukawa ukipendi Chams Cha CCM ila chadema ni kibovu kuliko hata CCM yenyewe tangu lini chadema wanajua uchumi? Lakini pia akina demokrasia Kama Ccm hiv umewahi kuona hata ilani ya CHADEMA? Ebu kuwa serious.
 
Kwanza kabisa me sio mpenzi wa vyama vya Siasa ila nimekuwa mfuatiliaji wa siasa za Tanzania.
Wewe ni m CCM kindakindaki. mnafahamika kwa kujivunia na kuusifu u dictator wa Jiwe, badala ya kuuonea haya.
Miaka minne bila ya chembe ya aibu, wengine mmewazuiwa kufanya siasa, lakini bado mnawaogopa.
Mnajijua pamoja na makelele na vitisho vyote, hamjaweza kugusa nyoyo za waTZ, 90% ya mnayofanya sio mahitaji yao ni yenu na mikogo yenu.
Kiburi chenu chatokana na tegemeo la kubebwa na walofaidika na teuzi na matumizi ovu ya vyombo vya dola.
Kama mwana ambae amekuwa akiandamwa na kuonewa na wazazi wake,mwaka huu HATUOGOPI tena.
 
Wewe ni m CCM kindakindaki. mnafahamika kwa kujivunia na kuusifu u dictator wa Jiwe, badala ya kuuonea haya.
Miaka minne bila ya chembe ya aibu, wengine mmewazuiwa kufanya siasa, lakini bado mnawaogopa.
Mnajijua pamoja na makelele na vitisho vyote, hamjaweza kugusa nyoyo za waTZ, 90% ya mnayofanya sio mahitaji yao ni yenu na mikogo yenu.
Kiburi chenu chatokana na tegemeo la kubebwa na walofaidika na teuzi na matumizi ovu ya vyombo vya dola.
Kama mwana ambae amekuwa akiandamwa na kuonewa na wazazi wake,mwaka huu HATUOGOPI tena.
Mzee una ushabiki maandazi
 
Umeandika mambo mengi wakati huwa mnapata msaada toka kwa Tume feki ya uchaguzi, na jeshi la polisi; hayo yote uliyoandika hayana maana.
40% ni mbali sana... 17%watajikamua sana.
 
Back
Top Bottom