Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Hapa ni uzushi mtupu kwani kyela kuna vitongoji vingapi? na CCM imesambaratishwa kivipi? Unamaanisha chadema wameikamata Kyela?.Tupe jumla ya vitongoji vilivyochukuliwa na CCM na vile vilivyochukuliwa na chadema. KUshindwa kwa mpambe wa Mwakyembe katika kitongoji ndio kushindwa kwa Mwakyembe?. Hapa ni kujifariji tu. Umejaa uzushi mtupu.
Mkuu,
Vipi zile habari zako fake za vikao vya NEC unaona hazitoshi na unaanza kuingilia na Kyela?
Sisi hatuhitaji kupiga simu kujua yanayotokea Kyela, tunayaona yakitendeka. Utashangaa sana mwaka huu na hao wapiganaji wako.
Mpigia simu huyo rafiki yako Mwakyembe na mwulize mbona anashindwa hata kusalimiana na majirani zake?
Vinginevyo ya Kyela niachie mimi engineer wa Majungu according to Masanilo (aka Ze Comedy_ niendelee kuwaletea za jikoni.
Buchanan,
Hii habari mbona niliileta siku ile ile ya uchaguzi?
1. mheshimiwa aliweka wapambe wake .....akafanya kampeni ya wiki nzima.
2. ikaweka mkakati wa kuwatungua hao wapambe wote wa Mwakyembe.
3. kundi likawaunga mkono.
4. Wao wanasema lengo lilikuwa kumpa kipigo mbunge
5. pia kuwatisha madiwani wachache ambao bado wanamuunga mkono Mwakyembe
6. wajiandae kupoteza nafasi zao kama wataendelea kumshabikia huyo msanii.
7. hata kitongoji anakotoka Mwakyembe (Ikolo) nacho kikatekwa.
8. Kilumbu, ambaye ndiye mfuasi mkubwa wa Mwakyembe aliangushwa na mzee mmoja mganga wa kienyeji.
9. Ukiwa karibu na mwakyembe hapa Kyela kwasasa jua kitumbua chako kisiasa kiko hataraini.
10. Mimi naona alifanya makosa makubwa sana kuweka wapambe wake
11. maana hii imeonyesha watu wengi kwamba Dr ni weak
12. waliokuwa wanamuunga mkono, taratibu wanaanza kutafuta namba za Mwakalialinga ili wamsalimie.
13. Hizo ndio siasa za Kyela.
Kweli wewe huijui Kyela, labda ni wale wale wa mpaka kupiga simu.
Rhoda Mwamunyange anataka kugombea ubunge kupitia UWT na tayari anaunganisha nguvu na kundi moja hapa.
Kyela kuna wengi tu wanataka kugombea na tunawakaribisha wote, ila mchuano mpaka sasa ni wa Mwakyembe na Mwakalinga.
Wewe unafikiri uongozi ni kuwa balozi tu? Endelea kuota ndoto hivyo hivyo.