KING MIDAS
JF-Expert Member
- Dec 1, 2010
- 8,589
- 16,936
UTANGULIZI
Chakra ni vituo vya nishati katika mwili wa mwanadamu. Vituo hivi vinaaminika kuunganishwa na ustawi wa kimwili, kiroho, na kihisia! Kulingana na Patanjali, baba wa sayansi za kiyoga, katika kitabu chake kiitwacho "The Yoga Sutras", kuna jumla ya chakra 114. Lakini katika somo letu tutajifunza 7 au 9 peke yake.
Kila chakra inahusishwa na rangi maalum na inasimamia kazi maalum katika mwili, kama vile afya ya kimwili, ubunifu, na hisia.
Kwa kuzielewa na kuziamsha chakra hizi, mtu anaweza kuboresha ustawi wake kwa ujumla na kuishi maisha yenye usawa zaidi.
Katika utangulizi huu, tutachunguza chakra 7, moja baada ya nyingine, zilizomo ndani ya mwili, na njia tofauti ya kuziamsha zote, na chakra nyingine 2 za ziada. Hizi 2, moja chini na nyingine juu, ziko nje kabisa ya mwili. Kwa hiyo, kwa jumla tutachunguza chakra 9.
Chakra ya 6 hujulikana kama "third eye" au jicho la tatu. Tutakapofika hapo tutajifunza kuwa kumbe hii dunia ya nje tunayoiona ni kivuli tu cha dunia ya ndani tusiyoiona, na kwamba macho ya kimwili ni kwa ajili ya dunia ya nje na jicho la tatu ni kwa ajili ya dunia ya ndani.
Tutajifunza pia jinsi ya kufumba na kufumbua kwa jicho la tatu, kwa kushirikiana na "pineal grand" (au antena ya jicho la tatu) na akili isiyotambua (au "subnconscious mind").
Baadaye tutajifunza kuhusu kanuni za ulimwengu. Kuna Kanuni au Amri 12 zinazoendesha ulimwengu huu kimwili! Kama tutakavyojifunza chakra, tutajifunza amri hizi moja baada ya nyingine hadi tuzielewe zote. Tukizielewa tutauelewa ulimwengu kwa kiwango cha juu.
Utafiti wa mada hizi umekamilika. Na usingekamilika bila Dipak Tanna, rafiki yangu wa kiroho. Dipak, huyo hapo kwenye picha upande wa kulia, ameshirikiana nami katika utafiti wa mada hizi tangu mwaka 2022; na hata sasa bado anaendelea kushirikiana nami.
Lengo la kufundisha mada hizi si kumbadili mtu dini au imani. Ni kusaka maarifa sahihi, pamoja na wasomaji wangu, kutoka katika kila pembe ya dunia hii ya kimazingaombwe. Hivyo, kuwa huru kujifunza mambo usiyoyajua.
Kwa upande wa kanuni za ulimwengu, mtu yeyote yuko huru kujifunza—hata kama wewe ni Mkristo au Mwislamu! Ni kanuni zilizoumbwa kwa ajili ya ulimwengu huu, bila kujali dini au imani ya mtu.
Watu waliofanikiwa sana katika dunia hii wanatumia chakra na kanuni za ulimwengu kutawala dunia; na hawataki mimi na wewe tuyajue maarifa haya, kwani watashindwa kututawala. Kuwa mmoja wao kwa kuanza na chakra.
—Enock Maregesi, mwanafalsafa na mwandishi wa vitabu
Chakra ni vituo vya nishati katika mwili wa mwanadamu. Vituo hivi vinaaminika kuunganishwa na ustawi wa kimwili, kiroho, na kihisia! Kulingana na Patanjali, baba wa sayansi za kiyoga, katika kitabu chake kiitwacho "The Yoga Sutras", kuna jumla ya chakra 114. Lakini katika somo letu tutajifunza 7 au 9 peke yake.
Kila chakra inahusishwa na rangi maalum na inasimamia kazi maalum katika mwili, kama vile afya ya kimwili, ubunifu, na hisia.
Kwa kuzielewa na kuziamsha chakra hizi, mtu anaweza kuboresha ustawi wake kwa ujumla na kuishi maisha yenye usawa zaidi.
Katika utangulizi huu, tutachunguza chakra 7, moja baada ya nyingine, zilizomo ndani ya mwili, na njia tofauti ya kuziamsha zote, na chakra nyingine 2 za ziada. Hizi 2, moja chini na nyingine juu, ziko nje kabisa ya mwili. Kwa hiyo, kwa jumla tutachunguza chakra 9.
Chakra ya 6 hujulikana kama "third eye" au jicho la tatu. Tutakapofika hapo tutajifunza kuwa kumbe hii dunia ya nje tunayoiona ni kivuli tu cha dunia ya ndani tusiyoiona, na kwamba macho ya kimwili ni kwa ajili ya dunia ya nje na jicho la tatu ni kwa ajili ya dunia ya ndani.
Tutajifunza pia jinsi ya kufumba na kufumbua kwa jicho la tatu, kwa kushirikiana na "pineal grand" (au antena ya jicho la tatu) na akili isiyotambua (au "subnconscious mind").
Baadaye tutajifunza kuhusu kanuni za ulimwengu. Kuna Kanuni au Amri 12 zinazoendesha ulimwengu huu kimwili! Kama tutakavyojifunza chakra, tutajifunza amri hizi moja baada ya nyingine hadi tuzielewe zote. Tukizielewa tutauelewa ulimwengu kwa kiwango cha juu.
Utafiti wa mada hizi umekamilika. Na usingekamilika bila Dipak Tanna, rafiki yangu wa kiroho. Dipak, huyo hapo kwenye picha upande wa kulia, ameshirikiana nami katika utafiti wa mada hizi tangu mwaka 2022; na hata sasa bado anaendelea kushirikiana nami.
Lengo la kufundisha mada hizi si kumbadili mtu dini au imani. Ni kusaka maarifa sahihi, pamoja na wasomaji wangu, kutoka katika kila pembe ya dunia hii ya kimazingaombwe. Hivyo, kuwa huru kujifunza mambo usiyoyajua.
Kwa upande wa kanuni za ulimwengu, mtu yeyote yuko huru kujifunza—hata kama wewe ni Mkristo au Mwislamu! Ni kanuni zilizoumbwa kwa ajili ya ulimwengu huu, bila kujali dini au imani ya mtu.
Watu waliofanikiwa sana katika dunia hii wanatumia chakra na kanuni za ulimwengu kutawala dunia; na hawataki mimi na wewe tuyajue maarifa haya, kwani watashindwa kututawala. Kuwa mmoja wao kwa kuanza na chakra.
—Enock Maregesi, mwanafalsafa na mwandishi wa vitabu