Pre GE2025 CHADEMA yatoa wito kwa Rais Samia avunje Jeshi la Polisi na aliunde upya

Pre GE2025 CHADEMA yatoa wito kwa Rais Samia avunje Jeshi la Polisi na aliunde upya

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Erythrocyte

JF-Expert Member
Joined
Nov 6, 2012
Posts
128,308
Reaction score
245,426
Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) kimeendelea kutoa wito kwa Amiri Jeshi Mkuu na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan kulifumua Jeshi la Polisi nchini kwa kile ilichodai kuwa limeshindwa kutimiza majukumu yake na kwamba interejensia yake imefeli kwa kiasi kikubwa

Mkurugenzi wa Itifaki, Mawasiliano na Mambo ya nje wa chama hicho John Mrema amezungumza hayo wakati akizungumza na wanahabari leo, Ijumaa Agosti 30.2024, mkutano uliolenga kukanusha taarifa iliyotolewa na Jeshi la Polisi iliyotoka mapema leo ikidai kuwa viongozi wa chama hicho wamepanga njama za siri za kufanya matukio ya uvunjifu wa amani ikiwemo kuvamia kwenye vituo vya Polisi

Kuhusu uwepo wa madai ya watu kutekwa na kupotea, CHADEMA imeendelea kumshauri Rais Dkt. Samia kuingilia kati jambo hilo na kuunda tume maalum yenye hadhi ya kijaji ili ifanye uchunguzi wa mambo hayo kwa kuwa haikubaliki kuona Jeshi la Polisi linalotuhumiwa kuhusika kwa matukio hayo kwa namna moja au nyingine kuonekana likifanya uchunguzi

Katika hatua nyingine CHADEMA imetoa wito kwa Jeshi la Polisi nchini kuacha kuwachukulia viongozi wa chama hicho kama wahalifu, na kwamba Jeshi hilo linapaswa kutoka hadharani kufuta kauli hiyo

Screenshot_2024-08-30-17-30-36-1.png
Screenshot_2024-08-30-17-30-36-2.png
 
Intelijensia ya polisi ipo vizuri na Nchi ipo salama isipokuwa vijiutekaji tu vinasumbuasumbua.
 
Jeshi la polisi linatakiwa kufumuliwa hasa ngazi ya SACP kwenda vyeo vya CP wastaafishwe wote.

Hii itasaidia kurejesha usimamizi wa nidhamu na utendaji wa walio chini yao kuzingatia kanuni na GPO ya polisi wanapotumwa askari kwenda kukamata watuhumiwa.

27 August 2024​

Masauni Akutana na Uongozi wa Jeshi la Polisi Kujadili Hali ya Amani na Usalama​

Dodoma. Waziri wa Mambo ya Ndani, engineer Hamad Masauni leo amekutana na viongozi wa juu wa Jeshi la Polisi Tanzania kujadili hali ya amani na usalama ikiwemo matukio ya uhalifu yanayotkea nchini na hatua zilizochukuliwa.
1725029792527.png


Kikao hiko pia kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya ndani, Daniel Sillo, ambapo kwa upande wa Jeshi la Polisi ujumbe wake uliongozwa na Inspekta Jenerali wa Polisi, Camillus Wambura.


Kikao hiki kinakuja ikiwa ni siku chache tangu Jeshi la Polisi kupitia kwa msemaji wake kutoa taarifa za matukio mbalimbali ya kiuhalifu yanayohusu watu kupotea na mauaji ambayo Polisi ilieleza yalitokana na sababu mbalimbali ikiwemo masuala ya kujichukulia sheria mkononi, wivu wa mapenzi na imani za kishirikina.


Lakini pia wadau mbalimbali ikiwemo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Asasi za Kiraia na vyama vya siasa wamekuwa wakipaza sauti kufuatia kuripotiwa kwa matukio ya utekaji na mauaji ya watu wazima na watoto.

Baadhi ya wadau hao ikiwemo vyama vya siasa wamewatupia lawama Jeshi la Polisi wakiwashtumu kuhusika jambo ambalo wamelikanusha.


Kikao hiko cha Waziri Masauni kilihudhuriwa na viongozi wote wa kamisheni za Polisi ikiwemo Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimaliwatu, Suzan Kaganda, Kamishna wa Fedha na Lojistiki, Liberatus Sabas, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Awadh Juma Haji, Kamishna wa Sayansi ya Uchunguzi wa Jinai, Shabani Hiki.


Wengine ni Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai CP Ramadhani Kingai, Msemaji wa Jeshi la Polisi, ACP David Misime, Naibu Kamishna kutoka Kamisheni ya Intelijensia na Jinai, Kheriyangu Khamis Mgeni, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro
 
Umuhimu wa KATIBA MPYA unazidi kujidhihirisha.
Kuna mambo yanatakiwa yawemo kwenye katiba yamshurutishe Rais kufanya na akikataa imuwajibishe mara paap paaap!Na si kwa Rais tu.Hii inapaswa kuwataka viongozi na watendaji wote serikalini.Kuna shida ambayo inakua ni loop-hole kwa viongozi kujifanyia mambo au kutofanya kwa faida ya nchi.
 
Jeshi la polisi linatakiwa kufumuliwa hasa ngazi ya SACP kwenda vyeo vya CP wastaafishwe wote.

Hii itasaidia kurejesha usimamizi wa nidhamu na utendaji wa walio chini yao kuzingatia kanuni na GPO ya polisi wanapotumwa askari kwenda kukamata watuhumiwa.

27 August 2024​

Masauni Akutana na Uongozi wa Jeshi la Polisi Kujadili Hali ya Amani na Usalama​

Dodoma. Waziri wa Mambo ya Ndani, Mwandisi Hamad Masauni leo amekutana na viongozi wa juu wa Jeshi la Polisi Tanzania kujadili hali ya amani na usalama ikiwemo matukio ya uhalifu yanayotkea nchini na hatua zilizochukuliwa.
View attachment 3082900

Kikao hiko pia kimehudhuriwa na Naibu Waziri wa Mambo ya ndani, Daniel Sillo, ambapo kwa upande wa Jeshi la Polisi ujumbe wake uliongozwa na Inspekta Jenerali wa Polisi, Camillus Wambura.


Kikao hiki kinakuja ikiwa ni siku chache tangu Jeshi la Polisi kupitia kwa msemaji wake kutoa taarifa za matukio mbalimbali ya kiuhalifu yanayohusu watu kupotea na mauaji ambayo Polisi ilieleza yalitokana na sababu mbalimbali ikiwemo masuala ya kujichukulia sheria mkononi, wivu wa mapenzi na imani za kishirikina.


Lakini pia wadau mbalimbali ikiwemo Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora, Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS), Asasi za Kiraia na vyama vya siasa wamekuwa wakipaza sauti kufuatia kuripotiwa kwa matukio ya utekaji na mauaji ya watu wazima na watoto.

Baadhi ya wadau hao ikiwemo vyama vya siasa wamewatupia lawama Jeshi la Polisi wakiwashtumu kuhusika jambo ambalo wamelikanusha.


Kikao hiko cha Waziri Masauni kilihudhuriwa na viongozi wote wa kamisheni za Polisi ikiwemo Kamishna wa Utawala na Menejimenti ya Rasilimaliwatu, Suzan Kaganda, Kamishna wa Fedha na Lojistiki, Liberatus Sabas, Kamishna wa Operesheni na Mafunzo, Awadh Juma Haji, Kamishna wa Sayansi ya Uchunguzi wa Jinai, Shabani Hiki.


Wengine ni Mkurugenzi wa Upelelezi na Makosa ya Jinai CP Ramadhani Kingai, Msemaji wa Jeshi la Polisi, ACP David Misime, Naibu Kamishna kutoka Kamisheni ya Intelijensia na Jinai, Kheriyangu Khamis Mgeni, Kamanda wa Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, SACP Jumanne Muliro
Ndio walijadiliana kutunga hii sinema siyo?
 
Hii ni kwa sababu Jeshi hilo limeshindwa kazi na kuamua kutafuta Umaarufu

View attachment 3082886View attachment 3082887
Hili tamko limekuwa la chadema tu, lakini ukweli ni kuwa kunatakiwa kuwe na chombo kipya mfano (internal investigation bureau), ambayo itawawajibisha vyombo vyote chini law enforcement act ikiwemo polisi

Hawa watu hawatobadilika until kutakapokuwa na power ya kuwawajibisha. Ndipo wataamua kukaa kwenye mstari
 
Kuna mambo yanatakiwa yawemo kwenye katiba yamshurutishe Rais kufanya na akikataa imuwajibishe mara paap paaap!Na si kwa Rais tu.Hii inapaswa kuwataka viongozi na watendaji wote serikalini.Kuna shida ambayo inakua ni loop-hole kwa viongozi kujifanyia mambo au kutofanya kwa faida ya nchi.
Mkuu,

Hiyo nchi ya unayoiota tunaweza kuifikia miaka 300 ijayo. Huko wamefika Wamerekani na walichukua miaka zaidi ya 200 au 300 kufika. Hicho Kikifanyika sasa kwenye nchi zetu za kiafrika hizi nchi hazitatawalika. (Mfano Kenya) Amka usingizini.

Tutafuteni maendeleo kwanza huko tutafika tu.
 
Mkuu,

Hiyo nchi ya unayoiota tunaweza kuifikia miaka 300 ijayo. Huko wamefika Wamerekani na walichukua miaka zaidi ya 200 au 300 kufika. Hicho Kikifanyika sasa kwenye nchi zetu za kiafrika hizi nchi hazitatawalika. (Mfano Kenya) Amka usingizini.

Tutafuteni maendeleo kwanza huko tutafika tu.
Kuna mtu anazuia mtu mwingine kuwaza kadiri ya maono yake mkuu?Wewe waza 200 na wengine wawazo mitatu.
 
Kwa kuwa wasomi wapo wengi, "kujiunga na jeshi la polisi ni lazima uwe na shahada kutoka chuo kinachotambuliwa na serikali"
 
Vichekesho.

Haumpo serious hata kidogo.
 
Back
Top Bottom