Uchaguzi 2020 CHADEMA wanasubiri kwanza Ilani ya Uchaguzi ya CCM itolewe!

Uchaguzi 2020 CHADEMA wanasubiri kwanza Ilani ya Uchaguzi ya CCM itolewe!

MsemajiUkweli

JF-Expert Member
Joined
Jul 5, 2012
Posts
13,171
Reaction score
23,996
Siasa zina mbinu nyingi katika ushindi. Moja ya mbinu ni kujua adui wako ana silaha za aina gani kabla haujaingia kwenye mapambano!

Kwa mfano, Miaka ya nyuma, wapinzani walikuwa wanasubiri kwanza CCM iteuwe wagombea wake ili waliokatwa wajiunge kwenye vyama vyao. Kwa kutumia mbinu hii, vyama vya upinzani vilikuwa vinanufaika na kuongeza ruzuku.

Mwaka huu, CCM waliamua kutangaza wagombea wao siku nne kabla ya zoezi la kuchukua fomu na kurudisha halijafungwa. Mbinu hii kwa kiasi kikubwa imefanikiwa kwa sababu hata wale waliojiunga upinzani baada ya kukatwa wamejikuta katika wakati mgumu kutimiza malengo yao. Mfano mmojawapo ni aliyekuwa Mbunge wa CCM katika Jimbo la Nachingwea, Hassan Masala ambaye alijiunga ACT-Wazalendo baada ya jina lake kukatwa, jana ameamua tena kurudi CCM.

Inasemekana CHADEMA kwa sasa wanasubiri kwanza CCM watoe Ilani yao ya Uchaguzi 2020-2025 ili waisome na baadaye warekebishe Ilani yao katika maeneo ambayo wanadhani CCM hawakuyagusa au wameyagusa lakini sio kwa undani zaidi. CHADEMA wanachofanya ni kutengeneza mazingira ya kujibu mapigo ya Ilani ya CCM. Hii ni mbinu nzuri ya kivita pamoja na kwamba ina matatizo yake ambayo kwangu nayaona hayana athari ukilinganisha na faida zake.

Je, CCM watazindua Ilani yao ya Uchaguzi kesho au nao watasubiri/kuahilisha kama ambavyo CHADEMA wanafanya?.

Tusubiri Kesho katika Uzinduzi wa kampeni za CCM kupata jibu sahihi!
 
Hakuna Upinzani nchi hii
Hao ni Mamluki wakiwatumikia Mabwana zao
Hawa Mwaka huu watapokea kipigo cha Mbwa koko
Kufikisha 20% Itakuwa ni ushindi kwao
 
Baada ya CHADEMA kushindwa kuzindua ilani yao wanashinda humu JF wanachukua michango ya wadau na kuitumia kama ilani ambacho ni kivyume cha taratibu kwani ahadi yapaswa kutoka katika kitabu ambacho ndio mkataba wa wananchi na watawala.

Licha ya kusema kuwa hawatazindua ilani mapaka walienguliwa warejeshwe hali ibadilika na sasa wameanza kuokoteza hoja za wanajamiiforums na kuzitumia kama hoja bila kuonesha zimeandikwa wapi katika ilani.

Walioko ndani ya chama wanadai kuna ukata wa kulipia kwa mchapaji hivyo itahita mizinga kwa wanachama na watanzania kuwachangia kuokoa jahazi ambacho ni aibu kwa chama chenye ruzuku huku vyama vidogo vizivyo na ruzuku vikijitegemea na kumfanya lisu na kundi lake wakeshe humu jf kutafuta maoni wakaseme bila kuonesha yameandikwa wapi katika ilani.

Ilani ndio mkataba na kwa vyovyote ilipaswa kuonesha wapi wamesema nini zaidi ya kukutupuka na kuahidi na baadae waje waseme haipo kwenye ilani.

USSR
 
Magufuli hana chochote kipya cha kuahidi, na hata akiahidi itakuwa ni uongo na hataweza kutekeleza. Ifahamike Magufuli ana miradi miwili ya 15t+. Na hakuna mradi wowote uliofika robo. Kama ameshaweka hela kwenye hiyo miradi miwili, basi ni chini ya 7t tena za mkopo.

Ni wapi anaenda kupata 10t kwenye miaka yake mitano ili kumalizia hiyo miradi, na wakati huo huo ataoe ahadi ya kuongeza mishahara? Tujiandae kuongezewa kodi zaidi, na wakati huo huo ni lazima yeye na wanaccm wenzake wachezee katiba ili aongezewe muda wa kukaa madarakani, maana hana uwezo wa kumalizia hiyo miradi miwili ndani ya miaka mitano, iwapo tume isiyo huru ya uchaguzi itamtangaza.
 
Magufuli hana chochote kipya cha kuahidi, na hata akiahidi itakuwa ni uongo na hataweza kutekeleza. Ifahamike Magufuli ana miradi miwili ya 15t+. Na hakuna mradi wowote uliofika robo. Kama ameshaweka hela kwenye hiyo miradi miwili, basi ni chini ya 7t tena za mkopo...
Mkuu hii mada inamuongelea Magufuli au chadema?
 
Kwani wanajamii forum ni MABEBERU Hadi maoni yao yasisikilizwe?
 
Magufuli hana chochote kipya cha kuahidi, na hata akiahidi itakuwa ni uongo na hataweza kutekeleza. Ifahamike Magufuli ana miradi miwili ya 15t+. Na hakuna mradi wowote uliofika robo...

kuna mda unatoaga mada zenye mashiko lakini kuna mda yaani daah, bora ukae kimya tu
 
kuna mda unatoaga mada zenye mashiko lakini kuna mda yaani daah, bora ukae kimya tu
Hapo ameweka kitu gani chenye mashiko? JNHPP inakamilika mwakani mwezi wa sita na ataanza kupata umeme wa bwerere. Sgr ikivuka Dodoma inakamilika fasta.
 
Back
Top Bottom