Josephat Mgimwa
Member
- Apr 8, 2014
- 60
- 18
Hv juz wakati walimu wapatao 150 waligoma kuondoka katika ofisi za halmashauri ya manispaa ya Bukoba KWA kile walichodai kuwa wamechoshwa na dharau PAmoja na dhuluma inayofanywa na wahusika wakiwemo Maafisa utumishi na maafisa Elimu PAmoja na Kaimu mkurugenzi wa manispaa hiyo Kwa kutowapa fedha zao za kujikimu PAmoja na nauli walizotumia ktk safari ya kufika pale.
Inasikitisha zaidi pale ambapo chama cha walimu hawajachukua hatua yoyote kuhusiana na hilo. Haitoshi walimu hao toka walivyomwagwa na serikali sikivu hawakupata makazi wala mwelekeo wowote wa maisha.
Swali ni kwamba HIVI chama cha walimu hakioni matatizo ya walimu Ama si sehemu ya kazi zao? Walishindwa hata kuwapokea na kuwajulisha haki zao za msingi! Hv ni mikoa yote inafanyika HIVI? Nadhani kada ya ualimu inaweza kuwa ni moja kati ya kada za kuonewa na kukatwa makato mengi kuliko kada zote Kwa sababu walimu wenyewe hawaoneshi kujitambua na kudai haki zao huku chama cha walimu wakizidi kusimama upande wa serikali na kuchukua makato ya walimu bila kuwasaidia..
Walimu wapya hawana ABC yeyote kuhusu chama chao dhalimu..
Inasikitisha zaidi pale ambapo chama cha walimu hawajachukua hatua yoyote kuhusiana na hilo. Haitoshi walimu hao toka walivyomwagwa na serikali sikivu hawakupata makazi wala mwelekeo wowote wa maisha.
Swali ni kwamba HIVI chama cha walimu hakioni matatizo ya walimu Ama si sehemu ya kazi zao? Walishindwa hata kuwapokea na kuwajulisha haki zao za msingi! Hv ni mikoa yote inafanyika HIVI? Nadhani kada ya ualimu inaweza kuwa ni moja kati ya kada za kuonewa na kukatwa makato mengi kuliko kada zote Kwa sababu walimu wenyewe hawaoneshi kujitambua na kudai haki zao huku chama cha walimu wakizidi kusimama upande wa serikali na kuchukua makato ya walimu bila kuwasaidia..
Walimu wapya hawana ABC yeyote kuhusu chama chao dhalimu..