tatizo hakuna vigezo vya msingi vinavyo tumika kuteua watu hawana kuwa wakuu wa mikoa na Wilaya, wana angalia kwamba MTU ameitumikia kwa kiwango gani ccm, huyu alikua Mwenyekiti wa ccm Mkoa wa Iringa kabla ya kuteuliwa kuwa RC, lakini katika matukio tofauti amekua akitoa kauli tatanishi kama comedian badala ya kuwa kiongozi. Sasa kama watu wanajiteka, si wakamatwe tuone huo mfano wa watu waliojiteka!? Watu walio tekwa kwa siku za karibuni wapo mfano Sativa,alitekwa akapelekwa Polisi Oysterbay kisha Arusha halafu Katavi mbugani kabla ya kupigwa risasi, Mzee Kibao alitekwa kutoka kwenye Bus kisha kuuawa, huyo RC naye atusaidie kutuonyesha mifano ya watu 3 tu ambao wanajiteka !