Kijana Mbappe mnamuoverrate sana. Tena lile timu lake Balon d'Or ataisikia tu kwa wenzie. Nani akupe Balon d'Or wakati unacheza ligi ya wakulima na wavuvi?
Halaand amechagua sehemu sahihi, ila kuchukua Balon d'Or itategemea mafanikioya team nzima, haswa UEFA. Maana Halaand hana matumaini kwenye international football, team yake ya taifa haina maajabu.
Kuna team ukichezea, inakua rahisi sana kushinda Balon d'Or, hasa team za spain. Ukishinda UEFA tu, tuzo inakuhusu. Lakini kuna team ukichezea, hata ukishinda kila kitu, bado hutoboi. Hapa ndipo unaona baadhi ya wachezaji wako tayari kupunguza mishahara ili wakacheze Barcelona au Madrid.
Kwa maamuzi ya Mbappe kuendelea kubaki ligi ya ufaransa, sioni akishinda Balon d'Or hivi karibuni!