Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 2,060
- 5,648
Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) itakutana katika kikao cha dharura kesho, Ijumaa tarehe 29 Novemba 2024. Kikao hicho kitajadili matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji 2024 na kutoa msimamo rasmi wa Chama. Mwenyekiti wa Chama, Mhe. Freeman Mbowe, atakiongoza kikao hicho, na kauli rasmi itatolewa baada ya kikao kumalizika.