LGE2024 CHADEMA yatoa tamko baada ya Freeman Mbowe kukamatwa na Jeshi La Polisi

LGE2024 CHADEMA yatoa tamko baada ya Freeman Mbowe kukamatwa na Jeshi La Polisi

Uchaguzi wa Serikali za Mitaa 2024
CHADEMA kama wanataka salama waniteue mimi niwe mgombea wao. Siku naapishwa kwenye siku 100 za kwanza ni kufuta CCM na kuweka ndani viongozi wake wakuu wa wakati huo! Nitaagiza mahakama iwafungulie mashitaka ya uhaini hata kama haupo! Chama la kipumbavu hili! Linahofu kwa vile halijawahi kufanya chochote kwa nchi hii!
 
Wakuu,


Chama cha Demokrasia na Maendeleo CHADEMA kimesema kuwa viongozi wake akiwemo Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe pamoja na Mwenyekiti wa Kanda ya Nyassa Joseph Mbilinyi (SUGU) pamoja na wanachama wengine wamekamatwa na Jeshi la polisi mkoani Songwe.

Kupitia taarifa iliyotolewa na Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya Nje John Mrema imeleza kuwa viongozi hao wamekamatwa leo Novemba 22 katika Pori la Halungu lililopo wilayani Mbozi.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa polisi walivamia msafara na kumkamata Mbowe pamoja na viongozi mbalimbali aliokuwa ameambatana nao. Viongozi waliokamatwa wengine ni pamoja na Pascal Haongo ambaye ni Mbunge wa Mbozi Mashariki mstaafu na Mwenyekiti wa Chama Cha ACT Wazalendo Wilaya ya Mbozi Ezekia Zambi.

Wengine waliokamatwa ni Appolinary Boniface Mkuu wa Digital platform, Paul Joseph na Calvin Ndabila ambao ni maafisa habari Kanda ya Nyassa, Mwanaharakati Mdude Nyagali pamoja na wasaidizi wa Mbowe ambao ni Bwire, Adamoo na Lingwenya.

Hata hivyo CHADEMA imelaani kitendo cha kukamatwa kwa viongozi hao huku ikitoa wito kwa jumuiya za kimataifa kushirikiana nao kwa kile walichokiita uvunjifu wa kidemokrasia.

Jambo TV imefanya jitihada za kumtafuta Kamanda wa polisi Mkoa wa Songwe Kamishna Msaidizi Mwandamizi SACP Agustino Senga hata hivyo kupitia afisa habari wa Jeshi la polisi mkoani humo amesema kuwa watatoa taarifa rasmi baadae.
Nendeni kwenu Kilimanjaro cc mbeyahatuwataki
 
Back
Top Bottom